SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Miongozo

Sihaba Mikole

October 14, 2023

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera)

Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei kubwa

Kamera zake zinatoa picha nzuri kwenye mwanga mwingi na pia kwenye mwanga mdogo vitu vinatokea na kuonekana kwa uzuri

iphone 15 pro max camera layout

Kwenye hii post tutaangazia kinaga ubara wa kamera ya iphone 15 pro max katika kupiga picha na kurekodi video

Hii tathmini imetokana picha mbalimbali watu walizopiga na tathmini nyingine za wataalamu

Kwanza inabidi ujue kila kamera na sifa zake

Kamera kuu(main camera)

Hizi ni baadhi ya sifa za kamera kubwa ya iphone 15 pro max katika vipengele muhimu

Resolution: Megapixel 48

Aperture(Uwazi wa kupitisha mwanga): f/1.8

Ukubwa wa pixel: 1.22µm

Ulengaji: dual pixel PDAF

Optical Image Stabilization(OIS): ipo

Ukubwa wa sensa ya kamera: 1/1.28 inchi

Kwa sifa zilizoorodheshwa zinaashiria uwezo wa kamera kuwa na vigezo stahiki kupiga picha na kurekodi video katika ubora stahiki

Kiwango cha ukiubwa wa pixel ambayo ni 1.22µm kinaipa nafasi kamera kukusanya mwanga mwingi

Pixel zikiwa ndogo sana hufanya simu kuwa na wakati mgumu kupiga picha vizuri

Kamera ya Ultrawide

Hii ni kamera maalumu kwa ajili ya kupiga picha ama kurekodi video eneo kwa upana mkubwa wa ziada

Ndio maana inaitwa kamera ya ultrawide

Tuchukulie upo kwenye mkutano wa hadhara na unataka kuchukua picha ya watu wengi kwenye uwanja kuonekana

Basi kamera ya ultrawide ndio inayofaa kutumika kwenye mazingira kama hayo

Hizi ni sifa za ultrawide ya iPhone 15 Pro Max.

Resolution:Megapixel 12

Aperture(Uwazi wa kupitisha mwanga): f/2.2

Ukubwa wa pixel: 1.4µm

Ulengaji: dual pixel PDAF

Optical Image Stabilization(OIS): ipo

Ukubwa wa sensa ya kamera: 1/2.55 inchi

Kamera hii ubora wake ni mzuri ila sio kama kamera ya kubwa

Lenzi(sensa) yake ni ndogo yenye inchi 1/2.55 inchi

Hata hivyo sifa zake bado zinaweza kupiga picha yenye ubora mkubwa

Kamera ya Telephoto

Resolution:Megapixel 12

Aperture(Uwazi wa kupitisha mwanga): f/2.8

Ukubwa wa pixel: 1.12µm

Ulengaji: dual pixel PDAF

Optical Image Stabilization(OIS): ipo

Zoom:5x optical zoom

Ukubwa wa sensa ya kamera: 1/3.06 inchi

Kamera ya telephoto hutumika kupiga kitu ambacho kipo umbali mrefu kutoka simu inapopiga picha

Kiasi cha kwamba ukitumia kamera ya kawaida mtu anaiweza aisonekane vizuri

Lakini telephoto tena yenye optical zoom(zoom inayotumia lenzi na sio app ya simu) inasaidia kukinasa kitu ambacho kipo mbali bila kupunguza ubora wa simu

Mpaka sasa simu yenye telephoto nzuri zaidi ni Samsung Galaxy S23 Ultra

Ubora wa picha wa kila kamera

Kwenye hiki kipengele tutaangazia ubora wa picha nyakati za mchana yaani kwenye mwanga mwingi na nyakati za usiku ambapo kuna mwanga mdogo

Kitu kikubwa tunachokitazamia ni usahihi wa rangi, kiwango cha noise(chengachenga) na uimara wa kutofautisha rangi kwenye mwanga hafifu na mwanga mwingi bila kusahau muonekano wa vitu pindi picha ikikuzwa

Kamera kuu(mwanga mwingi)

Wakati wa mchana ambapo kuna mwanga mwingi kamera inachukua picha vizuri bila kupoteza usahihi wa rangi

Vitu vinavyoonekana kwenye eneo huonekana kwa usahihi wake wa rangi kwa kiwango kikubwa

Ukiikuza(kuzoom) picha kwa ajili ya kuona vitu vingine kiundani bado utaweza kuona hata kama maandishi ambayo yapo mbali

iphone 15 pro max main camera

Moja ya kitu unachoweza kukipata kutoka kwenye hii picha ni kuwa kamera kamera kuu inahitaji vitu visiwe mbali sana na kamera

Kadri kinachopigwa picha kinapokuwa kuna kiwango cha noise(chengachenga) kinajitokeza

Hili unaweza kuliona kwa kutazama muonekano wa kamera

Kwenye mwanga mdogo

Wakati wa usiku ambapo ndipo kuna mwanga hafifu kamera kuu inapiga kwa ustadi bila kuwa na kiwango cha noise cha aina yoyote

Lakini kwa vitu ambavyo vipo apando wa pembeni wa kitu kinacholengwa hasa kikiwa mbali inakuwa ngumu hata kutambua rangi

Kwa kitu ambacho kimelengwa ubora wa picha ni mzuri

Ukiangalia rangi za vitu haziathiriwi na kiwango kikubwa cha giza usiku

Kila kinaweza kuonekana na kutambulika kwa usahihi

main camera low light

Ukitazama picha za magari na picha hilo jengo la ghorofa, rangi za vitu zinaweza tambulika na kutofautisha

Hii ina maana kamera inajitahidi kwa kiasi kikubwa katika utofautishaji wa rangi

Ila sasa ukiangalia upande wa kushoto mwa jengo kuna sehemu ina giza kubwa kiasi cha kwamba ni ngumu kujua kitu kilichopo

Maana yake utofautishaji wa rangi ni changamoto mwanga ukiwa mdogo zaidi

Njia apple wameitumia kutatua tatizo ni kuwa na chagua la kuseti Night Mode, hii inafanya picha isiwe na noise hata kidogo kwa kitu kinacholengwa na vile ambavyo vipo pembeni

main camera night mode setup

Hii ni setting ya nighy mode inavyosaidia kuonyesha kila kitu kwa usahihi mkubwa

Ultrawide(mwanga mwingi)

Kwa kulinganisha ubora wa picha kati ya kamera kuu na ultrawide , ultrawide ipo nyuma kidogo

Hata hivyo vitu vinaonekana hata kama ukiikuza picha na kuwa kubwa

Utaona kiwango cha chengechenga kuwa kidogo

Utofautishaji wa rangi kwenye kamera hii una usahihi unaoridhisha hasa nyakati za mchana

iphone 15 pro max ultrawide day

Kama picha jinsi unavyoonyesha, kamera imeweza kunasa eneo pana wakati huo unaweza muonekano wa kila kilichopo kwa uzuei

Rangi za majani, maji, majengo na mawingu zina muonekano halisi

Hata kwa vitu ambavyo vipo pembeni hakuna meonekano wa chengachenga hata kidogo

Changamoto ya noises ipo kwa kiasi nyakati za usiku

Si kila kilichopo kwenye eneo pana kitaonekana kwa uzuri kama picha zilizopigwa

Telephoto(mwanga hafifu)

Kikawaida simu ambayo haitumii optical sensor kuzoom kitu cha mbali mara nyingi hupoteza ubora wa picha

iPhone 15 Pro Max kamera yake ina optical sensor inayoweza kunasa picha kwa kitu ambacho kipo mbali kwa kukuza mara tano kama kiwango cha juu

Ukilinganisha na samsung galaxy s23 ultra, samsung iko vizuri sana kwenye eneo hili

Kwenye mwanga mwingi hasa nyakati za mchana kamera ya telephoto inachukua picha vizuri

Na picha zinakuwa na muonekano usiopoteza ubora hata ukiizoom picha mara tano unapotumia hii kamera

iphone 15 pro telepho

Hii ni picha iliyochukuliwa na kamera ya telephoto kabla ya kuzoom(kuikuza)

Chukulia unataka kuliona bati kwa ukaribu kitu kitachokulazimisha kuikuza(kuzoom) kamera mara tano

Hii ndio picha iliyochukuliwa baada ya kuzoom

iphone 15 pro telephoto after zooming

Je kuna upungufu wa ubora kwa kutazama muonekano wa awali na wa muonekano baada ya kukuzwa?

Ubora wa video

iPhone 15 Pro Max inaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa kiwango cha fremu 60 kwa sekunde

Kamera kuu na kamera ya telephoto zina OIS ambapo kazi yake kubwa ni kutuliza video wakati wa kurekodi

Wakati unarekodi video huku ukiwa unatembea, iphone haitikisiki kwa kiwango kikubwa

Iko “stable” na nzuri kwa wanaopenda kurekodi video za selfie

Kiujumla video zake ziko safi kwa nyakati zote yaani usiku(kwenye mwanga hafifu) na kwenye mwanga mwingi

Hitimisho

iPhone 15 Pro Max ni moja ya simu nzuri zenye kamera nzuri

Kwa kiasi kikubwa kamera zake zinanasa picha nzuri japo si kwa mazingira yote simu itachukua kwa uzuri

Maana kwenye mwanga hafifu sana tegemea kiasi kidogo cha noises ama baadhi ya vitu kutoonekana kwa uzuri

Maoni 2 kuhusu “Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

ios thumbnail

Nini Maana ya iOS kwenye Simu za iPhone

Vifaa vyote vya kompyuta kuanzia kompyuta mpakato, simu janja, smartwatch nk huundwa na kitu kinaitwa mfumo endeshi Mfumo endeshi ni mfumo unasimamia na kumeneji vitu vyote vilivyopo kwenye kompyuta au […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram