SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya Redmi Note 10 Pro (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 16, 2022

Simu ya Redmi note 10 pro ni simu ya android ambayo ilitoka mwanzoni mwa mwaka 2021.

Mpaka kufikia sasa, hii simu inazizidi matoleo mapya mengi ya simu ikiwemo infinix note 11 pro

Pitia kwa umakini na tazama ubora wake kwenye display, memori, chaji na betri na utendaji wa processor.

Jambo utakaloliona ni kuwa redmi note 10 pro inazipita simu nyingi za android 11 na 12 zilizotoka 2022

matoleo ya redmi note 10 pro

Bei yake inavumulika sana kwa kutazama sifa za simu.

Kwani bei ya redmi note 10 pro ni chini ya laki sita kama ikinunualiwa toka nje ya nchi ila sio Tanzania

Bei ya Redmi Note 10 Pro Tanzania

Bei ya redmi note 10 pro kwenye maduka ya mitaa msimbazi kariakoo ni shilingi 850,000/=

Hii ni kwa redmi ya GB 128 na ram GB 6

Bei inashuka zaidi kama utainununua kwenye mtandao wa aliexpress

Kwani utaipata simu hii kwa bei ya shilingi 562,000/=

Na note 10 pro ya gb 128 na ram gb 8 inapatikana kwa 593,000/=

Ikiwa hauna haraka agiza redmi note 10 pro aliexpress ni rahisi sana

Sifa za Redmi Note 10 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 732G
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.3 GHz Kryo 470 Gold
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Kryo 470 Silver
  • GPU-Adreno 618
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 11
  • MIUI 12
Memori UFS 2.2, 128GB,64GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera nne(redmi macho manne)

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro),AF
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 562,000/=

Upi ubora wa simu ya Redmi note 10 pro

Ubora wa simu aina ya redmi note 10 pro upo kwenye utendaji wa processor.

taarifa za redmi note 10 pro

Simu ina processor yenye nguvu ya kufungua app yoyote kiurahisi.

Ina kioo kizuri kinachokoleza rangi kwa kiwango stahiki kinachoonyesha vitu kwa uhalisia

Kioo chake ni chepesi sababu ya kuwa na refresh rate kubwa

Chaji yake inajaza simu kwa dakika chache

Bei yake ni rafiki na na simu yenye vitu ambavyo zamani vilipatikana kwenye simu za daraja la juu

Ina utendaji mkubwa wa memori kwani inasafirisha data kwa kasi

Uwezo wa Network

Simu ya redmi note 10 pro inakubali aina zote za network kasoro mtandao wa 5G ambao haupo hapa Tanzania kwa sasa

Aina ya 4G simu inayokuja nayo ni LTE Cat 15

simu redmi note 10 pro upande wa network

4G ya LTE cat 15 inaweza kudownload faili kwa kasi inayofikia 800Mbps ambayo ni sawa na 100MB/s

Kama mtandao wa simu unakupa spidi hii basi inachukua sekunde 1.3 kupakua faili la ukubwa wa 1300MB

Simu ina network bands za 4G zipatazo 13

Na inakubali mitandao yote ya simu ya Tanzania unapotumia intaneti ya 4G

Ubora wa kioo cha Redmi note 10 pro

Amoled ndio kioo cha redmi note 10 pro ambacho hukoleza rangi kwa ustadi.

Amoled ni aina ya vioo vilivyo na contrast kubwa.

Contrast kubwa inafanya kioo cha simu kuwa na rangi nyingi

Hivyo vitu vinaonekana kwa uhalisia kwa kiasi kikubwa.

kioo cha redmi note 10

Kioo chake pia kina mfumo wa HDR10.

HDR10 huboresha muonekano wa rangi za vitu

Kiasi cha kuisadia simu kuweza kuonyesha vitu kama vinavyoonekana na jicho la binadamu

Na amoled ya hii simu ina resolution nzuri na kubwa yenye pixels 1080×2600

Unaposcroll(kuperuzi) kioo kipo fasta kwa sababu ya kuwa na refresh rate inayofikia 120Hz

Nguvu ya processor Snapdragon 732G

Ubongo wa simu ni processor.

Simu inayotumia processor yenye nguvu huwa bora kwenye nyanja karibu zote

Redmi note 10 pro inatumia processor ya snapdragon 732G

Ni processor ya daraja la kati inayoipita utendaji Helio G95 ya infinix note 10 pro

Na inaipita pia snapdragon 675 ya redmi note 10

processor ya simu ya redmi note 10 pro

Kwani alama zake kwenye app ya Geekbench zinafika 570 kwenye core moja

Kiujumla ni processor yenye core nane iliyogawanyika sehemu mbili

Ina core kubwa na core ndogo

Uwezo wa core kubwa

Kiutendaji, core kubwa inapiga mzigo kwa nguvu kubwa sana.

Nguvu inayoifanya simu kuweza kucheza gemu nyingi na za aina yoyote.

Hii inasababishwa na uwepo wa core mbili zenye nguvu ambazo zina spidi inayofikia 2.3GHz

Na nguvu kubwa kiutendaji inachangiwa na kutumika kwa muundo wa Kryo 460 ambao ni Cortex A76 iliyoboreshwa.

Cortex A76 ni core zenye nguvu na matumizi madogo ya chaji.

Japokuwa kiuwezo ipo nyuma ya processor ya simu aina ya MediaTek Dimensity 1200

MediaTek Dimensity 1200 ina Cortex A78 na imetumika kwenye simu ya vivo v23 pro

Uwezo wa core ndogo

Kuna jumla ya core ndogo sita.

Core ndogo zinamatumizi ya chini ya betri.

Hivyo inafanya simu kutumia umeme kidogo wakati wa kupiga simu

Kwa sababu kazi ndogo hutumia hizi core sita

Na matumizi madogo ya umeme yanachangiwa na kutumika kwa core aina ya Cortex A55.

Na pia core ndogo kuwa na kasi ya chini isiyozidi 1.8GHz

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya redmi note 10 pro inaweza kukaa na chaji kwa takribani masaa 118 endapo simu haitumiki mara kwa mara

Na ikiwa inatumia intaneti masaa yote simu inakaa na chaji masaa 14

Jifunze: ukaaji wa chaji wa redmi note 10 pro

Betri yake inapeleka umeme kwa kasi inayofikia wati 33

Kwenye simu hii, kasi ya wati 33 inajaza betri kwa 100% ndani ya dakika 81

Ni fasti chaji hii.

Ukubwa na aina ya memori

Memori ya redmi note 10 pro inasafirisha data kwa kasi kubwa inayoifanya simu kuwaka kwa haraka

Hii inasababishwa na memori aina ya UFS 2.2 ambayo ina spidi ya kuandika inayofikia 1200MB/s

Utendaji wa simu unategemea pia kasi ya memori kuandika na kusoma data kifupi kusafirisha data

Simu imegawanyika katika aina tatu upande wa memori

  1. Redmi note 10 pro ya GB 64 na RAM GB 6
  2. Redmi Note 10 Pro ya GB 128 na RAM GB 6
  3. Redmi Note 10 Pro ya GB 128 na RAM GB 8

Memori kubwa maana yake utahifadhi vitu vingi.

Ram kubwa inaongeza ufanisi kiutendaji wa simu

Uimara wa bodi ya Redmi note 10 pro

Bodi yake ni imara na ngumu kuharibika ama kupasuka kirahisi.

Ugumu wa bodi unachangiwa na simu kuundwa kwa vioo vya Gorilla Glass 5

Vioo vya gorilla 5 vinaweza visipasuke kabisa kama simu ikianguka kwa kimo cha mita 1.2 kutoka juu

Hutohitaji kuwa na screen protector wala kava.

Kwa sababu upande wa nyuma unalindwa pia na kioo cha gorilla glass

Binafsi, nimesoma materio yaliyounda kioo cha gorilla na kutazama majaribio ya kudondosha simu na maoni mengi ya watu.

Simu zenye vioo vya gorilla huwa ni imara na ngumu

Pia simu inaweza kuzuia maji yanayotiririka na vumbi pia kwani ina IP53

Ubora wa kamera

Hii ni simu ya redmi ya macho manne.

Kamera moja ina sensa kubwa kiasi cha 108MP

Kitu kinachopunguza ubora wake wa kamera ni kutumia teknolojia ya ulengaji ya PDAF

kamera ya redmi note 10 pro

PDAF ni nzuri lakini haiwezi kutoa picha nzuri sana kwa kitu kinachotembea kwa kasi kikiwa kinapigwa picha kama ndege mnyama

Simu inatoa picha nzuri za mchana na usiku

Japo nyakati za usiku kuna uwepo kiasi kidogo cha noises

Zitazame picha zilizopigwa na simu ya redmi note 10 pro

Pia fuatilia, simu zenye camera bora

Ubora wa Software

Redmi note 10 pro ni simu ya android 11 inayokuja na mfumo wa MIUI 12

Simu inakubali toleo jipya la android 12 na MIUI 13

Kama ukifanikiwa kuweka android mpya utapata vitu vya ziada kama uwezo wa kuonyesha app zinazotumia mic.

Na utaweza kutambua app zinazokutraki

Yapi Madhaifu ya redmi note 10 pro

Simu haziwezi kuzuia maji endapo umeizamisha kwenye kina cha mita moja

Maji lazima yaingie ndani ya muda mfupi

Xiaomi hawajazingatia kutumia dual pixel pdad kuboresha uwezo wa kamera

Lakini pia kamera zake hazina OIS(Optical Image Stabiliztion)

Kama unarekodi video na mkono ukawa unatisika basi video inaweza kutokea vibaya

Neno la Mwisho

Bei ya redmi note 10 pro inaifanya simu kuwa ya bei nafuu huku ikiwa na ubora mwingi

Lakini kuna washindani wenye sifa nzuri nyingi kuliko hii redmi

Kwa mfano, simu ya samsung a52 ina mengi inayofanana na redmi note 10 pro

Wakati samsung galaxy a52 inauwezo wa kuzuia maji kupita ndani ya simu endapo ikidumbukia kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu saa

Wakati huo bei ya samsung a52 inaendana na bei ya redmi tunayoizungumzia

Ila kiujumla redmi hii ni nzuri kuwa nayo

Maoni 4 kuhusu “Ubora na bei ya Redmi Note 10 Pro (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram