SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu Samsung Galaxy S23+ na Sifa Muhimu

Simu Mpya

Sihaba Mikole

February 6, 2023

Simu nyingine mpya ya Samsung kwa mwaka 2023 ni Samsung Galaxy S23+

Inafanana kwa kiasi kikubwa na simu ya Samsung Galaxy S23 Ultra  ila kuna Galaxy S23+ inavikosa

samsung galaxy s23+ showcase complete

Kwa maana hiyo bei ya Samsung Galaxy S23+ itakuwa chili ila inazidi milioni mbili

Kwenye hii posti, utafahamu ubora na vitu vipya vya hii simu ambavyo vinatofautiana na simu zingine

Bei ya Samsung Galaxy S23+ ya GB 256

Kwenye masoko ya dunia bei yake kwa sasa inasamama shilingi za Tanzania 2,400,000/=

Kwa Tanzania bei inaweza kuwa kubwa na hata ikazidi 2,700,000/=

Lakini itategemea na wapi unanunua hiyo simu

samsung galaxy s23+ summary

Bei kubwa ya simu inasababishwa na ukweli kwamba hii ni simu ya daraja la juu

Ni simu ambayo utakuta kamera kali, spika zinatoa sauti nzuri, kioo kinachoonyesha vizuri na mengineyo mengi ambayo yaeoonyeshwa kwenye hii post

Sifa za Samsung Galaxy S23+

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8 Gen 2
  • Core Zenye Sana(1) – 1×3.36 GHz Cortex-X3
  • Core Zenye Nguvu(2) – 2×2.8 GHz Cortex-A715
  • Core Zenye Nguvu Wastani-2×2.8 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(3) – 3×2.0 GHz Cortex-A510
  • GPU-Adreno 740
Display(Kioo) Dynamic Amoled 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
  • One UI 5.1
Memori UFS 4.0, 256GB, 512GB, na RAM 8GB
Kamera Kamera TATU

  1. 50MP,Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 10MP(ultrawide)
  3. 12MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 4700mAh-Li-Ion
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 2,400,000/=

 Upi Ubora wa Samsung Galaxy S23+

Kama ilivyoelezwa sifa nyingi za Galaxy s23 ultra zipo pia kwenye hii simu

Ina mfumo unaopleka chaji kwa kasi hivyo simu inawahi kujaa

Inatumia toleo jipya la android

Ni simu itakayokuwa inapata sapoti ya muda mrefu kwa karibu miaka minne

Ina mfumo wa memori unaosafirisha data kwa kasi kubwa

Ina kioo chenye uangavu mkubwa

Na pia ni simu yenye utendaji mkubwa wa kuweza kufungua app ya aina yoyote

Uwezo wa Network

Hii ni simu inayokuja na uwezo wa kukamata mtadao wa 5G na pia 4G

Inakubali aina zote za 5G yaani masafa mafupi, ya kati na marefu

Pia inatumia 4G aina ya LTE Cat 24 kama ilivyo kwa Galaxy S23 Ultra

samsung galaxy s23+ network

Pitia, aina za network za simu zinazopatikana Tanzania

LTE Cat 24 ina spidi ya kudownload inayofika 2400Mbps

Kwa Tanzania hakuna mtandao wa simu ya 4G unaotoa kasi hii

Na hata ikiwepo ghrama yake itakuwa kubwa na sio ndogo

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy S23+

Simu inatumia kioo cha dynamic amoled 2x chenye resolution  kubwa ya 1080 x 2340 pixels

Resolution inayovifanya vitu vionekane vizuri kwenye screen.

Ubora wa hiki kioo unachangiwa na uwepo wa HDR10+ na Refresh rate

samsung galaxy s23 plus display 2

HDR10+ hutengeneza mlinganyo sahihi wa rangi hasa tofauti kati ya nyeusi na nyeupe

Huwa inafanya vitu vionekane kwa usahihi kuendana na jinsi vinavyoonekana kwenye mazingira halisi

Uangavu wa kioo cha Samsung Galaxy S23+ unafika nits 1700

Huu uangavu unampa uwezo mtumiaji kuona vitu vizuri kama simu ikiwa inatumika kwenye mazingira yenye mwanga mwingi wa jua

Nguvu ya processor Snapdragon 8 Gen 2

Galaxy S23+ inatumia chip mpya ya Snapdragon 8 Gen 2 inayokuja na GPU ya Adreno 740

Snapdragon 8 gen 2 imegawanyika sehemu nne zenye core jumla ya nane

Na core yenye kasi kubwa zaidi ipo moja na inafika GHz 3.36 aina ya Cortex X3

Kwenye hii kurasa kuna maelezo zaidi: aina ya processor za simu na core zake

Aina ya core hutumika pale simu inapofanya kazi kubwa kwa mfano kucheza gemu kama la Call of Duty

samsung galaxy s23+ processor

Na core ndogo zaidi zipo tatu hufanya kazi pale unapokuwa kwenye matumizi ya kawaida kama kupiga simu, kutumia whatsapp nk

Mgawanyo huu uhakikisha simu inakuwa na ufanisi mzuri wa matumizi ya betri

Kwa sababu processor ikiwa na nguvu sana chaji inawahi kuisha

Na unapocheza gemu iwe kwenye simu au laptop, GPU ndio huwa inahusika na hiyo kazi

GPU ikiwa na nguvu ndogo simu husumbuka kucheza gemu vizuri ama muonekano wa gemu unakuwa sio wa kuvutia na pia simu inachemka sana.

GPU ya Adreno 740 ni imara kwenye kucheza gemu, kwani gemu nyingi hucheza kwa fps 60

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya S23+ ina ukubwa wa 4700mAh aina ya Li-Ion

Inaizidi kidogo kiikubwa betri ya Apple iPhone Pro ila kwenye matumizi ya simu utendaji wa betri huwa upo tofauti

samsung galaxy s23+ chaji

Matarijio ni kuwa betri inaweza kukaa na chaji kwa masaa zaidi 10 simu ikiwa inatumia intaneti ya 5G

Ina uwezo wa kupokea chaji yenye kasi ya wati 45

Hivyo simu inajaa kwa 65% kwa muda wa dakika 30

Ukubwa na aina ya memori

Galaxy S23+ inakuja na memori yenye kasi sana aina ya UFS 4.0

Kasi hii inaigeuza simu kuwa fasta wakati wa kuwasha na kufungua app mbalimbali

Na pia simu inakuwa fasta zaidi ukiwa unakopi mafaili kutoka kwenye kompyuta kwenda kwenye simu

Kuna matoleo ya aina mbili ya hii simu upande wa memori na zote zikiwa na ukubwa wa RAM wa GB 8

Kuna yenye ukubwa GB 256 na ya GB 512na hazina sehemu ya kuweka memori ya zaidi

Kama GB 256 ni ndogo kuweka mafaili mengi basi GB 512 inafaa lakini bei yake itakuwa kubwa zaidi

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy S23+

Bodi yake imeundwa na glasi ya Gorilla Victus 2 upande wa nyuma na mbele

Na upande wa pembeni simu imewekwa aluminium

Vioo vya Gorilla Victus 2 vimeundwa kuhimili kupasuka inapoangushwa kwenye sehemu mbaya

samsung galaxy s23+ showcase a

Kampuni ya gorilla wanasema kuwa toleo hili linachagizwa na kuongezeka kwa uzito wa simu

Kwenye majaribio yao kioo hakikuvunjika pale simu ilipoangushwa kwenye kimo cha mita 1

Huu ni kama urefu wa rula tatu za sentimita 30

Unaweza pitia hapa kuona majaribio ya kuangusha simu zenye victus 2

Kiujumla hii ni simu yenye bodi imara, hata ukipanga kuiuza baada ya miaka miwili bodi yake itabaki kama ilivyo kwa kiwango kikubwa

Ubora wa kamera

Simu ina kamera tatu yaani samsung macho matatu

Ambapo ina kamera aina ya ultrawide, telephoto na ultrawide

Ukibwa wa lenzi unatofautiana na kamera iliyopo kwenye S23 Ultra

samsung galaxt s23+ kamera

Ultra kamera yake ni kubwa yenye ukubwa wa 200MP wakati hii ina ukubwa ina ukubwa 50MP

Ila ubora wa picha pia ni mkubwa kwani megapixel pekee si kigezo cha kutoa picha bora

samsung galaxt s23+ kamera 2

Aina ya ulengaji inayotumia ni dual pixel pdaf ambayo imetumika pia kwenye simu iPhone 14 Pro Max

Dual pixel pdaf na yenyewe inaweza kukitambua kitu kinachostahili kupigwa picha kwa haraka

Simu ina utulivu kwenye kurekodi video kutokana na uwepo wa OIS(Optical Image Stabilization)

Kamera zake zinaweza kurekodi video zenye resolution kubwa za 8K na 4K kwa ubora mkubwa

Ubora wa Software

Samsung Galaxy S23+ inakuja na toleo la Android 13 na mfumo wa One UI 5.1

Moja ya kitu cha kuvutia kwenye One UI 5.1 ni uwezo wake wa kujibu simu ukiwa unaendesha gari ama ukiwa umelala

Simu ikipigwa huku ukiwa unaendesha au umelala, one ui 5.1 itajibu kwa njia ya maandishi yaani meseji

Kuna uboreshaji wa salama wa data zako kwenye Android 13

Matoleo ya nyuma ya android yalikuwa yanaruhusu app kuweza kufanya kazi hata simu ikiwa imelokiwa

Hivyo app za kutrack simu zilitumia huu mwanya, ila android 13 mfumo umebadilika.

Kwani simu ikilock basi kila kitu kinajifunga

Pitia Hapa: Vitu Vipya Kwneye Android 13

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy S23+

Galaxy S23+ haina sehemu ya kuweka memori za ziada

Pia hakuna sehemu ya kuweka earphone hivyo bluetooth itahusika

Na ikumbukwe bluetooth earphone nzuri hugharimu kiasi kikubwa ch pesa

Simu haiji na chaji hivyo kama hukuwahi miliki chaji yenye kasi itakulazimu ununue

Neno la Mwisho

Iwapo bajeti yako ni ndogo kuwa na Galaxy S23 Ultra, basi Samsung Galaxy S23+ ni mbadala mzuri

Kwani ufanano ni mkubwa na kuna vitu vichache ambavyo S23+ haina

Lakini kama bado pesa haitoshi utalazimika kuangalia brand zingine kama Xiaomi ama Tecno

Kuna Xiaomi 12 Pro na Tecno Phantom X2 Pro, kama hizo hazikuridhishi basi Sony lakini pia bei ni kubwa

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu Samsung Galaxy S23+ na Sifa Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram