SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu ya Tecno Yenye Camera Nzuri [Tecno Phantom X]

Miongozo

Sihaba Mikole

August 6, 2022

Kama umeshawahi kutumia simu za tecno na hukuwahi kuridhishwa na ubora wa kamera basi Tecno Phantom X inaweza kukubadilisha.

Tecno Phantom X ni moja ya tecno yenye camera nzuri kaitka upigaji picha na kurekodi video

Inazipita Tecno nyingi zilizopo sokoni

simu-nzuri-tecno-phantom-x

Ila kiuhalisia haiwezi kuwekwa kwenye kundi la simu zenye kamera nzuri na ubora mkubwa

Ubora wake unashindana zaidi na smartphone za Infinix

Kwenye hii posti utaona ubora wa picha ambazo Phantom X imezipiga na ufafanuzi wa kamera zake tatu

Utaona uwezo wa phantom x katika kupiga picha nyakati za mchana na usiku

Idadi na aina ya kamera za Tecno Phantom X

Simu ya tecno phantom x ni tecno macho matatu kwa maana ina aina tatu za kamera

Kamera hizo ni

  1. Wide (kamera kuu) yenye resolution ya 50MP
  2. Telephoto yenye resolution ya 13MP
  3. Ultrawide ya nyuzi 120 na resolution ya 8MP

Kamera ya Telephoto hutumika kupiga vitu ambavyo vipo mbali sana na kamera

Huwa zinatoa picha bila kupoteza ubora (kwa maana pixels) ukilinganisha na zoom ya app ya kamera

kamera ya tecno phantom idadi ya kamera

Ultrawide huwa inapiga picha eneo pana mfano kama unataka uwanja wa mpira uonekane wote basi utatumia kamera ya ultrawide

Kamera ya wide ni ile kamera ya kawaida ambayo ndio hutumika zaidi

Ukitazama resolution ya moja ya kamera ina 50MP.

Wingi wa megapixel si kigezo kinachoelezea ubora wa kamera ikiwemo phantom x

Kamera za iphone huwa zina megapixel 12 tu ila huwa zinatoa picha kali

Bali kuna vitu vya muhimu vinayoisaidia simu kutoa picha safi

Vitu vya muhimu vilivyopo kwenye kamera ya Tecno Phantom X

Kama kuna kitu cha msingi cha kutazama kwenye kamera basi ni aina ya ulengaji (autofocus)

Na uwepo wa HDR

Phantom X ina ulengaji ulio mzuri wa kutambua kukilenga kitu kwa ustadi

Hiyo inatokana na simu kuwa na autofocus ya Dual Pixel PDAF na Laser AF

Autofocus husaidia kutambua kinachopigwa kama kipo kwenye eneo linalotakiwa (focus)

Simu yenye dual pixel pdaf hutoa picha zinazoonekana vizuri ambazo zimepigwa kwenye mwanga mdogo

Na pia dual pixel pdaf hutoa picha vizuri ukiwa unapiga kitu kinachotembea kwa haraka mfano ukiwa unampiga picha ndege angani

Kwa sababu dual pixel pdaf huwa iko fasta kutambua na kukilenga kitu

Laser AF hutumia miale kutambua kinachopigwa picha.

Kamera hii inaweza kuona kitu hata kwenye giza

Uwepo wa HDR

Kamera ya tecno phantom x ina hdr ya kawaida na sio ile ya HDR10 au HDR10+

Umuhimu wa HDR ni kuboresha muonekano wa vitu vinavyopigwa picha au kurekodiwa

Lengo kubwa ni muonekano wa picha uendane na jinsi kitu kinavyoonekana na jicho la mwanadamu kwenye mazingira halisi.

Na huwa inasaidia sana kuonyesha vitu vizuri kwenye mwanga mdogo

Uwepo wa Optical Zoom

Optical zoom ni aina zoom(kukuza picha) inayotumia lenzi za kamera

Optical zoom ya phantom x inaweza kukuza kitu mara mbili

Ni ndogo ukilinganisha na Samsung Galaxy S22 ambayo inakuza kitu mara tatu

Japokuwa app ya simu (digital zoom) inaweza kuza kitu mara 30 lakini huwa zinapoteza ubora

Optical zoom haipotezi ubora pindi itumikapo

Uwezo wa kukusanya mwanga

Uwezo wa ukusanyaji mwanga hupimwa kwa kutazama ukubwa wa tundu unaopitisha mwanga kwenda kwenye lenzi

Hii hufahamika kama aperture vipimo vyake huandikwa f/{namba }

Mfano Tecno Phantom X aperture yake ni f/1.9

Hivyo upitishaji mwanga ni wa kiwango cha kulidhisha

Namba ikiwa kubwa maana yake mwanga unaopita ni mdogo na ikiwa ndogo maana yake simu inapitisha mwanga mwingi

Simu ikiwa inapitisha mwanga mwingi na picha hutokea vizuri pia

Muundo wa app ya Camera ya Tecno phantom X

App ya phantom x ukiifungua utakuta imeandikwa AI Camera

Hii ni kamera ya wide ile yenye 50MP

App ina machaguo mengi ikiwemo uwezo wa kuzima HDR kama huitaji

kamera ya tecno phantom app

Na pia ina kitu kinaitwa Super Night Mode

Ambayo inafaa kutumika kama mwanga ukiwa mdogo

Yenyewe inatumia algorithms(kanuni) ambazo zinaweza isaidia kamera kutoa picha vizuri nyakati za usiku

Ubora wa picha nyakati za Mchana

Kamera ya tecno phantom x inatoa picha nzuri kimuonekano

Upande wa rangi inajitahidi kwa kiasi kikubwa kuonyesha rangi sahihi

Hivyo tatizo la overexposure si kubwa sana

Changamoto kubwa japo ina overexposure ndogo, ila inaifanya kamera kutoonyesha rangi kwa uzuri.

kamera-ya-tecno-phantom-mchana

Ukiizoom picha mara moja ubora wa muonekano wa vitu unapungua ubora kiasi tofauti na picha iliyopigwa na iphone 13 pro max kwenye eneo hilo

Itazame hapa na ulinganishe: Picha ya jengo iliyopigwa kwa iPhone 13 pro Max

Ila kitu cha msingi ambacho ni kizuri zaidi ni uwezo wake wa kutofautisha rangi za vitu

Tazama upande wa kichaka kulia mwa mti

kamera ya tecno phantom mchana rangi

Picha inaoonyesha kivuri hakijaweza kuzuia rangi za majani kupotea

Baadhi ya kamera hupoteza kabisa uhalisia pale sehemu inapokuwa na giza tofauti na jinsi kitu kinavyoonekana

Ila hii imejitahidi kwa hilo

Japokuwa simu ina noise(vitu vinavyochafua ubora wa picha) zinazoweza onekana kwa uwazi

Selfie camera(kamera za mbele zipo mbili) inajitahidi kuonyesha vitu vizuri

Ila kwenye mwanga mkali selfie camera ya tecno phantom x inakumbana kuzidi kwa uwiano wa contrast

Kwa maana muangaza unakuwa mwingi mpaka unapoteza rangi halisi ya kitu

kamera ya tecno phantom mchana selfie

Hizo sehemu ambazo zimezungushiwa zimekuwa nyeupe badala ya nyekundu (pinki nadhani)

Hili tatizo hujulukana kama overxposure

Kama kamera za selfie zingekuwa na HDR hilo tatizo lingepunguzwa

Ila kiujumla kamera hii ni nzuri kwa kulinganisha na simu nyingi za tecno

Ubora wa picha nyakati za usiku

Kamera kubwa ya tecno inaonyesha vitu vilivyopo kwenye picha kwa uzuri kiasi fulani

Kama ilivyo kawaida  changamoto ya noises zipo kwa nyakati za usiku

Noise(vitu visivyohitajika kama ukungu) kwa kamera za simu huwa zipo

Ila simu zenye kamera kali zaidi huonekana kwa kiwango kidogo

kamera ya tecno phantom usiku

Kama picha inavyoonekana, karibu vitu vyote vinaokena kwa uzuri

Ili upate ubora mzuri itakubidi utumie Super Night Mode

Vinginevyo ubora wa picha unaweza usiwe mkubwa sana

Ubora wa kamera za Ultrawide na Telephoto

Uwezo wa kamera hizi mbili ni wa kiwango cha chini kiujumla

Upande wa kamera wa ultrawide hautoi picha nzuri

Hii inawezekana ikawa inachangiwa na resolution yake ya 8MP

Lakini Redmi Note 10 ina kamera ya ultrawide yenye 8MP lakini ubora wake ni wa kuridhisha

Ubora wa Video

Tecno Phantom X inaweza kurekodi video za ubora aina mbili

Yaani video za Full HD na 4K (UHD)

Inarekodi video za 4K kwa kiwango cha fremu 30 na 60 kwa sekunde

Ila seldie kamera inarekodi video za full hd pekee

Unaweza tazama hapa

Ila kwa bahati mbaya simu inakosa teknolojia ya OIS

OIS (Optical Image Stabilization) huondoa mitikisiko wakati wa kurekodi huku ukiwa unatembea

Hivyo video hutulia

Bei ya Tecno Phantom X

Kikawaida simu ikiwa na kamera nzuri basi bei yake huchangamka pia

Kwa kuwa Tecno Phantom X ni tecno yenye camera nzuri basi bei yake haiwezi kuwa sawa na tecno zingine

Kwani bei yake inazidi milioni moja

Japokuwa kuna vitu vingine pia ambavyo huchangia bei kuwa juu.

Fuatilia: Ubora na bei ya Tecno Phantom X

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram