SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Vivo Y22 na Sifa Muhimu (2023)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 13, 2023

Vivo Y22 ni simu iliyotoka mwaka 2022 mwezi septemba

Hii ni simu ya daraja la kati hivyo ina baadhi ya vitu vyenye ubora wa kuridhisha nyingine ni za kawaida

vivo y22 showcase

Hivyo basi bei ya vivo y22 ni chini ya laki tano kwa hapa Tanzania

Ni moja ya simu ya bei nafuu zinazozalishwa na kampuni ya Vivo japo inakosa vitu vingi vilivyopo kwenye Samsung Galaxy A34 5G

Bei ya Vivo Y22 ya GB 64

Kwa Tanzania, vivo y22 inauzwa kwa gharama ya shilingi 400,000/=

Hii bei inaendana na simu ya Tecno Spark 10 Pro ya mwaka 2023, na simu zenye tabia zinazofanana nyingi

vivo y22 summary

Inavyoonekana bei za simu zimeongezeka kwa kutazama sifa za vivo y22 hasa upande wa utendaji

Kwani utendaji wake ni wa kati kutokana na aina ya chip utakayotumia

Ila hii ni moja ya simu za bei rahisi yenye kamera yenye unafuu

Kufanya maamuzi ya kuimiliki, inabidi uelewe sifa zote za hii simujanja kwenye kila kipengele

Sifa za Vivo Y22

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Helio G85
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 12
  • Funtouch 12
Memori 128GB,64G na RAM 6GB,4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.55inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 400,000/=

Upi Ubora wa Vivo Y22

Kamera yake inajitahidi kutoa picha nzuri kwa kiasi fulani ukizingatia na bei yake

Ukaaji wa chaji ni mkubwa na wa masaa mengi

Inaruhusu kuongeza ukubwa wa ram, hivyo utaweza fungua mafaili mengi bila shida

Ni simu inayokuja na sehemu ya kuweka earpgone na pia ina redio

Maana simu za madaraja ya juu yamesitisha kuweka redio na sehemu ya earphone

Na inapatikana kwe bei inayovumilika

Kiujumla ni simu iliyopo kati kwa kati ikitegemeana na aina ya matumizi yako

Fuatalia mada ya yote uwelewe nini kinachomaanishwa

Uwezo wa Network

Uwezo wake wa network unaishia kwenye mtandao wa 4G tu

4G yake ni aina ya LTE Cat 7 yenye kasi ya 300Mbps ambayo ni sawa na 37MB/s

Kwa maana kama unapakua gemu ya Call of duty kule play store yenye GB 2 karibu sekunde 60 kumaliza kudownload

vivo y22 network

Ila hii inategemea na nguvu ya mtandao wa simu unaotumia

Kama kuna sehemu ina mtandao wa faiba usio na kikomo basi kasi hii unaifikia kwa urahisi

Ni kasi ya kawaida ukilinganisha na simu ya Oppo A78 5G

Ubora wa kioo cha Vivo Y22

Vivo Y22 inakuja na kioo cha IPS LCD chenye resoulution ya 720 x 1612 pixels

Hiki ni kiwango kidogo cha resolution ikizangitiwa vioo vya IPS LCD havifikii vioo vya AMOLED

Uonyeshaji wa vitu upande wa rangi si wa kuvutia hasa rangi nyeusi

vivo y22 display

Kwenye eneo ambalo hii simu ipo nyuma ni kioo

Kwani kioo chake hakina refresh rate kubwa ya 90Hz kama ilivyo kwa Tecno Spark 10 Pro

Kwa bei ya hii simu ilipaswa ije na kioo zaidi ya hiki ambacho wamekiweka

Ila wapo watu wanaozingatia vitu vingine kama ukaaji wa chaji zaidi kuliko muonekano wa vitu kwenye screen

Nguvu ya processor MediaTek Helio G85

Vivo Y22 inatumia processor ya MediaTek Helio G85

Ni chip nzuri ila sio nzuri kwa kufanya vitu vizito hasa kucheza gemu kwenye resolution kubwa

Ukicheza gemu kama Fortnite utalazimika kupunguza settings za graphics ziwe chini ili kuepuka kugandaganda na kucheza gemu kwa angalau fremu 21

vivo y22 processor

Kama ukiwa unaangalia video za 4K za youtube simu inakumbana na changamoto ya kuwa “slow”

Ila inafanya kazi kwa uzuri ukiwa unafanya kazi zingine na magemu mengine yanacheza  vizuri

Hivyo uwezo wa chip ni wa kawaida na hii inachangiwa na simu kutumia Cortex A75 kwenye core kubwa mbili

Inashangaza kwani core kubwa zenye utendaji unaoridhisha kiasi ni Cortex A78

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Vivo Y22 ina uwezo wa kupeleka umeme mpaka wati 18

Kasi ya wati 18 inajaza hii simu kwa masaa yanayokaribia matatu

Kasi hii sio kubwa kiivyo kwa sababu betri ya simu ni kubwa ina 5000mAh

vivo y22 charge

Ukubwa wa beti wa 5000mAh unaifanya simu kukaa na chaji masaa mengi

Kama ukiwa unaperuzi intaneti muda wote simu inachukua wastani wa masaa 12 mpaka chaji kuisha

Ukaaji wa chaji unachangiwa na processor kuwa na nguvu ya kawaida na kioo chake chengwe mwangaza wa wastani wa nits 500

Nits 500 inaweza kuonyesha vitu ukiwa unaitumia simu kwenye jua kali japo si kwa mwanga mkubwa

Ukubwa na aina ya memori

Hii simu zipo za matoleo mawili tu upande wa memori

Kuna ya GB 128 na RAM ya GB 6, na ya GB 64 na RAM ya GB 4

Ukubwa huu unaweza ukaifadhi mafaili mengi ila kama unadownload mafaili makubwa inaweza kujaza simu

Vivo hii ina sehemu ya kuweka memori kadi

Kwa maana simu ikijaa utaweza kuongeza memori kupitia memori kadi]

Chip iliyomo kwenye simu inakubali memori za aina yaani eMMC au UFS 2.1

Lakini haijaainishwa na aina ipi ya memori ambayo vivo y22 inatumia

Uimara wa bodi ya Vivo Y22

Kupata simu yenye viwango vya IP kwa bei ya chini ya laki tano sio kitu unachoweza kukiona mara kwa mara

Bodi ya vivo y22 inaweza kuzuia maji tiririka kwani ina IP5X na IPX4

vivo y22 body

Kwa maana pia simu inaweza kuzuia vumbi kupenya ndani ya simu

Upadne wa nyuma, simu imewekwa plastiki kimuonekana ni kama plastiki ngumu kuchunika

Lakini kiuhakika zaidi ni mpaka itumike muda mrefu ndio utajua kuwa  uimara wa plastiki yake hukoje

Haina kioo kigumu cha gorilla upande wa screen, sio mbaya hasa ukizingatia na bei yake kiujumla

Ubora wa kamera

Kwenye wa kamera hakuna vitu vingi muhimu na kuna kamera mbili tu

Kamera kubwa ina megapixel 50 na kamera ya pili aina ya macro ina megapixel 2

Kamera ya macro ni maalumu pale unapotaka kukipiga kitu ambacho kipo karibu sana na kamera ya simu

vivo y22 kamera

Ubora wa picha kwenye kamera kubwa ni kuridhisha kwenye mwanga mwingi

Ila kwenye mwanga haififu utendaji ni wa kiwango cha chini

Kwenye mwanga wa kutosha vitu vinaonekana vizuri japo kuna changamoto wa usahihi wa rangi

vivo y22 kamera 2

Kwa maana kamera inakuwa inang’arisha kitu tofauti na muoekano wake wa asili

Kwa mpenzi wa mitandao ya kijamii anaweza kuvutiwa nayo ila kamera bora huwa zinajitahidi kukitoa kitu kama kinavyoonekana

Upande wa video simu inaweza kurekodi video za full hd pekee yake kwani processor ya Helio G85 haina uwezo wa kuchakata video za 4K

Ubora wa Software

Simu ni ya mwaka 2022 hivyo ni ina Android 12, hakuna taarifa kama inaweza kupokea toleo la Android 13

Tutakutaarifu kama itawezekanika

Na pia ina mfumo wa vivo unaitwa Funtouch 12

vivo y22 software

Funtouch 12 haiji na applikesheni nyingi ambazo wewe huzihitaji kama ilivyo kwa mifumo mingine kama MIUI na HIOS

Pia ni mfumo unaoruhusu kuongeza kiwango cha RAM mpaka GB 1

Yapi Madhaifu ya Vivo Y22

Kama ilivyotangulia kuelezwa ni kuwa vivo y22 ni simu ambayo ipo kati kwa kati

Madhaifu yapo mengi na mazuri yapo pia, tutaeleza machache

Mfumo wa kamera unakosa kamera aina ya Ultrawide kwa ajili ya kupoga eneo pana

Utendaji wa chip ni wa kiwango cha wastani

Pia inatumia vioo vya lcd wakati kuna simu za bei ya laki nne zina vioo vya AMOLED mfano mzuri ni Redmi Note 10

Chaji yake haina kasi kubwa sana wakati simu nyingi za daraja kati unakutana na chaji ya wati 33

Neno la Mwisho

Vivo Y22 ni simu inayofaa kumzawadia mtu tena ambaye anapenda kupiga simu, intaneti, mitandao ya kijamii yaani matumizi ya kawaida

Kwa sababu ukaaji wa chaji ni mzuri

Ila kama unataka uwe unacheza magemu mengi, kufanyia kazi za kupiga picha, ni vizuri ukaangalia mbadala

Na izingatiwe bei ya hii simu inaipeleka kwenye ushidnani na matoleo mapya ya tecno moja kwa moja

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Vivo Y22 na Sifa Muhimu (2023)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu 14 mpya za Vivo za ubora mkubwa na bei zake (2024)

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka mwaka huu 2024 Vivo imeachia matoleo mengi ya simu Katika matoleo hayo yapo ya bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa Kwa maana […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram