SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Brand

Sihaba Mikole

March 8, 2024

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024

Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024

Tusubiri tuone, hata hivyo hapa kuna baadhi ya simu mpya za nokia zilizotoka mwaka 2023

Pamoja na kutoka 2023 bado ni simu mpya kwani hakuna toleo jipya kwa sasa la mwaka huu

Nokia C210

Bei ya Nokia C210: 260,000/= ,Ukubwa wa Memori: 32GB, RAM:  3GB

Simu ya Nokia C210 ni toleo la hivi karibuni kabisa la Nokia lilitoka mwezi agosti 2023

Ni simu ya daraja la chini na utendaji wake sio mkubwa

nokia c210

Inatumia chip yenye nguvu ndogo ya Snapdragon 662

Nokia C210 kioo chake ni cha IPS LCD chenye resolution 720p ambayo ni viwango vya kawaida sana kwa nyakati za sasa

Hii simu inamfaa kwa mtumiaji mwenye matumizi madogo ya simu

Nokia G310

Bei ya Nokia G310: 490,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Nokia G310 ni nokia ya 5G na yenyewe iliingia sokoni mnamo mwezi wa nane ya mwaka 2023

Kioo chake kina resolution ndogo

Nokia G310

Utendaji wake unachagizwa na chip ya Snapdragon 480+ 5G

Hii ni chip ya daraja la chini yenye mtandao wa 5G

Ina kamera tatu ambapo kamera kubwa ina megapixel 50 bila kuwa na ulengaji wa PDAF

Nokia 150 (2023)

Bei ya Nokia 150: 120,000/= ,Ukubwa wa Memori: 4MB, RAM:  

Simu ya Nokia 150 (2023) ni simu ya batani ambayo imetoka 2023

Betri yake ni ndogo ukizingatia simu za batani huwa hazitumii moto mwingi

nokia 150

Hata memori yake ni ndogo kwani ina MB 4

Kwa maana hiyo mnunuaji wa hii simu hana budi kununua memori kadi ya ziada

Kwa wapenzi wa simu za batani basi hili ni chaguo zuri

Nokia G42

Bei ya Nokia G42: 430,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Simu nyingine ya daraja lachini yenye 5G ambayo ilitoka mwezi juni 2023

Utendaji wake sio mkubwa kutokana na kutumia chip ya Snapdragon 480+ 5G

nokia g42

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh na chaji yake ina kasi ya kupeleka umeme wa 20W

Hivyo kwa kiasi fulani betri haitochukua muda mrefu kujaa

Kamera zake zina lenzi za wide, ultrawide na macro na kamera kubwa ina megapixel 50

Nokia C300

Bei ya Nokia C300: 350,000/= ,Ukubwa wa Memori: 32GB, RAM:  3GB

Betri ya Nokia C300 ukubwa wake ni mAh 4000

Na chaji yake inapeleka umeme wa wati 10

Nokia C300

Pamoja na udogo wa betri simu inaweza kuchukua masaa mengi kujaza betri

Kamera zake zipo tatu na kamera kubwa ina megapixel 13

Kiujumla mfumo wake wa kamera sio wa kutoa picha nzuri ukifananisha na simu za samsung s-series

Nokia C110

Bei ya Nokia C110: 280,000/= ,Ukubwa wa Memori: 32GB, RAM:  3GB

Simu ya Nokia C110 ni nokia ya daraja la chini yenye utendaji mdogo kati ya nokia nyingi zilizoorodheshwa

Kitu kinachofanya kuwa na utendaji wa chini ni kuwa na processor ambayo ina nguvu ndogo

nokia c110

Nokia C110 inatumia processor ya Mediatek Helio P22

Hii simu inalenga watumiaji ambao wana matumizi ya kawaida ya simu na wale ambao hawana bajeti ya kumiliki simu janja zenye bei kubwa

Lakini ndio hivyo simu za bei nafuu huwa zina changamoto ya utendaji nmdogo

Nokia XR21

Bei ya Nokia XR21: 1,700,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Kati ya simu nyingi za nokia zilizopo kwenye orodha Nokia XR21 ina ubora unaoendana na viwango vya simu nyingi za sasa

Ila bei yake ni kubwa kwa sababu inaendana na simu zenye ubora mkubwa kuliko hii nokia

nokia xr21

Unaweza kuziona hizi simu hapa: Simu mpya matoleo ya 2024

Nokia XR21 inatumia processor ya Snapdragon 695 5G na utendaji wake ni wa wastani

Ina kamera mbili za wide na ultrawide huku kamera yenye ulengaji wa PDAF ina megapixel 64

Chaji yake inapeleka umeme wa wati 33, hivyo betri haichukui muda mrefu kujaa

Nokia C12 Pro

Bei ya Nokia C12 Pro: 240,000/= ,Ukubwa wa Memori: 64GB, RAM:  2GB

Simu nyingine ya daraja la chini ya nokia ambayo inawafaa wenye matumizi ya kawaida

Inatumia chip iliyotengenezwa na kampuni ya china ya Unisoc SC9863A1

Nokia C12 Pro

Unisoc SC9863A1 utendaji wake sio mkubwa hivyo usitarajie ubora mkubwa kutoka kwa Nokia C12 Pro

Kioo chake ni cha aina IPS LCD chenye resolution ndogo ya HD

Kamera yake moja ubora wake sio mzuri

Hii simu ina kamera moja tu upande wa nyuma

Nokia C32

Bei ya Nokia C32: 780,000/= ,Ukubwa wa Memori: 64GB, RAM:  4GB

Simu ya Nokia C32 ina ufanano wa kiwango kikubwa na Nokia C12 Pro

Tofauti kubwa inapatikana upande wa kamera

nokia c32

Nokia C32 ina kamera nzuri kidogo na ina ukubwa wa megapixel 50

Betri yake ukubwa ni 5000mAh ila chaji yake haina kasi kubwa

Chaji inapeleka umeme wa wati 10 tu

Nokia C22

Bei ya Nokia C22: 680,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Nokia C22 pia ni moja ya nokia ya bei nafuu ambayo na yenyewe utendaji sio mkubwa kivile

Kwani processor inayotumia haina nguvu kutokana na kuwa na core ndogo kwenye kila sehemu

Nokia C22

Ni simu inayomfaa mtumiaji mwenye matumzi ya wastani

Ila kama unapenda kamera nzuri Nokia C22 sio chaguo zuri

Kwani ina kamera mbili na moja ukubwa wake ni 13MP

Kioo chake kina resoltuion ya 720 x 1600 pixels ambayo sio kubwa kwa viwango vya sasa

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram