SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya simu ya Samsung Galaxy A33 5G[Simu Mpya]

Simu Mpya

Sihaba Mikole

April 10, 2022

Simu ya samsung galaxy a33 5g ni simu ya daraja la kati inayoundwa na kamera nne.

Kwa jina lingine simu ya macho manne.

Galaxy A53 ni simu mpya ambayo imeingia sokoni aprili 2022

samsung galaxy a33 5g

Simu ina ubora mwingi kwenye display, utendaji wa processor na uimara wa kuzuia maji kupenya

Kiujumla, sifa zake zina ubora kwenye nyanja zaidi ya tano kama utakavyoona kwenye posti hii.

Bei ya Samsung Galaxy A33 5G Tanzania

Bei ya samsung galaxy a33 kwa baadhi ya nchi za asia inaanzia shilingi 825,ooo/=

Kwa Tanzania bei inaweza ikazidi kidogo pindi hizi simu zitakopoingia kwa wingi

Bei isikushtushe sana.

Kwa sababu ni samsung ya a-series yenye ubora kwenye sehemu nyingi karibu zote.

Ila kuna vitu simu inavikosa kama vinavyojionyosha kwenye jedwari linoloonyesha sifa

Sifa za Samsung Galaxy A33 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 1280
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.4GHz Cortex A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0GHz Cortex A55
  • GPU-Mali-G68
Display(Kioo) Super AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • One UI 4.1
Memori 128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.4inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 824,512.40/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy A33 5G

Kuujua ubora wa simu mpya ya samsung galaxy a33 5g tazama kioo chake.

Kioo cha simu kinazalisha rangi nyingi

Betri yake inakaa na moto muda mrefu

Taarifa za samsung galaxy a33

Simu ina utendaji wa kiwango cha kutosheleza

Ina ulinzi madhubuti kwenye screen, ulinzi unaoifanya simu kuwa ngumu

Hata sehemu zingine za simu zina ubora wa kuridhisha

Jifunze, vitu vya kuzingatia unaponunua simu yoyote

Kiubora, galaxy a33 inafanana vitu vingi na simu ya samsung galaxy a53 5g

Network

Samsung galaxy a33 inasapoti mitandao ya aina yote ikiwemo 4g na 5g

Simu ina network bands 15 za 4g ikiwemo bands zote zinazotumiwa na mitandao ya Tanzania

Zitambue: network bands za Tanzania za 4G

phone network a33 samsung

Kasi ya juu kabisa ya kudownload upande wa 4g inafikia 2Gbps

Na mtandao wa 5g una network bands 12.

5G ya samsung galaxy a33 inatumia 5g aina ya sub-6

Sub-6 hutumia miundombinu ya 4G kusafirisha data

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A33 5G

Kioo cha samsung galaxy a33 5g ni cha aina ya super amoled.

Samsung imepunguza refresh rate mpaka kufikia 90Hz

Wakati samsung galaxy a53 refresh rate yake ni 120Hz

Hata hivyo 90Hz inatosha kusukuma gemu kwa spidi inayoridhisha

Resolution yake pia ni nzuri aina ya FHD+(Full hd plus)

FHD+ ina pixel 1080 x 2400

Nguvu ya processor Exynos 1280

Exynos 1280 ni processor yenye nguvu kubwa.

Na gemu nyingi inasukuma bila simu kupata joto jingi.

Ila kuna magemu yenye graphics kubwa yanasababisha simu kupata joto.

Tazama hii video

https://www.youtube.com/watch?v=NXSFYISsZHU

Tumeifafanua hii processor kinaga ubaga kwenye kurasa ya galaxy a53

Uwezo wa betri na chaji

Simu ya samsung galaxy a33 5g inatumia betri kubwa la aina ya Li-Po

Betri ina ukubwa wa 5000mAh

Na simu inaweza kupitisha umeme mwingi wa wati 25

Kwa bahati mbaya simu haiji na chaji.

Hivyo ukinunua itakulazimu kununua chaji yake.

Sababu wanazozisema Samsung ni ulinzi juu ya mazingira.

Binafsi, haingii akilini bali ni mbinu mpya ya biashara

Ukubwa na aina ya memori

Ipo aina moja tu ya samsung galaxy a33 5g upande wa memori

Samsung a33 utakayoimiliki itakuwa na ukubwa wa GB 128

Na ram yenye ukubwa wa 8GB

Ni sazi inayotosha kuhifadhi mafaili na app nyingi

Na ram ya GB 8 inasaidia simu kufungua mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa urahisi

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A33 5G

Upande wa screen simu ina kioo cha gorilla 5

Kwa mujibu wa corning waundaji wa vioo vya gorilla, gorilla 5 ni kioo kigumu kuvunjika endapo simu ikidondoka kwa urefu wa mita 1.2

Upande wa nyuma kuna plastiki.

Hii ni simu mpya nyingine ya 2022 isiyopitisha maji kwa muda wa nusu saa endapo ikizamishwa kwenye maji ya kina cha mita moja

Kiuhalisia galaxy a33 ina bodi ngumu na imara inayoweza kudumu muda mrefu

Ubora wa kamera

Simu ina kamera nne

Kati ya kamera hizo ni moja tu yenye teknolojia ya OIS

Na simu inatumia autofocus ya kawaida aina ya PDAF

Kwa bahati mbaya kamera za samsung galaxy a33 hazina kamera ya telephoto.

kamera ya samsung galaxy a33

Hivyo mtumiaji wa simu atategemea digital zoom inayoweza kuzoom mara 10.

Changamoto ya digital zoom ni picha kupungua resolution

Upande wa video simu inaweza kurekodi video aina za 4k na full hd kwa spidi ya kawaida

Ubora wa Software

Simu inatumia android 12 na skin ya One UI 4.1

Ukiwa na one ui 4.1 utaweza kuongeza ram (2gb, 4gb, 6gb au 8gb)

Waakti android 12 imeongeza kitu kipya kwenye kuscreenshot.

Utaweza ku-screenshot ukurasa mzima kwa ukubwa utakaotaka

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A33 5G

Simu haiji na chaji hivyo utalazimika kununua chaji kutoka kwa samsung kama hauna chaji aina ya USB C

Pia samsung galaxy a33 haina sehemu ya earphone.

Hivyo utalazimika kununua adapter kama utahitaji kutumia earphone

Kamera zake hazitumii teknolojia bora za autofocus aina dual pixel pdaf au multidirection pdaf

Haina kamera aina telephoto na wala haina optical zoom

Neno la Mwisho

Simu ya samsung galaxy a33 5g ni moja ya simu bora ya daraja kati

Lakini mapungufu iliyonayo machache yanamshawishi mtu kutazama chaguao lingine.

Kwa mfano simu ya redmi note 11 pro+ 5g inachuana na matoleo mapya ya samsung kwenye kila kitu

Lakini ukitaka simu imara kwenye kila nyanja na ya bei rahisi, samsung galaxy a33 5g ni simu ya kuimiliki

Maoni 7 kuhusu “Ubora na bei ya simu ya Samsung Galaxy A33 5G[Simu Mpya]

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram