SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya simu mpya ya Google Pixel Fold

Simu Mpya

Sihaba Mikole

August 28, 2023

Fold ni aina ya simu za kujikunja.

Kwa muda mrefu makampuni ya Samsung, Huawei na Oppo wamekuwa wakitengneza simu za aina hii

Hivi karibuni tecno na pixel pia zimeingia katika uzalishaji wa  simu za fold

google pixel fold showcase

Google wametoa simujanja ya fold inayotambulika kama Google Pixel Fold

Kikawaida simu za kukunja huuzwa kwa gharama kubwa

Kwa maana hiyo bei ya google pixel fold inazidi milioni nne kwa Tanzania na duniani kwa ujumla

Bei ya Google Pixel Fold

Simu ina miezi miwili tangu ilipoachiwa

Bei yake ni shilingi milioni nne na laki tano (4,500,000)

Ni bei inayoendana na simu za samsung fold

Ni kiasi kikubwa cha pesa ukilinganisha na kipato cha watanzania wengi

Ila kwa mwenye uwezo, atapata simu yenye ubora katika utendaji, kamera, kioo chenye kuonyesha vitu vingi kwa wakati mmoja na kwa ukuibwa, na memori kubwa yenye kutosheleza kuhifadhi vitu vingi

Ni moja ya simu nzuri ukiangalia sifa ilizo nazo.

Sifa za Google Pixel Fold

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Google Tensor G2
  • Core Zenye nguvu sana(2) – 2×2.85 GHz Cortex-X1
  • Core zenye nguvu(2)-2×2.35 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.80 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G710 MP7
Display(Kioo) Foldable OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
Memori UFS 3.1, 256GB,512GB,na RAM 12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 48MP,dual pixel PDAF(wide)
  2. 10.8MP(ultrawide)
  3. 10.5MP(Telephoto)
Muundo Urefu-7.6inchi
Chaji na Betri
  • 4821mAh-Li-Po
  • Chaji-100W
Bei ya simu(TSH) 4,500,000/=

Upi ubora wa Google Pixel Fold

Kioo chake kina uwezo wa kuonyesha vitu kwa ukubwa kama ukikunjua

Inatumia kioo chenye ustadi mzuri kwenye uwasilishaji wa rangi

Ina betri kubwa ya kukaa na chaji muda mrefu

Mfumo wake wa kamera ni mzuri kwenye upigaji picha na kurekodi video

Utendaji wake ni mkubwa kwa sababu simu ina chip yenye nguvu

Inatumia muundo wa memori wenye kasi ya kusafirisha data kwa haraka

Mfumo wa chaji unapokea umeme mwingi unaoweza kujaza betri kwa muda mfupi

Uwezo wa Network

Google Pixel Fold ni simu ya 5G kama ilivyo kwa matoleo mengine ya daraja la kati na la juu za siku hizi

Na inasapoti pia aina zingine za network

Hii simu inakubali aina zote za 5G zikiwemo zinazotumiwa na mitandao ya simu nchini

Hivyo basi 5G ya Vodacom, airtel na Tigo hazitokuwa na shida kwenye pixel fold

Hata hivyo, 5g haijasambaa sana hapa nchini

Inapatikana tu baadhi ya maeneno ya Dar Es Salaam

Upande wa 4G inatumia LTE Cat 24 ambayo kasi yake ya kudownload 2Gbps

Kwa bahati mbaya 4G ya maeneo mengi duniani haifiki kasi hii

Hii ni kasi inayopatikana kwenye 5G aina ya mmWave

Ubora wa kioo cha Google Pixel Fold

Kioo cha google pixel fold kina upana wa inchi 7.6 kikiwa kimekunjuliwa

Huu upana ni pungufu kwa kima cha inchi 2.4 wa vioo vya vishikwambi walivyopewa walimu

Ila zingatia kuwa resolution ya kioo cha google fold ni kubwa na ina kioo cha Amoled

google pixel fold

Yaani muonekano wa vitu ni mzuri kutokana na kuwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Kwani ina HDR10+ na pia refresh rate yake inafika 120Hz

Kwa maana utakapokuwa unatachi skrini utaona simu kuwa ipo nyepesi

Uang’avu wa kioo unafika nits 1000

Nits 1000 inasaidia skrini kuonyesha vizuri hata ukiwa juani

Nguvu ya processor Google Tensor G2

Simu ya Google Pixel Fold imewezeshwa utendaji na chip ya Google Tensor G2

Matoleo mapya ya google yanatumia processor zinazoundwa na goole wenyewe wakati zamani zilikuwa zinatumia chip za snapdragon

Ina idadi ya core nane ambazo zimegawanyika katika sehemu tatu

Core yenye nguvu sana ni aina ya Cortex X1

Kwenye app ya kupima nguvu za processor ya geekbench 6, google tensor ina wastani za alama 1400

Hiki ni kiwango kinachoshahabiana na processor ya iPhone 14 Pro Max iitwayo Appple A15 Bionic

Ndio maana gemu zinacheza kwa fremu  nyingi

Na kila aina ya app inafunguka pasipo kugandaganda

Uwezo wa betri na chaji

Betri yake ina ukubwa wa 4821mAh

Ukubwa wa betri hautofautiani sana na betri nyingi za siku hizi ambazo zina ukubwa wa 5000mAh

Hii ina maana kuwa ukaaji wa chaji unazidi masaa 12 ukiwa kwenye intaneti muda wote

google pixel fold chaji

Chaji inasapaoti mfumo wa PD3.0 yenye uwezo wa kupokea umeme wa wati 100

Ukiwa na chaji yenye kasi hiyo simu inaweza kujaa ndani ya dakika 25

Pia hii simu inasapoti wireless chaji

Ukubwa na aina ya memori

Matoleo ya Google Pixel Fold upande wa memori yapo mawili yenye ukubwa wa RAM ya GB 12

Kuna yenye GB 256 na GB 512 ambazo ni kubwa na zinaweza hifadhi vitu vingi

Inatumia memori aina ya UFS 3.0

Kasi ya UFS 3.0 kwenye kusafirisha data ni 2400MBps

Kwa maana kama unakopi kitu kwenda kwenye hii simu kitamalazika ndani muda mfupi

Uimara wa bodi ya Google Pixel Fold

Google ni simu imara kwani ina viwango ip vinavyoonyesha uwezo kwa kuzuia maji kuingia ndani ya simu pindi ikizama kwenye maji

Lakini jua simu inapaswa itolewe kwenye maji ndani ya nusu saa

Kwenye skrini kuna protekta ya kioo cha Corning Gorilla Glass Victus

Wenyewe gorilla wanadai kuwa ni ngumu kioo kupasuka pale simu inapodondoshwa kwa kimo cha mita mbili

Hata umakini ni muhimu kwenye matumizi ya simu

Ubora wa kamera

Simu ina idadi ya kamera zipatazo tatu

Kuna kamera ya kupiga eneo pana, na umbali mrefu yaani telephoto

Kamera kuu na ya telephoto zina ulengaji wa dual pixel pdaf

Uwepo wa hii kitu unafanya simu kuweza kukilenga kitu kwa ustadi na kukusanya data sahihi za kinachopigwa picha

google pixel fold kamera

Ubora wa picha nyakati za mchana ni mkubwa na wa kustaajabu

Rangi za vitu vinaonekana kwa usahihi mkubwa na unaoendana na uhalisia

Ubora wa picha unapungua ikiwa simu inapiga kwenye kiza kingi sana

Ubora wa Software

Google Pixel Fold inatumia mfumo wa Android 13 asilia (stock android)

Kutokana na simu kuweza kutanuka, google wameweza kutumia faida ya uwepo wa kioo kipana

Kwani inakupa uwezo wa kutenganisha skrini na kutumia app mbili kwa wakati mmoja

Kwa mfano, upande wa kushoto ukawa unaangalia video youtube na upande wa kulia ukawa unaandika barua

Upana wa kioo unatoa fursa kubwa ya kutumia app nyingi kwa wakati mmoja bila shida

Washindani wa Google Pixel Fold

Mshindani mkubwa wa pixel si mwingine bali ni samsung fold

Google pixel Fold ina kimo kidogo ambacho ni inchi 5.8

Ila samsung galaxy z fold 5 urefu wake ni 6.2

Hiki ni kitu kimoja wapo kinachoweza mfanya mtu aaachane na pixel

Na pia samsung galaxy z fold 5 zinaboreka kadri matoleo mapya yanavyotoka

Neno la Mwisho

Ushindani kwenye simu za kujikunja unazidi kuimalika

Changamoto ni kuwa bei za hizi simu ni kama zinalenga watu wachache wenye kipato kizuri

Ukiangalia bei ya google pixel fold inamfaa mtumiaji mwenye bajeti kubwa

Na bei yake inaendana sana na ubora ila bei hii unapata matoleo mazuri ya simujanja za kawaida na chenji inabaki

Ila kama unataka kuonja teknolojia ya folding sio mbaya kununua

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 pro thumbnail

Bei ya Google Pixel 8 Pro na Sifa zake Muhimu

Simu ya Google Pixel 8 Pro imezinduliwa mwezi wa kumi (oktoba) 2023 Ni simu ya daraja la juu kama ilivyo kwa iphone na samsung matoleo ya S-series Kwa maana hiyo […]

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

huawei mate60 pro

Huawei Mate 60 Pro Pigo kwa Marekani?

Kama ni mfuatiliaji wa habari za teknolojia utakuwa unafahamu vikwazo vya Marekani dhidi ya huawei Huawei kutoka china imekuwa na wakati mgumu wa kutumia teknolojia mbalimbali zenye mafungamano na marekani […]

No Featured Image

Bei ya Simu mpya ya Sony Xperia 1 V na Sifa Zake

Sony, kampuni ya japan imeachia toleo lingine jipya la xperia mwezi julai 2023 Toleo hilo ni Sony Xperia 1 IV ambalo ni la daraja la juu kwenye makundi ya simu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram