SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Tecno Camon 17 na Sifa Zake Kiundani (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 30, 2022

Kama unataka Tecno macho matatu basi ni simu ya Tecno Camon 17 ya mwaka 2021

Uzuri ni kuwa bei ya Tecno Camon 17 kwa Tanzania haizidi shilingi laki nne kwa maeneo mengi.

Ila bei yake inaonekana kuwa juu kiasi linapokuja ubora na uwezo wa simu kiutendaji.

simu ya tecno camon 17 mbele na nyuma

Hivyo baada ya kufahamu bei yake itakulazimu kupitia sifa moja baada ya nyingine ya Camon 17

Muongozo uliopo hapa utakujulisha ubora na udhaifu wa Camon 17 baada ya kuona sifa zake zote

Bei ya Tecno Camon 17 Tanzania

Kwenye maduka ya simu kariakoo bei ya Tecno Camon 17 ya 128GB na Ram ya 4GB ni shilingi 400,000/=

Maduka mngine wanaiuza simu kwa bei ya shilingi 440,000/=

Hii ni bei inayovumilika japo kwa mtu anaependa simu yenye uwezo mkubwa ataona bei kuwa ni kubwa

Hivyo itamlazimu kuangalia machaguo mbadala utakayoyaona baadae kwenye makala hii.

Kwa kuzingatia sifa zake laki nne ni bei kubwa kidogo

Sifa za Tecno Camon 17

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G85
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) –  6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 11
  • HIOS 7.6
Memori 128GB na RAM 6GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
  3. QVGA
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 440,000/=

Upi ubora wa Tecno Camon 17

Ubora wa tecno camon 17 upo kwenye utendaji, kioo na memori kubwa

Pia uwezo wake wa kupokea toleo jipya la android 12.

tecno camon 17 summary

Ni nadra kukuta simu ya tecno ikipata android mpya

Kioo cha hii simu ni chepesi wakati wa kutachi

Na uwezo wake wa kukaa na chaji masaa mengi ni mkubwa.

Ufanisi wa sehemu zingine unatofautiana kiuwezo, fuatilia zaidi uwezo,ubora wa nyanja zote za hii simu

Uwezo wa Network

Simu ya Tecno Camon 17 ni simu ya 4G aina ya LTE Cat 7

LTE Cat 7 inaweza kudownload faili kwa spidi inayofikia 300Mbps

tecno camon 17 network

Ni spidi inayoweza kudownload faili kwa sekunde chache kama mtandao wa simu unatoa spidi hiyo

4G yake ina masafa yote yanayotumika na mitandao ya simu ya Tanzania

Ni simu ambayo haina 5G ila kwa Tanzania hakuna laini ya simu inayotumia 5G kwa sasa

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 17

Kioo cha tecno camon 17 ni cha ips lcd chenye refresh rate ya 90Hz

Refresh rate ya 90Hz inakifanya kiookuwa kilaini unapoperuzi vitu kama orodha ya meseji

Ila ubora wa kioo chake umepunguzwa na resolution ndogo ya 720 x 1600 pixels

Na pia ips lcd huonesha rangi chache tofauti na kioo cha samsung galaxy s9 aina ya amoled

Uangavu wake wa kioo una nits 450.

Huu uangavu unaweza usioneshe vitu vizuri simu ikiwa kwenye jua kali sana

Nguvu ya processor MediaTek Helio G85

Tecno camon 17 inatumia chipset ya Helio G85 katika kufanya kazi zake.

Helio G85 inafanana na processor ya Helio G75 ambayo imetumika kwenye Infinix Hot 11

Ni chip aina ya octa core kwa maana ina core nane

Ina uwezo wa wastani kiutendaji

Geekbench inaipa alama 358

Processor hii inajitahidi kucheza gemu nyingi kutokana na aina na uwezo wa core kubwa.

Uwezo wa core kubwa

Helio G85 ina jumla ya core kubwa mbili zenye spidi inayofikia 2.0GHz

Core zake zimeundwa kwa muundo wa Cortex A75

Cortex A75 ina utendaji wa kufanya kazi karibu bilioni 6 kwa wakati mmoja

Ila ni muundo wenye uwezo wa kati

Uwezo wa core ndogo

Core ndogo zipo sita aina ya cortex a55 kwenye Mediatek helio g85 zenye spidi inayofikia 1.8 GHz

Tecno Camon 17 inatumia cortex a55 kwa ajili ya kazi ndogo kama kutuma meseji au kupiga simu.

Muundo huu unaifanya simu kukaa na chaji masaa ya kutosha

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Tecno Camon 17 inapeka umeme wa kima cha kati wa kisi cha wati 18

Chaji yake ina uwezo wa kujaza betri kwa masaa yanayozidi matatu.

Hii inatokana na beti ya camon 17 kuwa na ukubwa wa 5000mAh aina ya Li-Po.

Ukubwa huu unaipa simu uwezo wa kukaa na chaji masaa zaidi ya 14 simu ikiwa inatumia intaneti muda wote

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili ya Tecno Camon 17 yanatofautiana ukubwa wa memori kwenye RAM

Kuna camon 17 ya GB 128 na ram ya gb4 na nyingine ina ram ya gb 6

Haijaainishwa na Tecno aina ya memori iliyotumika

Kwani processor ya MediaTek Helio G85 inakubali memori ya eMMC 5.1 na UFS 2.1

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 17

Moja ya sehemu inayofanya bei ya tecno camon 17 kuwa kubwa ni aina ya bodi ya simu

Simu imeundwa kwa bodi ya plastiki ambazo si imara sana hasa inapoanguka kimo kirefu cha mita mbili

Na pia haina viwango vyovyote vya IP .

Viwango IP(Ingression Protection) vinaonyesha uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi

Urefu wa simu ni inchi 6.6 hivyo ni simu ndefu

Ubora wa kamera

Camon 17 ina kamera tatu.

Ni kamera moja angalau yenye ubora stahiki kutoa picha nzuri.

Hiyo ni kamera kuu yenye resolution ya 48MP

Lakini imetumia autofocus aina ya PDAF inayozidiwa ubora na dual pixel pdaf

simu ya tecno camon upande wa kamera

Kamera ya tatu ni aina ya QVGA.

QVGA ni aina ya kamera za kizamani ambazo zina resolution ndogo kwa viwango vya kisasa

Kamera zake zinaweza kurekodi video za aina moja tu za full hd kwa spidi ya 30fps

jifunze, jinsi ya kuchagua kamera nzuri za simu

Ubora wa Software

Ukinunua camon 17 kwa mara ya kwanza utapata android 11

Lakini hii ni simu ya tecno inayoweza kupokea toleo jipya la android 12

Kitu kinachoifanya simu kuendelea kuwa mpya

HiOS 7.6 ya Tecno inaweza kukuonyesha hali ya hewa ya eneo ulilopo kwa wakati uliopo

Pia HiOS 7.6 ina app ya kuhariri video na kuzieguza jinsi unavyotaka zitokee

Yapi Madhaifu ya Tecno Camon 17

Kamera ya Tecno Camon 17 haina OIS ambayo hutumika kutuliza video wakati wa kurekodi

Bei ya simu haiendani na uwezo wa processor kiutendaji.

Kwani utendaji wake ni wa kiwango cha kati

Simu haina viwango vinavyoonyesha uwezo wa kuzuia maji tiririka.

Baadhi ya simu za laki nne zinatumia kioo cha amoled tofauti na camon 17 yenye ips lcd

Simu haina kamera ya ultrawide kwa ajili ya kuchukua eneo pana

Neno la Mwisho

Bei ya Tecno Camon 17 inaweza kununua simu aina ya Xiaomi Redmi Note 10T 5G

Wakati  simu ya Xiaomi Redmi Note 10T 5G ina processor yenye nguvu na inakubali mtandao wa 5G

Na redmi note 10t 5g inalindwa ni kioo kigumu kuchubuka cha gorilla 3

Kwa nyakati za sasa bei ya tecno 17 inafaa kuuzwa kwa bei ya laki tatu na nusu

 

Maoni 3 kuhusu “Bei ya Simu ya Tecno Camon 17 na Sifa Zake Kiundani (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram