SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Infinix Zero Ultra na Ubora Wake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

October 24, 2022

Simu ya infinix zero ultra ni simu nyingine ya 5G kutoka brand ya Infinix ya 2022

Utaweza kutumia mtandao wa 5G wa Vodacom kwa hapa Tanzania

Kwa kuwa ni moja ya simu bora ya 5G, bei ya infinix zero ultra inazidi shilingi milioni moja

infinix zero ultra

Uwepo wa teknolojia yenye kasi kubwa ya mawasiliano haitoshi kukujulisha ubora na kasoro zake hasa ukifananisha na simu zingine za 5G kutoka Samsund, Oppo, Xiaomi, Realme nk

Hivyo hii posti inafafanua kinaga ubaga sifa,bei na ubora wa infinix zero ultra

Bei ya Infinix Zero Ultra ya GB 256

Hii simu ya infinix ina toleo moja tu ambayo ina ukubwa wa GB 256

Bei yake inaanzia shilingi 1,500,000/= (milioni moja na nusu) kwa hapa Tanzania

infinix zero ultra summary

Simu inauzwa kiwango hiko kutokana na ubora wake kwenye kamera, display (kioo), chaji na utendaji

Changamoto kubwa kwa infinix zero ultra inakuja kwa washindani wake hasa Redmi Note 11 5G Pro Plus

Hizi simu mbili zinaendana kwenye nyanja nyingi ila redmi ina bei nafuu zaidi (shilingi 920,000)

Sifa za Infinix Zero Ultra

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 920
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.5GHz Cortex A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0GHz Cortex A55
  • GPU-Mali G68
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • XOS 12
Memori UFS 2.1,256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera TATU (macho matatu)

  1. 200MP,PDAF(wide)
  2. 13MP(ultrawide)
  3. 2MP
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-180W
Bei ya simu(TSH) 1,500,000/=

Upi ubora wa Infinix Zero Ultra

Ubora wa infinix umejikita zaidi kwenye spidi ya chaji na uwezo mkubwa wa processor

Ni moja ya simu inayochukua muda mfupi kujaza betri ya simu

Ina kioo kinachoonyesha vitu kwa ustadi

Ni simu mpya ambayo inakuja na mtandao wenye kasi zaidi

Ni simu ndefu na pana na yenye kamera iliyo na lenzi kubwa

Kiuhalisia infinix zero ultra ina kasoro ndogo sana

Hii inaweza ikawa ni SIMU BORA YA INFINIX katika simu zote walizowahi tengeneza mpaka sasa

Fuatilia kila kipengele ujue kwa nini

Uwezo wa Network

Baada ya kuzinduliwa kwa Infinix Note 12 VIP yenye 5G basi infinix wameweka tena 5G kwenye toleo jipya

Kununua simu ya 5G sio upotezaji wa pesa kwa sababu Tanzania ina huu mtandao

Inakubali aina zote za 5G ambazo ni SA, NSA na Sub-6

infinix zero ultra network

Vodacom Tanzania inatumia 5G aina ya NSA inayomaanisha Non Stand Alone

Kuelewa teknolojia hii ya mawasiliano inakubidi upitie, maana ya 5G

Kwa sasa kupata spidi inayofika 200Mbps ni kawaida hapa nchini ila si maeneo yote yenye 5G

Pia inakubali mtandao wa 4G na 3G vilevile

Ubora wa kioo cha Infinix Zero Ultra

Kioo cha infinix ultra zero ni aina ya AMOLED lakini sio Super Amoled

Vioo vya amoled huwa vinaonyesha rangi nyingi kitu kinachofanya vitu kuonekana kwa rangi zake sahihi kwa aslimi kubwa

Uzuri pia kioo chake kinakuja a refresh rate inayofikia 120Hz

zero ultra display

Umuhimu wa refresh rate kubwa ni simu kuwa nyepesi ukitachi kwa kuperuzi na pia gemu huchezeka vizuri

Pia resolution yake ni kubwa yenye pixels 1080 x 2400

Kadri kioo kinavyokuwa na pixels nyingi ndivyo simu inavyoonyesha vitu kwa ustadi

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 920

Processor ya Mediatek dimensity 920 inaifanaya simu ya infinix zero ultra kuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi bila simu kukwama kwama

Japokuwa kiuwezo haifikii simu ya iphone 14 pro max kwa sababu dimensity 920 ni chip ya kundi la kati

Kwenye app ya geekbench, dimensity ina alama 811

infinix zero ultra processor

Uwezo mkubwa wa processor yake unaweza kuonekana zaidi kwenye kucheza gemu

Kwani gemu nyingi zinaweza kucheza kwa fremu zaidi ya fremu 60 kwa muonekano wa Ultra HD

Nguvu kubwa inasababishwa na processor kutumia muundo wa Cortex A78 kwenye core mbili zenye nguvu zaidi

Na pia spidi ya mizunguko ya core kubwa kuwa ni 2.5GHz

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Infinix Zero Ultra inapeleka umeme unaofikia wati 180

Ni umeme mkubwa hivyo betri inachukuwa muda mchache kujaa

Kwa mujibu wa Infinix, chaji yake inajaa kwa DAKIKA 12

Hii ni zaidi ya fast chaji ukizangitia ukubwa wa betri ni 4500mAh aina ya Li-Po

Utunzaji wa chaji unaweza kuzidi zaidi ya masaa 14 ikiwa simu inatumia intaneti muda wote

Lakini swala la utunzaji wa chaji inategemea sana na aina ya matumizi

Kwa mcheza magemu betri huwai kuisha

Ukubwa na aina ya memori

Simu ya Infinix Zero Ultra ina toleo moja tu upande wa memori

Ukubwa wa memori ni 256GB na RAM ya GB 8

Aina ya memori haijainishwa ila chip ya dimensity 920 inasapoti memori aina ya UFS pekee

Hivyo usafirishaji wa data ni wa haraka na hivyo utendaji unaongezeka

Uimara wa bodi ya Infinix Zero Ultra

Hii simu inakuja na bodi ya kioo upande wa nyuma na mbele

Wenyewe infinix wanaita “Glass and Star Trail Design

Vyovyote vile, bodi za vioo huepusha rangi ya simu kuchunika kwa haraka

Ila haikuanishwa kama vioo ni vya aina ya Gorilla

Bahati mbaya simu haina ulinzi wa kuzuia maji kupenya ndani ya simu

Kikawaida simu za bei zaidi ya milioni huwa zinakuwa na IP ratings ambazo huonyesha uwezo simu kuzuia maji kupenya

Ubora wa kamera

Infinix Zero Ultra ina kamera tatu kwa jina lingine infinix macho matatu

Kamera kubwa zaidi ina megapixel 200

Kwenye mwanga hafifu picha zinaonekana kwa vizuri

Na kamera ya 200MP inakoleza zaidi rangi ukilinganisha na kamera ya kawaida ya kawaida ya 12MP

kamera infinix zero ultra 2

Ila zoom yake haitoi picha nzuri hasa ukiikuza picha mara 10

Inazidiwa mbali sana na simu ya samsung galaxy s22 ultra 5G

Sio kesi sana, kamera zake zina ulengaji unaoweza kukipiga kitu kilicho kwenye mwendo kwa usahihi mkubwa

Inatokana na kamera yake kuwa na ulengaji wa dual pixel pdaf

kamera infinix zero ultra

Upande wa video pia ni wa kuvutia

Kamera yake inaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa fremu 30fps

Ukirekodi video ukiwa unatembea bado itatokea vizuri bila kutingishika

Hii inatokana na kamera kuwekewa OIS (Optical Image Stabilization)

Ubora wa Software

Simu inakuja na android toleo la 12 ikiwa na mfumo XOS 12

Muonekano wa XOS 12 unakurahisishia kuingia apps za Instagram na youtube kwa haraka

Kwa maana zimeekwa kwenye folda moja kwenye home screen

xos infinix zero ultra

Hivyo ukiwasha simu mara ya kwanza utazikuta hizo apps kwenye screen

Kitu kingine ni kuwa XOS 12 inakupa uwezo wa kuongeza ukubwa wa RAM

Japokuwa RAM ya GB 8 inatosha sana kwa sasa ila kuna nyakati kiasi kikubwa cha RAM kinahitajika

Ukizingatia XOS 12 inakuja na applikesheni nyingi sana ambazo hutoweza kuzitoa

Yapi Madhaifu ya Infinix Zero Ultra

Kamera za Infinix Zero Ultra hazina optical zoom

Optical zoom hii ni aina ya zoom inayotumia lenzi kukikuza kitu cha mbali

Hivyo ubora haupotei ukilinganisha na zoom ya app ya simu

Kukosekana kwa IP67 ni kasoro nyingine

Simu kama Samsung Galaxy A53 ina IP67 hivyo haipitishi maji

Wakati huo galaxy a53 inapatikana kwa bei ya 800,000/=

Utatambua kasoro zingine za Infinix zero ultra kwa kuitazama simu ya Redmi Note 11 Pro+ 5G

Matumaini ni kuwa haya mapungufu yatarekebishwa kwenye matoleo mapya ya infinix

Neno la Mwisho

Infinix inazidi kupiga hatua katika kuzikabili simu za makampuni mengine

Na kwa sasa infinix inajaribu kulipata soko la 5G ambapo litashika kasi siku za mbeleni

Kasoro kubwa ya infinix ni kuwa simu zao nzuri zinakuwa na bei kubwa iliyopitiliza

Kitu kinachoweza kumshawishi mtumiaji wa simu kutafuta simu mbadala yenye sifa sawa au zaidi na kwa bei ya chini zaidi

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu ya Infinix Zero Ultra na Ubora Wake

  • Wanasimu nzuri Lakini kwanini nisinunue simu mbadala yenye sifa sawa nahiyo Lakini inabei nafuu? Ukilinganisha kwamba simu Bora zipo nyingi na infinix wanajitafuta

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram