SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

March 14, 2024

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni

Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 Pro+ ni shilingi laki sita, hii ikiwa na ukubwa wa GB 256

sperk 20 pro+

Kuzijua sifa za spark 20 Pro+ itakupa picha ya jumla na sababu ya simu kuwa na bei hiyo

Na hivyo pia kuwa na ufahamu iwapo simu ina vigezo vinavyokizi mahitaji yako

Hivyo basi kitu cha kwanza tutazame sifa zake.

Sifa za Tecno Spark 20 Pro+

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Helio G99 Ultimate
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
Memori  256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera MBILI

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 0.08MP
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 650,000/=

Tutazamie ubora na udhaifu wa sifa muhimu za hii Tecno

Uwezo wa Network

Tecno Spark 20 Pro+ ni simu ya 4G kwa maana haina mtandao wa 5G

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 13 ambayo kasi yake ya juu kabisa ni 650Mbps

Iwapo kuna mtandao wa simu unaotoa kasi hii basi simu itakuwa inapakuwa mafaili kwa muda mfupi

Ila kwa sasa kasi kubwa zaidi utaipata ukiwa unatumia 5G kwa hapa Tanzania

Kwa mfano 5G ya Tigo ina kasi mpaka 1Gbps (zaidi ya 1000Mbps)

Kwa bahati mbaya 5G imesambaa maeneo machache sana nchini

Ubora wa kioo cha Tecno Spark 20 Pro+

Kioo cha Tecno Spark 20 Pro+ kina uoneshaji mzuri wa vitu na muonekano mzuri wa rangi

Kioo chake ni cha AMOLED chenye resolution ya 1080×2436 pixels

Mbali na resolution kubwa, kioo kina refresh rate inayofika 120Hz

display

Uzuri wa refresh rate kubwa huifanya simu kuwa fasta wakati wa kutachi(kuperuzi)

Ila huwa ina ulaji mkubwa wa chaji

Hata hivyo mfumo wa tecno unaruhusu kuzima na kuweka refresh rate ya kawaida

Kwa simu nyingi za gharama za mwaka 2024 zimekuwa zikitumia vioo vya LTPO AMOLED ambazo huwa na uwezo wa kudhibiti kiwango cha refresh rate kulingana na aina ya matumizi

Nguvu ya processor Helio G99 Ultimate

Nguvu ya processor ya Helio G99 Ultimate ni ya wastani

Hii ndio chip iliyotumika na simu ya spark 20 pro plus, na inacheza gemu nyingi kwa ufanisi mkubwa

Njia nzuri ya kupima nguvu ya processor ni namba za fps unapocheza gemu

Zikiwa kubwa zaidi ya 60 basi hiyo chip ni nzuri

chip

Helio G99 Ultimate inazalisha mpaka FPS 80 kwa gemu ya PUBG Mobile ila kwenye setting ndogo za graphics

Haina nguvu kubwa kama Snapdragon 8 gen 3 ila ni processor nzuri kwa simu za daraja la kati

Helio G99 Ultimate ina core mbili zenye nguvu ya wastani zinazotumia Cortex A76

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Tecno Spark 20 Pro+ ina ukubwa wa 5000mAh na chaji yake inapeleka umeme wa wati 33

Simu nyingi zenye chaji ya wati 33 hujaza betri ya simu kwa dakika 80 kama muda wa juu kabisa

Na betri ya mAh 5000 inaweza kustahimili kukaa na chaji kwa zaidi ya masaa 10

chaji

Ila kwa mpenzi wa magemu ukaaji wa chaji hauwezi kuzidi masaa kumi

Magemu huifanya processor kutumia nguvu kubwa inayotumia umeme mwingi

Chaji yake ni ya USB Type C (zile zenye kichwa kipana)

Ukubwa na aina ya memori

Kuna toleo la aina moja tu la Tecno Spark 20 Pro+ upande wa memori

Ukubwa wake wa memori ni GB 256 na RAM 8GB

Memori hii inatosheleza kuhifadhi mafaili mengi  na RAM ya GB 8 inasaidia kufungua vitu kwa wakati mmoja bila kukwama

RAM ndogo inakuwa na changamoto ya kujaa kwa haraka hivyo kuna nyakati unakuta simu inaganda ganda

Aina ya memori ya hii simu ni UFS 2.2 inayoweza kusafirisha data kwa kasi inayofika 1200MBps

Uimara wa bodi ya Tecno Spark 20 Pro+

Bodi ya Tecno Spark 20 Pro+ imetengenezwa kwa glasi upande wa mbele na nyuma kuna plastiki

Ina viwango vya IP53 vinavyoashilia uwezo wa simu kuzuia maji ya kiwango cha kuchuruzika

Ila maji yanaweza penya kama ikizama kwenye kina kikubwa

bodi

Kiujumla umakini ni kitu cha muhimu kwa hii simu

Pamoja na uwepo wa kioo upande wa mbele kununua screen protekta kutaimarisha uimara wa simu

Maana hata vioo vya Gorilla hupasuka pia

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera mbili ila kiuhalisia kamera ipo moja tu

Kamera yake ina megapixel 108 inarekodi video za resolution ya 1440p kwa fremu za 30fps

Kwa picha chache nilizoziona ni kuwa ubora wa picha ni mzuri ila kwenye kamera ya selfie kamera inang’arisha sana kiasi cha kutokutoa muonekano halisi wa kitu

Changamoto hii nimeiona kwenye simu nyingi za infinix

camera

Inawezekana ikawa kwa sababu inalenga watu wanaopenda kuposti mitandaoni

Hivyo inaondoa uhitaji wa filters

Lakini kamera inayotoa vitu kwa muonekano wa asili ndio nzuri zaidi

Ubora wa Software

Tecno Spark 14 Pro inakuja na toleo la Android 14

Kitu kikubwa kwenye toleo la Android 14 ni matumizi ya akili bandia

Ina mfumo wa akili bandia unaotengeneza wallpaper

Kwa bahati mbaya mfumo huu hautengenezi picha kwa kuandika maneno kuelezea namna picha unavyotaka iwe

Ni mfumo ndio unaotengeneza wallpapers kwa namna unavyoamua

Washindani wa Tecno Spark 20 Pro+

Tecno Spark 20 Pro+ inaenda kukutana na ushindani kutoka matoleo ya Samsung Galaxy A55, Samsung Galaxy A35, Redmi Note 13 Pro, Oppo A79

Tukianza na redmi note 13 ina sifa zinazofanana kwenye kioo na kamera

Ila ina kamera mbili za ziada zenye lenzi ultrawide na macro

Na pia inakuja na mtandao wa 5G

Ushindani upo kwenye bei, kwani Redmi Note 13 ina bei sawa na Tecno Spark 20 Pro+

Oppo A79 inazidiwa ubora wa kioo na hata kamera ila sifa nyingine zinafanana ikiwemo utendaji

Ila bei ya Oppo A79 ipo chini na ina 5G, hii inaweza mshawishi mtumiaji kutumia oppo a79 badala ya spark

Neno la Mwisho

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ inaendana na bei ya simu nyingi za daraja la kati

Na sifa zake nyingi ni za kuvutia ila kuacha kuweka mtandao wa 5G inaweza ikawa ni changamoto hasa kwa kipindi ambapo simu mpya nyingi zinatoka

Japo kwa soko la hapa nchini 5g inapatikana maeneo machache, ila simu ya 5G inampa mtu kujiamini pindi mtandao ukisambaa maeneo mengi

Maoni 5 kuhusu “Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

tecno camon premier 30

Ubora wa simu za Tecno Camon 30 na bei zake(Pro, Premier)

Tangu mwezi wa nne kampuni ya walitoa matoleo ya Tecno Camon 30 Matoleo ya Camon 30 yapo matatu ambayo ni ya daraja la kati yaani mid range Ubora wa kiujumla […]

tecno camon 30 thumb

Bei ya Tecno Camon 30 Pro na Sifa Muhimu

Simu ya Tecno Camon 30 Pro ilitangazwa mwezi februari ila imetoka rasmi mwezi wa nne 2024 Ni simu ya daraja la kati(midrange) hivyo bei yake sio sawa na Tecno matoleo […]

tecno camon 30 premier thumbnail

Bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G na Sifa zake muhimu

Kwenye matoleo bora ya simu kutoka Tecno, matoleo ya Tecno Camon huja na ubora katika vipengele vingi Hata bei za matoleo ya Camon huzizidi bei za Tecno Spark na Tecno […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company