SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Samsung Galaxy S22 na Sifa Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 4, 2022

Simu ya samsung galaxy s22 ni simu mpya ya daraja la juu ambayo imetoka mwaka 2022

Kitu ambacho kinafanya bei ya samsung galaxy s22 kuzidi milioni hapa Tanzania na duniani kiujumla

Kikubwa utakachokijua kwenye hii post ambacho kinasababisha simu kuwa na bei kubwa ni ubora wake wa processor.

muonekano wa samsung galaxy s22

Si processor pekee bali ubora wa galaxy s22 upo kwenye sifa karibu zote.

Hivyo ukielewa sifa muhimu za galaxy s22 ndio utafahamu kiundani sababu ya bei yake kubwa.

Bei ya Samsung Galaxy S22 Tanzania

Bei halisi ya samsung galaxy s22 kwenye soko la dunia(amazon) ni shilingi 1,627,500.00/=

Lakini maduka mengi ya simu dar es salaam wanauiza samsung s22 kwa shilingi 2,200,000/=

Swali lakujiuliza,

Bei yake ya zaidi milioni inaendana na ubora wake?

Kwa kutazama sifa za galaxy s22 upande wa kioo, bodi, kamera, chipset, network na mengine bei yake inaakisi ubora

Fuatalia sifa na maelezo yake kwenye hii post uweze kujua ubora wa galaxy s22 upo wapi hasa

Sifa za samasunga galaxy s22

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 2200
  • Core Kubwa Zaidi(1) – 1×3.00 GHz Cortex-X2
  • Core Yenya Nguvu(3)-3×2.40 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.70 GHz Cortex-A510
  • GPU-Xclipse 920
Display(Kioo) Dynamic AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • One UI 4.1
Memori UFS 3.1, 256GB, 128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu (samsung macho matatu)

  1. 50MP, Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 10MP(Telephoto) PDAF
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 3700mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 2,200,000/=

Upi ubora wa simu aina ya Samsung Galaxy S22

Simu ya samsung galaxy s22 ina ubora mkubwa hasa kwenye utendaji wa processor

Simu ina kioo kinachoonyesha vitu kwa uhalisia kwa kiasi kikubwa

taarifa fupi kuhusu samsung galaxy s22

Chaji yake ni fast chaji inayojaza betri kwa dakika chache

Ni samsung macho matatu inayotoa picha nzuri hata kwenye mwanga hafifu

Ni simu yenye network ya 5G

Mfumo wake wa memori una kasi kubwa ya kusafirisha data nyingi kwa wakati mmoja

Ina GPU nzuri inayoweza kucheza gemu kwa ubora wa juu kwa urahisi

Uwezo wa Network

Samsung S22 ni simu ya 5G na inasapoti mtandao wa 4G pia

Aina ya LTE inayotumia ni LTE Cat 20

Spidi ya juu kabisa ya kudownload ya Cat 20 ni 3000Mbps

amsung galaxy s22 network

Ni spidi inayokaribia 5G

Network ya 4G ya galaxy s22 ina masafa yapatayo 22 yakiwemo yanayotumiwa na mitandao ya simu nchini Tanzania

5G yake pia ina masafa mengi

Kufahamu masafa ya mitandao ya simu ya 4G pitia, jinsi ya kujua ubora wa simu yoyote

Ubora wa kioo cha samsung galaxy s22

Samsung galaxy s22 inatumia kioo aina ya dynamic amoled

Dynamic amoled ni tofauti na super amoled.

Dynamic ina ongezeko la rangi na uangavu wake ni mkubwa zaidi

Hivyo mwanga wa kioo ukiwa mdogo screen inaonyesha vitu ukilinganisha na super amoled

Tazama video hii inayoonyesha utofauti wa super amoled na dynamic amoled

Ubora wa kioo cha samsung unachagizwa na uwepo wa HDR10+ na refresh rate kubwa ya 120Hz

HDR10+ inarekebisha muonekano wa picha au video kuendana na jinsi kitu kinavyoonekana kwenye mazingira yake halisi

Refresh ya 120Hz inaifanya simu kuwa nyepesi wakati wa kucheza gemu za simu

Na kikubwa, uangavu wa kioo unafika nits 1300

Hivyo hautopata tabu pindi simu inapotumika kwenye jua kali

Nguvu ya processor Exynos 2200

Kuna matoleo mawili ya samsung mpya ya galaxy s22 upande wa processor.

Samsung za marekani zinatunia chip ya snapdragon 8 gen 1

Wakati za nchi zingine zinatumia Exynos 2200

Makala hii inaangazia uwezo wa chip ya Exynos 2200

samsung galaxy s22 processor exynoss 2200

Exynos 2200 ni chip yenye nguvu ambayo inashika nafasi ya tatu kwa sasa

Kwenye geekbench ina alama zaidi ya 1100

Ni alama nyingi ukifananisha na chip iliyotumika kwenye simu ya Tecno Camon 18 Premier

Nguvu kubwa ya exynoss 2200 inachangiwa na muundo mpya wa core kubwa na core ndogo

Ni miundo inayoipa processor uwezo wa juu

Uwezo wa core kubwa

Exynos 2200 ina jumla ya core nne zenye nguvu ambazo zimegawanyika mara mbili.

Kuna core moja yenye nguvu sana ambayo inatumia muudo wa Cortex X2

Spidi ya core hii inafika 3.00 GHz kwa maana chip inaweza kufanya maelekezo kwa mizunguko bilioni tatu kwa sekunde

Kila mzunguko mmoja unaweza kufanya kazi 10 kwa wakati mmoja

Hii core ina ulaji mkubwa wa chaji lakini ufanisi ni mkubwa

Core tatu kubwa zingine zina spidi ya 2.4 GHz na zinatumia pia Cortex X2

Uwezo wa core ndogo

Chip ina jumla ya core zenye nguvu ndogo zipatazo nne

Core ndogo zinatumia muundo wa Cortex A710

Hizi core huwa na mizunguko michache ipatayo bilioni moja na laki saba kwa sekunde

Cortex A710 inatumia umeme mdogo na nguvu yake ni kubwa kuliko Cortex A55 ambayo imetumika kwenye simu nyingi za android ikiwemo Redmi note 11 pro plus 5g

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya samsung galaxy s22 ina ukubwa wa 3700 mAh

Ukubwa wa betri ni wa wastani unaoifanya simu kukaa na chaji masaa 87 kama ikiwa haitumiki mara kwa mara

GSMArena wanadai galaxy s22 inakaa na chaji masaa 11 simu ikiwa kwenye intaneti muda wote

Chaji inajaza betri kwa 100% kwa dakika zipatazo 63

Hivyo simu inachukuwa muda mchache sana kujaa

Spidi kubwa ya kuchaji inasababishwa na umeme wa wati 25 ambao chaji inaweza kupeleka kwenye betri

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo ya aina mbili ya galaxy s22 upande wa memori

Kuna galaxy ya ukubwa wa 128GB na nyingine ina ukubwa wa 256GB

Zote zina RAM yenye ukubwa wa RAM 8GB

Aina ya memori ambazo samsung imetumia ni UFS 3.1

UFS 3.1 huwa ina kasi kubwa sana kusafirisha data

Hivyo inafanya simu kuwaka na kufungua app kwa haraka

Na memori yenye kasi inaongeza utendaji mkubwa wa simu

Uimara wa bodi ya samsung galaxy s22

Samsung galaxy s22 ina bodi ngumu kuvunjika

Uimara wake unasababishwa na simu kutumia vioo vya gorilla glass victus+ upande wa nyuma na kwenye display

Na upande wa pembeni simu imewekewa fremu za aluminiamu

samsung galaxy s22 bodi

Vioo vya gorilla glass victus+ vinaipa simu uwezo kutokupasuka kama ikianguka kwa kimo cha mita mbili toka juu

Na pia ni vioo ambavyo ni vigumu kuchunika

Kiufupi tu, hutohitaji kuweka kava wala screen protector kutokana na ugumu wa kioo

Ubora wa kamera

Samsung galaxy s22 ina kamera tatu ambapo kamera kubwa ina resolution ya 50MP

Kwa picha nyingi ambazo nimeziona, kamera ya samsung inatoa picha nzuri iwe usiku ama iwe mchana

Hii inasababishwa na simu kutumia autofocus nzuri aina ya dual pixel pdaf

samsung galaxy s22 camera

Nyakati za mchana kamera ina balansi rangi vizuri na kwa usahihi hivyo tone ni ya kuridhisha

Nyakati za usiku kuna noise ya kiasi kidogo sana

Zitazame picha zilizopigwa na galaxy s22 hapa, ubora wa picha za kamera ya galaxy s22

Pia jifunze; jinsi ya kujua simu yenye camera nzuri

Ubora wa Software

Galaxy S22 inakuja na mfumo endeshi wa android 12

Android 12 ina ongezeko wa vitu kama uwezo kuonyesha app zinazotumia mic na kamera

Hivyo inakupa fursa ya kufahamu app ambazo zinakutrack

Lakini pia android ina kitu kinaitwa Corol Extraction

Yaani muonekano wa rangi wa vitu vingine unakopi rangi ya wallpaper unayoitumia kwenye simu

Yapi Madhaifu ya samsung galaxy s22

Udhaifu mkubwa wa galaxy s22 ni uwezo wake wa kukaa na chaji masaa machache

Samsung s22 inazidiwa na simu ya iphone 13 pro max kwenye upande wa ukaaji na chaji

Hilo linachangiwa na simu kuwa na betri dogo sana

Neno la Mwisho

Matoleo mapya ya samsung galaxy s-series kwa mwaka 2022 ni matoleo yanayohusisha simu bora

Kwa mwenye bajeti kubwa na ya kutosheleza anaweza akamiliki hii simu na kufurahia ubora wake

Ila kama bajeti ni ndogo unaweza kutazama machaguo mengine kama realme, vivo,oppo na sony

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

samsung s24 plus thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy S24+ na Sifa Zake

Kisifa Samsung Galaxy S24 Plus ina sifa nyingi zinazoendana kwa kiasi kikubwa na Samsung Galaxy S24 Ultra Kwa maana Galaxy S24+ ubora wake unazipita simu nyingi na mkubwa, hivyo bei […]

samsung s24 ultra thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy S24 Ultra na Sifa zake

Hivi karibuni simu mpya ya Samsung Galaxy S23 Ultra imeingia sokoni huku bei yake ikiwa haitofautiani sana na Apple iPhone 15 Pro Max Kwenye soko la dunia bei ya samsung […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram