SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Camon 20 na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 30, 2023

Tecno Camon 20 ni simu ya mwaka 2023 ambayo imeingia sokoni mnamo mwezi Mei

Kiubora ni simu inayoweza kuwekwa kwenye kundi la kati hivyo bei yake sio sawa na matoleo ya Spark

Kwani bei ya tecno camon 20 kwa Tanzania inazidi laki tano

Ukimiliki hii simu kitu kimoja wapo utakachoweza kunufaika nacho ni kioo kizuri na kamera yenye lenzi kubwa

Unapaswa uifahamu hii simu kiundani ujue inavyotofautiana na Tecno Camon 20 Pro 5G

Bei ya Tecno Camon 20 ya GB 256

Tecno ambayo ukubwa wake unafika GB 256 kwa Tanzania inauzwa shilingi 600,000/=

Kwenye nyanja ya kioo, uimara wa bodi, ukubwa wa memori na hata kamera ina ubora unaoshahibiana kwa kiwango kikubwa na bei yake

Kwa hiyo kiwango hiki cha bei ni shindani japo simu itakumbana na changamoto kutoka kwa washindani wengine

Simu zenye bei sawa na hii baadhi huja na vitu vya ziada ikiwemo 5G ambayo haipo kwenye camon 20

Utaona washindani wake na utofauti uliopo baina yao

Sifa za Tecno Camon 20

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G85
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) Amoled
Softawre
  • Android 13
  • HIOS 13
Memori 256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
  3. QVGA
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 600,000/=

Upi ubora wa Tecno Camon 20

Camon 20 inakuja na chaji inayojaza betri kwa haraka ndani ya muda mfupi

Betri yake ni kubwa na inakaa na chaji masaa mengi

Inakuja na memori kubwa inayotosheleza kujaza vitu na kuweka applikesheni za kutosha

Ina kioo chenye uwezo wa kuonyesha rangi kwa usahihi mkubwa

Kamera zake zinatoa picha nzuri hasa kwenye mwanga mwingi

Uwezo wa Network

Upande wa network simu inaendana na toleo la Tecno Spark 10 Pro

Kwa sababu camon 20 inasapoti mpaka mtandao wa 4G aina ya LTE Cat 7

Kasi ya LTE Cat 7 ni 300Mbps sawa na 37.5MBps yaani kama unapakuwa faili la ukubwa wa MB 750 simu itachukua sekunde 20 tu kumaliza

Pia kasi ya ku-upload(kupakia) ni 100Mbps, bado ni kubwa kwa viwango vya spidi za network hapa nchini

Sio rahisi kwa hapa nchini kuweza kupata kasi hii kwenye simu za mkononi

Kwa sasa kasi hii inawezekana ukiwa na mtandao wa 5G lakini kumbuka 5G bado haijasambaa maeneo mengi

Pia simu ina masafa yote yanayotumiwa nchini hivyo laini zote zitafanya kazi

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 20

Tecno Camon 20 inatumia kioo cha AMOLED ambacho kina resolution ya 1080 x 2400 pixels

Kiubora, vioo vya amoled huwa vina usahihi na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Pia ubora wake unachagizwa na kuwa na resolution ya kiwango kikubwa

Kwa maana muonekano wa vitu ni mzuri na wa kuvutia

Pamoja na kwamba kioo chake hakina HDR10+ ama Dolby Vision bado muonekano wa vitu ni mzuri

Kama hufahamu HDR10+ unaweza pitia hapa, maana ya hdr na umuhimu wake

Nguvu ya processor MediaTek Helio G85

Processor inayotumiwa na Tecno Camon 20 katika kazi zake ni mediatek helio g85

Utendaji wake ni wa wastani kwa maana haiwezi kuwekwa kwenye kundi la chip zenye nguvu

Sababu kubwa ni aina ya muundo unaotumiwa kwenye core mbili zenye nguvu sana

Muundo uliotumika ni Cortex A75 tofauti kabisa na Camon 20 Pro 5G inayotumia muundo wa Cortex A78

Cortex A75 una matumizi madogo ya umeme lakini utendaji unakuwa unapungua

Ndio maana gemu kama  PUBG linacheza kwa resolution sio kubwa sana kwa kiwango cha 45fps

Ambapo kwa simu zenye nguvu zaidi inafika 85fps

Hata hivyo vitu vingi vitafanya kazi bila tatizo

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya hii simu ni kubwa kwani ina ujazo wa 5000mAh

Na chaji ina kasi ya wati 33 ambayo inajaza hii betri kwa muda wa dakika 70 (kutoka 0% hadi 100%)

Kwa ukubwa wa betri hii simu inakaa na chaji kwa masaa yanayozidi 14 kama ikiwa intaneti muda wote

Na kwa matumizi ya kawaida inaweza chukua hata siku bila kuisha chaji

Aina ya chaji iliyonayo ni zile usb type c(chaji zenye kichwa kipana)

Ukubwa na aina ya memori

Aina ya memori haijaainishwa kwa sababu chip iliyonayo ina sapoti UFS na eMMC hivyo ni ngumu kusema

Ila kama ni UFS ndio itakuwa nzuri zaidi. UFS ni mfumo unaisukuma data nyingi na kwa kasi

Yaani kama ukiwasha simu utaona inafunguka kwa haraka

Kiuzoefu ni kuwa memori za eMMC huwa zinafanya simu kuwa nzito kadri muda unavyokwenda na kadi memori inavyojaa

Camon 20 ipo ya aina moja tu na ina RAM ya GB 8 na memori ya GB 256

Simu inaruhusu kuongeza ukubwa wa RAM kwa kiwango cha GB 5

RAM kubwa ni muhimu kwenye simu za android maana zinakulaga memori ya kutosha

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 20

Kwenye matoleo ya Camon 20 tecno wamejitahidi kuimarisha bodi za simu na kudondokewa na maji maji

Maji ya kiwango cha kuchuruzika hayaingi  ndani ya simu

Kwani ina viwango vya IP53 vinavyoosharia uwezo wa simu kuzuia vumbi na maji ya kiwango hiko

Ila haina uwezo wa kuzia maji kupenya kama ikizama kwenye kina kikubwa na kwenye maji mengi, na hata mvua kubwa

Hivyo hauna budi kuwa makini unapokuwa kwenye mazingira ya aina hiyo

Pia bodi ya hii simu ni ya plastiki ukiweka kava itakaa muda mrefu bila kupoteza ubora wa rangi

Ubora wa kamera

Hii simu ina jumla ya kamera zipatazo tatu

Kamera kubwa ina megapixel 64 na kiuhalisia simu ina kamera moja tu

Kw maana lenzi iliyoandikwa depth huwa haipigi picha bali kazi yake kubwa ni kufanya vipimo

Ubora wa kamera ni wa kuridhisha hasa kwenye mwanga mwingi

Ila ina changamoto ya kung’arisha kitu sana hivyo ile rangi halisi inakosekana

Kwa wapenda mitandao ya kijamii hii inaweza kuwavutia maana unaweza usihitaji app ya kamera kuweka uzuri kwenye sura yako

Upande wa video hauvutiii sana kwani inaweza kurekodi video za full hd pekee na haina OIS  wala EIS kwa ajili ya kutuliza kamera wakati unarekodi huku ukiwa unatembea

Na pia ubora wa picha ni wa kawaida

Ubora wa Software

Hii simu inakuja na Android 13 na HIOS 13 kama ilivyo kwa Camon 20 Pro 5G

Hivyo kufahamu kiundani pitia, Software ya android 13 kwenye camon 20 pro 5g

Washindani wa Tecno Camon 20

Kama ilivyofafanuliwa mwanzoni Camon 20 bei yake inaipeleka simu kwenye ushindani mkubwa

Simu ya kwanza ni Redmi Note 10 yenye kioo cha amoled, kamera za ultrawide na macro na chaji ya 33W na pia kamera inayorekodi video za 4K

Wakati huo bei ya Redmi ni shilingi 400,000/=

Sifa hizi pia zinapatikana kwenye Redmi Note 12 5G ambayo bei yake ni chini ya shilingi laki sita

Simu nyingine ni Realme 10 Pro+ yenye kioo cha amoled na refresh rate ya 120Hz, HDR10+, kamera yenye gyro-EIS na processor yenye utendaji mkubwa kuliko Helio G85

Na bei ya Reame 10 Pro+ ni shilingi 521,000/= kwa hapa nchini

Na kuna matoleo mengine mengi ambayo hatuwezi kuelezea yote

Neno la Mwisho

Matoleo ya Camon yameendelea kuwa ni moja ya matoleo mazuri kwa tecno

Baadhi ya vitu muhimu ya camon 19 vimetumika pia kwenye camon 20 mfano ni processor

Kioo chake ni kizuri na kina ustadi mkubwa wa kuonyesha vitu

Ila bei yake inaizamisha simu kwenye ushindani na simu nyingi ambazo zina vitu vizuri zaidi ya hii

Maoni 21 kuhusu “Bei ya Tecno Camon 20 na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

TECNO CAMON 20 WATERPROOF

Uimara wa Tecno Camon 20 Kuzuia Maji (Waterproof)

Kama umefuatilia sifa na bei ya Tecno Camon 20, utaona kuwa ina viwango vya IP53 IP53 ni nini hasa? Kwanza neno IP kirefu chake ni Ingress Protection Inaasharia kiwango cha […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram