SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Vivo Y66 na Ubora Wake 2023

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 16, 2023

Wapenzi wa simu za bei ndogo chini ya laki mbili vivo y66 inaweza ikawa ni simu nzuri

Ni simu ambayo imetoka mwaka 2017, miaka sita imepita sasa

vivo y66 showcase

Kwa nyakati za sasa yaani 2023 ubora wa hii simu ni mdogo ukilinganisha na simu ya vivo y22

Hivyo bei yake ni chini ya laki mbili kwa maeneo mengi Tanzania na nyingi ni used

Bei ya Vivo Y66 ya GB 32

Vivo Y66 ya GB 32 kwa Tanzania ni shilingi 150,000/=

Ila unapochukua hii simu uwe na akili kichwani kuwa ni toleo la zamani

Ni ngumu kupata mpya kwa mwaka 2023

Hivyo vitu vingi havina ubora mkubwa kuanzia utendaji hadi ubora wa kamera

Na haina uwezo wa kupokea toleo jipya na betri yake si kubwa

Ndio maana bei yake ni laki moja na nusu

Sifa za Vivo Y66

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – OCTA CORE
  • Core Zenye nguvu(2) –
  • Core Za kawaida(6) –
  • GPU-
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 6
  • Funtouch OS 3.0
Memori ,32GB na RAM 3GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 13MP,(wide)
Muundo Urefu-5.5inchi
Chaji na Betri
  • 3000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 150,000/=

Uwezo wa Network

Hii simu inakubali mtandao wa 4G na mitandao mingine

Kuna taarifa finyu kuhusu processor iliyotumika

Hivyo ni ngumu sana kujua aina ya 4G ambayo inatumia

Kwa miaka ya 2017 4G za simu nafuu ilikuwa ni LTE Cat 4 yenye kasi ya 100Mbps ambayo ni sawa na 12.5MBps

Kwa maaana kama unapakuwa kitu cha GB 1.2 itachukua karibu mbili kumalizika

Kwa miaka ya sasa ni spidi ya kawaida, ina masafa yote yanayotumiwa na mitandao ya simu Tanzania

Ubora wa kioo cha Vivo Y66

Kioo cha vivo y66 ni cha IPS LCD chenye resoution ndogo ya 1280 x 720 pixels

Teknolojia imebadilika, kioo cha lcd huwa sio kizuri kama kioo cha amoled

Na pia kiwango kidogo cha resolution pia inafanya muonekano wa vitu usiwe wa kuvutia sana na wenye kukolea

Hata hivyo ni simu ambayo imepita muda kidogo tangu itoke

Hivyo huwezi  ukatarajia teknolojia ya sasa iwepo kwenye kifaa cha miaka sita nyuma

Nguvu ya processor

Vivo y66 inatumia chip yenye idadi ya core zipatazo nane

Hakuna ufafanuzi kuhusu chip ambayo simu inatumia ila ni chip yenye nguvu ndogo

Kwa maana uwezo wa kufanya vitu vikubwa kama kucheza magemu simu haina

Ni vizuri vizuri ukafikiria toleo anagalau la Tecno Spark 9 kama unapenda sana magemu

Uwezo wa betri na chaji

Simu inakuja na betri yenye ujazo wa 3000mAh

Ni betri ndogo ambayo haiwezi kukaa na chaji masaa mengi kama ukiwa unatumia intaneti masaa yote mfululizo

Ila mwaka 2017 betri hii ilikuwa ni kubwa na inayotosheleza

Simu haina chaji inayopeleka umeme kwa kasi kubwa

Hivyo utakapokuwa unaichaji itakuwa inachukua muda hata kama betri yake ndogo

Ukubwa na aina ya memori

Vivo y66 ina toleo moja tu upande wa memori ambalo lina ukubwa wa GB 32 na RAM GB 3

GB 32 kwa nyakati hizi ni ndogo na simu inaweza ikajaa kwa haraka

Hivyo utalazimika kuwa unaweka memori kadi kubwa ili kupunguza mafaili pale memori ya simu inapokaribia kujaa

Haina uwezo wa kuongeza ukubwa wa RAM kama ilivyo baadhi ya simu za siku hizi

Uimara wa bodi ya Vivo Y66

Vivo Y66 ina bodi ya plastiki na haiwezi zuia maji kama simu ikizama kwenye kina kikubwa

Kwa maana ni vizuri ukawa unaitumia simu kwa tahadhari ya kutoiangusha kizembe

vivo y66 bodi

Na utalazimika kuweka screen protekta kwa ulinzi wa kioo

Kiujumla simu haina bodi imara kiivyo

Ubora wa kamera

Simu ina kamera moja tu ambayo haina PDAF

Ina uwezo wa kurekodi video za hd

vivo y66 kamera

Haina kamera zingine kama ultrawide na telephoto

Selfie kamera yake ina ukubwa wa megapixel 16

Kitu cha kuvutia angalau ni kuwa kamera yake ina HDR ila sio kamera inayoendana na viwango vya leo

Ubora wa Software

Vivo y66 inakuja na toleo la kitambo sana la Android 6 na Funtouch Os 3.0

Kwa sasa toleo jipya la Android ni Android 13 na hivi karibuni la 14 litatoka

Hata hivyo applikesheni nyingi bado zinasapoti android 6 hivyo utapata app karibu zote za muhimu

Ila baada ya miaka kadhaa mbeleni inaweza isiwe hivyo

Yapi Madhaifu ya Vivo Y66

Simu ni ya dhamani hivyo ukilinganisha na matoeo ya simu mpya ni kuwa simu ina mapungufu mengi

Ila kubwa ni kuwa utendaji wake ni mdogo na kamera yake haina uwezo mkubwa

Kioo chake kina resolution ndogo vilevile

Neno la Mwisho

Je Vivo Y66 ni simu ya kuwa nayo 2023?

Hapana sikushauri kununua hii simu kwa sasa labda kama bajeti yako ni ndogo sana

Hii simu itakuletea shida ikiwemo ukosefu wa matoleo mapya ya android na ukaaji wa chaji mdogo

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Vivo Y66 na Ubora Wake 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu 14 mpya za Vivo za ubora mkubwa na bei zake (2024)

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka mwaka huu 2024 Vivo imeachia matoleo mengi ya simu Katika matoleo hayo yapo ya bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa Kwa maana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram