SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Bora za Nokia 2022

Brand

Sihaba Mikole

February 17, 2022

Smartphone za nokia ni moja ya simu simu ambazo hupokea matoleo mapya ya android mara kwa mara pale yanapotoka.

Japokuwa si simu zote za Nokia zina ubora mkubwa.

Matoleo mengi ya Nokia hayawezi kushindana na simu bora za Samsung kwenye engo nyingi.

Ila kuna Simu bora za nokia huuzwa kwa bei nafuu.

Na simu hizo zina vitu vingi vizuri vinavyopatikana kwenye brand za simu za oppo na pia simu za xiaomi.

Baadhi ya Nokia zina sifa sawa na smartphone za Tecno.

Ila kama umechoka na simu mbaya na unataka kutumia kila toleo la android basi zipo kali ambazo zipo kwenye orodha.

Tutazame ubora na mapungufu ya kila simu ya nokia zilizopo kwenye orodha.

Nokia X100

Simu ya nokia x100 inatumia chip ya kawaida ambayo inasapoti mtandao wa 5G

Processor ya snapdragon 480 haina nguvu kubwa sana ukilinganisha na processor zingine za zingine.

Sifa za smartphone ya nokia x100 zinaifanya simu kuwa na ubora wa kati kama sio wa chini

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 480 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 460
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori 128GB na RAM 6GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(main, wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 4470mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 509,080/=

Kwa kuzichambua kila sifa, kamera nne za nokia hazina OIS wala teknolojia ya dual pixel PDAG.

OIS na dual pixel hutuliza kamera ya simu na kurenga vizuri kitu kinachopigwa picha hasa kinachotembea.

Kamera zake haziwezi chukua video za 4K.

4K huwa na resolution kubwa.

Mfumo wa chaji wa nokia unapeleka umeme wa wastani.

Umeme wa 18W unajaza betri lake la 4470mAh kwa muda mrefu.

Display kwa maana si ya kuvutia, inatumia IPS LCD ambayo huonyesha rangi vibaya kulinganisha na AMOLED.

Inatumia mfumo wa memori wa kawaida, na ukubwa wake ni 128GB

Bei ya hii simu ni kubwa ukilinganisha na sifa zake.

Zipo simu za xiomi za 5g zenye bei sawa na Nokia X100.

Ndio, bei ni kubwa kwa sababu simu haina viwango vya IP vinavyoonyesha ubora wa simu kuzuia maji kupenya.

Nokia G300

Simu ya Nokia G300 inatumia chip ya Snapdragon 480 ambayo imetumika pia kwenye nokia x100.

Hivyo nokia g300 ni smartphone ya 5g.

Kiubora nokia x100 ni nzuri kuliko hata nokia g300 kwa kuzingatia sifa.

Upande wa kamera na display unaweza kumvutia kwa mtu anayeanza kutumia samrtphone.

Lakini ni simu yenye ubora ambao unazidiwa na simu ya infinix zero 5g kwa kuzingatia sifa.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 480 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 460
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori  64GB na RAM 4GB
Kamera Kamera tatu

  1. 16MP,PDAF(main, wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(depth)
  4. 8MP(selfie camera)
Muundo Urefu-6.52inchi
Chaji na Betri
  • 4470mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 347,076.86/=

Simu ina kamera tatu ambazo haziwezi chukua video za 4k.

Na hazina dual pixel, optical zoom wala OIS.

Ukitataka kufahamu optical zoom kwenye kamera tazama simu za samsung galaxy s22

Betri lake ni kubwa na linaweza chukua muda kujaa kutokana na mfumo wa chaji wa nokia kupeleka umeme wa wastani wa 18W.

Simu ina kioo cha IPS LCD  chenye resolution ngodo ya 720 x 1600.

Resolution ya 720p hainyoshi pia picha na video kwa uang’avu.

Simu ni nzuri ukiwa unatumia ndani ila ukitumia kwenye jua miale ya jua itafanya screen kuonekana na kiza kidogo.

Sababu kubwa kioo kina nits ndogo.

Pia memori yake haina kasi kubwa.

Nokia G300 ni simu ya bei nafuu ya 5G.

Nokia G50

Simu ya nokia g50 pia ina 5G kutokana na kutumia processor Snapdragon 480.

Ina vitu vingi vinavyofanana na Nokia G300.

Isipokuwa g50 ina kamera zenye ubora sawa na nokia x100

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 480 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 460
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori , 64GB, 128GB na RAM 4GB,6GB
Kamera Kamera TATU

  1. 48MP,PDAF
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(depth)
  4. 8MP(Selfie Camera)
Muundo Urefu-6.82inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 536,848/=

Simu ni ndefu kwa kimo n betri yake ni kubwa.

Chaji inapeleka umeme wa wati 18 ambao  unafanya simu kujaa muda mrefu.

Kamera tatu hazina telephoto ambayo inaweza kupiga picha kitu ambacho kipo mbali na kuonekana vizuri.

Pia simu haina uwezo wa kuzuia maji kupenya kama simu ikizama kwenye maji.

Nokia hizi zipo za 64GB na 128GB ni simu ghari.

Kutokana na kutomia processor ya ubora wa kawaida na display yenye ubora wa chini ya IPS LCD, simu inaweza kukaa na chaji muda mrefu.

Bei ya simu ni kubwa ukilinganisha ubora.

Nokia XR20

Simu ya XR20 ina sifa nyingi sawa na Nokia G50.

Tofauti ipo kwenye kamera.

XR20 ina kamera mbili ambazo hazina vitu vinavyofanya kamera kuwa bora.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 480 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 460
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 11
Memori  64GB,128GB na RAM 4GB,6GB
Kamera Kamera mbili

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 13MP(ultrawide)
  3. 8MP(Selfie Kamera)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 4630mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,168,167.08/=

Nokia 8.3 5G

Simu ya Nokia 8.3 5G inatumia processor yenye nguvu na ubora wa kati ya Snapdragon 765 5G.

Speed ya internet ya 5g ya processor ya Snapdragon 765  ni kubwa kuliko ile iliyoko Infinix zero 5g.

Speed ya kudownload inaweza fika mpaka 7Gbps kwenye eneo lenye network nzuri ya 5g mfano mtandao wa simu wa marekani ya 5G ya T-Mobile.

Speed kubwa inachangiwa na modem ya snapdragon x52 5g.

Nokia 8.3 ina maboresha mengi ukilinganisha na Nokia matoleo ya G.

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 765G 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 1×2.4GHz kryo 475, 1×2.2GHz kryo 475
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 475
  • GPU-Adreno 620
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 10
Memori UFS 2.1, 64GB,128GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera nne

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
  5. 24(Selfie Kamera)
Muundo Urefu-6.81inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 798,330/=

Mfumo wa memori wa hii simu una kasi ya wastani.

Mfumo wake ni aina ya UFS 2.1 japo kasi yake si kubwa kama ya UFS 3.1

Kamera zipo nne.

Kamera yake kuu ina gyr-EIS ambayo hufanya kamera itulie wakati unachukua video huku ukiwa unatembea.

Kamera zake zinaweza chukua video za 4k.

Display si ya kuvutia yenye kuonyesha vitu kwa ubora mkubwa.

Betri yake ya 4500mAh inapeleka umeme wa wastani unaofanya simu kuchukua muda kujaa.

Umeme mdogo ni mzuri unachangia betri kudumu.

Hasara ya fast charge ni kuua betri mapema.

Simu ina android 10 ila inaweza kuupdate kwenda android 11.

Kwa bahati mbaya simu haina gorilla glass wala IP68 inayozuia maji kupenya.

Simu yenye bei kubwa kama hi vitu vya namna hiyo ni vya muhimu.

Nokia 8V 5G UW

Simu ya Nokia 8V 5G UW inafanana kila kitu na NOKIA 8.3 5G.

Ikiwemo kutumia processor ya snapdragon 765 5g.

Ila ipo tofauti upande wa memori

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 765G 5G
  • Core Zenye nguvu(2) – 1×2.4GHz kryo 475, 1×2.2GHz kryo 475
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 475
  • GPU-Adreno 620
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 10
Memori eMMC 5.1, 64GB na RAM 6GB
Kamera Kamera NNE

  1. 64MP,PDAF(main)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.81inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 1,619,800/=

Mfumo wa memori uliopo kwenye simu hii ni eMMC.

eMMc inazidiwa kasi na UFS 2.1

Nokia G20

Simu ya Nokia inatumia processor yenye nguvu ndogo ya Cortex A53

Ifahamu sifa za nokia g20 kupitia link hii: sifa za nokia g20

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G35
  • Core Zenye nguvu(2) – 4×2.3GHz Cortex A53
  • Core Za kawaida(6) – 4×1.8GHz Cortex A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori 64GB, 128GB na RAM 4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.52inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 444,288/=

Nokia G10

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G25
  • Core Zenye nguvu(2) – 4×2.0 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(6) – 4×1.5 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori eMMC 5.1, 32GB,64GB na RAM 3GB, 4GB
Kamera Kamera tatu

  1. 13MP,AF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 2MP(depth)
  4. 8MP(selfie kamera)
Muundo Urefu-6.52inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 370,240/=

Nokia 3.4

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 460
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A73
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A53
  • GPU-Adreno 610
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
Memori eMMC 5.1, 32GB,64GB na RAM 3GB,4GB
Kamera Kamera TATU

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(depth)
  4. 8MP(selfie camera)
Muundo Urefu-6.39inchi
Chaji na Betri
  • 4000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 358,670/=

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

OnePlus 11R

Simu 15 za OnePlus na Bei zake (Aina zote)

OnePlus inaweza ikawa ni jina geni kwa watumiaji wengi smartphone Tanzania Ila OnePlus ni moja ya kampuni kutoka china inayotengeneza simujanja za madaraja ya kati na ya juu Simu nyingi […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram