SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya OPPO A77 na Ubora Wake (Oppo Mpya)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 2, 2022

Simu ya OPPO A77 ni simu janja ya android 12 iliyoingia sokoni mwezi juni 2022

Simu hii inaingia katika kundi la kati kutokana na sifa na ubora wake

Bei ya OPPO A77 inazidi shilingi laki tano kwa hapa Tanzania

Japokuwa ina bei kubwa, ila ubora wake ni wa wastani hasa upande wa utendaji na kamera

Bei ya OPPO A77 ya GB 128 Tanzania

Oppo yenye GB 128 inauzwa shilingi 540,000 kwa hapa nchini

Kuna utofauti wa 2% wa bei ya hii simu kati ya Kenya na TZ

Kwani hii simu nchini Kenya inapatikana kwa shilingi 524,000

Bei yake si ya kiushindani kutokana na sifa zake na pia uwezo wake wa processor kiutendaji

Ukizifuatilia sifa za oppo A77 zinaweza zikakufanya kutafuta simu mbadala kutokana na aina ya bei

Sifa za Oppo A77

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G35
  • Core ndogo(8) – 8×2.3GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(-) –
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 12
  • ColorOs 12.1
Memori eMMC 5.1, 128GB na RAM 4GB
Kamera Kamera nne

  1. 50MP, AF(wide)
  2. 2MP
Muundo Urefu-6.56inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 540,000/=

Ni upi Ubora wa Simu ya Oppo A77?

Oppo A77 ina memori kubwa inayoweza kuhifadhi na kuweka applikesheni nyingi

Mtumiaji hatopata wasi wasi wa simu kujaa

Ni simu inayokaa na chaji masaa mengi ikizingatiwa chip yake inatumia umeme mdogo

Ujaaji wa chaji ni wa haraka sana

Kwani chaji yake inapeleka umeme mwingi wa kutosha

Pia ina kamera kuu yenye megapixel nyingi japokuwa wingi wa megapixel si kigezo cha simu kuwa na kamera nzuri

Simu inakuja na toleo jipya la android ambapo kuna baadhi ya simu mpya bado zinakuja na Android 11

Ila si vitu vyote vya oppo a77 vipo kwenye viwango vya simu nyingi zinauzwa zaidi ya laki tano

Fuatilia makala yote ufahamu nyanja ambazo simu ipo vizuri na zile ambazo hazipo vizuri

Uwezo wa Network

Oppo A77 ni simu ya 4G

4G inayotumia ni aina ya LTE Cat 7 yenye kasi ya juu kabisa ya kupakuwa faili ya 300Mbps

Kwa Tanzania, hakuna mtandao wa simu kwa sasa unaotoa spidi hiyo

Kama ungekuwepo basi simu ingekuwa inamaliza kudownload faili la ukubwa wa 3600MB kwa sekunde 100

Ambazo ni sawa na dakika moja na sekunde 40

Uzuri ni kuwa ina masafa yote yanayotumiwa na mitandao ya simu nchini

Hivyo basi, intaneti za 4G za laini zote zitafanya kazi

Pia pitia: Maana ya 5G kiundani

Ubora wa kioo cha OPPO A77

Moja ya kitu kinachoifanya bei ya OPPO A77 kuonekana kuwa kubwa ni aina ya kioo inachotumia

Kioo cha Oppo A77 ni cha IPS LCD chenye resolution 1612 x 720 pixels

Hiyo ni resolution yenye pixel chache kitu kinachofanya muonekano wa vitu kutokuwa  na ubora mkubwa sana kama vioo vya pixels nyingi

Baadhi ya simu kama Redmi Note 10 Pro zinatumia vioo vya AMOLED

AMOLED ina rangi nyingi zinazochangia vitu kuwa na muonekano halisi kwa kiasi kikubwa

IPS LCD huwa hazionyeshi rangi nyeusi halisi.

Tazama, jinsi kioo cha amoled cha samsung a52 kinavyoonyesha rangi nyeusi

Pia refresh rate yake ni ya kawaida inayoendana na uwezo wa processor

Nguvu ya processor Meditek Helio G35

Processor ya Mediatek helio G35 ndio inayoipa nguvu simu ya OPPO A77

Ni chip ya daraja la chini kwani inaundwa na core zenye nguvu ndogo pekee

Ina jumla ya core zipatazo nane.

Hivyo ni simu inayomfaa mtumiaji asiyetumia applikesheni zinazotumia nguvu kubwa

Ukiwa na simu yenye chip dhaifu kuna vitu vingi hutovifanya kwa ufanisi

Ni vizuri ukajua namna ya kujua simu yenye processor yenye nguvu

Pitia hapa: Jinsi ya kujua simu nzuri kwa kuangalia uwezo wa processor

Kwenye app ya Geekbench helio g35 ina alama 171 ambayo inaendana kwa kiasi fulani na chip ya Exynos 850

Exynos 850 imetumika kwenye simu ya Samsung Galaxy A13

Uwezo wa GPU ya PowerVR GE8320

Kirefu cha GPU ni Graphics Processing Unit

Ni aina ya processor ambayo ina kazi ya kuonyesha picha na kuchora picha za michoro ya 2D na 3D na kuonyesha video kwenye screen

Bila GPU simu haiwezi kucheza magemu.

Picha ambazo GPU inaziandaa huitwa frame, na huandaa kwa kuzingatia resolution

GPU ikiwa inaweza kuonyesha fremu nyingi kwa sekunde basi uwezo wake ni mkubwa

PowerVr GE8320 ina uwezo mdogo wa kucheza gemu kwenye ubora wa juu

Gemu ya simu ya PUBG inacheza kwa fremu 24 kwa sekunde (24fps), kikawaida chip nzuri huzalisha zaidi ya 60fps

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Oppo A77 ina ukubwa wa 5000mAh

Huu ni ukubwa unaoifanya simu kuweza kukaa na chaji masaa mengi (zaidi ya 14)

Ikizingatiwa, simu haitumii processor inayokula moto mwingi, na kioo chake hakina ulaji mkubwa wa chaji

Chaji yake inapeleka umeme mwingi

Ambao unaweza ukajaza betri ndani ya dakika 80 kama ilivyo kwa Redmi Note 10

Kwani chaji ya oppo a77 inapeleka umeme wa wati 33

Ukubwa na aina ya memori

Hii simu inatumia memori aina ya eMMC 5.1

Uwezo wa memori kusafirisha data nyingi huongeza utendaji wa simu

Lakini eMMC 5.1 inaweza kusafirisha data kwa spidi ya 600MBps

Ni kasi kubwa ila sio kubwa kama simu zinazotumia UFS 2.1 au NVMe ya iPhone 12 Pro Max

Kuna toeo moja tu la oppo a77 upande wa memori

Toleo hilo lina GB 128 na GB 4

Ukubwa wa memori kwa kiasi kikubwa unachangia simu kuuzwa kwa bei kubwa

Hata simu za makampuni nyingine bei huongezeka kutokana na ukubwa wa memori na RAM

Ubora wa kamera

Simu ina kamera mbili ambapo kamera moja ina kiwango kidogo cha megapixel (2MP)

Kamera nzuri za simu huwa zinakuwa na simu zenye resolution ya kuanzia 10MP

Mfumo mzima wa kamera za hii simu ni wa kawaida sana

Kwani inatumia ulengaji AF, utambuzi wake wa kitu kinachopigwa si mkubwa kama PDAF.

Kwenye mwanga hafifu kamera kuu haitoi picha nzuri

Ila kwenye mwanga mwingi (hasa mchana) picha zinatokea vizuri japo huwezi linganisha na Tecno yenye kamera nzuri

Japokuwa kamera kubwa ina 50MP ila simu haiwezi kurekodi video za 4K

Hii inatokana na nguvu ndogo ya processor

Ubora wa Software ya ColorOS 12.1

Ukiondoa mfumo wa Samsung wa One UI 4.1, ColorOS ni mfumo mzuri unaorahisha matumizi ya simu

Oppo A77 inatumia ColorOS 12.1 na Android 12

Aina za emoji ambazo ColorOS 12.1 ni wa kipekee zenye muundo wa 3D

Kitu kizuri ni kuwa mfumo unaruhusu kuhariri (editing) emoji na kuweka kwenye muundo unaoutaka wewe

Jambo jingine la kupendeza ni uwezo wa simu kutumia applikesheni mpaka tatu kwa wakati mmoja

ColorOS 12.1 inaweza kuzigawanyisha app katika sehemu tofauti

App ya kwanza unaweza kuiweka upande wa kushoto mwa screen ya pili kulia, na zote zikawa zinatumika wakati mmoja

Yapi Madhaifu ya Oppo A77

Oppo A77 inatumia processor yenye nguvu ndogo huku bei yake ikiwa kubwa

Kamera zake hazitoi picha zenye ubora mkubwa hasa nyakati za usiku

Simu inatumia kioo cha LCD chenye resolution ndogo

Haina 5G, Vodacom wamezindua uanzishwaji wa mtandao wa 5G

Hivyo Tanzania itaanza kunufaika na teknolojia hii mpya ya mawasiliano

Haina viwango IP(Ingression Protection) kwa ajili ya ulinzi wa maji na vumbi

Neno la Mwisho

Kama unahitaji simu nzuri kwa ajili shughuli za kawaida basi bei ya oppo a77 haiwezi kukuzuia kuwa nayo

Lakini kama unahitaji zaidi ya simu, kuna machaguo mengi ya simu mazuri yanauzwa kwa chini ya laki tano

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram