SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na bei ya simu ya Redmi note 9 (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 16, 2022

Simu ya redmi note 9 ilitoka rasmi mwaka 2020

Kwa miaka miwili iliyopita ilikuwa ni moja ya simu nzuri ya daraja la kati.

Lakini uimara wake wa bodi, kamera, chaji na processor zinaipa simu nafasi ya kushindana na simu nyingi mpya za android 11

simu ya redmi note 9 upande wa mbele na nyuma

Bei ya redmi note 9 ni chini ya shilingi laki tano

Ukizielewa kiundani sifa zake, unaweza kushawishika kuitumia kwani zina ubora kwenye sehemu nyingi

Bei ya Redmi Note 9  Tanzania

Bei ya redmi note 9 pro kwenye soko la kidunia ni shilingi 438,858/=

Hii ni redmi yenye ukubwa wa GB 128 na RAM GB 6

Ni bei inayovumilika hasa unapotazama ubora wa sehemu mbali mbali za simu.

Kwa wauza simu ndani ya Tanzania bei yake inaweza kuzidi  laki tano.

Kitu cha muhimu, zielewe kiufasaha sifa za simu yoyote kabla ya kununua, ili ujue kama itakidhi mahitaji yako

Sifa za Redmi Note 9

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G85
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 10
  • MIUI 11
Memori  128GB,64GB, na RAM 6GB,3GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.53inchi
Chaji na Betri
  • 5020mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 438,858/=

Upi ubora wa simu ya Redmi Note 9

Ubora wa redmi note 9 unapatikana kwenye mfumo wake wa chaji

Simu ina uwezo wa kuchaji simu nyingine

Betri yake ni kubwa inayoweza kutunza chaji muda mrefu

Utendaji wake unaweza kusukuma gemu nyingi za ubora tofauti

Simu inapokea toleo lingine la android ya mwaka 2021

Uwezo wa Network

Simu ina uwezo wa kutumia intaneti za aina zote isipokuwa 5G

Netwrok bands za 4G zinasapoti mitandao yote ya simu ya hapa Tanzania .

network ya redmi note 9 4g

Hii ni kwa sababu simu ina network bands zipatazo kumi ikiwemo zile zinazotumika na mitandao ya hapa nchini

Aina ya 4G yake ni LTE Cat 7 yenye spidi inayofikia 300Mbps.

Hiki ni kiwango kinaweza kudownload faili la ukubwa wa 1200MB kwa sekunde chache

Ubora wa kioo cha Redmi Note 9

Kioo cha redmi note 9 ni cha aina ya ips lcd

Kina uangavu wa wastani unaofikia nits 450.

Ukiwa unatumia simu juani unaweza pata shida kuona vitu vya kwenye display

Kiubora, ips lcd ina ubora mdogo ila resolution kubwa inaisidia simu kuonyesha vitu kwa ustadi.

Kwani resolution yake ina pixels 1080 x 2340

Nguvu ya processor ya MediaTek Helio G85

Simu ya redmi note 9 inapewa nguvu na processor ya Helio G85.

Hii ni processor ya daraja la kati yenye core nane.

Ina core zenye nguvu sana na zenye nguvu ndogo

processor chipset ya redmi note 9

Utendaji wa helio g85 ni wa wastani hasa kwa kutizama data za geekbench na antutu.

Kwenye geekbench processor inapata alama 358

Na antutu inaipa alama 231,800

Nguvu ya wasatani kiutendaji inasababishwa na muundo na uwezo wa core kubwa hasa,

Uwezo wa core kubwa

Kuna core kubwa mbili zenye spidi inayofikia 2.0GHz

Na zinatumia Cotex A75.

Core ya Cortex A75 haina nguvu kubwa sana ukilinganisha na Cortex A78.

Ndio maana kiutendaji processor haipati alama zinazofuka 500 kwenye geekbench.

Huu ni muundo unaoweza kusukuma gemu ya Fortnite kwenye resolution ndogo na kwa spidi ya 30fps

Uwezo wa core ndogo

Core ndogo zipo sita na zina spidi isiyovuka 1.8GHz

Hizi core zimeundwa kwa muundo wenye ufanisi mkubwa katika matumizi madogo ya umeme

Muundo huo ni Cortex A55

Cortex A55 hutumika pale processor inapochakata kazi zinazotumia nguvu ndogo

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya redmi note 9 pro ina ukubwa wa 5020mAh

Chaji yake inaweza kueleka ueme unaofikia wati 18.

Huu ni umeme unaoweza kujaza simu kwa za zaidi ya masaa matatu

Wati 18 ni umeme mdogo ukilinganisha na ukubwa wa betri

Betri yake inakaa na chaji masaa 125 kama simu ikiwa inatumika mara chache.

Na ukiwa unatumia intaneti masaa mengi mfululizo simu inaisha chaji baada ya masaa 18.

Fuatilia, uwezo wa simu ya redmi kukaa na chaji(Majaribio ya gsmarena)

Ukubwa na aina ya memori

Simu inakuja katika aina nne upande wamemori

Kuna redmi ya 64GB ram ya 3GB, 64GB ram ya 4GB,128GB ram ya 4GB na 128GB ram ya 6GB

Huu ni ukubwa unaotunza mafaili na video za kutosha

Uimara wa bodi ya Redmi Note 9 Pro

Redmi note 9 pro ina bodi ambazo si imara sana upande wa nyuma

Kwa sababu imetengenezwa kwa plastiki.

Lakini kwenye screen ni kugumu kupasuka na kuchunika.

Hiyo inatokana na simu kuwa na kioo cha gorilla glass 5

Ubora wa kamera

Simu ina kamera zipatazo nne

Kamera kuu ina sensa kubwa ya megapixel 48

kamera macho manne ya redmi note 9

Lakini mufmo wake wa kamera hauna dual pixel pdaf wala OIS.

Dual pixel pdaf inaipa kamera ya simu ubora wa kulenga kwa ustadi kitu kinachotembea pindi unapochukua picha au video.

Kamera yake inaweza kurekodi video za aina moja ambayo ni full hd kwa spidi ya 30fps

Ubora wa Software

Simu hii inakuja na android 10 ila inakubali kuwekewa toleo la android 11

Na pia inakuja na MIUI 11 na inakubali MIUI 12.5

MIUI 12.5 ina app nzuri ya kuscreen shot.

Kwani inaweza kuscreenshot kitu kwa urefu unaohitaji hata ukurasa mzima

Yapi Madhaifu ya Redmi Note 9

Utendaji wa redmi note 9 ni wa wastani kwa maana hauna nguvu kubwa sana

Mfumo wake wa kamera hauna OIS

Chaji yake inajaza betri kwa masaa mengi kwa sababu ya spidi ndogo

Simu haitumii kioo cha amoled ambavyo vinaonyesha vitu kwa uangavu mkubwa

4G yake ina bands chache tofauti na simu za redmi zingine

Simu haina kamera ya telephoto wa optical zoom

Neno la Mwisho

Hii simu ni nzuri.

Ila bei yake inaonekana kuwa kubwa kwa mwaka huu.

Kuna simu ya Redmi Note 10 5G inayouzwa chini ya laki nne ina utendaji mkubwa kuliko Note 9

Kwa hiyo kama muuzaji anaiuza chini ya kaki tatu na nusu hapo itakuwa sawa.

Lakini kwa bei ya laki nne utapata simu bora kuliko hii.

Chaguo ni lako.

Wazo moja kuhusu “Ubora na bei ya simu ya Redmi note 9 (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram