SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Tecno Camon 18 Premier na Sifa Zake Muhimu (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 1, 2022

Tecno Camon 18 Premier ni simu bora ya Tecno ambayo imetoka mwishoni mwa mwaka 2021

Ubora wake unaifanya bei ya Tecno Camon 18 Premier kuzidi shilingi laki saba kwa mikoa mingi Tanzania

tecno camon 18 premier

Ubora wa camon 18 premier uko wazi kwa kuzitazama sifa zake muhimu zipatazo nane

Kwenye hii post utajua bei yake, ubora wa kioo, chaji na nguvu kubwa ya utendaji ya hii tecno mpya

Bei ya Tecno Camon 18 Premier Tanzania

Kwa maduka ya simu ya kariakoo bei ya tecno camon 18 premier yenye ukubwa wa GB 256 na RAM ya 8GB ni shilingi 750,000/=

Ukiendelea kusoma makala utagundua kuwa camon 18 premier ina kasoro chache

Kwa hiyo haishangazi bei yake kuwa kubwa

Fuatilia sifa za simu hii kwenye kila nyanja uelewe ubora wa tecno hii ya 2021

Sifa za Tecno Camon 18 Premier

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G96
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.05 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 11
  • HIOS 8.0
Memori UFS ,256GB,RAM 8GB,
Kamera Kamera TATU

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 8MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4750mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 760,000/=

Upi ubora wa simu ya Tecno Camon 18 Premier

Ubora wa simu aina ya tecno camon 18 premier upo kwenye kamera, chaji na betri, kioo na ukubwa wa memori

Kioo cha simu ni chepesi hasa ukiwa unacheza magemu

Chaji yake inawahi kujaza betri kwa haraka ndani dakika chache

Tecno camon 18 premier summary

Kamera yake imewekewa mfumo wa kipekee wa kutuliza video wakati wa kurekodi

Network ya simu inaweza kudownload mafaili makubwa kwa spidi kubwa

Kuna vitu ambavyo tecno wameviweka vinavyoongeza uwezo mkubwa wa simu

Fuatilia maelezo yote uvifahamu hivyo vitu

Uwezo wa Network

Camon 18 premier ni simu yenye 4G aina ya LTE Cat 13

Cat 13 ina spidi ya kudownload inayoweza kuzidi 600Mbps

Kama simu inadownload faili la ukubwa wa 1.2GB basi simu itachukuwa sekunde kama 10 kudownload faili lote.

Tecno camon 18 premier network

Ila kwa bahati mbaya mitandao ya Tanzania haina spidi kubwa ya 4G

Kwa mfano halotel kwa maeneo mengi spidi yake ya juu ya kudownload ni 42Mbps

Premier inasapoti intaneti ya 4G ya mitandao yote nchini

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 18 Premier

Kioo cha tecno camon 18 premier ni kioo kinachoonyesha vitu kwa rangi halisi kwa kiasi kikubwa.

Hiyo inatokana na kuwa na kioo cha amoled

Uzuri wa kioo pia umeongezwa na kuwa refresh kubwa ya 120Hz

Simu ikiwa na refresh inayozidi 90Hz inakuwa nyepesi sana wakati wa kutachi(ku-scroll)

Na inafanya simu kucheza gemu kwa ustadi

Tecno hii ina resolution kubwa ambayo inaongeza ubora wa muonekano wa vitu.

Resolution yake ni 1080 x 2400 pixels

Kiujumla camon premier ina kioo kizuri

Nguvu ya processor MediaTek Helio G96

Simu ya tecno camon 18 premier inatumia chip ya mediatek helio g96 kufanya kazi zake

mediatek helio g96 ni processor ya daraja la kati ambayo utendaji wake ni mkubwa.

Ni processor inayoweza kucheza gemu la Call of Duty: Mobile kwa spidi ya 42fps

tecno camon 18 premier processor

Geekbench inaipa alama nyingi zipatazo 536 kwenye core moja.

Hivyo camon 18 premeier ina nguvu zaidi kuliko  camon 17 na 18

Kinachoipa helio g96 ni muundo wa kiuwezo wa core kubwa na core ndogo

Uwezo wa core kubwa

Helio G96 ina core kubwa zenye nguvu sana zipatazo mbili

Spidi ya kila inaweza kufika 2.05 GHz

Na zinatumia muundo wa Cortex A76

Cortex A76 inaweza kufanya kazi nne kwa mzunguko mmoja kwa kila sekunde

Wakati huo processor inafanya mizunguko bilioni 2.05 kwa sekunde

Kwa maana hiyo processor inaweza kupiga kazi kubwa kuliko Cortex A75 ambayo ipo kwenye Infinix Hot 11

Uwezo wa core ndogo

Processor inatumia core ndogo zipatazo sita zenye spidi ya 2.0 GHz

Zimeundwa kwa mtindo wa Cortex 55

Ni muundo ambao unatumia nguvu ndogo

Processor ya Helio G85 inatumia muundo huo ila utendaji wake sio mkubwa kama Helio G96

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya camon 18 premier ina ukubwa wa 4750 mAh aina ya Li-Po

Betri inajaa kwa haraka kwa sababu inatumia chaji inayopeleka umeme mwingi wa wati 33

Mara nyingi chaji ya 33W hujaza betri chini ya masaa mawili

Simu inakaa na chaji masaa yapatayo 112 kama ikiwa haitumiki mara nyingi

Ukubwa na aina ya memori

Kuna toleo la aina moja tu la tecno camon 18 premier kwenye memori

Memori yake ina ukubwa wa 256GB aina ya UFS 2.2

Memori yake inaiongezea simu uwezo wa utendaji

Kutokana na uwezo wake wa kusafirisha data kwa kasi kubwa

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 18 Premier

Hii ni moja ya simu ya tecno ambayo inewekewa glassi upande wa nyuma.

Tecno hawajaonesha kampuni iliyounda kioo chake.

Lakini kiujumla bodi ya kioo inaipa ulinzi wa ziada simu hasa kutoka kwenye michubuko

tecno camon 18 premier bodi ya simu

Na kioo pia kimewekewa glassi

Kama utakuwa huaimini simu sana unaweza kununua screen protector

Ubora wa kamera

Smartphone ya Tecno camon 18 premier ni tecno macho matatu

Kamera yake ya ultrawide imewekewa gimbal OIS

Hivyo kuna utulivu wa kurekodi video ukiwa unatembea

Simu inatumia teknolojia ya ulengaji ya pdaf ambayo sio bora sana kama dual pixel

tecno camon 18 premier camera

Kizuri cha tecno premier ni kutokutegemea digital zoom (zoom ya app) pekee bali ina kamera ya Telephoto

Telephoto ni kamera inayopiga picha kwa umbali mrefu bila kupoteza pixels.

Camon inaweza kuzoom mara tano kama unatumia telephoto

Simu inaweza kurekodi mpaka video za 4k

Ubora wa Software

Simu inakuja na mfumo endeshi wa android 11 na software ya HIOS 8.0

HIOS 8.0 ina mpangilio mzuri kwenye settings

ecno camon hios 8.1

Settings ni rahisi kufikika na ina icon zinazomuelewesha kwa uzuri mtumiaji wa simu

Yapi Madhaifu ya Tecno Camon 18 Premier

Simu haina viwango vya IP53 wala IP68

Hii inamaanisha haina uwezo wa kuzuia maji kupenya ndani ya simu

Tecno walipaswa kutumia processor yenye nguvu zaidi ya Helio G96

Kwa sababu utendaji wa G96 hauendani na ubora wa kiujumla wa simu

Neno la Mwisho

Kama unatafuta simu bora ya tecno kwa 2022 basi ni Tecno Camon 18 Premier.

Japokuwa utendaji wa chip unaweza kuifanya bei yake iwe kubwa lakini ni simu nzuri ya tecno ya kuwa nayo

Camon premier inaweza kushindana na matoleo mengi mapya ya daraja la kati kutoka vivo, redmi, oppo na samsung

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu ya Tecno Camon 18 Premier na Sifa Zake Muhimu (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram