SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 9 na Sifa Muhimu 2023

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 16, 2023

Tecno Spark 9 ni simu ya mwaka 2022 ambayo haina tofauti sana na Tecno Spark 10 ya 2023

Ni simu ya bei nafuu hata kwa mwaka huu ikizingatiwa ina toleo la android 12

Bei ya Tecno Spark 9 kwa Tanzania haizidi laki tatu na nusu kulingana na eneo na ukubwa wa memori

Unafuu wa bei unasababishwa na simu kuwalenga watu ambao hawatumii simu kwa vitu vinavyohitaji nguvu kubwa

Hivyo tarajia sifa nyingi zenye ubora wa kawaida sana

Bei ya Tecno Spark 9 ya GB 128

Tecno Spark 9 ya GB 128 kwa Tanzania inauzwa kwa shilingi 340,000

Ni mara chache kukuta simu yenye ukubwa wa GB 128 kuuzwa kwa bei ya chini ya laki nne

Zipo sababu nyingi hasa za kuitendaji, spark 9 ni simu ya toleo la daraja la chini

Uwezo wake hauwezi ukawa mkubwa kama Tecno Spark 10 Pro au simu ya Vivo Y22

Kuna watu matumizi yao ya simu ni kwa ajili ya mitandao ya kijamii na mawasiliano

Aina hii ya watumiaji ndio hii simu inawalenga, zifuatilie sifa zake uifahamu kiundani

Sifa za Tecno Spark 9

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Helio G37
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.3 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • HIOS 8.6
Memori eMMC 5.1, 64GB,128GB na RAM ,6GB,3GB, 4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 13MP,AF(wide)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 340,000/=

Upi ubora wa Tecno Spark 9

Simu inakuja na kioo chenye refresh rate kubwa hivyo unapotachi inakuwa na mwitikio mzuri

Betri yake ni kubwa inayoweza kukaa na chaji muda mrefu bila kuisha haraka

Ina kioo na chip ambazo zinatumia umeme kidogo wa betri

Ina bei inayovumilika kwa watu wengi wenye bajeti ndogo ya kununua simu

Memori yake ni kubwa inayoweza kuhifadhi mafaili mengi

Ni simu ya 4G hivyo nguvu ya intaneti si mbaya

Sifa zingine ni za kawaida ama za chini kama utakavyoona kwenye hii post

Uwezo wa Network

Tecno Spark 9 ina uwezo wa kutumia network mpaka ya 4G

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 7 yenye kasi ya 300Mbps ambayo ni sawa na 37.5Mbps

Kama unadownload gemu ya Call of duty ya GB 2 kule playstore simu itachukua sekunde 54 kumaliza kudownload

Kitu cha kuzingatia ni kuwa ili upate kasi hii basi kampuni ya mtandao wa simu inabidi uwe una kasi kubwa

Kwa Tanzania sio rahisi kuipata 4G yenye kasi hii

Simu ina masafa yote ya mitandao ya simu iliyopo hapa nchini

Hivyo laini zote zinafanya kazi bila tatizo linapokuja swala la intanet

Ila ukilinganisha na simu kama ya oppo A78 kwenye network, utofauti ni mbingu na ardhi

Ubora wa kioo cha Tecno Spark 9

Spark 9 inatumia kioo cha IPS LCD chenye refresh rate ya 90Hz

IPS LCD ni vioo ambavyo huwa zina taa kwa nyuma zinazosaidia screen kuonyesha vitu

Tofauti na vioo vya amoled ambavyo huzalisha mwanga vyenyewe bila kutumia taa

Ndio maana rangi nyeusi kwenye amoled hukorea sana tofauti na IPS LCD

Resolution ya simu ni ndogo pia kwani ni 720 x 1600 pixels

Kwa miaka ya karibuni simu za kawaida huwa zinakuja na 1080 x 1600 pixels ambayo huwa na muonekano wa rangi za vitu uliokolea vizuri

Ila kumbuka spark 9 ni simu ya bei nafuu sio rahisi kuwa na vitu vingi vya kuvutia

Nguvu ya processor MediaTek Helio G37

Kwenye ufanyaji kazi, spark 10 inatumia processor mediatek helio g37 toka kampuni ya mediatek

Processor ndio ubongo wa vifaa vya kielektronik kama simu na kompyuta

Mediatek helio g37 ina core nane, nne za mwanzo zina kasi inayofika 2.3ghz na zingine nne zina 1.8ghz

Ila zote zinatumia muundo wenye utendaji mdogo wa Cortex A53

Kwa mpenzi wa magemu atapata wakati mgumu kucheza magemu makubwa kwa uzuri

Uwezekano wa simu kupata joto ni mkubwa unapocheza gemu la PUBG

Kutokana na uwepo wa Cortex a53 inafanya simu kutumia uememe mdogo

Kwa sababu haitumii nguvu kuwa

Uwezo wa betri na chaji

Simu inakuja na betri ya 5000mAh

Hiki ni kiwango kitakachofanya simu kukaa muda mrefu na chaji hata ukiwa unatumia intaneti

Ila simu haina fast chaji hivyo itachukua muda mrefu kujaa ukizingatia betri ya simu ni kubwa

Yote yote ukaaji wa chaji ni wa kiwango cha kuridhisha

Ukubwa na aina ya memori

Tecno spark 10 inatumia memori aina ya eMMC ambazo kasi zake sio kubwa kama UFS

Kuna matoleo matatu ya spark 9 upande wa memori

Matoleo mawili yana GB 64 na toleo moja lina GB 128 na mgawanyo wa RAM ni GB 3, 4 na 6

Kiwango cha memori kinatosheleza kabisa kuhifadhi mafaili mengi

Na hata kama ikijaa simu ina sehemu ya kuongeza memori kadi ya ziada

Uimara wa bodi ya Tecno Spark 9

Bodi ya tecno spark 9 ni plastiki upande wa nyuma na pembeni

Simu haina uwezo wa kuzuia maji iwapo ikidumbukia kwenye mkusanyiko wa maji mengi

Lakini pia uwezo wa kuzuia vumbi ndani ya simu haupo kutokana na kutokuwepo na viwango vya IP

Hivyo ni muhimu kuwa makini na simu hasa utumiapo kwenye mazingira yenye maji au mvua

Na ni vizuri ukaweka kava ili ubora wa plastiki usipungue kwa haraka

Ubora wa kamera

Simu ina kamera mbili ila kamera ya pili haijainishwa aina ya lenzi inayotumia

Ila kamera kubwa ina megapixel 13 bila uwepo wa teknolojia ya PDAF ambayo ni ya kawaida kwa simu nyingi siku hizi

Kiwango cha megapixel sio kibaya kwani simu kama iphone 13 pro max kamera yake ina megapixel 12 na inatoa picha nzuri

Hii ina maana megapixel sio kigezo pekee cha kamera nzuri kuna vigezo vingi ambavyo spark 9 inakosa

Kwa kuangalia mfumo mzima kwa kamera ya hii simu ni kuwa ina ubora wa kawaida

Upigaji wake wa picha hauwezi ukawa wa kiwango kikubwa kama Tecno Camon 19 Pro

Ubora wa Software

Tecno Spark 9 inakunja na mfumo wa Android 12 na HiOS 8.6

Ukiwa na HiOS 8.6 inakuwezesha kubadilisha video kuwa audio

Kwa mfano umepakuwa video ya wimbo wowote hutokuwa na haja ya kudownload app ya kubadilisha video kuwa audio kwa simu inakuja nayo

Kitu kingine ni HiOS 8.6 inakupa nafasi ya kuongeza ukubwa wa RAM

Kwa mfano kama unanunua spark 9 ya ram bg 3, hii ram sio kubwa lakini inaweza kuongezwa

Lakini haitoshi ni mfumo unaokuletea app ya kuhariri video utakazokuwa unarekodi kwenye simu yako

Changamoto ya mfumo huu ni kuwa una matangazo mengi ya notification.

Yapi Madhaifu ya Tecno Spark 9

Kama ilivyotangulia kuelezwa ni kuwa hii ni simu ya bei nafuu hivyo vipo vitu vingi vyenye ubora wa kawaida

Moja, ni chip kutokuwa na utendaji mkubwa hasa kwenye magemu

Kamera zake sio za kuvutia na haina kamera ya ultrawide

Simu inatumia aina ya memori ambayo kwa sasa wakati wake unapita

Siku hizi simu nyingi zinatumia walau UFS 2.1 na sio eMMC

Neno la Mwisho

Spark 9 ni simu janja ya mwaka 2022 ila bado inafaa hata kwa mwaka 2023

Ukiangalia matoleo mapya ya tecno spark 10 utaona kuwa kuna tofauti ndogo na tena unakuta kwa kiwango kikubwa zipo sawa

Basi kama bajeti yako ni ndogo sana sio mbaya ukajivutia hii simu kusukuma siku

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram