SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Mbalimbali za Vodacom Tanzania na Bei Yake

Brand

Sihaba Mikole

July 5, 2023

Hii ni orodha inayohusisha simu ambazo zinauzwa na kampuni ya vodacom na bei zake

Kwenye orodha kuna simu zipatazo nane (8) za bei nafuu, kati na bei kubwa

Ni simu zenye ubora wa kawaida na nyingine ubora mkubwa ila zinaweza saidia kwa shughuri za kawaida za kila siku

Simu zenye ubora wa chini zinauzwa chini ya laki tatu

Kwa mtu mwenye kiasi kidogo cha pesa ni vizuri ukafuatilia kila simu ya vodacom na bei yake kujua kama zinakustahili ama la.

Na pia ukinunua baadhi ya simu vodacom wanatoa GB za intaneti

Oppo A16K

Oppo A16K ni simu ya mwaka 2021 ambayo ni ya daraja la chini

Vodacom wanaiuza oppo a16k kwa kiwango cha shilingi 280,000 (laki mbili na themanini)

Ina jumla ya kamera moja tu ambayo uwezo sio mkubwa

Kiutendaji pia uwezo wake ni mdogo kwa sababu inatumia processor yenye nguvu ndogo aina ya MediaTek Helio G35

Inatumia kioo cha ips lcd ambacho resolution yake ni 720 x 1600 pixels (ni ndogo pia)

Betri yake ina ukubwa wa 4230mAh ambayo ni mkubwa

Na ukaaji wa chaji ni wa kuridhisha, ni simu ya 4G

Samsung Galaxy A04E

Simu ya Samsung Galaxy A04E ni simu ya android iliyotoka mwaka 2022

Kiuwezo inaendana na oppo a16K kwa maana zote zinatumia processor zenye muundo mmoja japo zina majina tofauti

Samsung galaxy A04E ina kamera mbili ila moja ndio inayopiga picha na ina megapixel 13

Kioo chake na chenyewe ni cha IPS LCD na resolution ya 720 x 1600 pixels

Ukubwa wa betri ya hii simu ni 5000mAh kwa maana ukaaji wa chaji ni wa masaa mengi

Simu inakuja na android toleo la 12 yaani Android 12

Bei ya Samsung Galaxy A04E kwenye maduka ya Vodacom ni 270,000 (laki mbili na sabini)

Tecno Pop 7

Simu ya Tecno Pop 7 ni simu ya mwaka 2023 unaweza iita tecno mpya 2023

Inakuja na RAM ya GB 2 ambayo sio kubwa kwa viwango vya sasa

Na ukubwa wa memori ni GB 64

Kwenye upande wa mfumo endeshi inatumia Android 12 Go edition

Go Edition ni mfumo wa android kwa ajili ya simu zenye RAM ndogo bila hivyo simu inakuwa nzito

Na yenyewe inatumia kioo cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1612 pixels

Voda wanaiuza hii simu kwa kima cha shilingi 240,000 (laki mbili na arobaini)

Vivo Y02

Vivo Y02 ni simu ambayo imetoka mwishoni mwa mwaka 2022

Ni simu ya daraja la chini hivyo ina bei ndogo

Kwani Vodacom wanaiuza kwa kiwango cha shilingi 265,000 (laki mbili na sitini na tano)

Bei ndogo ya vivo y02 inatokana na simu kutumia processor ya MediaTek Helio P22 ambayo ina nguvu ndogo

Na pia kuwa na skrini aina ya IPS LCD yenye resolution ya 720×1600 pixels

Na bodi yake upande wa nyuma na pembeni plastiki

Memori ya hii simu ina GB 32 tu na RAM ya GB 3 au 2 ambazo bado ni ndogo pia

Ina kamera moja tu yenye megapixel 8

Infinix Smart 7 Plus

Infinix Smart 7 Plus ni moja ya simu mpya ya Infinix ya mwaka 2023

Sifa zote za Tecno Pop 7 ndio sifa za smart 7 plus

Isipokuwa memori ya infinix smart 7 ina gb 64 ILA RAM yake ni ya GB 4

RAM ya GB ni kubwa kiasi ambayo inatosheleza kufungua vitu vingi

Kwa sababu hiyo bei ya infinix smart 7 plus inaongezeka kidogo

Maduka ya Vodacom wanaiuza kwa kiasi cha shilingi 260,000 (laki mbili na sitini)

Itel p17 Pro

Kwenye hii orodha itel P17 Pro ndio simu ya bei ndogo zaidi kuliko zingine zinazouzwa na vodacom

Bei yake ni shilingi 165,000 (laki moja na sitini na tano)

Hii inatokana na kutumia processor ambayo ina utendaji wa chini

Processor hiyo ni Spreadtrum SC7731 ambayo ina core nne

Processor za siku hizi huwa na idadi ya core zipatazo nane

Pia memori yake ni GB 32 na RAM ya GB 2 pekee

Inatumia kioo cha IPS LCD chenye resolution ndogo kama ilivyo kwa simu zingine zilizotangulia

Tecno Camon 20

Tecno Camon 20 ni simu mpya kabisa ambayo imetoka mwaka 2023

Ukinunua hii simu kwenye maduka ya vodacom unapata ofa GB 96

Hii ni kwa mujibu wa ukurasa rasmi wa Vodacom Tanzania

Bei yake haijainishwa hivyo ni vizuri ukawatembelea kupata taarifa zake kiundani

Lakini kiujumla inaendana kama ilivyoelezwa hapa, bei ya camon 20

Kwenye kundi hili hii ni simu ya daraja la kati na nzuri kwenye maeneo mengi tofauti na simu kuanzia namba moja hadi sita

Samsung Galaxy S23 Ultra

Hii ndio simu bora kwa hapa na moja ya simu kali duniani

Kama unataka ubora kwenye kamera, utendaji, ukaaji na chaji, network na kila kitu unachokijua wewe basi samsung galaxy s23 ultra ndio chaguo lenyewe.

Kumbuka hii sio simu ya laki mbili wala laki moja na nusu ni simu ya milioni mbili kwenda mbele

Hivyo bei yake kwenye maduka ya vodacom ni kuanzia mbili kwenda mbele

Fahamu: Ubora na Upekee wa Samsung Galaxy S23 Ultra

Maoni 18 kuhusu “Simu Mbalimbali za Vodacom Tanzania na Bei Yake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram