SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Nini Maana ya iOS kwenye Simu za iPhone

Android/iOS

Sihaba Mikole

July 30, 2023

Vifaa vyote vya kompyuta kuanzia kompyuta mpakato, simu janja, smartwatch nk huundwa na kitu kinaitwa mfumo endeshi

Mfumo endeshi ni mfumo unasimamia na kumeneji vitu vyote vilivyopo kwenye kompyuta au simu

Unapotumia simu kupiga picha, kuongea na mtu kazi ya kujua kifaa kipi kitumike kutoa huduma husika inafanywa na mfumo endeshi

Mifumo endeshi upande wa simu janja ipo ya aina nyingi ila inayotumiwa na watu wengi ni Android na iOS

Hivyo iOS ni mfumo endeshi uliotengenezwa na kampuni ya apple kwa ajili ya kutumika kwenye vifaa vya kampuni hiyo hasa simu janja za iPhones

ios showcase

Ufanyaji kazi wa iOS unatofautiana na Android kwani muundo wa ios ni tofauti

Hizi ni sifa za mfumo wa iOS

App za iOS

Mfumo endeshi wa iOS unatumia applikesheni ya apple app store kupata appliksheni kwa ajili ya kutumiwa kwenye iphones

Kwenye app store kuna app za kulipia na za bure kama ilivyo kwa simu za android

Lakini sio kila ya android inapatikana kwenye iOS

Kama ilvyoelezwa utendaji wa mifumo endeshi inatofautiana

Na pia haipo huru kama android ndio maana app store ina idadi ya app zipatazo milio maja na laki mbili mpaka kufikia mwaka 2021

Ambapo google play store mpaka kufikia mwaka 2017 ilikuwa na app milioni 3

Muundo wa faili upande wa app za iOS ni .ipa huku kwenye android ikiitwa .apk

iOS hutumiwa kwenye simu za apple tu

Mfumo endeshi wa iOS haukutengenezwa kutumika kwenye vifaa tofauti na vilivyoundwa na kampuni ya apple

Yaani huwezi kuikuta iphone orijino ikitumia mfumo endeshi wa android

Ama kukuta simu ya samsung ikitumia mfumo endeshi wa iOS

Hii ni tofauti na mifumo mingine kama windows ya microsoft  na android ya google

Pamoja na kuwa Google ni wamiliki wa android na wenyewe wanatengeneza simu ila android utaikuta kwenye tecno, infinix, sony, samsung, nokia, oppo nk, ni mfumo huria

Ila iOS utaikuta kwenye iphones zote pekee yake kwa sababu ni mfumo uliofungwa kutumika kwenye kampuni moja tu.

iOS inaruhusu multitasking

Maana ya multitasking ni uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja

Matoleo ya mwanzoni ya iOS yaliwekwa ukomo mkubwa sana wa kufungua app nyingi kwa wakati mmoja

Ni kuanzia toleo la iOS 4 ndiyo iliyokuja kuruhusu vitu vya aina saba kuweza kufanya kazi wakati simu ikifanya kazi nyingine

Vitu hivyo ni kusikiliza audio, kuchota taarifa za eneo, notification, kudownload vitu na mengineyo

Hii inamaanisha unaweza kufungua app ya kusikiliz miziki wakati huo kuna ujumbe wa notification umetokea na wakati huo huo kuna app inadownload mziki

Hii ndio maana ya multitasking, sio kitu kigeni hata android ipo

iOS inasapoti Face ID

Kwenye swala usalama iOS ina mfumo unaofungua ama kuiloki simu kwa kutumia sura ya mtu

Ufanisi wa face id ya ios ni mkubwa kuliko simu nyingi za matoleo ya kati

Kwa hiyo kwenye iphone kuna njia kama tatu za kulocki simu

Ambazo ni fingerprint, password na ya kutumia sura

Kuna hatua chache za kufuata kuiseti simu kutumia sura kama password

Ina mifumo saidizi kwa waremavu

iOS kama ilivyo kwa android, ios ina mifumo mbalimbali ya kumsaidia mremavu kutumia simu

Kwa mfano mfumo wa VoiceOver unasoma vitu vyote vya kwenye simu kwa sauti

accessebility ios

Kusoma kwa sauti kunamuwezesha mremavu wa macho kujua wapi anatachi

Na inamuwezesha mtumiaji wa simu kutumia simu kwa kutikisa simu

Hitimisho

Kwa haya machache yanatosha kukufafanulia maana ya iOS kwenye vifaa vyote vya apple

Ila ni mambo mengi yameachwa yaliyomo kwenye mfumo huu wa simu za iphones

Kwa hiyo kama ukisikia android au ios basi jua kuwa hii ni mifumo endeshi kwa ajili ya simu janja tofaut tofauti

Wazo moja kuhusu “Nini Maana ya iOS kwenye Simu za iPhone

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Related Articles

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

simu za bei rahisi

Simu used za bei rahisi za madaraja ya kati na juu

Kuna simu za bei kubwa ambazo zilizotoka miaka ya nyuma na kwa sasa hazipatikani zikiwa mpya Matoleo yake yalikuwa yanalenga watumiaji wanaopenda vitu vya gharama hivyo kuwa na vitu vingi […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 624 213 048

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram