SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 9, 2023

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne

Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14

Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini bado haijazinduliwa rasmi

google pixel 8 appearance

Hivyo matoleo ya google mapya yakizinduliwa yatairasimisha android 14

Google Pixel inakuja na teknolojia ya akili bandia(artificial intelligence ) kwenye baadhi ya app

Yaani simu itaweza kutambua vitu kwenye picha, kutafsiri kwa haraka na mengineyo mengi

Sifa za muhimu zinazotarajiwa

Google Pixel 8 na Pro inaangaziwa kuja na memori zenye muundo wa UFS 4

UFS 4 ina ufanisi wa kutumia umeme kidogo na kuwa na kasi kubwa ya kusafirisha data

Kwenye software pixel mpya zitapewa nguvu na Android 14

Kwa watalaam tayari wamekuwa wakiijaribu android 14 tangu mwezi wa pili

Japo simu nyingi zinatoka na android 13, kwa mwaka huu mwishoni simu mpya zitakuwa zinatumia android mpya kabisa

Simu inatarajiwa kuja na kioo cha amoled kilichowezeshwa na teknolojia ya HDR10+ kama ilivyo kwa simu nyingine za daraja la juu

Na vitu vingine vitafafanuliwa pindi ikiingia rasmi sokoni mwezi wa kumi

Akili bandia(AI)

Google wameendelea kuweka mkazo kwenye matumizi ya Artificial Intelligence(kwa maana isiyo rasmi tuite akili bandia)

Simu hii inakuja na kitu kinaitwa Magic Eraser na Photo Unblur

Kwa mfano umepiga picha kwenye eneo la watu wengi

Baada ya kupiga picha kuna watu wakatokea kwenye picha, magic eraser inakupa uwezo wa kuwaondoa watu wote na vitu vingine usivyotaka kuonekana bila kuathiri chochote kwenye picha

Photo Unblur inakuwezesha kurekebisha muonekano wa picha kama imetokea vibaya

Mapinduzi mingine ni kwenye tafsiri ya lugha

Kwa mfano unataka kuchati na mtu ambaye hajui kiswahili anafahamu kichina au kiigeleza pekee

Meseji app ya google inaweza kubadili ujumbe wako ni kuwa kichina hapo hapo na kisha kumtumia meseji mlengwa

Huna haja ya kwenda google search kutafuta maana ya ujumbe unaotaka kutuma

Bei tarajiwa

Bei rasmi haijatajwa kwa sasa

Ila kwa kuangalia mlolongo wa bei za google pixel za miaka ya nyuma, hii simu bei yake itakuwa zaidi ya milioni moja

Google Pixel hutoa simu za madaraja ya juu hivyo bei yake lazima iwe kubwa

Hata ukiangalia sifa zake zinazotarajiwa zinakupa picha ya bei itakavyokuwa

Kama wewe ni mpenzi wa google pixel na unahitaji ikiwa mpya unatakiwa ujipange kama ilivyo kwa simu za iphone au samsung s23

Ushindani sokoni

Kuna Samsung Galaxy S23 ambayo imetoka mapema mwaka 2023

Hivi karibuni apple watazindua toleo la iphone 15

Google kwa miaka mingi imekuwa na shea ndogo sana kwenye soko la simu za tabaka la juu

iPhone zimekuwa zikitawala kwa muda mrefu ikifuatiwa kwa mbali na simu za samsung

Kwa takwimu za mwaka 2022, apple inalishikilia soko la simu za bei ya juu kwa asilimia 75

Wakati Samsung yenyewe inashikilia kwa 17% tu

Hali hii ya soko inatarajiwa kuendelea mwaka huu hasa ujio mpya wa iphone

Mbali ya iphone na samsung kuna kampuni za China zinatoa simu  kali kwa bei nafuu kuliko google pixel

Kampuni hizo ni kama Xiaomi na OPPO bila kusahau Vivo

Ukitafuta orodha ya simu zenye kamera nzuri huwezi kukosa hizo brand za china

Kamera ndio kipengele kikubwa kinachoifanya pixel kupendwa duniani

Hivyo kwenye nyanja hiyo ana kazi ya kufanya

Muonekano

Simu za Google Pixel 8 Pro zinatarajiwa kuwa katika rangi tatu kwa mujibu wa picha zilizovuja kwenye mtandao wa Twitter(sasa ni X)

Rangi hizo ni nyeusi, kijivu na bluu

Hizi sio taarifa rasmi ila zinatokana na tetesi za hivi karibuni kutoka kwa watu mbalimbali

Upande wa nyuma kamera zake zitakuwa kwenye mpangilio wa mlalo huku kamera zikiwa zimeongozana kimstari

Ni tofauti na mpangilio wa kamera za iphone ambazo zipo kimuundo wa diaogonal

Na samsung ambazo zenyewe huwa zipo kwenye muundo wa wima

Matarajio

Ujio wa Google Pixel 8 utawapa watu wenye pesa kutosheleza chaguo la ziada kwenye upande wa simu za daraja la juu

Soko litaendelea kuwa kali

Kampuni zingine za simu zitaongeza juhudi kwenye tafiti ili kutoa simu zitakazoendelea kupata shea kwenye soko.

Maoni 3 kuhusu “Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 pro thumbnail

Bei ya Google Pixel 8 Pro na Sifa zake Muhimu

Simu ya Google Pixel 8 Pro imezinduliwa mwezi wa kumi (oktoba) 2023 Ni simu ya daraja la juu kama ilivyo kwa iphone na samsung matoleo ya S-series Kwa maana hiyo […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

google pixel fold thumbnail

Ubora na bei ya simu mpya ya Google Pixel Fold

Fold ni aina ya simu za kujikunja. Kwa muda mrefu makampuni ya Samsung, Huawei na Oppo wamekuwa wakitengneza simu za aina hii Hivi karibuni tecno na pixel pia zimeingia katika […]

simu za bei rahisi

Simu used za bei rahisi za madaraja ya kati na juu

Kuna simu za bei kubwa ambazo zilizotoka miaka ya nyuma na kwa sasa hazipatikani zikiwa mpya Matoleo yake yalikuwa yanalenga watumiaji wanaopenda vitu vya gharama hivyo kuwa na vitu vingi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram