SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy S24+ na Sifa Zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

February 20, 2024

Kisifa Samsung Galaxy S24 Plus ina sifa nyingi zinazoendana kwa kiasi kikubwa na Samsung Galaxy S24 Ultra

Kwa maana Galaxy S24+ ubora wake unazipita simu nyingi na mkubwa, hivyo bei yake imechangamka pia

samsung s24 plus showcase

Kwa Tanzania, bei ya Samsung Galaxy S24 Plus ni shilingi milioni mbili na nusu, hii ni bei ya Samsung yenye ukubwa wa GB 256

Bei hii ni kubwa kuliko Infinix Hot 40 Pro ya GB 256 na kinachofanya bei ya Samsung kuwa ni sifa zake ambazo ni kubwa sana

Kuanzia kamera, utendaji, kioo na uimara wa simu bila kusahau software huwezi kukuta kwenye simu za daraja la chini

Sifa za Samsung Galaxy S24+

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8 Gen 3
  • Core Kubwa Sana(1) – 1×3.39GHz Cortex-X4
  • Core Kubwa Kiasi(3) – 3×3.1GHz Cortex-A720
  • Core za Wastani(2)-2×2.9GHz Cortex-A720
  • Core Ndogo(2)-2×2.2GHz Cortex-A520
  • GPU-Adreno 750
Display(Kioo) Dynamic LTPO AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6.1
Memori UFS 4.0, 256GB,512GB na RAM 12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 10(Telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4900mAh
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 2,500,000/=

Uwezo wa network

Samsung Galaxy S24+ inasapoti mpaka mtandao wa 5G kama ilivyo kwa samsung ultra

Aina ya 4G ambayo simu inayo ni ile inayoweza kufika kasi ya 10000Mbps kwa kupakuwa mafaili

Kwa hapa nchini kasi kubwa utaipata kama unatumia mtandao wa 5G

Kwa bahati mbaya 5G bado haijasambaa maeneo mengi ya nchi

Kwa wakazi wa Dar Es Salaam kwenye baadhi ya maeneo unaweza pata teknolojia hii ya mawasiliano

Ubora wa kioo

Kioo cha Samsung Galaxy S24 Plus ni cha aina ya amoled

Ila amoled yake ni ile inayoitwa Dynamic LTPO Amoled chenye resolution ya 1440 x 3120 pixels

Hii simu kioo chake kinauwezo wa kuonyesha rangi nyingi kutokana na uwepo wa HDR10+

Uangavu wa kioo unafika mpaka nits 2600

Uangavu huu unasaidia kioo kuweza kuonyesha vizuri kwenye mazingira yoyote

Kama ujuavyo ukiwa juani inakubidi uongeze mwanga ili skrini ioneshe vizuri

Nguvu ya processor Snapdragon 8 Gen 3

Simu ya Samsung Galaxy 8 Gen 3 inatumia chip ya snapdragon 8 gen 3 kwa matoleo ya Marekani

Wakati nchi nyingine zinakuja na processor ya Exynos 2400 ambayo huundwa na kutengenezwa na samsung yenyewe

Kimuundo hizi chip mbili hazitofautiani sana na kwa kiasi kikubwa zipo sawa

Kwa hapa, tutaizungumzia Snapdragon 8 Gen 3

Kwenye app ya Geekbench 5 inayotumiwa kupima nguvu za processor, snapdragon 8 gen 3 inaonyesha kuwa na nguvu kubwa kuliko hata processor nyingi za Apple

Kama unavyojua kwa miaka mingi chip za apple zimekuwa kinara kwenye utendaji mkubwa

Ila kwa matoleo mapya ya Snapdragon yamepunguza hii tofauti kwa kiwango kikubwa

Kwa mtumiaji wa kawaida anaweza asione tofauti ya wazi

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya hii simu ni kubwa na ina mAh zipatazo 4900

GSMArena tovuti kubwa ya udadisi kuhusu sifa za simu inasema kuwa wastani wa simu kukaa na chaji ni masaa kumi na mbili

Kwenye kucheza gemu, intaneti na hata kuangalia video

Utofauti wa muda hautofautiani sana na Samsung Galaxy S24 Ultra

Ila inazidiwa kwa mbali sana na Apple iPhone 15 Pro Max na OnePlus 12

Cha kushangaza ni kwamba betri ya iphone sio kubwa kama Samsung

Upande wa chaji simu inasapoti chaji yenye kasi mpaka wati 45

Chaji ni nzuri hasa kipindi cha umeme unaokatika mara kwa mara

Kwani ndani ya nusu betri inajaa kwa asilimia 75

Kwa mtumiaji mkubwa sana wa simu ataichaji galaxy s24 plus mara mbili tu kwa siku

Ukubwa na aina ya memori

Samsung hii ina matoleo matatu upande wa memori na zote zina RAM ya GB 12

Mfumo wa memori unaotumiwa na hii simu ni UFS 4.1

Kasi yake ya kusoma na kuandika data kwenye memori ni mara mbili ya mfumo wa UFS 3.0

Hii kasi inaipa simu nguvu ya ziada katik utendaji wake wa kazi mbalimbali

Kwa kifupi kuna Samsung Galaxy S24+ ya GB 256 na 512

Na zote hazina sehemu ya kuweka memori kadi kama ilivyo simu nyingi za daraja la juu zinazotoka miaka hii

Ukubwa huo unatosha kuhofadhi mafaili na app nyingi

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy S24+

Hii ni simu yenye waterproof kwa maana haiwezi pitisha maji kama ikizama kwenye kina fulani

Ukiizamisha kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu saa maji hayawezi kuingia

Pia ina uwezo wa kuzuia maji tiririka kama mvua hivyo hutokuwa na wasi ukiwa upo mvua kubwa ambayo imenyesha ghafla ukiwa njiani

Uimara wa Galaxy S24 Plus haupo tu kwenye waterproof bali ugumu wake pia inapoanguka

Upande wa skrini simu ina kioo cha Gorilla Glass Victus 2 ambacho kina uvumilivu wa kutopasuka pindi ikidondoka kwenye kina cha mita mbili

Hata hivyo kioo ni kioo tu hivyo umakini ni kitu cha msingi

Upande wa nyuma ya simu kuna kioo cha Gorilla Glass Victus 2 vile vile

Ubora wa kamera

Kamera za Samsung Galaxy S24+ zipo tatu ambapo kamera kubwa zaidi ina megapixel 50 na zinatumia ulengaji wa dual pxiel pdaf

Kiujumla kamera za hii simu zinatoa picha nzuri na zenye usahihi wa rangi

Tofauti na kamera ya Samsung Galaxy S24 Ultra ni kuwa nyakati za usiku utaona kiwango fulani cha noise ukiikuza picha kwenye hii simu ya Samsung Galaxy S24+

Kiwango ambacho ni ngumu kugundua kwenye Galaxy Ultra

Mambo mengine yapo sawa ikiwemo kurekodi mpaka video za 8K kwa maudhui ya HDR10+

Ni ngumu kukuta HDR10+ kwenye simu za daraja la kati

Pitia hapa kujua: Maana ya HDR na umuhimu wake

Ubora wa Software

Kwa mara ya kwanza Samsung watakuwa wanatoa matoleo mapya ya Android kwa kipindi cha miaka 7 kwenye simu zote mpya za s-series

Miaka ya nyuma simu za samsung zilikuwa zinapata maboresh kwa muda mfupi sana

Yaana kama ukinunua galaxy yenye android 10 toleo la mwisho utakalopata ni android 12

Lakini kwa sasa Simu inakuja na Android 14 hivyo ukinunua utaweza kupata mpaka toleo la android 21

Vitu vingne vya kuvutia vya hii simu ni uwepo wa mifumo ya Akili Bandia(artificial inteligence)

Kwa mfano inaweza kubadilisha lugha kiingereza kuwa kwa kiswahili wakati mtu anaekupigia simu akiwa anaongea kiingereza

Inaondoa mipaka ya lugha kwenye mawasiliano

Washindani wa Samsung Galaxy S24+

Karibu simu zote za madaraja ya juu yanaweza kutoa ushindani mkali kwa toleo hili la Samsung

Mfano Apple iPhone 15 Pro Max ni kikwazo kikubwa kwa samsung hasa soko la China na USA

Samsung imeshindwa kufanya vizuri kwenye soko la China kwa miaka mingi

Huawei na iPhone ndizo zinazotawala kule

Kwa marekani, karibu ya 60% ya watumiaji wa simu wanatumia iPhone

Neno la Mwisho

Kama bajeti yako haina uwezo wa kumiliki Samsung Galaxy S24 Ultra basi mbadala mzuri S24 Plus

Sifa za Samsung Galaxy S24+ hazina tofauti sana na ile galaxy kubwa

Haina haja ya kuwaza sana kama unaweza kununua simu yenye bei ya milioni mbili kama ilivyo kwa hii samsung

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram