Tecno Camon 18 ni tecno macho matatu ya mwaka 2021 iliyoborehswa ubora kutoka kwa Camon 17
Ubora uliongezeka unaifanya bei ya tecno camon 18 kuzidi shilingi laki nne.
Lakini upande wa sifa za msingi unaifanya bei yake ionekane kubwa
Kwenye hii posti utafahamu bei camon 18 na sifa zake kwenye idara muhimu.
Ukijua sifa za simu itakusaidia kujua ubora wake na kufanya maamuzi sahihi
Bei ya Tecno Camon 18 Tanzania
Kwa dar es salaam maeneo ya kinondoni bei Tecno camon 18 ya ukubwa wa ukubwa GB 128 na ram GB 4 ni shilingi 445,000/=
Maduka ya simu ya kariakoo yanaiuza simu kwa 460,000/=
Ongezeko la bei linachangiwa na maboresho ya kwenye utendaji, kamera na kimo cha simu.
Lakini ukizitazama sifa za camon 18 kiundani utangundua kuwa ni simu moja na camon 17
Zifuatilie kwenye jedwari na ufafanuzi wake
Sifa za Tecno Camon 18
Sehemu Za Simu | Sifa za Simu |
---|---|
Network | 2g, 3g, 4g |
Processor(SoC) |
|
Display(Kioo) | IPS LCD, Refresh rate:90Hz |
Softawre |
|
Memori | 128GB, RAM 6GB,4GB |
Kamera | Kamera TATU
|
Muundo | Urefu-6.8 inchi |
Chaji na Betri |
|
Bei ya simu(TSH) | 460,000/= |
Upi ubora wa Tecno camon 18
Ubora wa simu ya tecno camon 18 upo kwenye maboresho ya software, kamera na processor.
Camon inakuja na toleo jipya la HiOS.
Utendaji wa simu umeongezeka ukifananisha Camon toleo la 17
Simu ina betri inayokaa na chaji masaa mengi
Resolution za kamera zimeongezwa ubora
Simu ni ndefu na ina muonekano wa kuvutia macho
Lakini sehemu zingine hazina tofauti na mtangulizi.
Fuatilia ufafanuzi wa kila sifa kuielewa camon 18 na 17 ufanano wao
Uwezo wa Network
Moja ya simu ya 4G aina ya LTE Cat 7 ni Camon 18
Simu yenye Cat 7 ina uwezo wa kudownload faili kwa spidi ianyofikia 300Mbps
4G yake inakubali intaneti ya 4g ya mitandao yote ya Tanzania.
Kwa sababu ina masafa yanayotumika hapa nchini
Ubora wa kioo cha Tecno camon 18
Kioo cha Tecno camon 18 ni cha aina ya IPS LCD chenye refresh rate ya 90Hz
Ni kiasi kinachoifaya simu kuwa fasta ukiwa unaigusa kwenda chini na juu (ku-scroll)
Ubora wa kioo unanogeshwa na resolution kubwa ya 1080 x 2460 pixels
Hivyo vitu vitaonekano kwa uzuri japo simu haina HDR10
Uangavu wake sio mkubwa kiasi cha konyesha vitu kwa ustadi simu ikiwa juani
Kiujumla kioo cha ips lcd huwa na ubora mdogo ukifananisha na vioo vya oled vya simu za sony xperia
Nguvu ya processor MediaTek Helio G88
Utendaji wa simu ya Tecno camon 18 unaweza kucheza gemu kubwa nyingi.
Hilo inasababishwa na simu kutumia chip ya Helio G88.
Helio G88 ni processor ya simu yenye core nane zilizo gawanyika katika sehemu mbili.
Sehemu za core kubwa ndio inachangia simu kuwa na uwezo mzuri kiutendaji.
Na sehemu ya core ndogo unaifanya simu kuwa na matumizi madogo ya betri
Core kubwa zina spidi inayofikia 2.0 GHz na ni za aina ya Cortex A75
Na core ndogo zina spidi inayofikia 1.8 GHz na za aina ya Cortex A55
Cortex A75 ina uwezo mkubwa wa wastani.
Kama unataka kujua aina ya processor, basi pitia hapa jinsi ya kujua uwezo wa processor za simu
Uwezo wa betri na chaji
Camon 18 ina betri kubwa lenye ujazo wa 5000mAh
Hili ni aina ya betri linalokaa na chaji muda mrefu
Ila chaji yake haipeleki umeme mwingi.
Kwani unajaza chaji kwa wati 18.
Hivyo simu inaweza kuchukua muda mwingi mpaka kujaa kwa asilimia 100
Ukubwa na aina ya memori
Kuna matoleo ya aina mbili ya Tecno hii zenye ukubwa wa GB 128
Kinachotofautiana ni ukubwa wa RAM
Kwani ipo yenye ram ya 4GB na ram ya 6GB
Lakini haijainishwa aina ya memori kama ni eMMC 5.1 au UFS 2.1
Uimara wa bodi ya Tecno Camon 18
Bodi ya simu imeundwa kwa plastiki upande wa nyuma
Na kwenye display kuna glasi lakini sio kioo cha gorilla
Pia simu inakosa uwezo wa kuzuia maji kupenya kama ikizamishwa kina kirefu
Simu ni ndefu, upana na urefu wake ni inchi 6.8
Ubora wa kamera
Tecno camon 18 ina kamera zipatazo tatu.
Huku kamera kubwa ikiwa na resolution ya 48MP
Na inatumia teknolojia ya ulengaji aina ya PDAF
PDAF hailengi vizuri vitu vinavyotembea kwa kasi ukilinganisha na dual pixel pdaf
Kamera nyingine ya depth ina pixel chache.
Hii ni kamera inayotumika kukadiria umbali kati ya simu na kitu kinachoigwa picha
Na pia simu ina kamera ya macro kwa ajili ya kupiga picha vitu vya karibu sana na kamera
Kiujumla kamera zake si nzuri sana hasa upande wa kurekodi video
Kwani inarekodi video za full hd pekee na hazina OIS
Ubora wa Software
Camon 18 inakuja na toleo la android 11 lenye mfumo wa HIOS 8.0
HIOS 8.0 inakupa kitu kinaitwa “Always On Display”
Always On Display huonyesha taarifa ya baadhi ya app bila kufungua simu.
Kama kuna meseji mpya basi screen itaonesha idadi ya meseji zilizoingia
Yapi Madhaifu ya Tecno camon 18
Simu haina kamera ya kupiga eneo pana sana kwa nyuzi 120
Hizi ni kamera zinazofahamika kama ultrawide.
Pia Tecno wameendelea kutumia ulengaji aina ya pdaf
Simu inaweza kuingia maji kwani haina ulinzi hata wa kuzuia maji tiririka
Kioo chake kinakosa uwezo wa kuboresha muonekano wa vitu kwa maana haina HDR10
Kamera za hii simu haziwezi kurekodi video za 4K
Utendaji wa processor bado ni wa wastani wakati huo bei yake imepanda kidogo
Neno la Mwisho
Tecno Camon 18 ni simu nzuri ya Tecno kati ya tecno mpya za 2021 na 2022.
Ila bei yake inamshawishi mtumiaji kutafuta simu mbadala
Kuna simu kama ya Vivo t1 5g inaendana bei na camon 18
Lakini camon 18 haisogei kiubora kwa vivo t1
Hivyo tecno wanapaswa waishushe bei ya simu.
Lakini kwa mtu anaejali ukubwa wa memori pekee basi simu ina bei rafiki sana
Maoni 2 kuhusu “Bei ya Simu ya Tecno Camon 18 na Sifa Muhimu (2022)”
Umeongea mambo mengi safi sana nmeelewa mno ahsante
Ahsante kwa uchanganuzi , ni mtu makini mwenye maarifa mengi, hongera!