SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Vivo Y20 na Sifa Zake Muhimu [2022]

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 6, 2022

Simu ya vivo y20 ni simu ya android ambayo imetoka mwaka 2020

Ni simu ambayo inaweza ikachuana na baadhi ya simu mpya za daraja la chini kama itel a58

vivo y20

Bei ya vivo y20 inazidi shilingi laki tatu kwa maduka mengi ya simu dar es salaam Tanzania

Lakini bei inatofautiana na ukubwa wa memori

Ukiitazama bei na sifa za simu utagundua y20 ni simu ya bei rahisi yenye bei kubwa kuliko ubora

Fuatilia posti yote kujifunza

Bei ya Vivo Y20 Tanzania

Bei ya vivo y20 yenye ukubwa wa 64GB na RAM ya 3GB ni shilingi 390,000/=

Kama unafahamu vigezo vinavyoifanya simu kuwa nzuri inaweza ikawa ngumu kukubaliana na bei yake

Kwa sababu sifa zake zinaendana na simu ya redmi 9a na infinix hot 12i

Lakini hizo simu zinaweza patikana chini ya laki tatu

Ila ina sifa za kuzifuatilia ambazo zinaweza kukuvutia kuimiliki simu bila kujali gharama zake

Sifa za simu ya Vivo Y20

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 460
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×1.8 GHz Kryo 240
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.6 GHz Kryo 240
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
  • Funtouch 10.5
Memori eMMC 5.1,64GB, na RAM 3GB,6GB,4GB
Kamera Kamera tatu (vivo macho matatu)

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.51inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 390,000/=

Upi ubora wa vivo y20

Ubora wa simu aina ya vivo y20 ni uwezo wake wa kukaa na chaji muda mrefu

Ina chaji inayopeleka umeme wa wastani

Ni simu ambayo inakubali mtandao wa 4G

samsung galaxy y20 summary

Hivyo mtumiaji atapata kasi nzuri ya intaneti

Lakini kiuumla ubora kwenye nyanja zingine ni wa viwango vya chini usioendana na bei yake

Fuatilia uwezo wa y20 kwenye utendaji, processor, kioo na kasi ya kuchaji ufahamu ubora wake kiujumla

Uwezo wa Network

Vivo y20 ni simu ya 4G aina LTE Cat 13

LTE Cat 4 ni 4g ambayo spidi yake ya juu kabisa ya kudownload ni 390Mbps

vivo y20 network

Ni spidi ambayo ni ndogo ukilinganisha na simu kama samsung galaxy s21 ultra 5G

Simu inakubali intaneti ya 4g ya mitandao yote ya simu inayopatikana Tanzania

Kwa sababu ina masafa ya 4g yapatayo 14

Pitia ukura huu wenye kuelezea, masafa ya mtandao wa 4G ya mitandao ya simu Tanzania

Ubora wa kioo cha vivo y20

Kioo cha vivo y20 ni cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1600 pixels

Ubora wa kioo katika uonyeshaji wa vitu kwa usahihi si mkubwa hasa kama simu haina HDR10

Na resolution ndogo ya 720p inapunguza muonekano mzuri wa vitu

Hivyo vivo y20 ina kioo chenye ubora mdogo na uangavu ambao sio mkubwa

Hivyo ukiwa unaitumia simu juani inaweza kukupa shida kuona vitu vizuri kwenye screen

Nguvu ya processor Snapdragon 460

Vivo y20 inatumia processor ya snapdragon 460 katika kufanya kazi zote ambazo mtumiaji wa simu anazifanya

Snapdragon 460 ina jumla ya core zipatazo nane (octa core) lakini ina nguvu ndogo

Utendaji wake hauwezi kucheza gemu kubwa kwa urahisi

Simu inaweza ikawa inapata joto sana hivyo simu italazimika kucheza gemu kwa ubora wa chini

Hii inasababishwa na processor kutumia muundo wa Kryo 260 silver

Kryo 260 silver inafanana na Cortex A53 ambayo huwa na mizunguko michache ya kuchakata data

Processor ina core 4 zeneye spidi ya 1.8 na core nne zingine zina spidi

Uwezo wa betri na chaji

Vivo y23 ni moja ya simu ambayo inaweza kukaa na chaji masaa yanayozidi 14 simu ikiwa kwenye intaneti muda

Kwa sababu simu ina betri lenye ujazo mkuwa wa 5000mAh

Simu nyingi ambazo betri zake ni kubwa kuliko 4000mAh hukaa na chaji kwa masaa yanayozidi 10

Pia ukaaji wa chaji wa muda mrefu unachangiwa na nguvu ndogo ya processor yake

Chaji yake inapeleka umeme wa wastani wa wati 18

Hivyo simu inaweza kuzidi masaa matatu kujaa kwa 100%

Ukubwa na aina ya memori

Memori ya vivo y20 ni aina ya eMMC yenye ukubwa wa 64GB

Utakutana na vivo zinazotofautiana na ukubwa wa RAM pekee

Kuna vivo yenye ram ya 3GB, 4GB na 6GB

Lakini usafirishaji wa data ni mdogo ukilinganisha na simu ambazo zinatumia memori aina ya UFS

Uimara wa bodi ya vivo y20

Kama ilivyo kawaida ya simu nyingi za daraja la chini ni kuwa na bodi ya plastiki

Y20 ni simu ambayo ina viwango vya chini hivyo usitegemee simu kuwa na vioo vigumu

vivo y20 network bodi

Upande wa nyuma na upande wa mbele kote kuna plastiki

Mtumiaji atalazimia kununua kava ya simu kulinda ubora na kuimarisha uimara wa simu pindi inapoanguka kwa kimo kirefu

Ubora wa kamera

Simu ya vivo y20 ina jumla ya kamera tatu

Katika hizi kamera, ni kamera moja ambayo imewekewa teknolojia ya ulengaji ya PDAF

vivo y20 kamera

PDAF haina spidi kubwa ya kutambua kitu kinachopigwa picha ukilinganisha na dual pixel pdaf

Kamera nyingine ni aina ya marco maalumu kwa kupiga vitu kwa ukaribu

Kamera ya y20 inaweza kuchukua video ya aina moja

Ambayo ni video ya ubora wa full hd kwa spidi ndogo ya 30 fps

Ubora wa Software

Vivo y20 ni simu ya android 10 yenye inayotumoia software ya functouch 10.5

Kwa mwaka 2022, kuna toleo la android 12 hivyo baadhi ya simu zinapokea toleo jipya la androdi

Lakini vivo hii hawezai kupokea hata toleo la android 11

Hata hivyo android 10 bado ni mfumo endeshi wa simu unaokuja na vitu vizuri vingi

Na pia inaweza kutumia app mpya kwa kipindi cha miaka mingi

Yapi Madhaifu ya vivo y20

Kiujumla vivo y20 ni simu ya viwango vya chini ambayo ina madhaifu mengi

Madhaifu yake yanatokana na simu kuwa na bei ambayo inaweza kukupa simu nzuri zaidi

Y20 ina kioo chenye resolution ndogo

Simu haina ulinzi wa kuzuia maji kupenya

Simu pia ina ubora hafifu wa kamera

Kwani kamera haziwezi kurekodi video za 4k

Utendaji wa simu ni mdogo sanan kwa sababu ina chip ambayo nguvu yake haiwezi kufanya kazi kubwa kwa ufanisi

Neno la Mwisho

Kama utapata vivo y20 kwa bei ya chini 300,000/= utakuwa umeinunua kwa bei sahihi

Kinyume na hapo ni vizuri ukatafuta simu ya Redmi Note 10 5G

Redmi note 10 5g ina nguvu kubwa inayoifanya simu kuweza kufungua app ya aina yoyote kwa urahisi

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu 14 mpya za Vivo za ubora mkubwa na bei zake (2024)

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka mwaka huu 2024 Vivo imeachia matoleo mengi ya simu Katika matoleo hayo yapo ya bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa Kwa maana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram