SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Samsung Galaxy A13 na Sifa Muhimu (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

July 3, 2022

Mnamo mwezi machi 2022 Samsung waliingiza sokoni simu ya Samsung Galaxy A13

Ni Samsung ya daraja la kati hivyo gharama yake imechangamka kidogo

samsung galaxy a13 showcase

Kwani bei ya Samsung Galaxy A13 kwa Tanzania inazidi laki tatu na nusu

Lakini kiubora Galaxy A13 inaigeuza simu kuwa ya gharama hasa kama utafananisha na simu za android nyingine.

Bei ya Samsung Galaxy A13 ya GB 64 Tanzania

Galaxy A13 yenye ujazo wa GB 64 na RAM GB 4 inafika shilingi 450,000/=

Hii ni bei kwa baadhi ya maduka Dar Es Salaam kariakoo simu ikiwa mpya

samsung galaxy a13 summary

Ila sasa ukitazama uwezo wa simu kiutendaji utagundua bei yake haistahili kuzidi laki tatu

Kwa sababu sifa zake zinaendana sana na Redmi 9a inayopatikana kwa bei ya chini ya laki tatu.

Ziangazie sifa zake ikupe picha kwa nini simu ina gharama kubwa.

Sifa za Samsung Galaxy A13

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 850
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52
Display(Kioo) PLS LCD
Softawre
  • Android 12
  • One UI 4.1
Memori eMMC 5.1, 128GB,64GB,32GB na RAM 3GB,6GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 450,000/=

Ni upi ubora wa simu ya Samsung Galaxy A13?

Galaxy 13 inakuja na matoleo mengi upande wa memori

Matoleo mengine yanaleta memori inayoweza kuhifadhi mafaili mengi

Ina betri kubwa inayodumu na chaji muda mrefu

Ni simu ambayo imewekewa kioo kigumu kwenye screen

Hivyo kuchunika na kupasuka si rahisi

Ni simu iliyo na sehemu ya memori kadi tofauti na simu nyingi za google pixel

Lakini kama sifa za simu zinavyoonyesha bei yake ina mkanganyiko ukitazama uwezo wa simu kwenye nyanja zote

Uwezo wa Network

Simu ya Samsung A13 ni simu ya 4G aina ya LTE Cat 7

Spidi yake ya juu kabisa ya kudownload inafika 300Mbps

Kama ukiwa marekani au china spidi hii unaifikia kiurahisi tu

samsung galaxy a13 network

Ila Tanzania kasi ya intaneti bado ni ndogo japokuwa kuna 4G

Na ina masafa yote yanayopatikana nchini

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A13

Kioo cha samsung galaxy a13 ni cha PLS LCD

Ni aina nyingine ya LCD ambayo haina tofauti kubwa na IPS LCD

Koo chake kinatumia resolution ya 1080 x 2408 pixels

samsung galaxy a13 kioo

Walau ufanisi wa kuonyesha vitu unakuwa mzuri

Japo si sawa na simu zenye vioo vya OLED au AMOLED

Kibaya Galaxy A13 haina hdr10 na refresh rate yake ni ya kawaida

Nguvu ya processor Exynos 850

Samsung A13 inatumia chip ya Exynos 850 katika kufanya kazi zake

Ukichaguwa simu yenye processor dhaifu jua kuwa umechagua simu mbaya

Nguvu ya processor huwa inajulisha ubora wa simu na bei yake

Exynos 850 ina utendaji mdogo

samsung galaxy a13 processor exynos

Hiyo inatokana na chip kuwa na core nane zote zikiwa zinatumia muundo wa Cortex A55

Cortex A55 inafanya kazi(decode) chache kwa mzunguko mmoja ukilinganisha na muundo wa Cortex A76

Hii inafanya processor kutumia umeme mdogo kutokana na kufanya kazi chache

Ndio maana Exynos 850 kwenye app ya Geekbench ina alama 160

Sio simu nzuri kucheza magemu

Uwezo wa betri na chaji

Hii simu ina betri kubwa yenye uwezo wa kukaa na chaji muda mrefu

Ukaaji wa chaji unachangiwa sana na processor yake kutumia umeme mdogo

Hivyo haitoshangaza betri yake ya 5000mAh kukaa na chaji masaa zaidi ya 15 simu ikiwa kwenye intaneti muda wote

Ila simu inaweza chukua masaa mengi kujaa

Chaji ni ya wati 15

Kiasi hiki cha umeme kinaweza kikajaza betri ya 5000mAh kwa masaa yanayozidi matatu

Aina ya chaji ni ile yenye pini nene inayofahamika kama USB Type-C 2.0

Ukubwa na aina ya memori

Simu ina matoleo matano yanayoanzia na ukubwa wa GB 32 na RAM GB 3 mpaka GB 128 kwa RAM a GB 6

Japokuwa simu inatoa storage kubwa lakini aina ya memori inazotumia zinasafirisha data taratibu

Galaxy A13 inatumia memori ya eMMC 5.1 ambayo spidi yake ya juu ni 250MBps

Wakati memori za UFS 2.1 spidi yake inatembea mpaka 1200MBps

Hii ina maana gani?

Kama unakopi faili la ukubwa 2500MB, Samsung hii itakopi kwa sekunde 10

Wakati simu yenye UFS 2.1 itakopi kwa sekunde mbili (2)

Memori ikiwa na kasi kubwa hufanya simu kuwaka ama kuzimika kwa haraka

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A13

Bodi ya samsung galaxy a13 imetengenezwa kwa plastiki upande wa nyuma

Na imewekewa kioo cha Gorilla Glass 5 kwenye screen

Hiki huwa ni kioo kinachostahamili kuvunjiaka kama simu ikianguka kwa kimo cha mita 1.2

samsung galaxy a13 bodi

Hii simu ina sehemu ya kuweka memori kadi

Na ni simu ya laini mbili

Ubora wa kamera

Simu ina kamera nne hivyo unaweza kuita samsung macho manne

samsung galaxy a13 kamera

Ila ni kamera moja tu inayokidhi uwezo wa kutoa picha nzuri na kurekodi video za 4K

Kamera hiyo ni aina ya Wide yenye resolution ya 50MP

Na yenye kutumia ulengaji wa PDAF

Kamera zingine ni depth ambazo hutumika kuweka ukungu(bokeh effect) upande wa nyuma wa kitu kinachpigwa picha

amsung galaxy a13 bokeh effect

Kamera ya ultrawide inaweza kupiga picha eneo pana kwa nyuzi 123

Pamoja na kuwa na kamera ya 50MP, Galaxy A13 haiwezi kurekodi video za 4K

Kwani processor yake ina nguvu ndogo kuweza kufanya kazi hiyo

Ubora wa Software

Galaxy A13 inakuja na Android 12 pamoja na mfumo wa One UI 4.1

One UI 4.1 ina kitu kinaitwa Ram plus

Ram plus inakupa uwezo wa kuongeza ukubwa wa RAM

Kitu kinachosaidia simu kuweza kufungua app nyingi kwa wakati mmoja na kwa urahisi

Ram plus inachukua sehemu ya memori ya simu

Ila inaweza isiwe na maana sana ukizingatia simu ina memori za eMMC 5.1

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A13

Bei ya Samsung Galaxy A13 ni kubwa kutokana na utendaji mdogo wa chip

Simu haijatumia kioo cha amoled

Kwa sababu simu ya redmi note 10 inayopatikana kwa bei ya chini ya laki nne na nusu ina kioo cha AMOLED

Simu haina kamera nzuri japokuwa ina jumla ya kamera nne

Inatumia memori zenye uwezo mdogo wa kusafirisha data

Chaji yake haipeleki umeme mwingi

Simu za laki nne nyingi huja na chaji ya umeme wa wati 33

Haina redio

Hitimisho

Kuna watumiaji wa simu huwa wanapenda brand maarufu bila kujari sifa za simu

Hivyo kwa mpenzi wa samsung hii ni simu itakayomfaa.

Lakini kama utendaji wa simu ni kipaumbele, basi haustahili kutoa laki nne kwenye hii simu

Yapo matoleo megi yaliyofafanuliwa kwenye tovuti hii.

Kiuhalisia Samsung Galaxy A13 inakaa kwa Redmi 10C

Wakati Redmi 10C inapatikana kwa bei ya chini ya laki tatu na nusu aliexpress

Pitia hapa ujifunze: Jinsi ya kununua simu mtandaoni kupitia aliexpress

 

Maoni 14 kuhusu “Bei ya Simu ya Samsung Galaxy A13 na Sifa Muhimu (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram