SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Maana ya 4K [Upande wa kamera ya simu].

Miongozo

Sihaba Mikole

May 11, 2022

Kama wewe ni mtu wa kusoma mabox ya TV utakuwa umeshwawahi kuona neno limeandikwa 4K

Hivyo utakuwa unajiuliza hasa nini maana ya 4k

4K ni aina ya ni aina ya resolution ambayo yenye idadi ya pixels zaidi ya milioni nane

Kwa maana inakuwa na idadi ya pixels 3800 kutoka kushoto kwenda kulia

Na pixels 2600 kutoka juu kwenda chini

Nini maana ya Pixels

Pixel ni nukta ndogo ambayo huwa na mchanganyiko wa rangi msingi tatu

Rangi hizo ni nyekundu, kijani na bluu

Mchanganyiko wa rangi wa hizo nukta ndio unatengeneza picha na video ambazo unaziona kwenye screen ya TV, Projector au Simu

Hizi nukta zikiwa nyingi ndivyo ubora wa muonekano wa picha au video unakuwa mzuri

4K kwenye kamera za simu

4K kwenye simu hutumika na kamera kurekodi video

Simu nyingi zina resolution za aina mbili tu

Huwa hazina screen za 4K kwa sababu kwenye haina umuhimu sana kutokana na udogo wa smartphone

Kwa hiyo simu hurekodi video hizo kwa ajili ya kutazama kwenye TV

Simu nyingi za madaraja ya kati na ya juu zinaweza kurekodi video za 4K kwa kasi ya 30fps, 60fps na hata 120fps

Kwa nini simu za bei rahizi hazirekodi 4k?

Kwanza unaporekodi video za 4K processor ya simu huwa inatumia nguvu kuchakata data za video

Kwa sababu inafanya mahesabu ya uchanganyaji wa rangi wa pixels zaidi ya milioni nane

Hivyo simu inahitajika kutumia chip yenye nguvu kubwa

Kwa bahati mbaya simu za bei rahisi huundwa na kamera zenye ubora haififu

Na pia zinatengenezwa na processor ambazo zina utendaji wa chini

Hivyo mwisho wa siku kamera za simu zinashindwa kabisa kurekodi video za 4K

Je video ya 4K inachukua nafasi kubwa?

Jibu la haraka haraka ni ndio

Kadri video inapojuwa na resolution ndivyo inavyochukuwa nafasi kubwa ya memori

Hii inatokana na resolution kubwa na pixels nyingi

Kwa maana nafasi kwenye kamera ya kawaida ni ndogo

Wakati ukirekodi kwa 4K inaweza kuchukua nafasi mara mbili zaidi

Tena memori inayochukuliwa inakuwa kubwa kama 4K inarekodiwa kwa frames zaidi ya 60 fps kama 120 fps

Je 4K ni bora kuliko Full HD na HD?

Jibu la kiujumla 4K ni bora kuliko aina zingine za video ikiwemo full hd

Lakini hii inategemea na vitu vingine vya zaidi

Iwapo kamera inayorekodi kwa full hd inaweza kurekodi ikiwa inatumia HDR10+

Basi hiyo kamera ya simu itatoa video yenye ubora wa juu kuliko kamera ya 4K ambayo haina HDR10+

Jina lingine la 4K

4K pia hufahamika kama Ultra HD (UHD) pia inafupishwa Ultra

Kwa hiyo ukiona neno UHD basi jua kuwa ni kitu kimoja na 4K

Simu zenye kamera za 4K

Hizi ni baadhi ya simu kutoka makampuni mbalimbali ambazo zimewezeshwa kamera zinazoweza kurekodi video za 4K (UHD)

Samsung Galaxy S21 Ultra

Simu ya samsung galaxy s21 ultra ina jumla ya kamera tatu

Kamera kuu zake zinaweza kupiga video za aina zote ikiwemo 8K na 4K pia

Pia kamera ya selfie ya samsung galaxy s21 inaweza kurekodi video za 4K vilevile

iPhone 13 Pro Max

iPhone 13 pro max ni simu ambayo ina kamera tatu kama ilivyo kwa galaxy s21 ultra

Kamera zake na zenyewe zinaweza kurekodi video za 8K na 4k

Pia selfie kamera na yenyewe inaweza kurekodi video za 4K vilevile

Redmi Note 10

Hii ni simu ya kamera nne

Inaweza kurekodi video za 4K kwa spidi ya 30fps

Ila selfie kamera haina uwezo kutoa video ya 4K

Oppo Find X3 Pro

Kamera za oppo find x3 pro zinarekodi video za ubora wa 4K kwa kasi inayofikia 60 fps

Kwa bahati mbaya kamera yake ya selfie zinarekodi video za full hd pekee

Tecno Camon 18 Premier

Hii pia ni simu yenye kamera ya 4K inayoweza kurekodi kwa kasi ya 30 fps

Ila selfie inarekodi video za 1080p pekee

Simu zingine za 4K ni Infinix Zero X Pro, Vivo X80 Pro, Xiaomi 12 Pro, OnePlus 10 Pro, Realme GT2 Pro

Maoni 4 kuhusu “Maana ya 4K [Upande wa kamera ya simu].

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram