SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G na Sifa Zake 2023

Sifa za simu

Sihaba Mikole

August 16, 2023

Simu ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra ni samsung ya mwaka 2020

Japo ina miaka ipatayo mitatu tangu itoke ila ni moja samsung kali mpaka wakati huu wa sasa

Bei ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G kwa sasa inazidi milioni ikiwa used

samsung note20 ulta 5g

Kwa Tanzania kuna changamoto ya kuipata ikiwa mpya, nyingi ni used

Hata hivyo utofauti wa bei yake unategemea na ukubwa wa memori

Bei ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G ya GB 128

Kwa sasa hapa Tanzania simu hii inapatakana kwa kiasi cha shilingi 1,200,00 yaani milioni moja na laki mbili

Hii ni bei ya note 20 ultra ambayo imetumika bila kujali imetumika wapi

Kama utalinganisha galaxy note 20 ultra na matoleo mapya ya daraja la kati utaona kuwa note inaziacha kwa kiwango kikubwa

Ikiwemo yale matoleo ya samsung a54 au samsung a14, bado samsung note 20 ultra ni kiboko

Na wala haishangazi bei yake kuendelea kuwa kubwa hata kwa miaka itakayofuata

Sifa za Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 990
  • Core Zenye nguvu sana(2) – 2×2.73 GHz Mongoose M5
  • Core Zenye nguvu wastani(2)- 2×2.50 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G77 MP11
Display(Kioo) Dynamic AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 10
  • One UI 5
Memori UFS 3.0,256GB,128GB,512GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.9inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 1,200,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G

Ina utendaji mkubwa kutokana na kutumia chip yenye nguvu kubwa

Inakuja na kioo chenye uoneshaji wa kiwango kikubwa cha rangi

Memori yake ina kasi kubwa ya kusafirisha data

Ni simu ndefu inayoweza kuonyesha vitu kwa upana mzuri na kuonekana kwa ustadi

Betri yake ni kubwa

Kamera yake inatoa picha vizuri hata kwenye mazingira yenye mwanga mdogo

Ni simu inayiosapoti 4G zenye kasi kubwa ya kupakuwa vitu

Uwezo wa Network

Galaxy Note 20 5G inasapoti mitandao yote ikiwemo 5G kama jina lake linavyojieleza

Kwenye upande wa 5G inasapoti masafa yote matatu kwa maana masafa ya kati, mafupi na marefu

Na pia inakubali 5g za NSA na SA, NSA ni 5G ambayo hutumia miundombinu ya 4G

Aina ya 4G simu inayotumia ni LTE Cat 24 yenye kasi inayofika 7350Mbps kwenye kudownload

Ni kasi kubwa ambayo huwezi kuipata kwenye mitandao ya 4G kwa hapa Tanzania

Kwa sasa 5G inapatikana kwenye mitandao ya Airtel, Vodacom na Tigo kwa baadhi ya maeneo ya Dar Es Salaam

Hivyo ukiwa kwenye eneo zuri stahiki utaweza kutumia mtandao huu wenye kasi zaidi

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G

Kioo cha samsung galaxy note 20 ultra 5G ni aina ya Amoled 2X ambavyo hutengenezwa na samsung wenyewe

Kioo cha hii simu kina resolution ya 1440 x 3088 pixels ambayo ni kubwa

Ufanisi katika kuonyesha vitu vizuri unachangiwa na uwepo HDR10+

HDR10+ inaongeza kiwango cha rangi hivyo kioo kuwa na uwezo wa kuonyesha vitu kwa rangi zinazoendana na uhaisia kwa kiwangio cha juu

Pia ina refresh rate inayofika 120Hz kitu kinachofanya kuperuzi kuwa ni kuzuri

Kuifupi, ubora wa kioo cha samsung ni mkubwa

Kama kioo kikiharibika inabidi uwe tayari kuingia gharama kupata kioo orijino

Maana bei ya kioo cha samsung note 20 ultra 5g ni kubwa

Nguvu ya processor Exynos 990

Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5g inatumia processor ya Exynos 990 kufanya kazi zake

Hii ni chip ambayo imegawanyika katika sehemu tatu huku sehemu zenye nguvu kubwa sana zikiwa zinatumia muundo wa Mongoose M5

Mongoose M5 huweza kuchakata kazi sita kwa wakati mmoja kwa kila mzunguko

Na mizunguko ya hii core ni 2.7GHz(yaani mizunguko bilioni mbili nukta saba)

Ndio maana app inayopima ubora wa processor iitwayo Geekbench inaipa exynoss 990 alama 900

Na pia uchezaji wa magemu ni mzuri kutokana na aina hii ya utendaji

Kwa mfano gemu ya armajet 2020 inacheza kwa kiwango cha 60fps, yaani muonekano wa gemu unakuwa mzuri bila kuganda ganda

Wakati huo samsung a54 ya mwaka 2023 inacheza gemu ya pubg mobile kwa kiwango cha 36fps huku galaxy note 20 ni 30fps

Hii inamaanisha Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G ina nguvu kubwa ya utendaji

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya hii simu ina ukubwa wa 4500mAh

Kutoka gsmarena, ni kuwa simu inadumu masaa 11 ikiwa ipo kwenye intaneti muda wote na refresh rate ikiwa 120Hz

Ila kama refresh rate umeiseti kuwa ndogo betri hutunza chaji mpaka masaa 13

Sio kiwango kikubwa sana ukilinganisha na simu zenye mabetri ya ukubwa wa 5000mAh

Ila ni muda unaoweza kutumia kufanya vitu hata ukiwa mbali na maeneo yenye umeme

Uzuri chaji inapeleka umeme mwingi wa kiwango cha wati 25

Hii chaji inaweza kujaza betri kwa kiwango cha 48% kwa muda wa nusu saa

Hivyo ndani ya dakika 80 simu inaweza kujaa kwa 100%

Ukubwa na aina ya memori

Upande wa memori simu zipo za aina tatu huku kubwa zaidi ikiwa na GB 512

Na ram pia zipo kwenye mgawanyo wa sehemu tatu

Yenye ram kubwa na memori kubwa bei yake inaongezeka kiasi

Aina ya memori inayotumiwa na hii ni simu UFS 3.0 ambayo kasi yake inafika 2400MBps kusafirisha data

Maana yake ni kuwa simu inauwezo wa kufungua apps kwa haraka na kwa sekunde chache

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G

Galaxy Note 20 Ultra ina viwango vya IP68 vinavyoashiria uwezo wa kuzuia maji kupenya

Iwapo simu ikizama kwenye kina cha mita 1.5 maji hayatoingia kwa muda wa nusu saa

Pia imewekewa skrini protekta aina ya kioo kutoka kwa kampuni ya gorilla

samsung note20 ulta bodi

Na upande wa nyuma pia kuna kioo cha gorilla victus

Kiujumla simu ina bodi imara isiyopoteza ubora wake kwa muda mrefu

Ubora wa kamera

Simu ina idadi ya kamera zipatazo tatu

Kuna kamera ya kupiga picha vitu vya mbali sana, eneo pana na kamera ya kawaida

Kamera mbili zinatumia teknolojia ya ulengaji ya PDFA na kamera kubwa pia ina Laser AF kwa ajili ya usiku

PDAF ulengaji sio wa haraka kama dual pixel pdaf

samsung note20 ulta kamera

Kama unakipiga kitu kinachokimbia kwa kasi kiwango cha kamera kurekodi kwa utulivu ni wa taratibu

Hata hivyo ubora wa picha ni wa kiwango cha kuvutia

Kuna kiwango kidogo cha noise hata picha ukiikuza kuwa kubwa

Usahihi wa rangi unajitahidi kuonyesha rangi sahihi za mazingira ya hiko kitu

Utofauitishaji wa rangi ni mkubwa na kamera haiathiriwi na mwangaza mwingi wakati wa mchana

Hata kwenye mwanga hafifu vitu vingi vinaweza kuonekana kwa uzuri bila kuathiriwa na kiwango kikubwa cha giza

Ubora wa Software

Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G ilitoka mwaka 2020 hivyo inakuja na android 10

Hata hivyo, simu inakubali kupokea toleo jipya Android 13

Android 13 ndio toleo la sasa kabisa, hivi karibuni android 14 itakuja kuchukua nafasi yake

Kitendo cha simu kuweza kupokea matoleo ya android yanaipa simu thamani zaidi

Washindani wa Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G

Mshindani wa kwanza ni iPhone 12 Pro Max

iPhone 12 Pro Max inakuja na masafa mengi zaidi ya 5G na utendaji wake ni mkubwa kuliko galaxy note 20 ultra 5g

iPhone ina kamera yenye ulengaji dual pixel pdaf yenye uweza wa kukitambua kitu kwa ustadi

Kwa bahati mbaya bei ya iphone 12 pro max inaizidi kiasi samsung

Mshindani mwingine ni Xiaomi 13 Ultra

Xiaomi 13 Ultra ni mpya ina vitu vya kisasa ambavyo vingine havipo kwenye galaxy note 20

Bei pia bei yake ni kubwa ila inatoa ushindani unaoweza mshawishi mtu kuacha kununua note20

Neno la Mwisho

Kwa muhitaji wa simu za viwango vya juu na hana bajeti kubwa, samsung galaxy note20 ultra 5G ni mbadala mzuri

Hakuna tofauti kubwa sana na matoleo mengi ya daraja la juu ya hivi karibuni

Zingatia kuwa simu nyingi za hii galaxy kwa hapa nchini kwetu ni used

Simu used zinapunguza gharama kama ukipata nzuri

Maoni 5 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy Note 20 Ultra 5G na Sifa Zake 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu Mpya za Samsung 2024 (za bei rahisi na ghari)

Kuna simu zaidi ya tisa zilizotengenezwa na kampuni ya Samsung kutoka Hapa kuna orodha ya simu kumi mpya za samsung ambazo zimetoka mwishoni mwa mwaka 2023 hadi mwaka 2024 Ni […]

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram