SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Google Pixel 8 Pro na Sifa zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

October 18, 2023

Simu ya Google Pixel 8 Pro imezinduliwa mwezi wa kumi (oktoba) 2023

Ni simu ya daraja la juu kama ilivyo kwa iphone na samsung matoleo ya S-series

Kwa maana hiyo bei ya google pixel 8 pro inatarajiwa kuwa zaidi ya milioni mbili kwa Tanzania

2-google pixel 8 pro showcase

Pixel 8 Pro ina ubora katika maeneo mengi kitu kinachosaidia kutimiza mahitaji ya mtumiaji kwenye kila nyanja

Ila kubwa zaidi simu za google huwa na kamera nzuri kuliko hata washindani wake

Ili kuielewa ubora wa hii simu itabidi uelewe sifa zake kila moja

Bei ya Google Pixel 8 Pro ya GB 128

Google Pixel 8 Pro yenye GB 128 inauzwa shilingi za Tanzania milioni 2 na laki nane

Kwenye duka la mtandaoni la Amazon bei yake inaanzia milion 2.6

Kuna tofauti ndogo kwa muhitaji asiye na haraka anaweza akaagaza kwa maana inachukua muda kidogo mpaka kukifikia

Bei ya simu inaendana sana na sifa zake japo baadhi ya chambuzi zimeonyesha mapungufu kwenye utendaji hasa upande wa magemu

Ila kitu unachopaswa kuzingatia ni kuwa Google wamejikita zaidi katika software kuliko hardware

Sifa za Google Pixel 8 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Google Tensor G3
  • Core Zenye nguvu kubwa(1) – 1×3.0 GHz Cortex-X3
  • Core Zenye nguvu(4)-4×2.45 GHz Cortex-A715
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.15 GHz Cortex-A510
  • GPU-mmortalis-G715s MC10
Display(Kioo) LTPO OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
Memori UFS 3.1,256GB,128GB,512GB,1TB na RAM 12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP, multi-directional PDAF(wide)
  2. 48MP(ultrawide), dual pixel PDAF
  3. 48MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 5050mAh-Li-Po
  • Chaji-30W
Bei ya simu(TSH) 2,800,000/=

Upi ubora wa Google Pixel 8 Pro

Kioo cha pixel 8 pro kina uwanda mpana wa uonyeshaji kiwango kikubwa cha rangi

Chaji yake inajaza betri kwa muda mfupi

Pia betri yake ni kubwa

Kamera zake zinapiga na kurekodi video kwa ubora mkubwa

Inatumia mfumo wa memori wenye kasi kubwa ya kusafirisha data

Utendaji wa simu kiujumla ni wa kuridhisha

Ni simu inayosapoti aina mbalimbali za network kwa maana hadi 5G

Uwezo wa network

Google Pixel 8 Pro ni simu ya 5G ambayo inasapoti pia aina nyingine za mitandao

Inakubali karibu masafa yote yanayotumiwa na simu mbalimbali duniani

Kw maana hiyo hata 5G za Airtel, Tigo na Vodacom zitafanya kazi vizuri

Hii simu inakubali mpaka 5G ya masafa marefu yenye kasi zaidi

Ikumbukwe kuwa mitandao ya Tanzania inatumia yenye masafa ya kati

Na kwa bahati mbaya sio mikoa yote yenye network 5G

Kwa sehemu network hii ipo Dar Es Salaam na Dodoma kwa airtel

Na Dar pia na kwa maeneo machache.

Ubora wa kioo cha Google Pixel 8 Pro

Kioo cha google pixel 8 pro ni aina ya LTPO OLED chenye refresh rate ya 120Hz

LTPO inasaidia kioo kutotumia refresh rate kila wakati

Kuna aina ya matumizi ambayo hayahitaji refresh rate 120Hz

LTPO inaweza kuyaainisha na kuseti kiwango kidogo cha refresh rate

Kioo cha hii simu kina uwezo wa kuonyesha rangi kutokana na uwepo wa HDR10+

Uangavu wa kioo ukiwa nje unaweza kufika mpaka nits 1400

Hivyo vitu vitaonekana vizuri tu ukiwa unatumia simu kwenye mazingira ya jua kali

Simu zenye uangavu mdogo humpa mtumiaji wakati wa kuona vitu kwenye kioo kama ukiwa juani

Uzuri ni kuwa kioo cha hii simu resolution ni kubwa pia ambayo ni 1344 x 2992 pixels

Nguvu ya processor

Simu za google kwa sasa wanatumia processor wanazounda wenyewe

Processor inayoiwezesha google pixel 8 pro kufanya kazi zake ni Google Tensor G3

Google Tensor G3 imegawanyika sehemu tatu na ina idadi ya core zipatazo tisa(9)

Processor nyingi za simu huja na core 8 lakini hiki sio kigezo cha chip kuwa na utendaji

google pixel 8 pro chip

Kwani Google Tensor G3 imeonyesha kiwango cha chini kwa baadhi ya gemu ukilinganisha na washindani wake ambao ni Snapdragon 8 Gen 2 iliyotumika kwenye Samsung Galaxy S23 Ultra na pia Apple A17 Pro iliyopo kwenye iPhone 15 Pro Max.

Moja ya kitu kinachoshangaza ni ufanisi wa matumizi ya betri

Google Tensor G3 inakula chaji zaidi ya snapdragon na apple a17 pro

Kwenye app ya kupima nguvu za processor inayoitwa Geekbench, Google Tensor G3 ina alama 1700 ambazo kwa levo yake ni ndogo

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Google Pixel 8 Pro ina ukubwa wa 5050mAh

Ukiwa mtumiaji sana wa simu kuanzia intaneti, kuangalia video za youtube, kucheza gemu na mambo mengine hii simu inaweza kudumu mpaka masaa kumi(10)

Ni masaa mengi kwa wastani ila ukitazama bei ya simu na washindani wake ambao ni Samsung Galaxy S23 Ultra na iPhone 15 Pro Max, betri ya google iko nyuma kwa zaidi ya masaa mawili

Sababu kubwa inasababishwa na processor yake ya Google Tensor G3 kuwa na ufanisi usioridhisha(tutaangalia kiundani)

Kwenye upande wa chaji, simu inasapoti chaji ya wati 30

Ambayo inaweza kujaza simu kwa 50% ndani ya nusu saa

Kimakadirio simu inaweza kujaa kwa 100% ndani ya dakika 80 yaani lisaa na dakika 20

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo manne ya pixel 8 pro upande wa memori

Unaweza kumiliki ya GB 128, 256, 512 na 1TB zote zikiwa na GB 12

RAM kubwa ni msaada sana kwenye simu kwani utaweza kufanya vitu kwa wakati mmoja pasipo kuganda ganda

RAM ikiwa ndogo kuna nyakati inawahi kujaa hivyo unalazimika kufunga baadhi ya app na huwa inakera

Kwa viwango hivi vya memori utaweza kuhifadhi mafaili mengi wala hutokuwa na wasiwasi wa whatsapp kujaza mapicha mengi kutoka kwenye magrupu.

Uimara wa bodi ya Google Pixel 8 Pro

Bodi ya Google pixel 8 Pro imeundwa kwa vioo vya Gorilla Victus mbele na nyuma

Ni vioo vigumu kupasuka na kuchunika (Ni stahimilivu kiujumla)

Ukiizamisha pixel 8 pro kwenye maji ya kiwango cha ndoo ya lita 20 au diaba kwa muda wa nusu saa maji hayatoingia ndani ya simu

Ina viwango vya IP68 vinavyoashiria uwezo wa simu kutopitisha maji wala vumbi

Kwa maana hivyo hutokuwa na wasi ukiwa unaitumia kwenye mvua kubwa

Simu inakuja na laini moja huku laini ya pili ikiwa ni eSIM

Ni mitandao miwili hapa Tanzania inayosapoti eSIM ambayo ni Vodacom na Airtel

Ubora wa kamera

Upande wa kamera Google Pixel 8 Pro inaziacha simu nyingi nyuma kwa ubora

Kwa kifupi ni kwamba simu ina jumla ya kamera zipatazo tatu

Huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 50

google pixel 8 pro photo quality

Hata hivyo ukubwa wa megapixel sio kielelezo pekee cha ubora wa simu upande wa kamera

Pitia hapa kujua, vitu vinavyoifanya simu kuwa na kamera nzuri kwa kutazama iPhone 15 Pro

Uzuri ni kuwa kamera zake mbili zinatumia ulengaji wa dual pixel pdaf na kamera kuu inatumia multi-direction ambazo hutambua kitu kinachopaswa kupigwa picha kwa haraka

Kuhusu kamera ya google pixel 8 pro hii ni mada nyingine ya kuitazama kiundani

Ubora wa Software

Google Pixel 8 Pro inatumia toleo jipya kabisa la nadroid ambalo ni Android 14

Android 14 inakupa uwezo wa kuunda wallpaper kwa kuipa malelezo

Kwa mfano, nataka wallapaper yenye miti katikati ya miti barabara inapita

Cha kufanya hayo maelezo unayaandika kwa kusema, “tengeneza wallpaper yenye  miti katikati ya miti barabara inapita”

Baada ya muda app itachakata na kukupa wallpaper unayotaka

Hii inaitwa artificial intelligence(akili bandia)

Washindani wa Google Pixel 8 Pro

Washindani wakubwa wa hii simu ni simu zote za madara ya juu

Hapa nazungumzia Samsung na iPhone

Pixel itakumbana na wakati mgumu kutoka kwa watu wanaotaka utendaji mkubwa

Hilo linatokana na bei yake kutendana na simu za madaraja ya juu na zenye uwezo mkubwa kwenye maeneo mengi sio kamera tu.

Neno la Mwisho

Google ubora wao mkubwa upo sana kwenye software

Kwa wapenda kamera nzuri hii ni bonge la simu kuwa nayo

Kwa wanaopenda kuona mapinduzi ya matumizi ya akili bandia(artificial intelligence) basi hii simu itakuonyesha mambo makubwa ya AI

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Google Pixel 8 Pro na Sifa zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

google pixel fold thumbnail

Ubora na bei ya simu mpya ya Google Pixel Fold

Fold ni aina ya simu za kujikunja. Kwa muda mrefu makampuni ya Samsung, Huawei na Oppo wamekuwa wakitengneza simu za aina hii Hivi karibuni tecno na pixel pia zimeingia katika […]

simu za bei rahisi

Simu used za bei rahisi za madaraja ya kati na juu

Kuna simu za bei kubwa ambazo zilizotoka miaka ya nyuma na kwa sasa hazipatikani zikiwa mpya Matoleo yake yalikuwa yanalenga watumiaji wanaopenda vitu vya gharama hivyo kuwa na vitu vingi […]

google pixel 7 pro thumbnail

Bei ya Google Pixel 7 Pro na Ubora wake 2023

Google pixel 7 Pro ni moja ya simu inayosifika kuwa na kamera bora kwenye orodha ya simu mbalimbali Ubora wa kamera unachagiza bei ya Google Poxel 7 Pro kukaribia milioni […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram