SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 10C na Sifa Muhimu

Simu Mpya

Sihaba Mikole

April 7, 2023

Tecno Spark 10C ni toleo jipya la tecno kwa mwaka 2023

Spark 10C ina tofauti ndogo sana na simu ya Tecno Spark 10

Na tofauti yao ipo kwenye camera na software, mengine yanafanana

tecno spark 10c showcase

Bei ya tecno spark 10c inazidi laki tatu na nusu japo kisifa inaleta maswali

Maswali hayo yanatokana na sifa za kiujumla za hii simu japo vipo vya kuvutia.

Bei ya Tecno Spark 10 ya GB 128

Bei ya Tecno Spark yenye GB 128 ni shilingi 410,000/=

Bei inaweza kuwa inasababishwa na kioo pamoja na ukubwa memori

tecno spark 10c summary

Vipengele vingi vya simu ni vya kawaida ambavyo kwenye simu zingine  bei zake ni chini ya laki nne

Kiulanganish, spark 10c inashabiana na Samsung Galaxy A04 ya mwaka 2022

Ni vizuri kuitazama kila kipengele kujua kama simu inakufaa kwa matumizi yako

Sifa za Tecno Spark 10

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Unisoc Tiger T606
  • Core Zenye nguvu(2) – 2 x 1.6GH Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6 x 1.6GH Cortex-A55
  • GPU-ARM Mali G57 MP1
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • HIOS 8
Memori 128GB, na RAM 8GB
Kamera Kamera MBILI

  1. 16MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 410,000/=

Upi ubora wa Tecno Spark 10C

Simu ina kioo chenye refresh rate kubwa inaypfika 90Hz, hivyo ni kizuri kwa magemu

Inakuja na nafasi kubwa ya kuhifadhi mafaili

Ukaaji wa chaji ni mkubwa kwani betri yake ni kubwa pia ina 5000mAh

Inakuja na ram kubwa na inaweza kuongeza ukubwa wa RAM

Inakubali mtandao wa 4G wenye kasi kubwa

Ina muonekano wa kuvutia na ina glasi kwa nyuma

Uwezo wa Network

Tecno spark 10c ni simu ya 4G kwa maana haina 5G

Aina 4G inayotumia ni LTE Cat 7 yenye kasi ya 300mbps ambayo ni  sawa na 37.8

Yaani kama unadownload applikesheni ya whatsapp yenye MB 37, simu itamaliza kuipakua kwa sekunde moja tu

tecno spark 10c network

Ila jua ni ngumu kupata kasi hii kwenye mitandao ya simu za mkononi kwa hapa Tanzania

Simu ina masafa yote ya 4G yanayotumiwa hapa nchini

Hivyo kila mtando utafanya kazi vizuri

Ubora wa kioo cha Tecno Spark 10C

Kioo cha tecno kina ubora wa kawaida kwa sababu kinatumia teknolojia ya IPS LCD

Na resolution yake ni 720p ambayo iko sawa na spark ya mwaka 2022

Kwa viwango vya sasa resolutuion inayopendekezwa ni 1080p yaani full hd.

tecno spark 10c display

Ila haishangazi sana ukizingatia ni simu ya daraja la chini na inawalenga watumiaji wenye matumizi ya kawaida

Kiujumla ubora wa vioo vya IPS LCD huzidiwa na vioo vya amoled

Simu yenye kioo cha amoled ni tecno phantom x2 pro ambayo bei yake inazidi milion

Pitia hapa: Sifa za tecno phantom x2 pro, uijue kinagaubaga

Nguvu ya processor Unisoc Tiger T606

Processor ya unisoc tiger t606 ndio chip inayoiwezesha simu ya spark 10c

Ni chip iliyogawanyika katika sehemu mbili, sehemu ya kwanza ina jumla ya core 2

Hizi ni core zenye nguvu kubwa kwenye hii simu na zinatumia muundo wa Cortex A75

Na kwenye core zenye nguvu ndogo zipo sita zikiwa zinatumia muundo wa Cortex A55

tecno spark 10c processor

Kwa mgawanyo huu inamaanisha uwezo wa simu kiutendaji ni mdogo

Sio simu nzuri kwa mtu anaependa kucheza gemu kubwa kama za mpira, za mapigano na nyinginezo

Lakini pia ni chip inayotumia umeme kiasi kidogo hivyo betri inakaa muda mrefu na chaji

Uwezo wa betri na chaji

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh hivyo unaweza kutumia muda mrefu bila kuhofu chaji kuisha haraka

Uwezo wa kukaa na chaji ni mkubwa kwa sababu processor yake haitumii umeme mwingi

Spark 10C inakuja na chaji yenye uwezo wa kupeleka umeme wa wati 18

tecno spark 10c chaji

Kwa kipindi cha nyuma kiwango hiki kilikuwa kinachukuliwa kama fast chaji

Ila siku hizi kuna simu zinapeleka mpaka wati 120 zinazojaza simu kwa dakika 17 tu

Na simu za kawaida huwa zinakuja na chaji kuanzia wati 25

Wati 18 ni nzuri ila simu inachukua muda kujaa kwa 100%

Ukubwa na aina ya memori

Tecno spark 10c inakuja na toleo moja tu upande wa memori

Toleo hilo lina ukubwa wa GB 128

Kwa mtumiaji asiependa kupakuwa vitu vingi hili toleo zuri kwake na anaweza asijaze simu yote

Haijaainishwa ni aina ipi ya memori inayotumika na hii simu

Uimara wa bodi ya Tecno Spark 10C

Bodi ya Tecno Spark 10C inakuja na kioo upande wa nyuma

Kioo kinachotumika sio gorilla na hivyo kuna umuhimu wa kutumia kava

tecno spark 10c bodi

Na uzuri tecno simu zake mpya huwa zinakuja makava ukifungua box

Simu hii haina uwezo wa kuzuia maji endapo ikizama kwenye maji ya kina kirefu

Kwa sababu haina viwango vya IP68, hivyo kuwa makini na matumizi yako hasa ukiwa kwenye mvua au ufukweni

Ubora wa kamera

Simu ina kamera mbili kamera kubwa ina megapixel 16 ni tofauti na spark 10 yenye megapixel 50

Ubora wa kamera unaangaliwa kwa vitu vingi sio megapixel pekee  kama simu ina mfumo mzuri wa kamera, kamera kuanzia megapixel 10 zinaweza kutoa picha kali

tecno spark 10c kamera

Kama unabisha tazama kamera za iPhone 13 Pro Max ambazo zote zina 12MP

Ziangalie, simu zenye kamera nzuri ikiwepo iphone 13 pro max

Upande wa Tecno Spark 10C haina mfumo mzuri wa kamera kuanzia kamera kuu hata selfie

Hii inapelekea ubora wa picha kuwa mdogo hata nyakati za mchana

Ukiitazama hii picha chini utaona noise(chengachenga) kwa mbali na rangi za majani kuwa mwangaza mwingi kuliko uhalisia

tecno spark 10c camera

Hii inasababishwa na kamera kukosa angalau HDR10 na uchakataji wa kiwango cha chini wa ISP(processor)

Kwenye video simu inaweza kurekodi video za full hd pekee na haiwezi kurekodi video za 4K

Na pia haina OIS(Optical Image Stabilization) hivyo ukiwa unarekodi video huku unatembea inabidi utulize mkono ili video isitokee ikiwa na mitikisikomitikisiko.

Ubora wa Software

Utofauti mwingine kati ya Tecno Spark 10 na Spark 10C ni upande wa software

Spark 10C inatumia mifumo ya nyuma

Kwani inakuja na Android 12 na HiOS 8

Android 12 ni bado toleo zuri lakini kwa simu mpya inafaa ije na toleo la Android 13

Ikizingatiwa hakuna uhakika kama  simu itakuwa inapokea matoleo mapya ya android huko mbeleni

Hata hivyo utaweza kuongeza ukubwa wa RAM mpaka GB 4

Yapi Madhaifu ya Tecno Spark 10C

Katika mrorongo wa matoleo ya Tecno spark 10, tecno spark 10c ina mapungufu mengi

Ubora wa picha ni wa kiwango cha chini

Processor yake ina nguvu ndogo kusukuma vitu vingi na gemu kubwa

Kioo chake hakina HDR10 wala HDR10+

Simu haina 5G ukizingatia kuna simu zina bei kama hii na zinakuja na 5G

Inatumia mfumo endeshi wa kipindi cha nyuma na kuacha mifumo endeshi mipya

Neno la Mwisho

Tecno Spark 10C ni toleo zuri kwa anayependa simujanja inayotunza chaji

Kama unaishi kwenye maeneo yenye umeme usio na uhakika hii simu itakusaidia

Ila kwa mtu anayependa kamera na simu yenye utendaji mkubwa basi hili sio chagua zuri kuwa nalo

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Tecno Spark 10C na Sifa Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

OnePlus 11R

Simu 15 za OnePlus na Bei zake (Aina zote)

OnePlus inaweza ikawa ni jina geni kwa watumiaji wengi smartphone Tanzania Ila OnePlus ni moja ya kampuni kutoka china inayotengeneza simujanja za madaraja ya kati na ya juu Simu nyingi […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram