SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sifa za simu ya Vivo V23 Pro na Bei Yake 2022

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 14, 2022

Simu ya vivo v23 pro ni simu ya android ya mwaka 2022 yenye ufanisi mkubwa kwenye utendaji.

Ukizipitia sifa zake zilizoainishwa utaona nguvu kubwa ya processor na kamera yenye uwezo wa kurekodi video za resolution mbalimbali.

simu ya vivo upande wa mbele na nyuma

Na bei ya vivo v23 inaendana na vitu bora vingi vilivyopo kwenye simu

Sifa za hii simu zinaifanya kuwa moja ya simu bora ya daraja la kati kwa mwaka 2022

Bei ya Vivo V23 Pro Tanzania

Bei ya vivo v23 pro inafika shilingi 1,188,956.95/= za Tanzania

Hii ni bei ya vivo v23 ya GB 128 na Ram ya GB 8

Kwa hiyo bei yake inaongezeka kutokana na ukubwa wa memori.

Japokuwa bei inaweza onekana kubwa ila sifa zake kwenye display, memori, kamera na nguvu ya utendaji zimefanya bei ya simu kuwa juu.

Zifuatelie sifa zake zote kiundani

Sifa za Vivo V23 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 1200 5G
  • Core Kubwa Zaidi(1) – 1×3.0 GHz Cortex-A78
  • Core Kubwa Kiasi(3) – 3×2.6 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(6) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G77 MC9
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • Funtouch 12
Memori UFS 3.1, 128GB, 256GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera (vivo ya macho matatu)

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.56inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-44W
Bei ya simu(TSH) 1,188,956.95/=

Upi ubora wa Simu ya Vivo V23 Pro

Ukianza kuitumia vivo v23 pro utauona ubora wake kwenye display

Display yake inaonyesha vitu kwa ustadi kutokana na aina ya teknoloji iliyotumika kwenye kioo

Simu inawahi kujaa chaji kwa haraka

taarifa fupi ya vivo v23 pro

Kamera ya vivo ina rsolution kubwa inayofaa zaidi wakati wa kuzoom

Utendaji wa simu ya vivo v23 pro una nguvu ya kufungua gemu na aplikesheni ya aina yoyote

Simu inakuja na memori kubwa inayoweza kuhifadhi mafaili mengi na ya kutosha

Haya ni machache lakini ina uimara katika nyanja karibu zote.

Tuzame kiundani

Uwezo wa Network

Vivo v23 pro ina uwezo wa kutumia mtandao wa 4G na 5G.

Aina ya 4G simu inayotumia ni LTE Cat 17.

LTE cat 17 ni mtandao wa 4g unaoweza kudownload kwa kasi inayofikia 1600Mbps

network ya vivo v23 pro

Kama intaneti ya mtandao wa simu inakupa kasi hii basi unaweza kudownload faili la ukubwa 1300MB(1.3GB) kwa sekunde saba tu

Japokuwa kasi ya intaneti ya ya LTE Cat 17 Tanzania inapatikana kwa makampuni ya fiber kama zuku na sio laini za simu.

Kiujumla simu inakubali network bands za 4G saba tu

Bands hizo ni B1, B3, B5, B8, B38, B40 na B41.

Kuna baadhi ya laini za simu zinaweza zisikubali network ya 4G hapa Tanzania kutokana na kukosekana kwa baadhi ya bands wanazozitumia kwa ajili ya 4G.

Ubora wa kioo cha Vivo V23 Pro

Kioo cha Vivo v23 Pro ni kizuri kuliko kioo cha simu ya samsung a03s

V23 Pro ina kioo cha aina ya amoled.

Moja ya kitu kizuri  kwenye kioo cha amoled ni kuwa na contrast kubwa.

Contrast kubwa inatengeza rangi nyingi

Hivyo inafanya kioo kuonyesha rangi za vitu kwa uhalisi wa asilimia za juu.

Na kizuri zaidi  kioo cha simu kinaundwa na teknolojia ya HDR10+

HDR10+ kinaongeza utajiri wa rangi zaidi na kufanya kioo kionyeshe vitu kama vinaonekana na jicho la binadamu kwenye mazingira halisi

Ubora wake wa kioo pia unachagizwa na refresh rate kubwa inayofikia 90Hz

Hiki kiasi kinafanya simu kuwa nyepesi unapotachi.

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 1200

Processor iliyotumika kuipa nguvu vivo v23 pro ni MediaTek Dimensity 1200

MediaTek Dimensity 1200 ni processor ya simu yenye core nane

Core zake zimegawanyika sehemu tatu.

processor ya vivo v23 pro dimesnity 1200

Dimensity 1200 inafanya vizuri sana kwenye applikesheni zinazopima nguvu ya chip ya simu

Kwenye app ya antutu mediatek dimensity ina alama 678,193

Geekbench inaipa alama 975 kwenye core moja

3DMark inaipa chipset alama 4180

Kifupi ni chip inayosukuma gemu yoyote.

Nguvu kubwa ya chipset inachagizwa na muundo na uwezo wa core zake kubwa na ndogo

Uwezo core kubwa

Core zenye nguvu ndogo zipo nne ila moja ina spidi inoyfikia 3.0GHz

Wakti core tatu zina spidi inayofikia 2.6GHz

Hizi core zina nguvu sana inayochangiwa na kutumia muundo wa Cortex A78

Cortex A78 inaifanya processor ya simu kuwa na utendaji imara pindi simu inapofungua applikesheni inayohitaji nguvu.

Kizuri ni kuwa Cortex A78 ina matumizi madogo ya umeme wakati ikifanya kazi kubwa

Uwezo wa core ndogo

Ubora wa core ndogo kwenye processor za simu hupimwa kwa matumizi madogo ya umeme.

Core nne zenye nguvu ndogo zina spidi inayofikia 1.8GHz

Hizi zimeundwa kwa Cortex A55

Cortex A55 hutumika pale simu inapofanya kazi zinazohitaji nguvu ndogo

Huu ni muundo unaokula umeme wa betri kidogo lakini utendaji upo juu kiasi

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya vivo v23 pro inaweza kupeleka umeme kwa kasi inayofikia wati 44.

Ni kasi inayoweza kujaza betri lake aina ya Li-Po la ukubwa wa 5000mAh chini ya dakika 70

Kwa mujibu wa gsmarena, simu inaweza tunza moto kwa masaa 110 ikiwa haitumiki mara kwa mara

Kwa uzeufu wangu, simu zenye betri ya 5000mAh zinaweza kukaa na chaji kwa zaidi ya masaa 14 ikiwa kwenye intaneti masaa yote bila kuzima data

Hivyo kwa ukubwa huu betri simu ya vivo v23 pro ni moja ya simu inayotunza chaji japokuwa ina processor yaenye nguvu sana.

Ukubwa na aina ya memori

Memori iliyopo kwenye V23 Pro ina kasi kubwa ya kuandika na kusoma data.

Hivyo kasi hiyo inaifanya simu kufungua app kwa haraka sana.

Hii spidi kubwa inasababishwa na kutumika kwa memori aina ya UFS 3.1

Hizi ni memori tofauti na zile zilizopo kwenye simu mpya nyingi za tecno ambazo ni aina eMMC

Kuna vivo ya 128GB na 256GB

Uchaguzi ni wako kulingana na matumizi yako ya simu

Uimara wa bodi ya Vivo V23 Pro

Bodi ya Vivo V23 Pro ni imara kwa sababu imetengenezwa kwa glasi upande wa nyuma na mbele.

Japokuwa haijaainishwa kampuni ambayo imeunda vioo vya simu hii.

Simu pia ni nyepesi kubeba kwani ina uzito wa gramu 171

Huu ni uzito unaoweza kukufanya usihisi kama umebeba simu

Na simu ni ndefu kiasi kwani ina inchi zinazofikia 6.56

Ubora wa kamera

Kamera ya vivo v23 pro ina kamera yenye sensa kubwa ya 108MP

Kwenye upande wa autofocus, imetumika teknolojia ya pdaf.

Pdaf ina ulengaji mzuri lakini haiwezi kuifikia dual pixel pdaf au Laser AF ambazo zimetumika pia kwenye iphone ya bei nafuu ya iPhone SE 2022

kamera ya vivo v23 pro macho matatu

Uzuri wa kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa spidi ya 30fps

Japokuwa simu hii haiwezi kuwekwa kwenye simu za vivo zenye kamera, lakini kamera yake imewezeshwa mfumo wa gyro-Eis

gyro-Eis ni aina nyingine ya teknolojia ya kamera kwa ajili ya kuituliza kamera pale anayerekodi video akiwa anatembea

Tofauti na OIS, gyro-EIS inatumia motion sensor.

Ubora wa Software

Vivo v23 pro ni simu ya android 12 inayotumia mfumo wa Funtouch 12

Simu ya android 12 inaweza kukuonyesha app inayotumia kamera na mic bila ruhusa yako

Hii itakusaidia kuzitambua app zinazokutrack.

Wakati Funtouch 12 inakupa uwezo wa kuongeza ram kwenye simu.

Kwa hiyo utaweza kutumia memori ya simu kama ram.

RAM inapokuwa kubwa inaongeza ufanisi wa simu kiutendaji kiasi fulani

Yapi Madhaifu ya Vivo V23 Pro

Udhaifu mkubwa wa simu hii ni kutokuwa na uwezo wa kuzuia maji kupenya.

Haina viwango vya aina yoyote vya IP-Ratings.

Kamera zake zinarekodi video kwaa spidi ndogo ya 30fps

Simu ina network bands za 4G chache sana.

Simu inakosa kamera ya telephoto na haina optical zoom

Neno la Mwisho

Simu ni nzuri na inaendana na bei yake

Washindani wakubwa wa hii simu ni, simu ya  Oppo Realme GT Neo 2T, OnePlus Nord 2 5G na Xiaomi 11T

Xiaomi 11T ndio mshindani mkubwa zaidi kuliko mwingine.

Bei ya xiaomi 11T ni chini ya shilingi 800,000 na ina bends za 4G nyingi

Kiuhalisia Xiaomi 11T inaizidi vivo v23 kwenye kila kitu

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu 14 mpya za Vivo za ubora mkubwa na bei zake (2024)

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka mwaka huu 2024 Vivo imeachia matoleo mengi ya simu Katika matoleo hayo yapo ya bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa Kwa maana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram