SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya Samsung galaxy a03s (Na sifa zake)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 14, 2022

Simu ya samsung galaxy a03s ni simu ya daraja la chini iliyotoka mwaka 2021.

Simu nyingi za daraja la chini huundwa na vitu vichache vyenye ubora mkubwa.

simu ya samsung galaxy upande wa mbele na nyuma

Na bei za simu za daraja la chini huwa zipo chini pia.

Ndio maana bei ya samsung galaxy a03s ni chini ya laki nne.

Hilo linatokana na sifa zake kuanzia utendaji, nguvu ya processor, kioo nk

Bei ya Samsung Galaxy a03s Tanzania

Baadhi ya maduka ya simu ya kariakoo samsung galaxy a03s inauzwa kwa bei ya shilingi 350,000/= mpaka 360,000/=

Ni bei ya Samsung A03s ya GB 64

Ila nchi zingine duniani bei yake ni shilingi 340,000/=

Ni samsung ya bei rahisi ila ina sifa nyingi ambazo haziifikii samsung za gharama

Sifa za Samsung Galaxy A03S

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio P35
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.35 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 11
  • One UI 3.1 Core
Memori eMMC 5.1, 32GB,64GB na RAM 2GB, 4GB, 3GB
Kamera Kamera tatu (simu ya macho matatu)

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 350,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy A03S

Ubora wa simu ya samsung a03s unapatikana kwa kiasi kikubwa kwenye betri na software

Software kwa maana ya skin ni nyepesi na rahisi kutumia

taarifa za samsung galaxy a03s kwa picha

Betri yake ni kubwa inayowaza kukaa na chaji muda mwingi

Spidi ya chaji yake haiwezi kuharibu betri

Lakini ubora wa vitu vingine si mkubwa, endelea kusoma hii makala na kuelewa nini ninachokimaanisha

Uwezo wa Network

Simu ya samsung galaxy inakubali mtandao wa 4G aina ya LTE Cat 7

LTE Cat 7 ni aina ya 4g yenye spidi ya kasi inayofikia 300Mbps

network ya samsung galaxy a03s

Zipo aina nyingi za 4G zenye spidi mara ya nne ya hii.

Kwa kiasi kikubwa ni spidi inayoperuzi na kudownload mafaili kwa kasi

Uzuri wa galaxy a03s ni kuwezeshwa network bands zinazokubali mitandao yote ya simu Tanzania

Ila simu haina 5G, kwa sasa hakuna laini ya simu inayokubali 5G Tanzania

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A03S

Kama ilivyo kwa simu ya vivo y21, kioo cha samsung galaxy a03s ni cha IPS LCD

IPS LCD ni vioo vizuri lakina havina rangi nyingi.

Kitu kinachosababisha screen kuonyesha baadhi ya vitu kwa rangi zisizo halisi ukilinganisha na vioo vya amoled

Simu haina resolution kubwa sana.

Resolution yake ina ukubwa wa 720 x 1600 pixels

Pia galaxy a03s haina teknolojia inayoboresha rangi zaidi aina ya HDR10

Nguvu ya processor  ya simu

Simu ya samsung galaxy a03s inapewa nguvu na processor ya MediaTek Helio P35

Ni processor yenye core nane ambazo zimetofautiana spidi.

Core nne za mwanzo spidi yake inafikia 2.35GHz

Na core nne zingine spidi yake inafikia 1.8GHz

processor ya helio p35 inayotumia na samsung galaxy a03s

Uwezo wa processor ya MediaTek Helio P35 kiutendaji ni mdogo

Inapata alama chache kwenye app zinazopima nguvu ya processor

Antutu kwa mfano, inaipa alama 100,496

Na GeekBench inaipa alama 171 kwenye core moja

Nguvu ndogo ya chip hii inasababishwa na kutumia muundo wa Cortex A53 kwenye core zote

Cortex A53 ni muundo kwa ajili ya kufanya kazi ndogo.

Hivyo simu hii inapata shida kwenye kucheza magemu yanayohitaji nguvu kubwa ya processor

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya samsung galaxy a03s inapeleka umeme wa wastani wa wati 15

Kiasi cha umeme ambacho kitachukua masaa zaidi ya matatu kujaza betri.

Hilo linasababishwa na betri yake aina ya Li-Po yenye ujazo wa 5000mAh

Simu yenye ujazo wa 5000mAh hukaa na chaji muda mrefu.

Kikawaida ni zaidi ya  masaa 13 simu ikiwa muda wote kwenye intaneti

Ukubwa na aina ya memori

Kasi ya memori ya samsung galaxy a03s si kubwa sana.

Kasi ndogo inatokana na aina ya memori ya eMMC 5.1 iliyotumika kwenye hii simu.

Moja ya kitu kinachoathiri utendaji wa simu ni spidi ya memori kwenye kuandika na kusoma data

Samsung a03s zipo za aina nne kwenye memori

  1. Samsung A03s ya GB 32, RAM GB 2
  2. Samsung A03s ya GB 32, RAM GB 3
  3. Samsung A03s ya GB 32, RAM GB 4
  4. Samsung A03s ya GB 64, RAM GB 4

Kama utakuwa unahitaji kuhifadhi mafaili mengi samsung ya gb 64 ndio inafaa zaidi

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A03S

Bodi ya samsung galaxy a03s imeundwa kwa plastiki

Hizi bodi huchunika rangi kadri muda unavyoenda

Na zinaweza kupasuka kirahisi simu ikianguka kwa kimo cha mita mbili kutoka juu.

Ni jambo la msingi kuweka kava na screen protector kuipa simu ulinzi wa ziada

Simu ni nyepesi kubeba kwani uzito wake ni gramu 196

Ubora wa kamera

Samsung galaxy a03s ni simu ya macho matatu ya bei nafuu.

Kamera kuu ina ukubwa wa 13MP yenye teknolojia ya ulengaji(autofocus) ya kawaida sio pdaf

Na kamera nyingine ya macro mahsusi kwa kupiga vitu kwa ukaribu ina resolution ndogo ya 2MP

kaa,era ya macho matatu ya samsung galaxy a03s

Na kamera nyingine hutumiwa na simu kupima umbali kati ya kamera na kinachopigwa simu

Hizi huitwa kamera za depth, huisaidia simu kujua ukubwa wa eneo linalopaswa kutokea kwenye simu.

Sio kamera muhimu sana sababu ni kitu kinachoweza kufanywa na software

Kamera zake zinarekodi video zenye ubora wa aina moja tu (full hd)

Ubora wa Software

Simu ya samsung galaxy a03s ni simu nyingine ya android 11 inayotumia software ya One UI  3.1 Core

One UI Core ni mfumo wa samsung unatumika kwenye simu zenye nguvu ndogo kiutendaji.

Ni mfumo ambao umeondoa baadhi ya app na kuacha applikesheni za msingi zinazohitajika mara kwa mara.

Kwa mfano Samsung S22 Ultra ina programu ya kufungua magemu, lakini kwenye A03S haipo

Mtindo huu unaongeza utendaji wa simu kiasi fulani

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A03S

Simu ya samsung galaxy a03s ina nguvu ndogo kiutendaji.

Ni simu isiyofaa kucheza gemu nzito na kufungua applikesheni nyingi kwa wakati mmoja

Kamera zake hazina OIS wala dual pixel pdaf

Na haziwezi kurekodi video za resolution kubwa

Simu haiwezi kuzuia maji kupenya.

Na bodi yake si imara kupasuka inapodondoka kimo kirefu

Memori zake ni ndogo na zinasafarisha data kwa kasi ndogo

Chaji yake inapeleka umeme mdogo

Neno la Mwisho

Kwa kuzingatia bei, samsung galaxy a03s ni simu ya bei nafuu inayofaa kumilikiwa

Ila unapaswa ujue, zipo simu za laki tatu na nusu zenye utendaji mkubwa kuliko hii.

Mfano ni simu ya Redmi 9T ina processor yenye nguvu na inaweza kusukuma magemu mengi kwa urahisi

Samsung galaxy a03s inamfaa zaidi mtu anayetumia smartphone kwa mara ya kwanza.

Maoni 6 kuhusu “Ubora na bei ya Samsung galaxy a03s (Na sifa zake)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram