SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Pop 2 F na Sifa Zake (simu ya laki na nusu)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 19, 2023

Iwapo unatafuta simujanja ya 150,000 yenye sifa za kawaida Tecno Pop 2 F inaingia hapa

Haina sifa nyingi nzuri kama Samsung Galaxy NOTE 10 ambayo imetoka mwaka mmoja na pop 2 F

tecno-pop-2f showcase

Kwa sababu hiyo bei ya Tecno Pop 2 F haiwezi kuzidi laki mbili popote pale hapa Tanzania

Hata hivyo, ukiimiliki usitarajie mambo makubwa mengi bali ni simu inayofaa kusukumizia siku mpaka utakapopata bajeti nzuri

Bei ya Tecno Pop 2 F ya GB 16

Simu hii ukubwa wake ni GB 16 na inauzwa kwa shilingi 150,000 dukani

Kama ukinunua kwa mtu unaweza kuipata hata kwa shilingi 75,000

Bei yake ndogo inasababishwa na vitu vingi ikiwemo memori ndogo, kamera, na utendaji wa chini kiujumla

Kama ukiangalia sifa zake utaona ufauti mkubwa ukilinganisha na toleo kama la Tecno Spark 10 au hata vivo y66 ya mwaka 2017

Sifa za Tecno Pop 2 F

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek MT6580M
  • Core Zenye nguvu(-) –
  • Core Za kawaida(4) – 1.3 GHz Cortex-A7
  • GPU-Mali-400MP2
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 8.1
  • Go Edition
Memori 16GB na RAM 1GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 5MP
Muundo Urefu-5.4inchi
Chaji na Betri
  • 2400mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 150,000/=

Upi ubora wa Tecno Pop 2 F

Ubora mkubwa wa hii simu ni kuwa na bei ndogo tu

Bei ambayo watu wengi wanaimudu kuinunua

Hivyo inawapa fursa kuweza kuwasiliana na kuingia mitandao ya kijamii na intaneti

Mambo mengine kama yanavyoonekana kwenye jedwari yanaweza yasiwavutie watu wengi

Ukizingatia matoleo ya miaka ya karibuni yanakuja na vitu vikubwa sana

Uwezo wa Network

Mtandao wa juu kabisa unaoweza kuutumia kwenye hii simu ni 3G

Wakati inatoka haikuwa inasapoti mtandao wa 4G

Hii inamaanisha hutoweza kupata kasi kubwa ya intaneti

Kwa sababu 4G na 5G ndizo zina kasi sana kwa sasa

Ila 3G inaweza kukupa kasi ya kulizisha kiasi japo kama unapoakuwa faili kubwa la GB 2 simu itachukua muda kumaliza kudownload.

Ubora wa kioo cha Tecno Pop 2 F

Kioo cha pop 2F ni aina ya IPS LCD

Ambacho hakina resolution kubwa, muonekano wa vitu si wa kuvutia sana

Hii inachangiwa na resolution ndogo ya 480 x 960 pixels

Kwa simu za siku hizi tena simu ya kawaida huwa zina 1080 x 1660 pixels

Kiwango kikubwa cha resolution kinafanya vitu vionekane vikiwa na rangi sahihi na zilizokolea kwa usahihi pia

Hata tecno pop 2 f ni simu ya bei ndogo na mambo yake  mengi hayawezi kulingana na simu za bei ghali

Nguvu ya processor MediaTek MT6580m

Hii simu inapewa nguvu na processor ya Mediatek mt6580M

Utendaji wake ni wa chini sana kwani haina core zenye nguvu hata moja

Mfano wa core zenye nguvu hujulikana kama Cortex A75 na kuendelea

Inaundwa na core zenye kasi ndogo

Kwa muundo huu, hii sio simu nzuri anayependa kucheza magemu, kufungua app nyingi kwa wakati mmoja

Ila ni simu nzuri kwa mtumiaji anayetumia simu kupiga simu na kutuma sms na intaneti kiasi

Kwa sababu kazi hizo hazihitaji nguvu kubwa

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Tecno Pop 2 F ni ndogo na ina 2400mAh

Ukubwa wa 2400mAh unakaa muda mfupi kama ukiwa upo kwenye intaneti masaa mengi mfululizo

Pia simu haina mfumo wa chaji unaopeleka umeme mwingi

Pamoja na betri ndogo ila simu itachukua muda kujaa

Inafaa kama mara nyingi upo kwenye maeneo yenye uhakika wa umeme

Ukubwa na aina ya memori

Memori ya simu ni ndogo pia ina GB 16 tu na RAM ya GB 1

Kiwango hiki cha memori lazima kiwahi kujaa

Kikawaida kuna sehemu ya memori inachukuliwa na mfumo endeshi wa simu na appliksheni zinazokuja na simu

Mwisho wa siku simu inaweza ikabaki na memori ya GB 8 kwa kuweka mafaili yako wewe binafsi

Kiwango kinawahi kujaa baada ya muda mfumi

Kutokana na udogo wa memori unaweza kuongeza memori kadi kwa sababu simu inayo hiyo simu

Uimara wa bodi ya Tecno Pop 2 F

Bodi ya hii simu inaundwa kwa plastiki

Ni muhimu kuweka kava kuifanya simu isichunike rangi kirahisi

tecno pop 2 f body

Kiujumla uimara wa bodi sio mkubwa

Na ni muhimu pia kuweka protekta kuilinda simu wakati ikidondoka bahati mbaya

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera moja tu yenye megapixel 5

Ukiwa unapenda kamera jua kua utahitaji simu yenye megapixel angalau 8 kabla ya kuangalia vitu vingine vinavyofanya kamera kuwa nzuri

tecno pop 2 F

Pitia: Simu zenye kamera nzuri za bei nafuu

Hata hviyo utaweza kurekodi video za full HD kwa kiwango cha 30fps

Ubora wa Software

Wakati inatoka ilikuwa inatumia Android 8.1

Ila leo huu matoleo ya android yamefika 13 yaani Android 13 na hivi karibuni Android 14 inakuja

Kwa bahati mbaya Tecno Pop 2 F haina uwezo wa kupokea toleo jipya

Kutokana na simu kuwa na utendaji mdogo na memori ndogo imeifanya simu kutumia Android aina ya Go Edition

Android Go Edition huwa inawekwa kwenye simu ambazo hazina nguvu kubwa, kwani ikiwekwa android ya kawaida simu inakuwa nzito zaidi

Washindani wa Tecno Pop 2 F

Kwa nyakati za miaka hii, simu hii ina washindani wengi wenye simu za bei nafuu

Japo nyingi zinauzwa kuanzia laki mbili na kuendelea

Simu hizo ni Samsung Galaxy a02, Redmi 9a, Redmi 10a na hata Tekno Spark 4

Hizo simu zinaiacha Tecno Pop 2 F kwa mbali japokuwa bei zake zinaongezeka kidogo

Neno la Mwisho

Kwa mwaka 2023, Tecno Pop 2 F sio simu ya kuwa nayo

Kwa sababu haina vitu vingi vinavyohitajika katika ulimwengu wa simu wa sasa

Ni simu ya kuwa nayo wakati ukijipanga kutafuta pesa ya kumiliki simu kali zaidi.

Maoni 3 kuhusu “Bei ya Tecno Pop 2 F na Sifa Zake (simu ya laki na nusu)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram