SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Smart 6 na Sifa za Muhimu 2023

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 20, 2023

Simu ya Infinix Smart 6 ni simu ya mwaka 2021 hivyo ni miaka miwili imepita

Kipindi imetoka ilikuwa inauzwa kwa bei nafuu

Kwa maana hiyo bei ya infinix smart 6 kwa mwaka 2023 haizidi laki mbili na nusu.

Ni simu ambayo inamlenga mtumiaji asiyehitaji mambo mengi

Ndio maana ukitazama sifa zake utakutakana na vitu ambavyo vina ubora wa kawaida sana

Bei ya Infinix Smart 6 ya GB 32

Infinix Smart 6 ambayo ukubwa wake ni GB 32 na RAM ya GB 2 inauzwa shilingi 250,000/=

Bei hiyo itatofautiana kutokana na maduka kwa hapa Tanzania

Sehemu zingine simu inapatikana chini ya hapo

Utakapoamua kuimiliki hii simu usitarajie kupata ubora mkubwa kama uliopo kwenye simu mpya za samsung galaxy au tecno za bei kubwa

Ni simu kwa ajili ya matumizi madogo madogo yaani inafaa kuwapa wazazi

Sifa za Infinix Smart 6

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Unisoc SC9863A
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×1.6 GHz Cortex-A55
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.2 GHz Cortex-A55
  • GPU-IMG8322
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11 (Go Edition)
  • XOS 7.6
Memori  64GB,32GB na RAM ,3GB,2GB
Kamera Kamera nne

  1. 8MP,AF(wide)
  2. 0.8MP(depth)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-10W
Bei ya simu(TSH) 250,000/=

Upi ubora wa Infinix Smart 6

Hii ni simu inayokaa na chaji muda mrefu kwani ina betri kubwa

Na pia ina chip yenye matumizi madogo ya betri

Ni simu ya bei nafuu yenye mtandao wa 4G

Baadhi ya simu za bei nafuu huishia kuweka 3G pekee yake

Ni simu ndefu inayokupa muonekano mkubwa wa vitu

Kama ni mtu unayependa kusoma vitabu, maandishi yake yataonekana kwa ukubwa stahiki

Mambo mengine ni ya viwango vya kawaida kama ilivyotangulia kuelezwa

Uwezo wa Network

Infinix Smart 6 inasapoti mitandao yote mpaka 4G kasoro 5g

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 7 yenye kasi ya kudownload 300Mbps sawa na 37.5MBps

Kwa maana kama unaweka whatsapp kwenye simu itachukua sekunde mbili simu kuiweka hiyo app

Spidi hii sio rahisi kuipata kwa nchini kwetu, ila pia ukifananisha na simu nyingine unaona kabisa uwezo wa network sio mkubwa kivile

Inakubali masafa yote ya simu yaliyopo nchini

Hivyo hakuna laini ya simu itakayokwama kutumika

Ubora wa kioo cha Infinix Smat 6

Kioo Cha Infinix smart ni IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1600 pixels

Kiwango Cha resolution sio kikubwa na pia vioo LCD huwa sio vizuri hasa kikiwa na resolution

Kwa maana hiyo muonekano wa rangi za vitu hautokuwa wa kuvutia kama ilivyo kwenye vioo vya amoled.

Uangavu wa kioo unafika mpaka nits 500

Hii inamaanisha vitu vinaonekana kwa uzuri kiasi ukiwa unaitumia simu kwenye mazingira yenye miale mingi ya jua

Kioo Cha hii simu Haina vitu vingine kama HDR, refresh rate kubwa nk

Nguvu ya processor Unisoc SC9863A

Simu inatumia processor ya unisoc sc9863a katika kufanya kazi zote

Hii processor imegawanyika sehemu mbili na zote zinatumia muundo wenye nguvu ndogo

Muundo huo wa core huitwa Cortex A55.

Hii chip inakosa nguvu kubwa japo Ina core zinazofika mane

Simu ikiwa na mafaili mengi na app nyingi zikiwa zinajifungua kwa pamoja usishangae ukakutana na simu kuwa nzito

Hii chip sio nziri kwa mpenzi wa magemu makubwa ya mapigano

Hiki kitu kinaifanya simu iwe inamfaa mtu anayetumia simu kwa shughuri za kawaida

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Infinix smart 6 Ina ukubwa wa 5000mAh

Ina chaji inayopeleka umeme kwa Kasi ya wastani ya wati 10

Kwa sababu betri ni kubwa, spidi ya chaji inaijaza betri kwa masaa yanayozidi matatu

Kutokana na simu kuwa na chip yenye nguvu ndogo na kioo chenye resolution ndogo ukaaji wa chaji ni mkubwa.

Simu ikiwa inatumia intaneti inaweza kukaa kwa masaa zaidi ya 14

Ukubwa na aina ya memori

Infinix Smart 6 IPO za aina mbili upande wa memori

Ndogo kabisa Ina GB 32 na Ram ya GB 2

Wakati kubwa Ina GB 64 na Ram ya GB 3

Ni vizuri ukachukua yenye GB 64 kwa sababu ya GB 32 ni ndogo na RAM yake itakuletea shida mbeleni

Mfumo wa android hutumia RAM nyingi na kumbuka kuna kiwango Cha memori kinatumiwa na mfumo endeshi pamoja na app zinazokuja na simu.

Hivyo utakuta kuna kiwango kikubwa Cha memori hutoweza kukitumia

Uimara wa bodi ya Infinix Smat 6

Bodi ya hi simu imeundwa kwa plastiki upande wa nyuma na pembeni

Na Haina viwango vya IP vinavyoonyesha uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi kuingia ndani ya simu

Bodi za plastiki wakati mwingine huwa ni rahisi kupoteza rangi zake

Ni vizuri ukawa unatumia kava muda mwingi kuitunza thamani ya simu

Pia ni vizuri kuweka screen protekta kwa sababu simu Haina vioo vigumu kama vya gorilla

Ubora wa kamera

Kamera za Infinix smart 6 zipo mbili ila kiuhakisia kuna kamera moja

Kwa sababu lenzi ya kamera ya pili kazi yake huwa ni kupima kiundani kitu kinachotakiwa kupigwa picha na umbali wa kamera ulipo

Kamera hizi huitwa depth, huwa hazina umuhimu miaka ya Sasa

Kamera ya kubwa Ina megapixel 8 huku ikiwa Haina ulengaji wa PDAF

Kama unampiga picha mtu anayekimbia au gari, picha yake inaweza isitokee vizuri

Mfumo mzima wa kamera sio wa kuridhisha kiuhakisia

Upande wa video kamera zinaweza kurekodi video za full hd pekee

Na pia hakuna OIS kitendo kitachohitaji kutuliza mkono wakati unarekodi kitu huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Hii simu ingekuwa ni nzito kupitiliza kama ingekuwa inatumia mfumo endeshi wa Android unaotumiwa na simu zingine.

Kuepuka Hilo, Infinix Smart 6 imewekewa mfumo wa Android 11 Go Edition

Go Edition ni mfumo wa android unaowekwa kwenye simu zenye ram na processor zenye nguvu ndogo

Mfumo unasaidia kiasi Fulani hivyo simu kuwa nzito itakuwa ni kwa kiasi kidogo.

Android Go Edition inakuja na vitu ambavyo vimepunguzwa

washindani wa Infinix Smat 6

Kama wewe ni mnunuaji basi inabidi uzifuatilie baadhi ya simu zinazoendana sifa

Simu hizi zina bei zinazoendana na sifa zinazopishana kidogo

Baadhi ni nzuri kuliko smart 6.

Simu hizi ni Samsung Galaxy A02, Redmi 9A, Samsung Galaxy A10 na Tecno Spark 8C

Kwenye hiyo kuna zenye sifa nzuri zaidi na bei ya kuvumilika

Neno la Mwisho

Iwapo wewe matumizi yako ni kupiga simu, kuingia Whatsapp, YouTube, kuwasiliana n wati mbalimbali, hii simu itakupunguzia mzigo wa kumiliki simu janja.

Ila kama kipaumbele chako ni kamera, memori kubwa, magemu na kazi zingine nzito ni Bora ukatafuta chagua mbadala

Tena simunzuri.com imefafanua matoleo mengi na sio mbaya ukauliza nasi tutakujibu kwa kadri ya uwezo wetu.

Maoni 10 kuhusu “Bei ya Infinix Smart 6 na Sifa za Muhimu 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram