SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

October 6, 2023

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023

Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu za android kwa muda mrefu

Hii inamaanisha apple wamekubali kufuata matakwa ya EU

Utendaji wake ni mkubwa kutokana na kutumia processor mpya

iphone 15 pro max

Japo kumeibuka na changamoto ya simu hizi kupata moto mwingi kitu kilichowalazimisha apple kutoa maboresho ya mfumo wa iOS

Kutokana na uwezo wake mkubwa kwenye maeneo mengi, bei ya Apple iPhone 15 Pro Max ni zaidi ya milioni mbili na nusu kwa hapa Tanzania

Bei ya iPhone 15 Pro Max ya GB 256

Bei ya iPhone 15 Pro Max yenye ukubwa wa gb 256 inafika shilingi milioni nne na laki sita (4,600,000) kwa hapa Tanzania

Kwa bei halisi ya Marekani na maeneo mengine duniani simu inauzwa kwa kima cha milioni tatu na laki nne

Kuna utofauti mkubwa wa bei kwa hapa nchini kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kodi na gharama za usafirishaji

Kwa mtu anayejua namna ya kuagiza vitu mtandaoni hasa kupitia Amazon anaweza nunua huko kwa kima cha chini

Ila kwa hapa Tanzania bei lazima iwe kubwa

Isikushangaze sana kuona iPhone kuwa na bei isiyoendana na vipato vya watanzania wengi

Hizi ni simu zinazotengenezwa kwa kuwalenga watu wenye vipato vikubwa na pia sifa zake ni kubwa sana.

Sifa za Apple iPhone 15 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Pro
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.78 GHz
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.11 GHz
  • GPU-Apple GPU (6-core graphics)
Display(Kioo) LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 17
Memori NVMe, 256GB,512GB,1TB na RAM 8GB
Kamera Kamera TATU

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12(Telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4441mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 4,600,00/=

Upi ubora wa iPhone 15 Pro Max

Simu ina kioo kionyeshacho picha kwa mwangaza mzuri na uangavu wa kuonyesha vitu kwa ustadi

Processor yake ina uwezo wa mkubwa hivyo inaifanya simu kuwa na utendaji wenye nguvu kwenye mambo mengi

Ni simu ya 5G na pia ina eSIM ambayo zimeanza kutumika na mitandao mbalimbali hapa nchini

Betri yake inakaa na moto muda mrefu kiasi cha kwamba hutohitaji kuichaji simu kila wakati

Inasapoti chaji yenye kupeleka umeme mwingi na hivyo kujaza betri kwa haraka

Ubora wa kamera ni wa kiwango kikubwa na ni moja ya simu zenye kamera nzuri kwa mwaka 2023

Uwezo wa network

iPhone 15 Pro Max ni simu yenye uwezo wa kusapoti mtandao wa 5G wa aina zote

Kumbuka kuna aina tatu za 5G zinazoweza kutumia miundombinu ya aina mbili

iPhone 15 Pro Max inasapoti mpaka 5G ya SA ambayo huwa ina kasi kubwa sana

Kwa hapa Tanzania mitandao yenye 5G inasapoti masafa ya kati

Hata hivyo network bado inaoatikana maeneo machache ya Dar Es Salaam, kwa maana haijasambaa nchi nzima

Ukitazama hii video hapa chini utaona kasi yake ya intaneti inatembea mpaka 4Gbps

Kwa mfano ukiwa unataka kupakua faili lenye ukubwa wa 1000MB, simu inachukua sekunde mbili tu kudownload kikamilifu

Yaani kwa mfano umekutana  na movie ya kikorea(sizoni) yenye ukubwa wa GB 7, basi series nzima utaipata ndani ya sekunde 14

Wakati huo ukilipia 5g ya Vodacom yenye kasi 30Mbps itakuchukua zaidi ya dakika 30 kuipata sizoni

Hii ni 5G aina ya mmWave kwa hapa nchini huwezi kuipata kasi ya kiwango hiki hata ukiwa na hii simu

Ubora wa kioo cha iPhone 15 Pro Max

Kimuonekano wa vitu kioo cha iPhone 15 Pro Max kinaonyesha vitu kwa uangavu mkubwa

Rangi zake za kioo zina kina kikubwa, hivyo vitu vingi vinaonekana kwa rangi zake halisi kwa kiasi kikubwa

Sababu kubwa ni kioo cha hii simu ni aina ya LTPO OLED apple wanakiita LTPO Super Retina XDR OLED

Ustadi wa rangi unachagizwa na uwepo wa teknolojia za HDR10 na Dolby Vision

HDR10 na Dolby Vision zinasaidia kuongeza kina cha rangi ya kioo hivyo kioo kinakuwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Kioo cha iPhone 15 Pro Max ni chepesi wakati ukiwa unascroll(kugusa kutoka kwenda chini) kwa sababu ya kuwa na refresh rate ya 120Hz

Kutumika kwa LTPO kunafanya kioo kidhibiti kiwango cha refresh rate kwani kikiachwa kama kilivyo inasababisha chaji kuisha haraka

Nguvu ya processor Apple A15 Pro

Kwa kutazama data za app ya Geekbench inaonyesha kuwa apple a15 pro ndio processor ya simu yenye nguvu kuliko zote kwa sasa

Kwa maana inaizidi hata ile chip iliyotumika kwenye Samsung Galaxy S23 Ultra

Ila kuna changamoto moja imejitokeza kwa watumiaji iPhone 15 Pro Max

Changamoto hiyo ni simu kupata joto sana baada ya muda mfupi wa matumizi

iphone 15 pro max processor

Apple wanadai baadhi ya apps zinaifanya processor ifanye kazi kupitiliza hivyo kusababisha processor kupata moto

Ila sababu kuu wanadai kuwa ni swala la software na sio uwezo wa chip

Sasa basi apple wamelizimika kutoa maboresho ya mfumo endeshi kutoka kutoka iOS 17 hadi iOS 17.0.3 kurekebisha tatizo

Upande wa utumiaji app zinazohitaji nguvu kubwa ya utendaji chip inafanya vizuri na haina mkwamo wowote

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya iPhone 15 Pro Max ina ukubwa wa 4441mAh

Katika matoleo yote mapya hii ndio iphone yenye betri kubwa

Hivyo ukaaji wake wa chaji unachukuwa masaa mengi

Kutoka tovuti ya GSMArena, hii simu ukiwa upo unaperuzi intaneti muda wote inachukua masaa 24 mpaka kuisha

Hii ina maana kuwa kwa siku unaweza kuichaji simu mara moja tu

Hata iphone 15 pro max haiwezi kudumu muda huo ukiwa unacheza gemu, unaangalia youtube, ukiwa unatimua tiktok ama instagram

Kiuhalisia kwa matumizi simu inaweza kudumu kwa kipindi cha masaa 11 tu

Hivyo kwa mtumiaji mkubwa wa simu itamlazimu kuichaji simu mara mbili kwa siku

Kwenye kiepengele hiki Samsung Galaxy S23 Ultra iko njema

Ukubwa na aina ya memori

iPhone 15 Pro Max inakuja katika matoleo ya aina tatu na zote zina RAM ya GB 8

Kuna yenye GB 256, 512 na 1TB

Hivi viwango vinatosheleza kuhifadhi mafaili mengi na app za kutosha

Ndio maana simu za daraja la juu siku hizi haziji na sehemu ya memori kadi

Ila jua kuwa hii simu inaweza ikatumia flash ama external hard disk cha msingi isapoti waya wa USB Type C

Uimara wa bodi

Apple wametumia materio mapya kwenye bodi za iPhone 15 Pro Max

Bodi hizo ni za aina ya Titanium

Ilitarajiwa kuwa titanium kuwa ni ngumu kuliko matoleo yaliyopita ambayo yanatumia glasi

Kwa bahati mbaya matokeo yako kinyume

Titanium imeonyesha kuvunjika kwa urahisi ukilinganisha na iPhone 14 Pro Max

Kama ilivyo kawaida, simu hii ina viwango vya IP68

Kwa maana haiwezi kuingia maji kwa muda wa nusu hata ikiwa imezamishwa kwenye kina cha mita 6 kwa muda wa nusu saa

Ubora wa kamera

Simu ina idadi ya kamera zipatazo tatu ambazo ni za wide, ultrawide na telephoto

Kamera aina ya ultrawide inapiga eneo pana sana kwa mfano uwanja wa mpira wote

Telephoto kazi yake ni kupiga vitu ambavyo vipo mbali na kamera

iphone 15 pro max ubora wa picha

Kamera yake inapiga picha vizuri hivyo usahihi wa rangi ni mkubwa

Yaani vitu vinaonekana kwa rangi zake harisi

Hakuna changachenga kwa nyakati za mchana

Na hata kwenye mwanga hafifu vitu vinaonekana kwa uzuri

Washindani wa iPhone 15 Pro Max

iPhone hii mpya haina tofauti kubwa na matoleo yaliyopita

Hii inamaanisha iPhone 14 Pro Max bado itaendelea kuwa simu yenye soko kubwa

Hivyo kuipa changamoto toleo jipya la iPhone

Kuna simu kali nyingine ya Samsung Galaxy S23 Ultra ambayo ukaaji wake wa chaji ni mkubwa

Hata kiutendaji hakuna tofauti inayoweza kuonekana kwa macho yenye utofauti mkubwa

Hitimisho

Kwa ujumla apple inatarajiwa kuendelea kushika hatatu kwenye kitengo cha simu za madaraja ya juu

Ila apple wana kazi ya kurekebisha changamoto za simu kupata moto ambazo zimelalamikiwa na watumiaji wengi

Hata hivyo hii ni simu kali

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

ios thumbnail

Nini Maana ya iOS kwenye Simu za iPhone

Vifaa vyote vya kompyuta kuanzia kompyuta mpakato, simu janja, smartwatch nk huundwa na kitu kinaitwa mfumo endeshi Mfumo endeshi ni mfumo unasimamia na kumeneji vitu vyote vilivyopo kwenye kompyuta au […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram