SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sifa za simu ya Infinix note 11 Pro [Madhaifu na Ubora]

Sifa za simu

Sihaba Mikole

March 26, 2022

Unafahamu kuwa simu ya infinix note 11 Pro ni simu inayoweza shindana na simu nyingi za tabaka la kati?

Hilo linatokana na aina ya processor(chipset) simu inayotumia.

Infinix note 11 Pro inaweza ikawa moja ya simu ya infinix yenye kamera nzuri.

picha ya simu ya infinix note 11 pro

Ukizitazama sifa za infinix note 11 pro utaona kuwa simu ina kioo kizuri na mfumo wa betri ulio imara kwa spidi ya kuchaji.

Note 11 Pro imekamilika kwenye idara nyingi na mapufungu yapo machache.

Sifa za infinix note 11 pro kiufupi

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G96
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.05 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 11
  •  XOS 10
Memori UFS 2.2, 128GB na RAM 8GB, 4G
Kamera Kamera tatu

  1. 64MP,PDAF(main)
  2. 13MP(telephoto)
  3. 2MP(depth)
  4. 16MP(selfie camera)
Muundo Urefu-6.95inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 650,000/=

Upi ubora wa simu ya Infinix note 11 Pro?

Ubora wa simu ya infinix unapatikana hasa kwenye processor, kioo, upana na urefu wa simu pamoja na mfumo wa chaji.

Infinix note 11 Pro inakuja na chaji inayojaza simu kwa muda mfupi.

Kimakadirio betri inaweza kujaa ndani ya dakika 70.

Kioo cha infinix note 11 pro kina refresh rate kubwa.

Simu inaweza kufungua app yoyote kwa urahisi kwa sababu ya processor yenye nguvu.

Kiubora hii simu inaikaribia simu ya infinix zero 5g

Kufahamu ubora wa simu hii kwenye kila nyanja iangazie simu katika nyanja nane zifuatazo.

Network

Infinix note 11 pro inakubali mtandao wa 4G.

4g yake ni ya kundi la 13 (cat 13).

network ya infinix note 11 pro

Ambayo spidi yake ya juu kudownload ni 390Mbps

Simu haina modem inayosapoti 5g

Kwa Tanzania hakuna mtandao wa simu wowote wenye minara ya 5G.

4G ya infinix note 11 pro inasapoti network bands 12 kati ya 24.

Kwa maana simu inaweza kutokubali 4g za baadhi ya mitandao.

Ila kwa Tanzania inakubali intaneti ya 4G za mitandao yote.

4g Network bands zinazopatikana Tanzania

Bands za 4G zilizomo ndani ya Infinix note 11 pro ni 1, 2, 3, 4, 5, 7, 8, 20, 28, 38, 41 na 40

Ili laini ya simu ikubali mtandao wa 4g kwenye note 11 pro inapaswa iwe na moja ya hizo band.

Hizi hapa ni aina za 4g bands za mitandao mitano inayotumiwa sana Tanzania.

Halotel – 7

Vodacom- 3

AirTel- 28

Tigo- 20 na 3

TTCL- 3 na 40

Kiufupi laini za mitandao yote nchini zitafanya kazi vizuri tu.

Ubora Kioo cha infinix 11 pro?

Ininix 11 Pro inatumia kioo cha IPS LCD.

Display yake ni kubwa inayoweza onyesha vitu kwa ubora.

Hilo linachangiwa na resolution kubwa ya 1080 x 2460 pixels

Hiki kioo ni kizuri kwa wapenzi wa magemu.

Kwa sababu kina refresh rate inayofikia 120Hz.

kioo chs infinix note 11 pro

Refresh rate ikiwa kubwa simu inakuwa nyepesi hasa ukiwa una-scroll kwenda juu au chini.

Uangavu wa kioo si mkubwa.

GSMArena walipima uangavu wake unaofikia 470nits.

Kwenye jua kali screen inaweza isionyeshe vitu vizuri.

Nguvu ya processor ipoje?

Simu ya infinix note 11 pro inatumia processor yenye utendaji mkubwa.

Processor yake ni MediaTek Helio G96.

processor ya simu ya infinix note 11 pro

Mifumo inayopima nguvu za processor kama 3DMark na geekbench inaonyesha MediaTek Helio G96 inazipita baadhi ya processor za Snapdragon.

Helio G96 ina core nane.

Kuna core zenye nguvu na zenye uwezo wa kawaida.

Uwezo wa Core zenye nguvu

Core zenye nguvu sana zipo mbili.

Kila core ina spidi ya 2.05 GHz

Core zote zinatumia muundo wenye nguvu aina ya Cortex A76.

Pitia maelezo ya kina yanayofafanua aina ya processor za simu zenye nguvu.

Cortex A76 inafanya utendaji wa simu kuwa sawa na baadhi ya laptop kama ARM Holding wanavyodai.

Muudo wa Cortex A76 una utendaji mkubwa na matumizi madogo ya betri ukilinganisha Cortex A73.

Uwezo wa core zenye nguvu ndogo

Ubora wa core ndogo unaangaliwa kwenye matumizi madogo ya betri.

Helio G96 ina core ndogo sita.

Kila core ina spidi ya 2.0 GHz

Na core zote zinatumia muundo wa Cortex A55.

ARM Holding wanasema Cortex A55 imeongeza utendaji kwa asilimi 18.

Na imeongeza utunzaji wa chaji kwa 15% ukilinganisha na Cortex A53.

Cortex A53 imetumika kwenye processor ya Helio G35 inayopatikana kwenye simu ya Xiaomi Redmi 9C.

Mpangalio wa processor ya Helio G96 unafanya simu ya Infinix note 11 pro kukaa na chaji muda mrefu.

Na utendaji mkubwa unaotumia umeme kidogo

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya infinix note 11 pro ni aina ya Li-Po yenye ujazo wa 5000mAh.

Chaji ya infinix note 11 pro inapeleka umeme wa wati 33.

Umeme wa wati 33 unaweza jazi betri ya ukubwa 5000mAh ndani ya dakika 75.

Lakini chaji ya infinix note 11 pro inajaza simu kwa dakika 125 (pitia hapa)

Infinix note 11 pro ni moja ya simu inayotunza chaji muda mrefu.

Ikiwa haitumiki simu inakaa na chaji masaa 128.

Simu ikiwa inatumia intaneti betri inaisha baada ya masaa 17 na dakika 34

Ukubwa na aina ya memori

Infinix note 11 pro inatumia memori aina ya UFS 2.2

Ni mfumo unaosafirisha data kwa kasi kubwa.

Kasi inayofanya simu kuwaka na kungua app kwa sekunde chache.

Memori za simu zina ukubwa wa 128GB.

Ukubwa unaweza kuhifadhi mafaili na app za kutosha.

Kuna infinix note 11 pro ya 4GB RAM na 8GB RAM.

RAM kubwa inasaidia simu kufungua vitu vingi kwa wakati mmoja bila kukwama.

Na RAM ya simu ni aina ya LPDDR4X

LPDDR4X ni aina ya RAM inayotumia umeme mdogo kwa kusafirisha data kwa kasi kubwa.

Uimara wa bodi

Bodi ya infinix note 11 pro ni plastiki upande wa nyuma na fremu.

Na display imewekewa glassi lakini sio vioo vya gorilla.

Mara nyingi plastiki haziwezi kuhimili kupasuka endapo simu imeanguka kwa kimo kirefu.

Hii simu ni ndefu inakaribia inchi 7

Na ina uzito wa gramu 209

Ubora wa kamera

Kamera za infinix note 11 zipo tatu.

Camera-ya-infinix-note-11-pro

Kamera mbili zinatumia teknolojia ya autofocus(ulengaji) aina ya PDAF.

Aina ya kamera tatu ni

  1. Wide
  2. Telephoto
  3. Macro

Kwa kulinganisha na simu zingine zenye kamera nzuri hii simu ina ubora wa kawaida.

Telephoto inaweza kuzoom kwa kutumia lens(optical zoom) mara mbili

Ubora wa video

Simu inaweza kurekodi video zenye ubora full hd(1440) pekee kwa spidi ya 30fps

Ni tofauti na simu ya xiaomi 12 pro

Selfie camera pia inarekodi picha ubora wa full hd pekee

Ubora wa picha

Ukizitazama picha zilizopigwa na gsmarena infinix note 11 pro inatoa picha nzuri nyakati za mchana.

Noise ziko kwa kiasi kidogo japokuwa simu ina shida ya contrast kwa vitu ambavyo vipo mbali

Infinix note 11 pro inatoa picha nzuri nyakati za usiku pia.

Japokuwa kuna changamoto kidogo ya dynamic range.

Kwa sababu baadhi ya vitu rangi zinatawala pakubwa(exposure kubwa)

Kwa mfano uangavu wa taa ni mkubwa kiasi cha kutengeneza ukungu mweupe kwa mbali kwenye giza

Lakini kamera inatoa pivha safi kwa kiasi kikubwa

Ubora wa Software

Simu ya infinix note 11 pro inakuja na android 11

Android 11 inawezeshwa na software ya Infinix ya XOS 10

xos 10 infinix note 11 pro

Hakuna taarifa za infinix note 11 pro kupokea toleo jipya la Android 12

Kuna mapya mengi yameongezeka ambayo hayapo kwenye android 11

Infinix wanasema XOS 10 inafungua app kwa haraka.

Kwa maana ukitachi icon ya app basi ndani ya sekunde chache app inafunguka

XOS 10 ina theme nyingi za kuboresha muonekano wa simu

Bei ya infinix note 11 pro

Bei ya infinix note 11 pro inafika shilingi 650,000/= kwa Tanzania hasa maduka ya kariakoo

Wengine wanauza 620,000/= moja ya comment ya akaunti rasmi ya instagram infinix Tanzania ilionyesha

Simu ni nzuri lakini bei ni kubwa kidogo

Kwa nini?

Bei hii inakupa simu bora kuliko hii ya Redmi note 11 pro 5g

Baadhi ya simu zinazotumia processor mpya za dimensity zinapatikana kwa bei ya chini ya 450,000/=

Mfano mzuri ni Redmi note 10 5G.

Bei ya infinix note 11 inaweza nunua simu kali kila idara ya Samsung Galaxy A52

Yapi madhaifu ya Infinix note 11 Pro?

Simu zinazouzwa kuanzia laki sita na kuendelea hutumia chip zenye nguvu zaidi ya processor Helio G96.

Infinix hawajaweka ulinzi wa kuzuia maji kupenya ndani ya simu.

Kwa maana infinix note 11 pro inakosa viwango vya IP67

Kamera hazikuwekewa teknolojia bora zaidi za kulenga(autofocus) kama dual pixel PDAF.

Simu nyingi za tabaka la kati hutumia GPS zaidi ya moja.

Ila infinix note 11 pro inatumia GPS moja pekee.

Network yake ina bands chache za 4G hivyo baadhi ya mitandao duniani ikagoma kutumika kwenye simu.

Maoni 6 kuhusu “Sifa za simu ya Infinix note 11 Pro [Madhaifu na Ubora]

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

OnePlus 11R

Simu 15 za OnePlus na Bei zake (Aina zote)

OnePlus inaweza ikawa ni jina geni kwa watumiaji wengi smartphone Tanzania Ila OnePlus ni moja ya kampuni kutoka china inayotengeneza simujanja za madaraja ya kati na ya juu Simu nyingi […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram