SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu zote mpya za Infinix na bei za kustaajabisha (2026)

Brand

Sihaba Mikole

June 20, 2026

Kuna bei za infinix mpya zinafikirisha

Maana zimekuja kitofauti sana kwa namna simu za Infinix zilivyozoeleka

Maana kuna infinix inayoenda hadi milioni mbili na nusu kwa Tanzania

Ila sifa za Infinix kwa mwaka 2026 nyingi ni za kiushindani

Ndio maana kuna tofauti kubwa sana kati ya Infinix Note 60 Pro na Infinix Note 50 Pro

Hizi ndio simu zenyewe na sifa zake

Zitazame kama zinaendana na bei na kama inakufaa

Infinix Note 60 Pro

Bei ya Infinix Note 60 Pro ya GB 256 na RAM ya GB 8 ni shilingi milioni 1.2 (1,200,000)

Ubora mkubwa wa hii simu ni utendaji ulioimarishwa na betri kubwa

Tofauti na simu ya mwaka uliopita

Infinix Note 60 Pro imepata maboresho kwenye skrini, esim, chaji ya wati 90

Na hata kamera yake ni nzuri na ina fingerprint ya kwenye kioo

Hivyo sifa zake zinaendana kabisa na bei ya simu

Infinix Note 60

Infinix Note 60 ya GB 256 ni shilingi laki tisa (900,000)

Hii simu pia ina utendaji mkubwa wa kusuma kila aina ya app na kwa haraka

Ni simu ya 5G yenye kusapoti laini za aina ya eSIM

Kwa sasa bado haijaingia rasmi kwa Tanzania

Na yenyewe ina betri kubwa la mAh 6500

Ukaaji wake wa chaji ni mkubwa na ina kioo himilivu simu inapoanguka

Infinix Note 60 Ultra

Bei ya Infinix Note 60 Ultra ni shilingi milioni mbili na nusu (2,500,000)

Kwa sehemu inafanana na Infinix Note 60 Pro

Ila hii ina maboresho ya ziada katika vipengele vifuatavyo

Kamera zipo tatu na ina kamera ya telephoto, nzuri sana kurekodi ukiwa mbali na unayemrekodi

Mfumo wake wa memori una kasi hivyo utendaji wake ni mkubwa zaidi

Betri lake ni kubwa lina mAh 7000, hapa chaji inakaa mpaka masaa 20 ukiwa kwenye intaneti

Kwa kifupi hii ndio infinix bora zaaidi kwa 2026

Infinix Hot 70

Bei ya Infinix Hot 70 ni shilingi 330,000 ya GB 128 na RAM 4

Ni simu maalum kwa matumizi ya kawaida ya kila siku

Kwa maana haina utendaji mkubwa na kamera kali kama za Infinix Note 60

Kwani ina kamera moja tu ya ukubwa wa megapixel 8

Kama ilivyo ada, betri ni kubwa ina mAh 60000

Infinix Smart 20

Simu ya Infinix Smart 20 inauzwa shilingi 350,000 ya GB 128

Kwenye hii linki kuna maelezo zaidi: infinix smart 20

Kiujumla ni simu inayomfaa mtumiaji mwenye mahitaji machache ya simu

Infinix Note Edge

Bei ya Infinix Note Edge ni shilingi laki saba na nusu (750,000)

Hizi ndio sababu za simu kuuzwa zaidi ya laki saba

Ina utendaji mkubwa wa kuruhusu kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja

Betri yake ni kubwa ina mAh 6500 na chaji ya wati 45, hivyo inakaa muda mrefu na wakati wa kuchaji haichukui muda kujaa

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 50 na Sifa Zake Mpya

Bei ya Tecno Spark 50 imeongozeka kuliko hata Spark 40 ilipotoka Kwa nini? Kuna sifa mpya mbili ambazo hazipo kwenye toleo lilopita Vitu vipya ni vichache ila vinatengeneza utofauti mkubwa […]

No Featured Image

Infinix Hot 60 ni bora kuliko Hot 70?

Infinix Hot 70 ni simu mpya imeingia rasmi sokoni mwezi mei 2026 Kwa Tanzania inatarajiwa kuingia rasmi mwezi huu Juni Sifa zake zinashtua ukiilinganisha na Infinix Hot 60 Utendaji na […]

infinix note 60 pro

Bei ya Infinix Note 60 Pro na Sifa Zake za Kishindani

Infinix Note 60 Pro ni bonge la simu inayozitoa “knock out” simu shindani nyingi Ukilinganisha na matoleo ya infinix yaliyopita, Infinix Note 60 Pro imeboreshwa pakubwa sana Ni simu ya […]

Bei ya Tecno Camon 50 na Sifa Zake Tofauti

Ukilinganisha na Tecno Camon 40, Camon 50 imeboreshwa upande wa betri, uimara wa bodi na kioo Hizi ndizo kubwa sifa ambazo zimetengeneza utofauti wa bei ukiondoa utofauti wa kimuonekano Ukishaiona […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: 0756 077262 au 0683 420543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company