SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu za Nokia na Bei Zake 2022

Brand

Sihaba Mikole

April 16, 2022

Hii ni orodha ya simu kumi za nokia na bei zake nchini Tanzania.

Ni nokia za mwaka 2020, 2021 na mpya kabisa za 2022

Utaziona nokia za ubora wa juu, wa kati na wa chini kwenye utendaji wa processor, kamera, betri na network bila kusahau aina ya kioo na memori

Ukipitia sifa za simu zote kumi za nokia utaweza kujua nokia sahihi inayokizi mahitaji yako.

Simu ya Nokia G21

Simu ya nokia g21 imetoka mnamo februari 2022.

Kioo cha nokia g21 kina refresh kubwa ya 90Hz inayoifanya simu kuwa nyepesi.

Simu inatumia processor aina ya Unisoc T606 yenye utendaji mkubwa wa kuweza kucheza magemu kama dream soccer kiurahisi

Memori zake hazina kasi kubwa kwani ni aina ya eMMC 5.1

Simu inakubali mtandao wa 4G na bands zake zinakubali mitando yote ya simu Tanzania

Zipo nokia g21 za GB 64 na ram ya GB 3 au GB 4,pia GB 128 na ram ya GB 4 au GB 6

Ni simu ya macho matatu yenye kamera za ubora wa kawauda

Bei ya Nokia G21

Bei ya nokia g21 ya ukubwa wa gb 128 na ram gb 4 ni shilingi 486,688.27/=

Hii ni bei ya soko la india.

Kwa maduka mengi ya simu ya kariakoo bei inaweza kuzidi laki tano

Simu ya Nokia C21 Plus

Nokia C21 plus ni simu ya daraja la mwisho ambayo imetoka mnamo februari 2022.

Simu ina utendaji mdogo kiasi cha kutumia umeme mdogo.

Betri yake ina ukubwa wa 5050mAh ambalo linachukua muda mrefu kuisha chaji

Na aina ya memori yake inasafirisha data kwa spidi ndogo kwani inatumia eMMC 5.1

Kioo chake kina resolution yenye pixels chache (720 x 1600)

Nokia c21 plus ina kamera mbili ambazo zinatumia autofocus ya kizamani

Simu ya nokia c21 plus zipo za aina nne, ambazo ni 32GB na RAM ya 2GB au 3GB, na nyingine ni 64GB na RAM ya 3GB au 4GB

Bei ya Nokia c21 plus

Bei ya nokia c21 plus kwa masoko ya nje inafika shilingi 306,936/=

Bei itaongezeka zaidi kama utanunua c21 plus ya GB 64

Simu ya Nokia 6.1 Plus

Nokia 6.1 Plus ni simu ya mwaka 2018

Imetokea kwenye orodha kwa sababu nokia 6.1 plus inaweza kupokea tolea la android la mwaka 2020

Hivyo ni simu nzuri kwa nyakati za sasa pia

Ina memori zenye ukubwa wa GB 32 na GB 64, ukubwa wa ram ni 4GB na 6GB

Ni simu ngumu na inatumia kioo cha ips lcd.

Utendaji wake ni wa wastani kwa sababu ya kutumika kwa kwa chip ya snapdragon 636

Kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4k, na betri lake sio kubwa

Saizi yake ni 3060mAh

Bei ya Nokia 6.1 Plus

Bei ya nokia 6.1 plus ya gb 64 inafika shilingi 372,000/=

Ni bei halisi kwa nchi zingine duniani.

Kwa Tanzania bei inaweza kuzidi kwani Nokia 6.1 ya gb 64 inauzwa shilingi 300,000/=

Simu ya Nokia XR20

Simu ya nokia xr20 ni nokia ya 5G yenye kamera mbili upande wa nyuma

Simu ina network bands za 4g nyingi

Ni simu ambayo haipitishi maji kutokana na kuwa na IP68

Kioo chake ni angavu na kina resolution kubwa ya 1080×2400 pixels

Ni nokia inayokubali toleo jipya la android 12 japokuwa ni simu ya 2021

Japo ni simu ya 5G ila utendaji wake ni wa wastani

Hii inasababishwa na kuwa na processor ya daraja la chini ya Snapdragon 480 5G

Nokia xr20 inalindwa na kioo kigumu kuvunjika aina ya gorilla victus

Bei ya Nokia XR20

Bei ya nokia xr20 ya gb 64 ni shilingi 1,476,792.00/=

Na yenye gb 128 inauzwa shilingi 1,625,400.00/=

Ukubwa wa bei unasababishwa na uimara wa simu katika vipengele vingi

Simu ya Nokia G11

Simu ya nokia g11 ni simu mpya ambayo imetoka machi 2022

Ni simu ambayo ina utendaji wa wastani kutokana na kuwa na processor ya daraja la kati

Processor yake ni Unisoc T606

Betri lake ni kubwa kwani ujazo wake ni 5050mAh, na chaji yake inapeleka umeme wa wastani

Kioo cha nokia g11 ni cha ips lcd chenye resolution ndogo ya pixels 720×1600

Nokia g11 ina matoleo mawili kwenye upande wa memori

Ipo ya gb 32 na gb 64 na ram za 3GB na 4GB

Bei ya Nokia G11

Bei ya nokia g11 ya GB 32 inafika shilingi 600,000/=

Bei inaweza zidi 650,000/= kwa nokia g11 ya gb 64

Simu ya Nokia X100

Nokia x100 ni simu ya macho manne ambayo imetoka mwaka 2021

Kamera zake zina ubora wa wastani

Kioo chake cha ips lcd kina resolution kubwa inayofikia 1080×2400

Ni simu ya 5g na 4g yake inakubali karibu mitandao yote ya simu Tanzania

Inatumia processor yenye nguvu ya wastani ya Snapdragon 480 5G

Kuna toleo la aina moja tu la nokia x100 upande wa memori.

Memori yake ina ukubwa wa GB 128 na RAM GB 6

Bei ya Nokia x100

Unaweza ipata nokia x100 ebay kwa bei shilingi 417,960.00/=

Hii ni bei ya nokia x100 ya gb 128

Bei inayoifanya kuwa moja simu ya 5g ya bei nafuu

Simu ya Nokia G20

Nokia G20 ni simu ya mwaka 2021 yenye android toleo la 11

Kwenye memori, G20 ina matoleo mawili pekee

Kuna ya ukubwa wa GB 64 na 128GB na RAM ya 4GB

Utendaji wa simu si mkubwa kutokana na kutumia chip ya daraja la chini ya MediaTek Helio G35

Ni simu ya macho manne yenye kamera za ubora wa wastani

Kioo chake cha IPS LCD kina resolution ndogo ya pixels 720×1600

Betri yake ni kubwa inayoweza kukaa na chaji muda mwingi

Ukubwa wa betri ni 5050mAh

Bei ya nokia g20

Bei ya nokia g20 inafika shilingi 365,039.02/=

Hii ni kwa g20 ya GB 64.

Hivyo bei ya simu ya nokia g20 ya 128GB inaweza kuvuka shilingi laki nne

Simu ya Nokia G50

Simu ya nokia g50 ilizinduliwa mwishoni mwa 2021.

Hii ni simu ya 5G inayotumia processor yenye nguvu ya wastani kiutendaji ya Snapdragon 480 5G

Simu ina bands nyingi za 4G zinazokubali mitandao ya simu yote hapa Tanzania

Ina memori za ukubwa wa GB 64 na GB 128, na Ram za 4G na 5gb

Chaji yake inapeleka umeme kwa spidi ndogo itakayojaza betri lake kubwa la 5000mAh masaa zaidi ya matatu.

Ila ni nokia inayokaa na chaji muda mrefu

Bei ya Nokia G50

Bei ya nokia g50 ya ukubwa wa GB 128 inauzwa shilingi 673,380.00/=

Kwa toleo la GB 64 linaweza kuuzwa chini ya 620,000/=

Bei yake ina unafuu ukilinganisha na nokia xr20

Simu ya Nokia X20

Simu ya nokia x20 ni simu ya 5G yenye ram kubwa zinazofikia gb 6 na gb 8

Kiutendaji inafanana na nokia g20

Ni simu ya mwaka 2021 inayoweza kupokea toleo jipya la android 12

Memori yake ina ukubwa wa 128GB unaoweza kuhifadhi vitu vingi

Kioo chake kina uangavu wa wastani na resolution kubwa ya 1080×2400 pixels

Betri yake si kubwa sana kwani lina 4470mAh na chaji yake inapeleka umeme wa wati 18.

Hii ni simu ya macho manne yenye kamera inayoweza kupiga picha eneo pana sana

Bei ya nokia x20

Bei ya nokia x20 inashangaza kwani inafika shilingi 808,056.00/=

Nadhani bei kubwa inasababishwa na simu kutumia network ya 5G yenye bands nyingi

Na simu kupokea matoleo mapya ya android mara kwa mara

Simu ya Nokia C21

Nokia C21 ni simu mpya inayotarajiwa kuzinduliwa mwezi wa nne 2022

Hakuna tetesi zinazozungumzia bei ya nokia c21.

Hivyo hatutaingalia kiundani mpaka uzinduzi rasmi utakapokuja

Maoni 3 kuhusu “Simu za Nokia na Bei Zake 2022

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

samsung fold 4 camera

Simu 10 Zenye Kamera Nzuri na Bora 2023

Mwaka 2023 yapo mateo ya simu yaliyoingia sokoni yakiwa na kamera nzuri na bora kwa kupigia picha na kurekodi video Kuna simu zenye kamera kali zaidi na mfumo mzuri kwenye […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram