SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya simu ya Samsung Galaxy A32 na Sifa Zake [2022]

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 6, 2022

Simu ya samsung galaxy a32 ni simu ya daraja la kati ambayo imetoka 2021

Pamoja na simu kutimiza mwaka ila galaxy a32 ina vitu vingi ambavyo vinakosekana kwenye baadhi ya simu mpya za 2022

Changamoto ni kuwa bei ya samsung galaxy a32 ni kubwa kuliko uhalisia

samsung galaxy a32

Kwani kwa Tanzania bei yake inazidi laki sita

Hii post itakaonyesha bei yake kutokana na ukubwa wa memori na sifa zake

Na utajua simu zingine zenye sifa zinazoizidi a32 kwenye nyanja na zenye bei nafuu zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A32 Tanzania

Bei halisi ya samsung galaxy kwenye masoko ya mtandaoni hasa amazon ni shilingi 533,341.00/=

Ila kwa Tanzania bei ni kubwa mara dufu kwa maduka mengi ya simu

Kwa mfano maduka mengi ya kariakoo wanaiuza simu kwa shilingi 700,000/=

Hii inasababishwa na aina ya kioo na uimara wa bodi

Lakini sifa za kiujumla za kiutendaj zinaifanya simu kutoendana na bei inayopatikana kwa sasa

Sifa za simu ya samsung galaxy a32

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek  Helio G80
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 11
  • One UI 3.1
Memori 128GB,64GB na RAM 8GB,6GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
  4. 5MP(depth)
Muundo Urefu-6.4 inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 700,000/=

Upi ubora wa samsung galaxy a32

Ubora wa samsung galaxy a32 upo hasa kwa kiasi kikubwa kwenye ubora wa kioo

Kioo chake kina ufanisi mzuri wa uonyeshaji vitu kwa rangi stahiki

Ina utendaji unaoweza kufungua app za kila aina bila simu kupata joto jingi

samsung galaxy a32 summary

Inakaa na chaji masaa mengi kutokana na kuwa na betri kubwa

Simu ina na memori kubwa inayoqweza kuhifadhi app na mafaili mengi

Ni moja ya samsung yenye kamera inazokupa machaguo mengi ya kupiga picha ama kurekodi video

Uwezo wa Network

Samsung galaxy a32 ni simu ya 4G aina ya LTE Cat 7

LTE Cat 7 spidi yake ya juu ya kupakua ni 300Mbps

samsung galaxy s32 network

Iwapo mtandao wa simu unakupa spidi basi simu inaweza kudownload faili la ukubwa wa 1200MB kwa sekunde 40

Uzuri ni kuwa galaxy hii ina nmasafa ya 4G yapatayo 10

Hivyo 4G ya mitandao ya smile, ttcl, tigo, halotel, airtel na vodacom itakubali kwenye simu hii

Ubora wa kioo cha samsung galaxy a32

Kioo cha samsung galaxy a32 ni cha super amoled

Super amoled hutongezwa na kampuni ya samsung yenyewe

Vioo vya amoled huwa na ufanisi mkubwa wa kuonyesha rangi hasa rangi nyeusi

Hiyo inatokana na vioo kuwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Pia ubora wake umeongezwa na kuwa na resolution kubwa ya 1080 x 2400 pixels

Na pia refresh rate ya 90Hz

Refresh rate kubwa inafaya simu kuwa nyepesi wakati wa kutachi

Tazama hii video uone utofauti kati ya simu yenye refresh rate ya 90Hz na 60Hz

Nguvu ya processor MediaTek Helio G80

Galaxy A32 inatumia chip ya MediaTek Helio G80 kufanya kazi zake

Helio G80 ni processor ya simu ya daraja la kati

Utendaji wake ni wastani kwani si mkubwa sana kama simu ya samsung s21 ultra

Kwani app ya antutu inaipa alama 231,000 na geeekbench 5 inaipa alama 353

samsung galaxy a32 processor

Ila ina uwezo wa kucheza gemu nyingi kwa ubora wa Full HD na kwa spidi inayozidi 30fps

Uwezo wa wasatani unachangiwa hasa na aina ya muundo wa core kubwa na core ndogo

Uwezo wa core kubwa

Helio G80 ina core zinazofanya kazi kubwa sana zipatazo mbili

Hizi core spidi yake ya juu ni 2.0 GHz ambayo ni ndogo kwa core kubwa nyingi

Spidi hiyo inamaanisha chip inaweza kufanya kazi kwa mizunguko bilioni mbili kwa sekunde

Na kila mzunguko mmoja unafanya kazi zipatazo 3

Kwa sabau zimetengenezwa kwa muundo wa Cortex A75

Wakati cortex A76 inafanya kazi nne kwa mzunguko mmoja

Uwezo wa core ndogo

Simu ya samsung galaxy 132 ina jumla ya core ndogo zipatazo sita

Simu inazitumia hizi core ikiwa inafanya kazi inayotumia nguvu ndogo

Kwa mfano kupiga simu, kutuma sms, kuchati whatsapp nk

Spidi ya juu kabisa ya kila core ndogo ni 1.8 GHz na zina muundo wa Cortex A55

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya galaxy a32 ina ukubwa wa 5000mAh

Kutokana na simu kuwa na utendaji wa wastani unafanya ukaaji wa chaji kuwa mkubwa

Simu nyingi zenye betri za 5000mAh hukaa na chaji masaa yanayoweza kuzidi 15

Kwa bahati mbaya simu ina spidi ndogo ya kuchaji

Kutokana na chaji yake kupeleka umeme usiozidi 15W kama kiwango cha juu

Hivyo betri inaweza kuchukua muda mrefu kujaa

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo manne ya samsung a32 upande wa memori

Kuna galaxy a32 ya 64GB na ram ya 4GB

Kuna ya 128GB na ram ya 4GB

Glaxy a32 ya 128GB na ram ya 6GB

Na kubwa kabisa ya 128GB na ram ya 8GB

Uimara wa bodi ya samsung galaxy a32

Bodi ya samsung galaxy a32 upande wa mbele imewekewa ki00 cha gorilla 5

Kuna majaribio mengi ambayo yameonyesha ugumu wa gorilla 5 kupasuka

samsung galaxy a32 bodi

Kwani inaweza simu inaweza isivunjike endapo ikianguka kwa kimo cha mita mbili kutoka juu

Lakini upande wa nyuma simu inatumia bodi ya plastiki

Hivyo kava ni muhimu kuepusha kuchunika kwa rangi

Ubora wa kamera

Simu ina jumla ya kamera nne

Kamera kubwa ina resolution ya 64MP

Ila kamera yake haiwezi kurekodi video za 4K

samsung galaxy a32 kamera

Na ulengaji sio mkubwa kutokana na simu kutumia autofocus ya PDAF badala ya dual pixel pdaf

Ina kamera aina ya ultrawide inayoweza kupiga na kurekodi eneo pana kwa nyuzi 123

Ubora wa Software

Simu ya samsung galaxy a32 ni simu ya android 11 inayokuja na software ya One UI 3.1

Katika software za android one ui huzishinda softaware nyingi

Ni nyepesi na ina vitu vingi bila kuwa na matangazo mengi

Yapi Madhaifu ya samsung galaxy a32

Simu haina uwezo wa kuzuia maji kwa sababu haina viwango vya ip67

Simu nzuri za matoleo ya kati huwa na angalau IP53

Kamera zake si za kuvutia

Kwani zina rekodi ubora wa full hd kwa kasi ndogo

Lakini pia, zinatumia teknolojia ya ulengaji ambayo kwa sasa inapitwa na wakati ya PDAF

Chaji yake inapeleka umeme mdogo unaojaza betri kwa masaa mengi

Neno la Mwisho

Bei ya samsung galaxy a32 kwa Tanzania inaweza kununua simu ya redmi note 10 5G na chenji ikabaki

Kiubora galaxy a32 inaachwa mbali na redmi kwenye swala la utendaji

Kiukweli simu zenye processor ya Helio G80 hazipaswi kuzidi laki nne

Maoni 3 kuhusu “Bei ya simu ya Samsung Galaxy A32 na Sifa Zake [2022]

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram