SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Hot 40 na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

January 10, 2024

Kuelekea mwishoni mwa mwaka 2023 infinix walitoa toleo jingine la simu aina ya Infinix Hot 40

Hili ni baada ya toleo la infinix hot 30 ambvalo limetoka mwaka 2023 pia

Infinix Hot 40 ina tofauti ndogo na watangulizi wake ila kuna utofauti kidogo kwenye mfumo wa software

Bei ya infinix hot 40 kwa hapa Tanzania inazidi shilingi laki tatu kutokana na ukubwa wa memori

Bei yake pia inawezwa kuathiriwa na eneo

Bei ya Infinix Hot 40 ya GB 128

Kwa Tanzania bei ya simu inaanzia shilingi laki tatu na nusu

Bei ni rafiki kiujumla ukilinganisha na ukubwa wa memori

Kwa maana memori inatosheleza kuhifadhi vitu vya kutosha

Na isitoshe inakuja na sehemu ya kuweka memori kadi

Japo ukubwa wa memori haupaswi kuwa kigezo pekee cha kukushawishi kununua simu

kwani kuna baadhi ya sifa hazina ubora mkubwa ila muhimu zingatia mahitaji yako kama yanafikiwa na sifa za simu husika

Sifa za Infinix Hot 40

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU -Mediatek Helio G88
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 13
  • XOS 13.5
Memori  256GB,128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 0.08MP
Muundo Urefu-6.78inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 350,000/=

Upi ubora wa Infinix Hot 40

Hot ina ubora katika maeneo matano ambayo yanweza mfurahisha mtumiaji wa kawaida

Kwanza simu ina mfumo wa chaji wenye kasi ya kujaza betri kwa haraka

Betri yake ni kubwa inaweza kukaa na chaji muda mrefu

Memori ni kubwa na bei ni rafiki kiasi fulani

Kamera yake kubwa ina megapixel nyingi japo hii ni kitu kimoja kati ya vitu vingi vinavyofanya kamera kuwa nzuri

Kwenye upande wa network uwezo wake ni wa wastani kama utakavyoona

Uwezo wa Network

Infinix Hot 40 inasapoti mpaka mtandao wa 4G kwani chip iliyotumika na simu haina uwezo wa 5G

Ndio maana inaweza semwa kwa sasa uwezo wake ni wa kawaida

Ikizingatiwa tayari mitandao ya Tigo, Airtel bila kusahau Vodacom inasapoti 5G kwa baadhi ya maeneo hapa Tanzania

Aina ya 4G ya hii simu ni LTE Cat 7 upande wa kudownload na LTE Cat 13 upande wa ku-upload

Yaani kwa maana kama hii spidi inapatikana kweli, itakuchukua sekunde mbili tu kuweka whatsapp kwenye simu

Kwa bahati mitandao ya simu hapa nchini mara nyingi 4G yao huwa ni ngumu kufika hata 100Mbps hata ukiwa eneo zuri

Kiufupi usitarajie kuipata kasi hii kwa Tanzania

Ukiondoa uwezo wa wastani wa network kuna ubora fulani wa kuridhisha upande wa kioo

Ubora wa kioo cha Infinix Hot 40

Kioo cha Infinix Hot 40 kinatumia teknolojia IPS LCD

Kwa sasa simu nyingi za kundi la kati hutumia vioo vya AMOLED

Kiubora amoled ipo juu hasa kwenye utajiri wa rangi ila kioo orijino cha infinix kinasapoti refresh rate kubwa inayofika 90Hz

Refresh rate inapokuwa kubwa husaidiwa simu kuwa nyepesi unapotachi ama kuperuzi

Changamoto kubwa ya refresh rate ya juu ni matumizi makubwa ya betri

Kama haina umuhimu kwako unaweza izima na kuseti refesh rate ya 60Hz

Ubora wa vitu vingi vya simu ikiwemo refresh rate vinaweza visiwe na maana yoyote kama haufahamu nguvu ya processor ya simu

Maana processor ndio ubongo wa simu janja na kompyuta

Nguvu ya processor Mediatek Helio G88

Hot 40 inatumia processor kutoka kwa kampuni ya Mediatek ya Taiwan

Chip hiyo inaitwa Mediatek helio G88 ambayo imegawanyika katika sehemu mbili ikiwa na jumla ya core nane

Kiutendaji uwezo wake sio mkubwa japo inaweza kucheza magemu mengi ila baadhi utalazimika kucheza kwa ubora wa chini wa graphgics kupata FPS nyingi

Kwa mfano gemu ya PUBG Mobile 2020 inacheza kwa viwango vya wastani wa FPS 30 kwenye ubora wa chini

Ila ukiweka Full HD yaani pixel 1080 fps zinapungua mpaka fps 19

Picha inayotolewa hapa ni kuwa helio g88 inaweza fanya kazi nyingi ila changamoto itakuja unapofungua app nyingi zinazotumia nguvu kubwa

Unaweza kuanga kiundani hapa, uwezo wa mediatek helio g88

Kufaidi uwezo wa mediatek helio g88 betri ya simu inabidi na yenyewe inabidi iwe na uwezo wa kuridhisha

Maana betri ikiwa ndogo simu inaweza wahi kuzimika ukiwa unacheza gemu kwani helio g88 ufanisi wake ni wa wastani

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Infinix Hot 40 ina ukubwa wa 5000mAh

Mara nyingi ukubwa huu unaweza kustahimili kukaa na chaji kwa zaidi ya masaa kumi kutegemeana na matumizi

Betri ikiwa kubwa hufanya simu kuchelewa kujaa kama chaji kasi yake ni ndogo

Chaji ya Hot 40 inaweza kupeleka umeme mpaka wati 33

infinix hot 40 chaji

Wati 33 inaweza kujaza betri ya 5000mAh ndani ya dakika 80

Chaji zenye kasi ndogo huchukuwa zaidi ya masaa matatu kujaza simu

Kwa maana hiyo hata video zako ambazo umeziweka kwenye simu unaweza kuzitazama kwa muda mrefu bila kuhofia chaji kuisha

Ni vizuri ukaelewa mfumo mzima wa memori wa hii simu

Ukubwa na aina ya memori

Infinix Hot 40 imegawanyika sehemu mbili upande wa memori

Kuna yenye ukubwa wa GB 128 na GB 256 na zote zina RAM ya GB 8

Kwa bahati mbaya ni kwamba mfumo wake wa memori ni eMMC

eMMC huwa na kasi ndogo ya kusafirisha data ukilinganisha na mfumo wa UFS

Inaweza leta changamoto ya simu kuwa nzito pindi inapojaa

Siku hizi kampuni nyingi za utengenezaji simu hutumia UFS hata kwa madaraja ya kati na ya chini

Inawezekana labda infinix wanajaribu kupunguza gharama za utengenezaji ndio maana hata bodi ya simu haina vitu vikubwa sana vya kulinganisha na iPhone 15 Pro Max

Uimara wa bodi ya Infinix Hot 40

Njia moja wapo ya kujua uimara wa bodi ya simu ni kwa kutazama viwango vya IP

IP huwa vinaonyesha uwezo wa simu kuzuia maji ndani ya simu kama ikizama kwenye kina fulani

Infinix Hot 40 haina viwango rasmi vya IP ya aina yoyote kama vile IP53

 

infinix hot 40 bodi

Maana yake ni kuwa mtumiaji anapaswa kuwa makini anapokuwa kwenye mvua ama mazingira yenye maji

Bodi ya infinix hot 40 ina muonekano wa kuvutia hasa mpangilio wake wa kamera zake tatu

Ila muonekano mzuri wa kamera na ubora wa kamera hivyo ni vitu viwili tofauti vya kutofautisha

Ubora wa kamera

Moja ya eneo lenye ubora hafifu kwenye Infinix Hot 40 ni upande wa kamera

Kamera yenye lenzi ya macro ina megapixel 2MP ili kupata picha nzuri kamera inabidi na walau megapixel 8

infinix hot 40 camera

Kamera kuu ina megapixel 50 ila inakosa mfumo mzuri wa ulengaji angalau PDAF japo pia ni wa kizamani kwani simu za sasa huja na dual pixel pdaf

Ni ngumu kuieleza kamera za hii simu kiundani kwani kuna hazijaelezwa

Upande wa kurekodi video kamera yake inaweza kurekodi mpaka video za full hd kwa kiwango cha 30fps

Haiwezi kurekodi video za 4K

Ubora wa Software

Infinix Hot 40 inatumia mfumo endeshi wa Android 13 na XOS 13.5

XOS 13.5 imejaribu kuiga baadhi ya vitu vya iphone 15 kama dynamic island

Dynamic island huwa inaziba sehemu ya kamera ya mbele na kuonyesha baadhi ya vitu

Kwenye infinix ukiichaji simu basi kiwango cha betri kujaa inakuwa inaonekana kwenye hiyo sehemu ya dynamic island

Washindani wa Infinix Hot 40

Kuna matoleo ya samsung ya bei nafuu ambayo yametoka mwishoni mwa mwaka 2023

Matoleo hayo ni Samsung Galaxy A05 na Samsung Galaxy A05S

Bila jusahau kuna itel ya chini za laki mbili pia zinaweza kuleta ushindani kama simu mbadala ya bei nafuu

Mshindani mwingine ni Redmi 12 na Redmi 12C ambazo bei yake inaendana na hii infinix

Kiujumla machaguo ni mengi kwa sasa

Neno la Mwisho

Bei ya infinix hot 40 ni rafiki hasa ukiangalia ukubwa wa memori

Sio simu nyingi zinaweza kupatikana kwa kima cha laki tatu na memori ikiwa ba ukubwa wa GB 128

Kwa mtumiaji mwenye matumizi ya wastani hatoona shida akiwa anaitumia hii simu

Maoni 3 kuhusu “Bei ya Infinix Hot 40 na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix mpya thumbnail

Simu za Infinix zinazotamba na bei zake (2024)

Mwishoni mwa mwaka 2023 na mwanzoni mwa 2024 kuna matoleo mapya ya infinix yalitoka Matoleo hayo mengi ni ya daraja la kati na la chini yaani yamegusa kila mtu kulingana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya Infinix Hot 40 Pro na Ubora wake

Simu ya Infinix Hot 40 Pro ni simu janja ya daraja la kati ambayo imetoka pamoja na simu ya infinix hot 40 Hot 40 Pro ina ubora wa ziada kwenye […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram