SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy Note 10 na Ubora wake 2023

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 17, 2023

Samsung Galaxy Note 10 ilitoka kwa mara ya kwanza mwaka 2019

Inaenda miaka minne na kuna matoleo mengi na mazuri yametoka ya simu kama Oppo A78

Pamoja na umri mkubwa bado Galaxy Note 10 inachuana na kuziacha nyuma simu nyingi

samsung galaxy note 10

Ndio maana bei ya samsung galaxy note 10 kwa Tanzania bado ni kubwa na inazidi laki saba dukani

Hapa utaelewa nyanja ambazo zinaendelea kuziweka hizi simu kwenye chati hasa ukiangalia sifa zake

Bei ya Samsung Galaxy Note 10 ya GB 256

Kwa Dar Es Salaam simu inauzwa kwa shilingi 750,000 ambayo memori yake ni GB 256

Ukitazama bei yake inaendana na simu ya na simu Tecno Camon 19 Pro 5G ila kisifa samsung iko vizuri maeneo mengi

Kuanzia kamera, kioo mpaka uwezo wa 4G ni wa kasi kubwa

Kitu utakochokosa kwenye hii simu ni 5G  na betri yake ambayo sio kubwa

Ila ni simu inayoweza kukidhi haja nyingi za mtumiaji kwa mwaka 2023 pasipo kuwa na shida

Sifa za Samsung Galaxy Note 10

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 9825
  • Core Zenye nguvu sana(2) – 2×2.73 GHz Mongoose M4
  • Core Zenye nguvu(2)-2×2.4 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.9 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G76 MP12 
Display(Kioo) Dynamic Amoled
Softawre
  • Android 9
  • One UI 4
Memori UFS 3.0, 256GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 12MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(Telephoto)
  3. 16MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.3inchi
Chaji na Betri
  • 3500mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 750,000/=

Upi ubora wa samsung galaxy note 10

Ni simu ambayo haipitishi maji kama ikizama kwenye kina kikubwa

Ina kioo kinachoonyesha vitu kwa uzuri na kwa rangi sahihi kwa kiwango kikubwa

Ina mgawanyo wa kamera unaokupa machaguo wa kupiga picha za umbali tofauti tofauti

Ubora wa picha bado ni mkubwa ukilinganisha na simu nyingi za hivi karibuni

Inapokea matoeo ya hivi karibuni ya android

Ina mfumo wa memori unaosafirisha data kwa kasi hivyo simu kuwa nyepesi

Chaji yake ina peleka umeme mwingi

Kiufupi simu ina kasoro chache ambazo zinasababishwa na hatua kubwa iliyopigwa hivi karibuni kwenye simujanja

Tuitazame kiundani kwenye nyanja zingine muhimu

Uwezo wa Network

Hii simu inasapoti mtando mpaka wa 4G aina ya LTE Cat 20

Kasi ya LTE Cat 20 ni 2000Mbps ambayo ni sawa na 250MBps

Kwa mfano kama ukipakuwa applikesheni ya whatsapp, simu itachukua chini ya sekunde moja kumaliza kudownload

Kwa bahati mbaya sio rahisi kuipata kasi hii kwa hapa Tanzania

Inakubali masafa yote ambayo yanatumika hapa nchini

Kwa kuwa simu ilikuwa ni ya 2019 basi 5G haiwezi kutumika humu

Ila kama unatamani 5G kuna samsung galaxy a54 yenye sifa nzuri zaidi ya hii

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy Note 10

Kioo cha Galaxy Note 10 ni aina ya Super Amoled ambacho kina reoslution kubwa ya 1080 x 2280 pixels

Kiwango cha resolution kinazidi baadhi ya simu mpya za 2023 ambazo hutumia 720 x 1660 pixels

Pixels nyingi huongeza uangavu na muonekano safi wa picha na video zinazonekana kwenye kioo

Uzuri mwingine wa kioo cha hii simu ni kuwa kina HDR10+

samsung galaxy note 10 display

HDR10+ husaidia kioo kuweza kutofautisha kwa uzuri kati ya rangi nyeusi kama vile kivuli na rangi nyeupe kama vile jua

Kitu kinachosababisha muonekano wa vitu huendane na mazingira halisi ya kitu kinavyoonekana

Ni nadra hata kwa simu za daraja la kati za 2023 kukuta walau HDR10

Mara nyingi huwa wanaweka refresh rate kubwa

Nguvu ya processor Exynos 9825

Simu inatumia chip ya Exynos 9825 kwa zile ambazo zilikuwa zinauzwa nje ya Marekani na China

Kwa soko la china na USA walikuwa wanapata samsung zinazotumia chip ya Snapdragon 855

Chip zote zina mfanano kwani zimegawanyika katika sehemu tatu, sehemu mbili zinatumia muundo wa Cortex A75 isipokuwa core kubwa zina kasi inayofika 2.73GHz

samsung galaxy note 10 processor

Kwa miaka ya hivi karibuni muundo wa cortex a75 haiwezi kuchukuliwa kuwa na nguvu

Kwani kuna miundo mipya kama Cortex A78 ambayo inapiga kazi kubwa na kwa matumizi madogo ya betri ya simu

Hata hivyo bado inaweza kufungua app nyingi kwa wakati mmoja na kucheza magemu mengi bila tatizo

Kama utendaji ni msisitizo mkubwa kwako ni vizuri ukaangalia simu kama Tecno Phantom X2 Pro yenye processor yenye nguvu kuliko hii

Ila bei pia lazima ipande

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Samsung galaxy note 10 ina ukubwa wa wastani tu wa 3000mAh

Ni betri ndogo hivyo ukaaji wa chaji sio mkubwa kwa sababu ya betri

Chaji inapeleka umeme wa wati 25 kiwango cha juu ambayo inajaza betri kwa haraka

Ukizingatia kuwa betri sio kubwa hivyo simu itawahi kujaa tu

Ukiwa unaperuzi intaneti muda wote simu inaweza kuchukua masaa takribani 11 kuisha chaji

Siku hizi simu nyingi zinakuja na betri kubwa na betri na zenye wastani wa ukaaji wa chaji wa masaa zaidi ya 15 ikiwa kwenye intaneti

Ukubwa na aina ya memori

Upande wa memori simu ina toleo moja tu

Toleo hilo lina ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 8

Na aina ya memori simu iliyonayo ni UFS 3.0 ambayo kasi yake ya usafirishaji wa data ni 2400MBps

Kiwango hiki kinafanya app kufunguka kwa haraka na simu kuwahi kuwaka pindi ukiwasha

Ukubwa wa memori ni wa kutosheleza kuhifadhi mafaili mengi na applikesheni za kutosha

Ukitaka kuongeza memori kadi hutoweza kwa sababu simu haina sehemu ya kuweka memori kadi

Hivyo tumia simu vizuri ila GB 256 ni kubwa pia

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy Note 10

Samsung Galaxy Note 10 haina bodi ndefu sana kutokana na urefu wake kuwa ni inchi 6.3

Upande wa nyuma na mbele imewekewa vioo aina ya gorilla 6 kutoka kampuni ya Gorilla ya marekani

Hivi huwa ni vioo vigumu kuchunika, hataka ukiweka sarafu pamoja na hii simu mfukoni sio rahisi kwa mikwaluzo kutokea

samsung galaxy note 10 body

Simu imethibitishwa na viwango vya IP68 ambavyo humaanisha kuwa simu haiwezi kupitisha maji iwapo itazama kwa kina cha mita moja na nusu kwa muda wa dakika 30

Kwa mantiki hiyo bodi ya galaxy note 10 ina bodi imara inayosaidia simu kukaa muda mrefu

Ubora wa kamera

Simu ina mfumo mzuri wa kamera kwani kuna lenzi ya telephoto kwa ajili ya kupiga kitu kilichopo mbali na kamera

Pia lenzi ya Ultrawide kwa ajili ya kupiga eneo kwa upana mkubwa mfano mkutano wa hadahara

Na pia kamera ya kawaida na kamera zote zina megapixel 12 ila ultrawide ina megapixel 16

Kumbuka kuwa simu yenye kuanzia megapixel 8 inaweza kupiga picha yenye ubora mkubwa na kurekodi video za 4K

samsung galaxy note 10 kamera

Inategemea kama vitu vingine vinapatikana kwenye kamera kuanzia ulengaji kama dual pixel pdaf, ois, mpaka ubora wa app inayopiga picha

Kwenye mwanga mwingi galaxy note 10 inapiga picha na rangi sahihi za vitu bila kuathiriwa na mwangaza mwingi wa jua

Japo kuna kuzidisha fulani kwa rangi ya anga na kufanya kuonekana ya bluu sana

Kiwang cha chengachenga (noises) ni ngumu kuonekana

Pia simu inaweza kurekodi video mpaka za 4K ambazo huwa na ubora mzuri unapotazama kwenye tv ya 4K

Ubora wa Software

Kama simu ikiwa mpya inakuwa na Android 9

Ila inasapoti mpaka toleo la miaka ya hivi karibuni la Android 12

Kuna simu nyingi tu za mwaka 2023 zinakuja na Android 12, hii ina maana simu itaendelea kutumia apps nyingi bila shida yoyote kwa miaka mingi ijayo

Mbali na android simu pia ina mfumo wa One UI 4.0

Ni mfumo mwepesi usiokuwa na matangazo kama baadhi ya kampuni zingine zinavyofanya

Washindani wa Samsung Galaxy Note 10

Kuna machaguo mbadala na yenye sifa zinazoendana na Galaxy Note 10

Kiujumla karibu sote mpya za laki nane ni washindani wa hii samsung

Lakini kwa kuzingatia muktadha wa mwaka simu iliyotoka washindani sahihi ni Apple iPhone XS, Xiaomi Mi 9, OnePlus 7 Pro na Samsung Galaxy S10

Hizi simu zina vitu karibu vyote vilivyopo kwenye note 10

Na baadhi ya hizo zinapatikana kwa bei ya chini

Neno la Mwisho

Pamoja na uzuri wa hii simu ila jua kwa sasa nyingi ni simu used na sio mpya

Kama ukifanya maamuzi ya kuimilii weka akilini kuwa hutoweza kuipata hii simu ikiwa mpya kwa sasa

Hivyo unavyonunua jaribu kuichunguza simu kwa makini kuhakikisha hununui kitu kibovu kitakachokusumbua mbeleni

Maoni 3 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy Note 10 na Ubora wake 2023

  • Nimeusubiri uchambuzi wa Hii simu kwa muda lakini nikaona kimya nikashawishika kuamia kampuni ya Xiaomi kwa sasa,nlitaka kununua hii simu ila,baada ya kuona simu hizi nyingi ni used nimeachana nazo
    Ila asante kwa uchambuzi wako unatufundisha mengi

  • Naweza kununua simu za Samsung Galaxy Kwa kulipia kidogo kidogo?.Na ni njia ipi naweza kuitumia kujua fake na original Samsung Galaxy?

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram