SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Vivo V23 5G na Sifa Zake (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 4, 2022

Simu ya vivo v23 5g ni android ya 5G ambayo imetoka mnamo januari ya 2022.

Kiuwezo vivo v23 5g inazidiwa na vivo v23 pro

Ila bei ya vivo v23 5g ni nafuu zaidi kwani inauzwa chini ya milioni moja

vivo v23 5g

Ukizisoma sifa zake utajua kwa nini simu inastahili kuuzwa bei hiyo

Hivyo kwenye hii post utafahamu bei ya simu kulingana na ukubwa wake na sifa zinazoifanya vivo kuwa na bei kubwa

Bei ya Vivo V23 5G Tanzania

Bei ya vivo v23 5G yenye ukubwa wa memori ya 128GB ni shilingi 914,184.29/= amazon

Hivyo kwa maduka ya Tanzania bei inaweza kuwa kubwa

Hii simu ya daraja la kati ina bei kubwa kiasi.

Bei inaendana na sifa zake ila kuna simu utazifahamu amabazo ubora wake ni mkubwa kuliko V23 lakini bei ni ndogo

Fuatilia sifa zake halafu zilinganishe na simu zitakazotajwa humu.

Sifa za simu ya Vivo V23 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 920
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.5 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G68 MC4
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • Funtouch 12
Memori UFS 2.1, 256GB,128GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera tatu (vivo macho matatu)

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.44inchi
Chaji na Betri
  • 4200mAh-Li-Po
  • Chaji-44W
Bei ya simu(TSH) 915,000/=

Upi ubora wa vivo v23 5g

Ubora wa vivo v23 5g upo kwenye uwezo wake wa utendaji

Simu ina nguvu na inakubali mtandao wa 5G

Ina kioo chenye rangi za vitu kwa ustadi

vivo v23 5g summary

Na ni kioo kwa kizuri kucheza gemu

Ina chaji inayopitisha umeme unaojaza betri kwa dakika chache

Na hata ukaaji wake wa chaji ni wa uda mrefu

Uwezo wa Network

Vivo v23 5g ni simu ya 5G inayosapoti mtandao wa 4G aina ya LTE Cat 18

Aina ya 5G ni ile ya masafa ya chini na ya kati kwani haina uwezo wa kutumia 5G yenye kasi sana ya mmWave

Pitia hii linki uitazame, simu ya samsung galaxy s22 ultra 5g yenye kasi kubwa ya 5G

vivo v23 5g network

LTE Cat 18 ina spidi ya juu ya kudownload inayofikia 1200Mbps

Kwa hiyo mafaili makubwa yanaweza kumalizika ndani ya sekunde chache

Lakini si kwa Tanzania hakuna mtandao wa simu wenye spidi hii

Simu ina masafa yote ya 4G yanayotumiwa na mitandao ya simu ya Tanzania

Ubora wa kioo cha vivo v23 5g

Kioo cha vivo v23 ni cha aina ya amoled

Vioo amoled huwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Hivyo ubora wa vitu vinavyoonekana kwenye screen ya vivo haupungui

Refresh rate ya 90Hz inaiongezea ubora kioo chake

Huku HDR10+ inaifanya kioo cha vivo kuonesha vitu kwa jinsi vinavyoonekana kwenye mazingira halisi

Lakini pia itakusaidia kuangalia video zenye ubora wa HDR za youtube

Nguvu ya processor Dimensity 920

Vivo v23 5g inatumia processor ya Mediatek dimensity 920 katika kufanya kazi zake

Dimensity 920 ni chip ya simu ya toleo la kati yenye idadi ya core nane

Ni processor yenye nguvu ya kusukuma gemu ya graphic kubwa ya PUBG Mobile kwa ubora wa Ultra HD na kwa spidi ya 64fps

Hii chip inaifanya simu isipate moto sana inapofanya kazi kubwa kwa sababu ina nguvu kubwa

vivo v23 5g processor

App ya kupima nguvu ya processor inaipa dimensity 920 alama 783

Nguvu kubwa ya chip inasababishwa na muundo wa Cortex A78 kwenye core mbili kubwa

Kwani inaweza kufanya mizunguko bilioni mbili na laki tano kwa sekunde

Na kila mzunguko mmoja unafanya idadi ya kazi zipatazo nne

Wakati core ndogo aina ya Cortex A55 inahakakikisha matumizi madogo ya umeme

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya vivo v23 5g inapeleka umeme wa wati 44

Huu ni umeme unaojaza betri lake la 4200mAh kwa lisaa tu

Betri lake linakaa na chaji muda mrefu

Kwenye data za gsmarena, vivo v23 5g inakaa na chaji masaa 103

Sio masaa mengi sana ukilinganisha na simu ya tecno camon 18 premierĀ 

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili tu ya vivo hii

Toleo la kwanza lina ukubwa wa 128GB na RAM ya 8GB

Na toleo la pili linaukubwa wa 256GB na RAM ya 12GB

Aina za memori za vivo ni za UFS

Hivyo ufungukaji wa app ni wa haraka na kukwama ni nadra

Uimara wa bodi ya vivo v23 5g

Bodi ya hii simu ni ngumu kutokana na kuwekewa glasi upande wa mbele na nyuma

Lakini kwa bahati mbaya simu haiwezi kuzuia maji kupenya

vivo v23 5g bodi

Hivyo mtumiaji anapaswa kuwa makini

Lakini pia, uwepo wa kioo upande wa nyuma unaiepusha bodi ya simu kuchunika rangi

Hivyo umuhimu wa kava sio mkubwa

Ubora wa kamera

Vivo v23 5g ni vivo macho matatu

Kamera zake zinapiga vizuri hasa nyakati za mchana

Ila usiku kuna kiwango kidogo sana cha noise kinachoweza kuonekana

vivo v23 5g camera

Lakini kiujumla kamera inatoa picha nzuri kwa viwango vya kawaida

Jifunze, jinsi ya kujua kamera nzuri ya simu

Simu inaweza kurekodi video za 4k na full hd kwa spidi ya 30fps

Kamera yake ya ultrawide inaweza kurekodi eneo pana sana kwa nyuzi 120

Ubora wa Software

Simu inakuja na mfumo endeshi wa Android 12 na Funtouch 12

Funtouch 12 ina mpangilio mzuri wa app pale unapotumia app nyingi (Mult Task)

Kwa maana inazipanga app kwa muundo wa grid

Muundo wa grid unatengeneza urahisi wa mtumiaji kuhama kutoka app moja na nyingine

Kwa upande wa android 12 inakupa uwezo wa mfumo wote kukopi rangi ya wallpaper

Tazama, vitu vipya vya android 12 ambavyo havikuwahi kuwepo

Yapi Madhaifu ya vivo v23 5g

Simu haina uwezo wa kuzuia maji kwani haina viwango vya ip67

Wakati simu kama ya samsung galaxy a53 5g inayoendana bei inayo

Lakini pia v23 haijatumia kioo cha gorilla

Na pia mfumo wake wa kamera si mzuri sana

Kwani hakuna kamera yoyote inayotumia mfumo wa ulengaji wa dual pixel pdaf

Neno la Mwisho

Bei ya vivo v23 5g inaweza kununua simu ya redmi note 11 pro plus 5g

Redmi imetumia chip moja na vivo v23

Lakini ina vitu vya ziada vingi ambavyo havipo kwenye hii vivo

Kwa mfano note 11 ina chaji inayopeleka umeme wa wati 120

Na hapo bei ya redmi ni chini ya laki nane kwa masoko ya aliexpress

Hapa kuna ufafanuzi wa kiundani, ubora wa simu ya redmi note 11 pro plus 5g

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu 14 mpya za Vivo za ubora mkubwa na bei zake (2024)

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka mwaka huu 2024 Vivo imeachia matoleo mengi ya simu Katika matoleo hayo yapo ya bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa Kwa maana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram