SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Nzuri Matoleo Mapya na Bei Zake 2023

Miongozo

Sihaba Mikole

February 11, 2023

Tangu mwaka 2023 umeingia, kuna matoleo mapya simu janja ambayo yametoka mwishoni mwa mwaka 2022 na mwanzoni 2023 na mengine yatatoka baadae.

Katika hizo simu mpya zipo za bei ndogo, kubwa, nzuri na mbaya

Hii post imeorodhesha simu nzuri matoleo mapya kwa mwaka huu wa 2023 na yale ya mwishoni mwa mwaka 2022.

simu nzuri

Simu Nzuri maana yake ni simu ambayo imekamilika kila idara na yenye mapungufu kidogo sana.

Hivyo bei zake haziwezi kuwa ndogo lazima ziwe juu.

Fuatililia ufafanuzi kuanzia kwenye ubora mpaka bei za kila simu

iPhone 14 Pro

Simu ya iPhone 14 Pro imetoka mwezi wa tisa 2022

Kwa upande wa apple bado ni simu mpya kwani hakuna toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 mpaka mwishoni mwa mwaka

Utendaji wa iPhone 14 Pro ni mkubwa sana kwa sababu ina chip(processor) ya Apple A16 Bionic

Ukaaji wake wa chaji unafika masaa 14 ukiwa unatumia intaneti muda wote

iphone 14 pro showcase

Ina kioo chenye uangavu mkubwa, kioo hiko wanakiita LTPO Super Retina XDR OLED

Kamera yake inapiga picha kwa ustadi kwa mazingira yote ya mwanga hafifu na mwanga mwingi

Unaweza ifuatalia hii simu kupitia, ubora kuhusu iPhone 14 Pro

Bei ya iPhone 14 Pro

Bei ya sasa ya iPhone 14 Pro inafika shilingi 2,600,000/=

Bei itazidi kama utahitaji iphone 14 Pro yenye memori kubwa zaidi kwani yako matoleo kama matatu

Xiaomi 12 Pro

Xiaomi ni kampuni ya China inayosifika kwa kuunda simu kali na kwa bei nafuu

Mwishoni mwa mwaka 2022 walizindua toleo la Xiaomi 12 Pro simu yenye kamera tatu huku kila kamera 50MP

Hii ni simu yenye kioo kiangavu na chenye ufanisi wa uoneshaji rangi kwa usahihi

Kwani kioo chake cha LTPO amoled chenye refresh rate ya 120Hz, Dolby Vision na HDR10+

xiaomi 12 pro

Xiaomi 12 Pro inakuja na chaji ya wati 120 ambayo inajaza simu kwa 100% ndani ya dakika 18 tu

Pia inauwezo wa kuchaji simu kwa “wireless” yaani bila kutumia waya wa chaji

Cha kufurahisha ni kuwa bei yake sio kubwa sana na inaendana na simu ya Oppo Reno8 5g ila oppo inazidiwa mbali

Bei ya Xiaomi 12 Pro

Xiaomi 12 Pro ya GB 128 inauzwa shilingi 1,200,000/= mpaka ikufikie hapa Tanzania

Gharama inaweza ikawa chini kabisa kama ukinunua kwa kuagiza nje yaani Aliexpress

Vivo X90 Pro

Vivo X90 Pro ni simu ya Android 13 ambayo imetoka imetoka mwezi novemba 2022

Hii ni simu bora kabisa ya vivo kwani ina utendaji wenye nguvu kutokana na kutumia chip ya Dimensity 9200

Kioo chake ni cha amoled chenye refresh rate ya 120Hz na resolution 1260 x 2800 pixels

vivo x90 pro

Hivyo swala la muonekano wa vitu kioo kinanyesha kwa ubora mkubwa

Vivo X90 Pro iko fasta kwa sababu inatumia memori aina ya UFS 4.0

Mfumo wake wa kamera una kamera tatu ambazo ufanisi wa upigaji picha ni wa kiwango kinachoendana na iPhone 14 Plus au samsung galaxy s23

Inakuja na chaji yenye kupeleka umeme mwingi hivyo betri yake 4870mAh inajaa 50% kwa dakika 8 tu

Bei ya Vivo X90 Pro

Bei ya Vivo X90 Pro inafika shilingi milioni mbili (2,000,000/=) ya GB 256

Hii ni bei ya Aliexpress hivyo kwa hapa Tanzania bei inaweza kuwa juu kidogo

Sony Xperia 5 IV

Simu ya Sony Xperia 5 IV imetoka mwezi septemba mwaka 2022

Ila ni simu inayochuana na simu zingine uzionazo kwenye orodha

Inatumia chip yenye utendaji mkubwa ya Snapdragon 8 Gen 1

sony 5 iv

Hivyo kama unacheza gemu simu haitogandaganda

Ina betri kubwa ya kukaa chaji masaa mengi kwani ukubwa wake ni 5000mAh

Ni simu yenye uwezo wa kuzuia maji kuingia ndani ya simu kutokana na kuwa na IP68

Ina kamera tatu zenye 12MP ila picha zake ni kali na za kuvutia

Bei ya Sony Xperia 5 IV

Bei ya sony xperia 5 iv kwa hapa Tanzania inaweza fika 1,800,000/=

Ni bei inayoshahibiana na ubora wa simu kwenye kila kipengele

OPPO Reno8 T 5G

Oppo Reno8 T 5G ni simu ambayo imeingia sokoni mwezi februari 2023

Ni simu inayotumia kioo cha AMOLED chenye uwezo wa kuonyesha rangi bilioni moja

Maana yake ni kuwa kioo kitaonyesha kitu kwa rangi zake halisi kwa kiwango kikubwa

oppo ren8 T 5G

Kwenye upande wa kamera simu haivutii sana

Kamera kuu(wide) ni nzuri lakini kamera zengine kiuhalisia ziko kama pambo kwani zina megapixel 2 ambayo ni ndogo

Chaji yake inakuja na uwezo wa kupeleka wati 67, hivyo chaji itawahi kujaa haraka

Bei ya Oppo Reno8 T 5G

Bei ya OPPO Reno8 T 5G ni shilingi za Kitanzania 800,000/=

Ni kiwango kidogo ukilinganisha na simu ziliainishwa hapa

Ila bei inaweza kuwa kubwa sababu simu ina kasoro kadhaa

Tecno Phantom X2 Pro

Kama unatafuta simu nzuri zaidi ya Tecno basi Tecno Phantom X2 Pro ndio jibu sahihi

Kiubora inaweza kuachwa mbali na Vivo X90 au Xiaomi 13 Pro ila ni simu ya daraja la juu yenye utendaji mkubwa

Utendaji mkubwa unasababishwa na simu kutumia chip ya Dimensity 9000

Ni tecno inayotumia kioo cha amoled ambavyo ubora wa uonyeshaji rangi za sahihi vitu ni mkubwa\

Ina betri kubwa na chaji yenye kasi

Hata mfumo wa kamera umeboreshwa, kamera zake zinaweza kuchukua video za 4K

Bei ya Tecno Phantom X2 Pro

Tecno ya GB 256 inapatikana kwa shilingi 1,500,000/=

Ni nadra kukutana na Tecno ikiwa na bei kubwa kiasi hiki lakini hii simujanja yenye maboresho mengi toka Tecno

Samsung Galaxy S23 Ultra

Kwenye hii orodha hakuna simu yenye kamera nzuri kama Samsung Galaxy S23 Ultra

Hii ni samsung mpya ya mwaka 2023 ina kamera nne zinazoweza toa picha nzuri iwe usiku ama mchana

samsung galaxy s23 ultra

Betri yake ni kubwa na ukaaji wa betri uanfika masaa 12 ukiwa unatumia intaneti ya 5G

Inatumia kioo aina ya dynamic amoled, na vioo vya amoled huwa ni vizuri tu kiujumla

Utendaji wake ni mkubwa kwani unakaribiana na simu iPhone 14 Pro Max

Bei ya Samsung Galaxy Ultra

Kwa hapa Tanzania hii simu utaipata kwa zaidi ya shilingi milioni 2.9

Ni samsung yenye kasoro chache sana

Inahitaji mtu mwenye bajeti kubwa kuimiliki

Samsung Galaxy S23+

Hili ni toleo jipya lingine ambalo limetoka pamoja na Samsung Galaxy S23 Ultra

Kisifa ni kuwa Galaxy S23+ inaendana na mkubwa isipokuwa utofauti upo kwenye kimo na kamera

Samsung hii ina macho matatu na haiji na peni

samsung galaxy s23+ thumbnail

Ila mfumo wake wa chaji unaweza kupokea wati 45 hivyo inafanya simu kujaa kwa dakika chache

Kwa mpenzi wa simu ya urefu wa wastajni, hili toleo linafaa

Unaweza ifahamu zaidi hii simu hapa, ubora uliopo kwenye Samsung Galaxy S23+

Bei ya Samsung Galaxy S23+

Bei ya Samsung S23+ inafika shilingi 2,400,000/= kwa toleo yenye memori ndogo

Ila bei itakuwa kubwa zaidi kwa S23+ za GB 512

Realme 10 Pro

Realme 10 Pro ni simu ya bei ndogo zaidi iliyotokea kwenye list

Ni simu ya 5G yenye utendaji wa wastani

Inatokana na Realme 10 Pro kutumia processor ya Snapdragon 695 5G

Ina kamera zipatazo mbili ila moja ndio inayoweza kutoa picha zinazovutia

realme 10 pro

Chaji yake inaweza kupeleka umeme wa wati 33

Si umeme mwingi sana ila unajaza simu kwa dakika chache

Utendaji wakw ni wa wastani

Bei ya Realme 10 Pro

Bei ya simu ya realme 10 pro inafika shiligni 610,000

Hii ni bei ya realme 10 pro ya GB 128 na RAM ya GB 8

Ukiiangalia ukubwa wa memori na sifa zake zingine, bei inaendana na ubora

Xiaomi 13 Pro

Xiomi 13 Pro iliingia sokoni mwezi desemba mwaka 2022

Ina miezi miwili na inatumia toleo jipya la android yaani Android 13

Kioo chake ni aina LTPO AMOLED chenye uwezo wa kuongeza au kupunguza refresh rate kutokana na matumizi

Ni simu inayokuja na chaji ya wati 120 hivyo ujaaji wa chaji ni wa dakika kadhaa.

xiaomi 13 pro

Ina kamera tatu zote zenye 50MP na zinapiga picha nzuri kwenye mazingira yoyote

Pia zinaweza kuchukua mpaka ya kiwango cha 8k

Utendaji wake unaendana na simu za samsung s23 kutokana na kuwa na processor ya aina ya Snapdragon 8 Gen 2

Bei ya Xiaomi 13 Pro

Bei ya Xiaomi 13 Pro ni shilingi 2,000,000/=

Hiyo bei inaakisi kwa kiasi kikubwa vitu ambavyo simu inayo

Maoni 8 kuhusu “Simu Nzuri Matoleo Mapya na Bei Zake 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram