SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 12 Pro Max Tanzania na Sifa Zake (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

August 6, 2022

Simu ya iPhone 12 Pro Max ni simu ya daraja la juu iliyotoka mwaka 2020

Japo ina miaka miwili ila bado inapokea matoleo mapya ya iOS

Kitu kinachoifanya simu kuendelea kuwa na thamani

iphone 12 pro max raw nuonekano

Kwani bei ya iphone 12 pro max kwa Tanzania inakaribia shilingi milioni mbili

Na hapo nyingi ni used sio mpya

Sifa za iPhone 12 pro max bado ni kubwa mno ukilinganisha na simu nyingi mpya za mwaka 2022 kama Tecno Camon 19 Pro 5G

Bei ya iPhone 12 Pro Max ya GB 128

Kwa Tanzania, iPhone 12 Pro Max yenye ukubwa wa GB 128 inapatikana kwa shilingi milioni 1.9

Hii ni simu janja ambayo imekamilika kila idara na inachuana na simu kama Xiaomi 12 Pro

iphone 12 pro max summary

Bei yake bado ni kubwa hata kwenye mtandao wa ebay na amazon

Sababu kubwa sifa zake nyingi bado zinaendana na wakati uliopo

Sifa za iPhone 12 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A14 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.1 GHz Firestorm
  • Core Za kawaida(4) –  4×1.8 GHz Icestorm
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED,
Softawre
  • iOS 14.1
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB na RAM ,6GB
Kamera Kamera nne

  1. 12MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(Telephoto)
  4. TOF 3D LiDAR scanner(depth)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 3687mAh-Li-Ion
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 1,900,000/=

Ni upi ubora wa simu ya iPhone 12 Pro Max

Ni simu inayokubali mtandao wenye kasi kubwa kwa maana 5G

Ni moja ya simu yenye kamera inayotoa picha nzuri katika kamera zake zote tatu

Ina uwezo wa kupokea toleo jipya la mfumo endeshi wa iOS

Ina memori zinazosafirisha data kwa kasi

Utendaji wa simu ni mkubwa unaozipita processor nyingi mpya za simu

iPhone 12 Pro Max ina uwezo wa kuzuia maji kupenya

Ina bodi ngumu kuvunjika na kuchunika pia

Uwezo wa Network

iPhone 12 Pro Max ni simu ya 5G inayokubali aina zote za 5G ikiwemo ile yenye kasi kubwa zaidi

Kwa maana ina 5G yenye kasi inayozidi 1000Mbps

Kwa Marekani, kasi 5G kwa mtandao wa T-Mobile inafika 1058Mbps verizon inazidi 2000Mbps

iphone 12 pro max network verizon usa

Yaani kama unadownload faili la 1200MB, simu itamaliza kudownload baada ya sekunde 9 tu

Ni kama ndoto ila ndio uhalisia ambao kwa Tanzania bado haupo

Na 4G yake ina masafa zaidi ya 30 hivyo mitandao ya 4G karibu yote duniani itafanya kazi kwenye hii simu

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 18 yenye kasi inayofikia 1200Mbps

Ila Tanzania hakuna mtandao unaoweza kukupa kasi hii

Ubora wa kioo cha iPhone 12 Pro Max

Katika kuonyesha vitu kiustadi iPhone huwa ina vioo vinavyojitahidi kuonyesha vitu kwa uharisia

Inatokana na simu kuwa na kioo aina ya OLED

Hivi vioo huwa vinaonyesha rangi nyingi na kwa usahihi

Ubora wake wa kioo unachagizwa na uwepo wa resolution kubwa ya 1284 x 2778 pixels

iphone 12 pro max display

Na pia kioo kuwa na HDR10, dolby vision na uangavu unaifikia nits 800 hadi 1200

HDR10 na Dolby Vision hizi ni teknolojia za vioo ambavyo hujaribu kurekebisha muonekano wa vitu uendane kama jicho la binadamu linavyoona kwenye mazingira halisi

Basi kioo chenye hivyo hdr au dolby vision huonyesha picha kwa uzuri zaidi kuliko simu zisikuwa nazo

Nguvu ya processor Apple A14 Bionic

Katika orodha tano ya processor za simu zenye nguvu Apple A14 Bionic imo

iPhone 12 Pro Max inatumia chip ya Apple A14 Bionic ambayo ina core sita

Core zenye nguvu zipo mbili hufahamika kwa jina la Firestorm

Na core zinatumika kwenye kazi ndogo ndogo huitwa Icestorm

iphone 12 pro max PROCESSOR

Utendaji wa apple a14 bionic unaweza kusukuma gemu ya PUGB Mobile 2018 kwenye resolution kubwa kwa kasi ya fremu 58 fps

Video zenye “graphics effects” kubwa kama Manhattan Offscreen zinacheza kwa fremu 180fps

Hii ni tofauti na MediaTek Helio G70 ambayo inacheza video hiyo hiyo kwa fremu 27fps

Helio G70 imetumika kwenye simu ya infinix hot 10t

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya apple iphone 12 pro max inapeleka umeme wa wastani wa wati 15 tu

Betri yake ina ukubwa wa 3687mAh Li-Ion hivyo betri inaweza isichukuwe muda mwingi kujaa

Ukaaji wa chaji wa iphone macho matatu ya 2020 ni wa kiwango kikubwa pamoja na kutokuwa na betri ya 5000mAh

Kwani ukiwa unaperuzi intaneti masaa mengi mfululizo simu inachukua masaa 14 chaji kuisha

Hiki ni kiwango cha simu ya Redmi Note 10 yenye betri ya 5000mAh

Ukubwa na aina ya memori

Apple iPhone 12 Pro Max ina matoleo ya aina tatu upande wa memori

Kuna ya GB 128, 256 na 512

Mfumo wa memori unaotumiwa na simu za apple ni NVMe

NVMe ina kasi ya kusafirisha data inayofikia 3GBps, ni mara tano ya mfumo wa eMMC 5.1

Simu ikiwa inatumia intaneti yenye kasi inahitaji kasi kubwa ya memori kwenye kuandika na kusoma data za faili

Vinginevyo uwezo wa simu utakuwa ni mdogo na faida ya intaneti yenye kasi hutoiona

Uimara wa bodi ya iPhone 12 Pro Max

Bodi ya iPhone 12 Pro Max haipitishi maji kama simu ikidumbukia kwenye kina cha maji ya mita sita kwa muda wa nusu saa

Hii inatokana na simu kuwa na viwango vya IP68

iphone 12 pro max raw used maji bodi

Upande wa nyuma simu imewekewa kioo cha gorilla glasi japo haijainishwa ni toleo lipi

Ila vioo vya gorilla huwa ni vigumu kuchunika na kupasuka

Upande wa pembeni imewekewa chuma wenyewe wanaibrandi kama Stainless Steel Frame

iphone 12 pro max raw used drop

Hii simu haina sehemu ya memori kadi wala sehemu earphone

Kiuhalisia simu ni ngumu na imara

Ubora wa kamera

Linapokuja swala la kamera simu za apple huwa zina ubora mzuri wa picha

Kwenye picha za mchana, iphone 12 pro max inatoa picha safi na kwa uwiano wa rangi ulio sahihi

Hata ukizoom kitu kilicho mbali bado vitu vinaonekana kwa kutambulika na kama inavyotakiwa

Pitia na itazame: picha zilizopigwa na simu ya iPhone 12 Pro Max

iphone 12 pro max kamera modified

Ubora wa picha unachangiwa na simu kuwa na ulengaji wa dual pixel pdaf kwenye kamera ya wide

Na kamera za ultrawide na telephoto zina OIS, ambayo hufanya video kurekodiwa kwa kutulia wakati unarekodi huku unatembea

Kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4k kwa fremu za 30fps na 60fps

iPhone 12 Pro Max inarekodi video na zinatokea vizuri kwa sababu ya kuwa na Dolby Vision HDR

Pitia Hapa kuelewa: Maana ya HDR na Umuhimu wake kwenye simu

Ubora wa Software

Kama utaipata simu ikiwa mpya basi kwa mara ya kwanza utakutana na mfumo endeshi wa iOS 14

iOS 14 ulikuwa ni mfumo wa mwanzo wa apple uliokuwa na kitu kinachofahamika kama app library

Apple library ni mtindo ambao unazikusanya app zinazofanana katika kundi moja

iphone 12 pro max app library

Kwa mfano app ambazo umeziongeza kwenye simu kwa nyakati zinazoendana zinaenda kwenye folder moja

App za mitandao ya kijamii na zenyewe mfumo unaziweka sehemu moja

Inasaidia kuweza kuipata app unayoitafuta kwa haraka

Yapi Madhaifu ya iPhone 12 Pro Max

Apple wamepuuzia kuweka radio kwenye simu zao ikiwemo hii

Kama utahitaji kusikilizia kipindi cha redio itakulazimu utafute app kama tunein

Kitu kinachoongeza gharama za kununua data

Pia apple inaongeza gharama nyingine ya kununua earphone za bluetooth

Kwa sababu iphone 12 pro max haina sehemu ya kuchomeka waya wa earphone

Chaji ya apple ni ndogo inayojaza simu kwa dakika 92

Wakati simu kama Mi 10 Ultra inajaza betri kwa dakika 27 tu

Kibaya kingine ni simu kutokuwa na sehemu ya memori kadi

Japokuwa simu zina ujazo mkubwa, lakini vitu vinaweza kujaa hasa kwa ile yenye GB 128

Neno la Mwisho

Kama unahitaji simu iliyo kamili kwenye idara nyingi basi bei ya iphone 12 pro max haiwezi kukutisha

Kwa sababu utakuwa unamiliki simu inayoweza dumu muda mrefu na yenye kupokea maboresho mengi ya iOS

Kwani sasa iPhone 12 Pro Max inaweza kupokea toleo la iOS 16

Maoni 4 kuhusu “Bei ya iPhone 12 Pro Max Tanzania na Sifa Zake (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram