SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

August 9, 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019

Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4

Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi bei ya tecno spark 4 na spark ni ndogo kwa kiasi kikubwa

Ni muhimu kujua kila kipengele cha sifa zake ili ujue iwapo inaendana na mahitaji yako

Kumbuka ina miaka minne tangu itoke

Bei ya spark 4  na spark 3 Pro (GB 32)

Tecno spark 3  Pro ya GB 32 kwa sasa inauzwa shilingi 140,000

Wakati huo spark 4 inauzwa kwa kima cha shilingi 150,000

Kwa sasa hizi simu janja nyingi zilizopo ni used

Kuna ugumu wa kupata matoleo mapya

Kwani kuna matoleo mengi ya Spark yametoka kuanzia mwaka 2020

Sifa za tecno spark 4 na spark 3 pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Quadcore
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz kryo 460
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 9
  • HIOS 5
Memori eMMC 5.1, 32GB na RAM 2GB
Kamera Kamera spark 4 tatu

  1. 13MP,AF(wide)
  2. QVGA
  3. QVGA

Spark 3 mbili

  1. 13MP
  2. 2MP
Muundo Urefu-6.52inchi(spark 4)

-6.2inchi (spark 3)

Chaji na Betri
  • 4000mAh-Li-Po (spark 4)
  • 3500mAh-spark 3
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 150,000/=

Upi ubora wa spark 3 na 4

Ubora mkubwa hizi simu ni kuwa na kupata mtandao wa 4G

Vitu vingi vilivyopo haviendani na nyakati za sasa

Ukizingatia kuwa spark 4 na 3 hazina uwezo wa kupokea matoleo mapya ya android

Kitu kinachochangia kuishusha simu thamani

Maana software huboresha baadhi ya vitu kwenye simu na kuipa maisha marefu ya kutumia apps nyingi kwa miaka mingi

Uwezo wa Network

Simu zote zinasapoti mtandao wa 4G aina ya LTE Cat 7

Kasi ya LTE Cat 7 kwenye kudownload inafika 300Mbps

Kwa maana kama unapakuwa faili la lenye ukubwa wa MB 75 kama whatsapp basi simu itamaliza baada ya sekunde mbili

Kitu cha kuzingatia ni kuwa swala la spidi hutegemea na uwezo wa kampuni ya mawasiliano unayotumia

Kwa hapa Tanzania hakuna mtandao wa simu unaotoa kasi 300Mbps

Maana kwa sasa hii ni kasi ya 5G kwenye mtandao wa vodacom

Ubora wa kioo

Kioo cha tecno spark 3 na spark 4 ni cha aina ya IPS LCD chenye resolution ya 720×1500 pixels

Ni resolution ndogo kwani kwa sasa zipo simu za daraja la chini zenye resolution kubwa zaidi ya hiyo.

Muonekano wa vitu hautokuwa wa kuvutia ukilinganisha na vioo vya amoled

Changamoto ni kuwa ujazo wa rangi kwenye vioo vya LCD sio mkubwa

Refresh rate yake pia ni ile ya kawaida kwani haifiki 90Hz wala 120Hz

Hata hivyo, bei yake inaendana na ubora wa vitu vilivyomo

Yaani hakuna kutarajia ubora mkubwa sana

Nguvu ya processor

Tecno Spark 3 Pro yenyewe inatumia chip ya Mediatek Helio A22 katika kufanya shughuli zake

Nguvu ya helio a22 ni ndogo kwani zina muundo wenye kutumia nguvu kidogo na umeme kidogo

Idadi ya core kwenye kila simu zipo nne na zote zinaundwa na muundo wenye utendaji hafifu

Usishangae baada ya muda kupita simu kuanza kuwa nzito hasa unapowasha intaneti

Kwenye app ya kupima nguvu ya processor ya Geekbech, helio a22 inazalisha alama 160

Ni ndogo sana kwa miaka hii

Kitu kizuri kwenye hii chip ni matumizi madogo ya umeme

Hivyo betri inaweza kukaa kidogo

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya Tecno Spark 4 ni 4000mAh

kwa sasa simu nyingi zinakuja na betri kubwa zaidi ya 5000mAh

Ukaaji wa chaji sio mkubwa kiivyo kutokana na betri yenyewe kuwa ndogo

Spark 3 Pro betri yake ina ukubwa wa 3500mAh

Na yenyewe ni ndogo

Kwa mantiki hii ni ngumu kwa hizi simu kufika masaa 13 ukiwa unatumia intaneti muda wote

Ila kwa matumizi ya kupiga simu kutuma sms simu itachukua muda mrefu kukaa na chaji na chaji

Ukubwa na aina ya memori

Hizi simu zipo za aina moja tu kwenye ukubwa wa memori

Zote zina ukubwa wa GB 32 na RAM ya GB 2 ila spark 4 ipo ya ram ya gb 3

Ukubwa wa memori unaweza kuhifadhi vitu vichache

Kama utakuwa ni mtumiaji sana apps za whatsapp na telegram simu itawahi kujaa

RAM ndogo ni kizingiti wakati unapotumia apps nyingi kwa wakati mmoja

Simu inaweza kuwa na utendaji wa chini

Uimara wa bodi

Hizi simu zimetengenezwa kwa bodi za plastiki upande wa nyuma

Baadhi ya bodi za plastiki huwa na kawaida ya kuchunika rangi japo inategemea na utunzaji

Ni vizuri ukawa unaweka kava mara kwa mara ili ubora wake usipungue kwa haraka

Hazina uwezo wa kuzuia maji kuingia ndani

Ni tofauti na simu kama za iphone ambazo zikizama ni ngumu maji kupenya

Ubora wa kamera

Spark 3 pro ina kamera zipatazo mbili

Huku spark 4 ikiwa na kamera tatu

Kamera kubwa ya spark 3 pro na spark 4 zinafanana, ni kamera ya aina moja yenye MP 13

Kamera za hizi simu kiujumla hazina ubora mkubwa hasa ukipiga kwenye mwanga hafifu

Zote zinaweza kurekodi video za full hd pekee yake

Ubora wa Software

Kwa sasa toleo jipya kabisa la android ni android 13

Spark 4 na 3 pro zenyewe zinatumia android 9

Na hazipoeki sapoti yoyote ya kupata toleo jipya

Android 9 bado inaweza kutumia app za aina zote

Maana waundaji wa app bado wanatoa sapoti kwa toleo hili

Ukizingatia ni 30% tu simu za android ndio zinatumia toleo la android 12

Washindani wa Tecno Spark 3 Pro na Spark 4

Kama ilivyotanguliwa kuelezwa mwanzoni, hizi ni simu zenye muda mrefu

Zinashindana na simu nyingi za bei ndogo

Mshindani wa kwanza ni matoleo ya spark yote yaliyokuja baadae mfano ni tecno spark 8C

Haya yameboreshwa kwa kiasi fulani na yana matoleo ya android ya hivi karibuni

Mshindani mwingi ni Redmi 9A na Redmi 10C bila kusahau Samsung Galaxy A104

Na hata simu used ya google pixel 3 ina ubora zaidi ya spark 3 na inapatikana kwa bei nafuu.

Hitimisho

Kiushauri zaidi ni kuwa hizi sio simu za kuwa nazo kwa sasa labda kama bajeti imebana sana

Tayari ina mambo mengi ambayo yameachwa na wakati

Ni vizuri ukajichanga kuongeza pesa ili ununue matoleo mapya zaidi yenye ubora wa ziada.

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram