SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Tecno Phantom X2 Pro na Ubora Wake (2023)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

January 19, 2023

Kampuni ya Tecno Mobile imeanza mwaka 2023 kwa kuja na simu mpya ya Tecno Phantom X2 Pro

Kama una mawazo kuwa tecno ni tecno tu hata iweje basi jua simujanja hii ni kali japo bei imechangamka

Kwani bei ya Tecno Phantom X2 Pro ni zaidi ya milioni moja, inashangaza.

tecno phantom x2 pro box

Tecno hii ni tofauti na tecno zote ambazo umewahi ona ama kusikia

Kwenye posti hii kuna ufafanuzi wa vitu muhimu vilivyoongeza ubora wa hii simu, fuatilia.

Bei ya Awali ya Tecno Phantom X2 Pro

Tecno Tanzania hawajatangaza bei yake hapa nchini

Ila nchini India bei yake imeainishwa kuwa ni shilingi 1,500,000/= (milioni moja na laki tano) za Tanzania

Ni moja ya simu ya bei kubwa ya Tecno.

Hii inatokana na mambo mengi ikiwemo kutumika kwa moja ya chip yenye nguvu kubwa duniani

tecno phantom x2 pro platform summary

Processor hii inaifanya simu kufanya kazi kwa haraka.

Lakini pia hii ni simu ya tecno itakayokuwa inapata matoleo mapya ya Android kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2023 mapka 2025

Matoleo mapya yanaifanya simu kupokea teknolojia mpya za Android

Sifa za simu ya Tecno Phantom X2 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Dimensity 9000
  • Core Zenye nguvu kubwa(1) – 1×3.05 GHz Cortex-X2
  • Core Zenye nguvu (3) – 3×2.85 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.80 GHz Cortex-A510
  • GPU-Mali-G710 MC10
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • HIOS 12
Memori UFS 3.1, 256GB na RAM 12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 50MP, PDAF(telephoto)
  3. 13MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 5160mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 1,500,000/=

Upi ubora wa Tecno Phantom X2 Pro

Ni simu yenye nguvu kubwa kiutendaji

Phantom X2 Pro ni simu janja inayokubali mtandao wa 5G

Ina ugumu unaoweza kuepusha simu kupasuka inapodondoka

Betri yake ni kubwa na inapeleka chaji kwa kasi

Ina muundo unaovutia kuushika na kimuonekano

Ina aina tatu za kamera zenye kutoa ubora mzuri wa picha

Pamoja na hayo mapungufu ni machache sana kama utakavyoona

Uwezo wa Network

Hii simu inasapoti mitandao yote ikiwemo 5G

Vodacom Tanzania inayo mtandao wa 5G kwa baadhi ya maeneo kwa mkoa wa Dar Es Salaam

Upande wa 4G inatumia LTE aina ya LTE Cat 24.

LTE Cat 24 inaweza kupakua kitu kwa kasi inayofika 3000Mbps ambayo ni sawa na 375MBps

tecno phantom x2 pro network

Kwa mfano kama unadownload faili la MB 375 itachukua sekunde moja tu kumalizika

Lakini kasi ya simu inategemea na uwezo wa mtandao wa simu husika.

Ni changamoto kuipata kasi hiyo kwa hapa Tanzania upande wa 4G ila 5G inawezekana

Simu ina masafa yote yanayotumika hapa nchini hivyo mitandao yote itakubali

Ubora wa kioo cha Tecno Phantom X2 Pro

Kioo cha Tecno Phantom X2 Pro ni aina ya AMOLED chenye resolution 1080 x 2400 pixels

Aina hii ya kioo huwa inafanya vitu viwe “sharp” na rangi kuwa yenye kukolea

Vioo vya amoled huwa vinaonyesha vitu kwa rangi zake halisi kwa kiasi kikubwa hasa rangi nyeusi

Kitu kingine ambacho kioo chake inacho ni refresh rate inayofikia 120Hz

tecno phantom x2 pro display

Kiwango hiki hufanya simu kuwa nyepesi(smooth) unapokua unatachi kioo kwa kupeleka juu na chini (scroll)

Kwa bahati kioo chake hakina teknolojia ya HDR10 ambayo huboresha vitu na kuvifanya vionekane kwa usahihi kama vinavyoonekana na jicho la binadamu

Ni kitu cha kuzingatia kwa sababu simu nyingi za bei ghari huweka HDR10

tecno phantom x2 display for photoshop

Upande wa uangavu, simu ina kiwango kidogo kwani nits zinafika 500.

Ambapo simu kama Redmi Note 10 nits zake zinaenda mpaka 1000.

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 9000

X2 Pro inafungua app kwa haraka na kufungua app nyingi kwa wakati mmoja bila simu kupata shida

Uwezo wake unaiwezesha simu kucheza gemu ya aina yoyote kwa graphics zenye ubora mkubwa

Magemu huwa yanahitaji chipset yenye nguvu

Phantom inatumia processor ya MediaTek Dimensity 9000

tecno phantom x2 processor perfomance

Kiuwezo, inaendana na chip iliyotumika kwenye Samsung Galaxy S22 ambayo ni Snapdragon 8 gen 1

Snapdragon 8 gen 1 iko kwenye ligi moja na processor yenye nguvu zaidi duniani kwa sasa kutoka apple (Apple A16 Bionic)

Dimensity 9000 imegewanyika katika sehemu tatu upande wa core

  1. Core yenye nguvu sana moja (1×3.05 GHz Cortex-X2)
  2. Core yenye nguvu zipo tatu (3×2.85 GHz Cortex-A710 )
  3. Na core zenye nguvu ndogo zipo nne (4×1.80 GHz Cortex-A510)

Core zenye nguvu ndogo ni kwa ajili ya matumizi yasiyohitaji nguvu kama kupiga, kutuma sms nk

Inasaidia kupunguza matumizi makubwa ya betri kwani core zenye huwa zinakula chaji nyingi

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Tecno Phantom X2 Pro ina ukubwa wa 5160mAh

Hii betri inakaa na chaji lakini si kwa kiwango kikubwa

Inashangaza betri yenye ujazo wa zaidi 5000mAh kushindwa kutunza chaji kwa masaa 14 simu ikiwa inaperuzi intaneti muda wote

tecno phantom x2 pro chaji

Kwa mujibu wa GSMArena Phantom X2 Pro inadumu kwa muda wa masaa 12 ikiwa inaperuzi muda wote

Chaji ina wati 45 lakini inajaa kwa 39% ndani ya nusu saa, sio muda wa kuridhisha kwa chaji ya 45W

Ila hiyo inachangiwa na betri kuwa kubwa sana pia

Ukubwa na aina ya memori

Simu ya Phantom ina toleo moja yenye ukubwa wa memori 256GB na RAM ya GB 12

Na simu haiji na sehemu ya kuweka memori kadi

GB 256 ni nyingi ila memori ina umuhimu wake pia

Memori inayotumia ni aina ya UFS 3.1 ambazo huwa na kasi inaypfika 1200MBps

Kasi hii inasaidia simu kukopi faili kwa haraka na pia kuendana na kasi ya mtandao wa 5G

5G huwa inadownload vitu kwa kasi hivyo inahitaji memori yenye kasi kubwa pia kusafirisha data

Uimara wa bodi ya Tecno Phantom X2 Pro

Kwenye skrini simu inalindwa na kioo cha Corning Gorilla Victus

Kwa mujibu kampuni ya gorilla, hiki kioo kilijaribiwa kuangushwa kwa urefu wa mita 2 toka juu kwenye eneo baya

Lakini simu haikupasuka.

Na kiuharisia vioo vya gorilla ni himilivu na vigumu kupasuka

tecno phantom x2 pro bodi

Ila upande wa nyuma una plastiki

Kwa bahati mbaya simu haina viwango vya IP vinavyoonyesha uwezo wa kutopitisha maji simu ikizama kwenye maji

Simu zinazouzwa kwa gharama kubwa huwa wanaweka aina hii ya ulinzi

Ulinzi unaokupa uhuru wa kuitumia simu hata kwenye mvua

Ubora wa kamera

Tecno Phantom X2 Pro ina jumla ya Kamera tatu (tecno macho matatu)

Kuna kamera ya kupiga vitu ambavyo vipo mbali sana na kamera ya simu

Kamera hii huitwa Telephoto ina 50MP

tecno phantom x2 pro camera

Na pia ina kamera ya kupiga eneo pana sana, hii huitwa (Ultrawide)

Na pia ina kamera ya kawaida inayopiga vitu vya karibu na vilivyopo kwenye upana wa wastani

Hii inaitwa Wide na ina 50MP

Kiujumla kamera zake zote zinapiga picha vizuri kwenye mazingira yote ya mwanga hafifu na mchana

tecno phantom x2 photo quality

Ila inatatizo moja ambalo ni Dynamic Range

Kwneye mwangaza mwingi, rangi ya vitu uhalisia wake unapungua kama maji, rangi ya blue uweupe unazidi

Ama nyakati zingine mtu anatokea anang’aa sana kuliko anavyoonekana

tecno phantom x2 photo quality 3

Kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa fremu 30 kwa sekunde

Ubora wa Software

Tecno Phantom X2 Pro inatumia mfumo endesh wa Android 12 na software ya HiOS 12

Android 12 imeshazungumziwa sana

Ila HiOS 12 inakuja na vitu vingi ikiwemo AI Gallery 5.0

tecno phantom x2 pro

AI Gallery 5.0 huu ni mfumo wa utambuzi unaweza kuziweka picha zinazoendana sehemu moja kwa hiyo huhitaji kuzipanga picha bali AI Gallery inaweza fanya hivyo

Huu mfumo unatumia teknolojia ya Artificial Intelligence (Akili bandia kwa kiswahili kisicho rasmi)

Kwa maana simu inakuwa na akili ya kutambua kuwa picha hii ina kitu fulani kinachoendana na kitu kilichopo kwenye picha nyingine

Yapi Madhaifu ya Tecno Phantom X2 Pro

Kasoro kubwa ya hii simu ni kukosekana kwa IP67 au IP68

Ukiona alama za IP67 au IP68 inamaanisha simu haipitishi maji wala vumbi

Tecno wamefuata njia ya iPhone kwa kutoa sehemu ya kuweka memori kadi

Ukaaji wa chaji hauwendani na ukubwa wa betri kwani inazidiwa na simu ya iphone 14 pro ambayo betri yake ni 4300mAh

Kioo(display) chake hakina HDR10+ na uangavu wake ni wa wastani

Neno la Mwisho

Tecno wanaendelea kuimarika na uthibithsho ni toleo la Phantom X2 Pro

Lakini kuna TATIZO.

Bei ya Tecno Phantom X2 Pro inaendana kwa kiasi kikubwa na simu ya Xiaomi 13 Pro

Vitu ambavyo havipo kwenye Phantom hii vinapatikana kwenye Xiaomi 13 Pro

Hii inamaanisha tecno wanaenda kukumbana na ushindani mkubwa kutoka kwa makampuni mengine

Inabidi tecno mobile wajitathmini kuhusu bei za vifaa vyao

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram