SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sifa za simu ya Nokia C30 [Sifa nzuri na Mbaya]

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 6, 2022

Simu ya Nokia C30 ni simu nzuri ya bei nafuu iliyotoka mwaka 2021.

Kiubora, simu haina ubora wa viwango vya iPhone 13 Pro Max au Galaxy C30

Lakini kwa kuangalia bei yake na sifa zake zinaifanya kuwa simu yenye ubora wa kati.

Baadhi ya vitu vina ubora mdogo na mengine yanavutia unaposoma sifa za nokia c30

Sifa za Simu ya Nokia C30

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Unisoc SC9863A
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×1.6 GHz Cortex-A55
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.2 GHz Cortex-A55
  • GPU-IMG8322
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
  • Go edition
Memori eMMC 5.1, 32GB, 64GB na RAM 3GB,2GB
Kamera Kamera mbili

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.82inchi
Chaji na Betri
  • 6000mAh-Li-Po
Bei ya simu(TSH) 253,691.32/=

Upi ubora wa Nokia C30

Simu hii ya Nokia ina betri kubwa.

Betri yake inaisadia simu kukaaa na chaji muda mrefu

Aina ya hardware za simu zinatumia umeme mdogo.

Simu ni ndefu.

Urefu unaokuonyesha vitu kwa ukubwa kwenye screen

Network

Nokia c30 inakubali mtandao wa 4G

Aina ya 4G iliyopo kwenye simu ni LTE Cat 7

LTE Cat 4 spidi yake ya kudownload inaweza kufikia 301Mbps

Ni spidi inayoweza kudownload file la ukubwa wa 1300MB kwa sekunde 40 inategemea na spidi ya mtandao husika

Simu ina network bands 10 tu za 4G.

Mitandao ya simu Tanzania yote itakubali kwenye simu hii

Ubora wa kioo cha Nokia C30

Kioo cha nokia c30 ni aina ya IPS LCD

Kiubora IPS LCD inazidiwa na vioo vya amoled unapozungumzia utajiri wa rangi

Resolution ya simu ni ya kawaida isiyoendana na viwango vya sasa

Kwani ina ukubwa wa 720×1600 pixels

Kioo kina nits chache na refresh rate ndogo

Refresh na resolution ndogo zinatumia umeme mdogo

Nguvu ya processor Unisoc SC9863A

Kila kazi inayofanyika kwenye simu ya Nokia C30 inachakatwa na processor ya Unisoc SC983A

Processor ya Unisoc SC983A ina core nane(octacore)

Hizo sehemu nane zimegawanyika mara mbili.

Kuna core kwa ajili ya kazi kubwa

Na core kwa ajili ya kazi ndogo

Uwezo wa Core kubwa

Core kubwa zipo nne

Kila core ina spidi ya 1.6GHz

Core zote zimeundwa kwa muundo wa Cortex 55

Processoe zenye nguvu hutumia cortex 55 kwenye core ndogo.

Hii inamaanisha Unisoc SC983A ni procesor yenye nguvu ndogo

Hata kwenye geekbench ina alama ndogo.

Kiuhalisia si chip nzuri kucheza gemu

Uwezo wa Core ndogo

Core ndogo zipo nne na zina muundo wa cortex a55

Huu ni muundo sawa na ule wa core kubwa.

Kinachotautiana ni spidi.

Core ndogo zina spidi ya 1.2GHz

Spidi ni ndogo zaidi

Uwezo wa betri na chaji

Nokia C30 ina betri aina ya Li-Po yenye ukubwa wa 6000mAh

Betri hili litakaa na chaji kwa masaa mengi.

Kitu kimoja wapo kinachokula chaji kwenye simu huwa ni processor

Processor ikiwa na nguvu ndogo basi matumizi ya umeme hupungua pakubwa

Lakini ubora wa simu pia huwa mdogo.

Nokia C30 haina fast chaji.

Kwa hiyo betri lake litajaa kwa muda mrefu

Ukubwa na aina ya memori

Nokia c30 inatumia memori aina ya eMMC  5.1.

eMMC  5.1 ina spidi ya taratibu katika usafirishaji wa data ukilinganisha na memori UFS

Hivyo basi baadhi ya app zitafunguka taratibu.

Na simu kuchelewa kuwaka

Kuna aina tatu za nokia c30 upande wa memori

  1. 32GB 2GB RAM
  2. 32GB 3GB RAM
  3. 64GB 3GB RAM

Ni ukubwa kwa kiasi unaohifadhi mafaili mengi

Uimara wa bodi ya Nokia C30

Bodi ya hii simu ya nokia imeudwa kwa plastiki upande wa nyuma na kwenye fremu

Na ina ulinzi wa kioo kwenye screen.

Lakini sio kioo cha gorilla

Bodi za plastiki si imara pale simu inapoanguka.

Mtumiaji analazimika kununua kava kuilinda simu bila kusahau screen protector.

Umakini unahitajika wakati wa kununua screen protector.

Wafanya biashara wengi Tanzania wanauza screen protector nyepesi kupasuka

Ubora wa kamera

Kuna kamera mbili tu upande wa nyuma.

Kamera aina ya depth na wide.

Kamera zote hazitumii teknolojia nzuri za kamera aina ya dual pixel pdaf

Kumbuka kamera ya depth haipingi picha

Bali hupima umbali kati ya kamera na kitu kinachpigwa picha ili kamera ilenge kwa usahihi

Ubora wa video

Simu inaweza kurekodi aina moja tu ya video zenye ubora wa full hd.

Video za full hd zinarekodiwa kwa spidi ya 30fps

Ni spidi ndogo ukilinganisha na uwezo wa kamera ya simu ya iPhone SE 2022

Ubora wa Software

Nokia c30 ni simu ya android 11 inayotumia android aina ya Go Edition

Anadroid Go Edition ni mfumo endeshi wa android uliotengenezwa kwa ajili ya simu zenye nguvu ndogo kiutendaji.

Ni mfumo unaolenga simu zenye RAM ndogo chini ya 2GB.

Ni mfumo unaotumia data kidogo ya data.

Simu hii isingeweza kuhimili aina zingine za android kutokana na uwezo mdogo iliyo nayo.

Bei ya Nokia C30 Tanzania

Bei ya nokia c30 kwenye masoko ya dunia inauzwa shilingi 254,000/= za Tanzania.

Baadhi ya maduka ya kariakoo wanauzaa hii simu kwa bei 300,000/= mpaka 350,000/=

Sio simu mbaya ila kwa bei yake unapata simu nzuri inayoizidi hii.

Tazama hapa: Simu za bei rahisi

Yapi Madhaifu ya Nokia C30

Simu ina nguvu ndogo ya kiutendaji kwa sababu ya processor ndogo

Nokia hii haina kamera ya telephoto na ultrawide.

Nokia c30 haiwezi kurekodi video za 4K

Simu inakosa fast chaji hivyo betri inachukua muda kujaa

Bodi yake imeundwa kwa plastiki ambazo zina kawaida ya kuwahi kuchunika.

Mtumiaji wa hii simu atalazimika kununua screen protector kutokana na simu kutokutumia vioo vya gorilla

Neno la Mwisho

Kwa mtu mwenye bajeti ndogo ya simu basi nokia c30 inaweza msaidia kusukuma siku.

Lakini kama unazingatia utendaji hii ni simu ya kuachana nayo.

Kwa wapenzi wa screen kubwa nokia c30 itakidhi hitaji lako

Kiujumla simu ya c30 inamfaa mtu anayeanza kutumia smartphone

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

samsung fold 4 camera

Simu 10 Zenye Kamera Nzuri na Bora 2023

Mwaka 2023 yapo mateo ya simu yaliyoingia sokoni yakiwa na kamera nzuri na bora kwa kupigia picha na kurekodi video Kuna simu zenye kamera kali zaidi na mfumo mzuri kwenye […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram