SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Samsung Galaxy A52 na Sifa Muhimu (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

August 7, 2022

Kampuni ya Samsung ilizindua simu nzuri ya kundi la kati aina ya Samsung Galaxy A52 mwanzoni mwa 2021

Utendaji wa Galaxy A52 ni wa kiwango kikubwa unaochuana na simu nyingi za android 2022

Hivyo inafanya bei ya samsung galaxy a52 izidi shilingi laki nane ikiwa mpya

amsung a52 display muonekano

Japokuwa kisifa ni simu inayopaswa kuuzwa chini ya laki nane kwa sasa ili iwe shindani

Ila simu ina vitu vingi vinavyoshawishi kuinunua kama utakavyoona baadae kwenye makala hii

Bei ya Samsung Galaxy A52 ya GB 128

Kwa hapa Tanzania hasa Dar Es Salaam bei ya samsung galaxy a52 ikiwa mpya ni shilingi 860, 000/=

Wauzaji wanaoiuza ikiwa imetumika wengi wanaiuza kwa shilingi 560,000/=

samsung a52 summary

Kwa bei isiyozidi laki sita inastahili zaidi kwa sasa kutokana na uwepo wa matoleo ya simu za xiaomi na Realme

Kuna simu mpya za laki nane za xiaomi ambazo zina sifa za ziada nyingi ambazo hazipo kwenye Samsung A52

Sifa za Samsung Galaxy A52

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 720G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.3 GHz Kryo 465 Gold
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Kryo 465 Silver
  • GPU-Adreno 618
Display(Kioo) Super AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 11
  • One UI 4.0
Memori UFS 2.1: 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
  4. 5MP(depth)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 860,000/=

Ni upi ubora wa simu ya Samsung Galaxy A52?

Galaxy A52 ni simu inayoweza kuzuia maji kupenya ndani

Ina kamera inayoweza kupiga eneo pana

Chaji yake inawahi kujaza betri kwa muda mfupi

Utendaji wake ni mkubwa kutokana na kutumia chip yenye nguvu

Ina kioo chenye uwezo wa kuonyesha rangi nyingi hivyo vitu vitaonekana kwa ufanisi

Ina nafasi kubwa za kuweka applikesheni na mafaili mengi

Kioo chake ni chepesi(smooth) kutachi na kuchezea magemu

Uwezo wa Network

Samsung A52 ni simu ya 4G inayokubali masafa 13 yakiwemo yanayotumiwa na mitandao ya simu ya Tanzania

Aina 4G simu inayotumia ni LTE Cat 15

Spidi ya juu kabisa ya kudownload faili ya LTE Cat 15 ni 800Mbps

Kasi hii inaweza kudownload faili la ukubwa 1000MB kwa sekunde kumi tu

samsung a52 network

Lakini hilo inategemea na nguvu ya mtandao wa simu kwa kiasi kikubwa

Kwa mfano Halotel kwa baadhi ya maeneo kasi yake ni 27Mbps

Hii ni 3% ya uwezo wa simu ya samsung galaxy a52 iliyonayo kwenye network

Hivyo, kwa faili la 1000MB itachukua sekunde 294 sawa na dakika tano(kimakadirio) kumalizika kudownload lote

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A52

Kioo cha Samsung Galaxy A52 ni aina ya super amoled ambavyo huundwa na samsung wenyewe

Kwenye usahihi wa rangi, super amoled huwa ipo mbele ya vioo vya IPS LCD

Rangi nyeusi inaonekana kwa kukolea sana kwenye super amoled

samsung a52 display

Uzuri wa kioo cha galaxy a52 ni kuwa na refresh rate kubwa ya 90Hz

Refresh rate kubwa inatengeneza uwepesi wa kutachi simu na kucheza gemu

Ubora wake wa kioo unachangiwa pia na resolution kubwa ya 1080 x 2400 pixels

Nguvu ya processor Snapdragon 720G

Kila kitu kinachofanywa na Galaxy A52 kinachakatwa na processor ya Snapdragon 720G

Ni chip yenye jumla ya core zipatazo nane

Kati ya hizo core zenye nguvu zipo mbili na core zenye utendaji mdogo zipo sita

samsung a52 processor

Core zenye nguvu kubwa zinaifanya simu kuweza kufanya kazi kubwa kwa urahisi

Kama unacheza la PUGB Mobile, processor itacheza kwa resolution kubwa na kwa kutoa 42fps

Ndio maana Geekbench inaipa chip alama 565 japo sio nyingi kama Apple A14 Bionic

Apple A14 Bionic imetumika kwenye simu ya iPhone 12 Pro Max

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Samsung Galaxy A52 inapeleka umeme wa wati 25

Ni umeme unaoweza jaza simu kwa 50% ndani ya nusu saa

Betri yake ina ukubwa wa 4500mAh

Betri hii inaweza kuisha chaji baada ya masaa 14 simu ikiwa inatumia intaneti masaa yote mfululizo

Hivyo unapata simu yenye utendaji mkubwa na ukaaji wa chaji wa kuridhisha

Ukubwa na aina ya memori

Kuna Samsung Galaxy A52 za GB 128 na 256

Kinachotofautiana sana ni ukubwa wa RAM

Kwani zipo zenye RAM ya 4GB, 6GB na 8GB

Ukipata yenye RAM kubwa inamaanisha simu itakuwa na uwezo wa kufungua apps nyingi kwa urahisi zaidi

samsung a52 nyuma

Ikizingatiwa aina ya RAM zake ni LPDDR4X yenye bandwidth ya juu kabisa 13Gbps

Aina ya memori zake ni UFS 2.1 ambazo usafirishaji wake wa data ni 1200MBps

Kwa maana kama unakopi faili la 2400MB kwenda kwenye simu basi itamalizika kukopi kwa sekunde mbili

Memori za UFS hufanya simu kufungua app kwa haraka

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A52

Hii simu inalindwa na kioo cha Gorilla 5 upande wa nyuma na mbele

Ni ngumu simu kupasuka kama ikianguka kwa kimo cha mita moja kwenye uso wa ardhi ulio flati

Lakini ikianguka kwa kimo cha 2m screen ya simu lazima ipasuke

samsung a52 bodi

Kioo cha gorilla ni kigumu pia kuchunika

Ukichukua sarafu ya shilingi mia na kuanza kuisugua kwenye kioo au nyuma hutoona mikwaruzo

Galaxy A52 ina viwango vya IP67

Hivyo hii ni simu ambayo haipitishi maji

samsung a52 bodi kwenye maji

Ukiingiza kwenye jagi la maji simu itaendelea kufanya kama kawaida ikiwa ndani ya maji

Ila kwa maji ya kina cha mita moja simu inavumilia kwa muda wa nusu saa

Ubora wa kamera

Ukilinganisha kamera ya iphone 12 pro max na ya Samsung Galaxy A52, utaona samsung ina ubora wa kawaida sana

Japo ukiitizama hii picha ambayo imepigwa na A52 inaonyesha inatoa picha zenye ubora mkubwa

Kama unalinganisha hii simu na simu ya Tecno Phantom X, utaona samsung pia ina kamera nzuri

Katika kamera nne kuna kamera moja tu yenye autofocus aina ya PDAF na OIS

samsung a52 bodi kwenye kamera

Kwa maana kamera zingine hazitotoa picha nzuri ukiwa unapiga picha kitu kinachokimbia kwa kasi

Simu inaweza kurekodi video za 4K kwa kiasi cha fremu 30

Na video za full hd zinaweza kurekodiwa mpaka kwa fremu 60 kwa sekunde

Kwa kuwa kamera kuu ina OIS, basi video itatokea kwa kutulia wakati wa kurekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Samsung Galaxy A52 ni simu ya android 11

Na inaweza kupokea toleo jipya la android 12

Mbali na android simu inakuja na mfumo wa One UI 4.1

One UI 4.1 ina maboresho mengi ikiwemo Camera, Audio Connection na upande wa Gallery

samsung galaxy software oneui camera

Kamera imeongezewa uwezo wa kuzoom wakati wa kuchukua picha na kurekodi video

Kwani app ya kamera inaweza kuzoom mara 20 ukiwa unarekodi video

Na inaweza kuzoom mara 10 kama unapiga picha

Hivyo basi inakurahisishia kurekodi kitu ambacho kipo mbali na kamera ya simu

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A52

Udhaifu mkubwa unaweza ukawa upo kwenye kamera

Hasa kamera za ultrawide na macro hazijawekewa aina yoyote autofocus

Na pia hazina OIS kwa ajili ya kurekodi video kwa utulivu

Pia display ya galaxy haijaboreshwa zaidi

Kwani haina HDR10 wala dolby vision ambazo huboresha muonekano wa vitu

Neno la Mwisho

Kama unahitaji simu ya daraja la kati ambayo ina ubora kwenye maeneo mengi basi Samsung Galaxy A52 lazima iwepo kwenye listi

Hivyo bei yake inakupasa uwe na bajeti ya kueleweka kidogo

Na hata kama utapata iliyotumika, umakini ni muhimu kutokana na baadhi kuwa mbovu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram