SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu za Realme za bei rahisi 2022 (na ubora wake)

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 24, 2022

Hii ni orodha ya simu kumi za Realme za bei rahisi kwa mwaka 2022

Kwenye orodha utazifahamu realme za daraja la chini na la kati

Kuna simu za realme zilizotoka mwaka 2020, 2021 na realme mpya za mwaka 2022

Ubora wa kila realme iliyopo na bei zake zitakuongoza kupata chaguo zuri linaloendana na unachokihitaji

Simu ya Realme C31

Simu mpya ya realme c31 imetoka mwishoni mwa mwezi machi mwaka 2022.

Ni simu yenye kioo cha aina ya ips lcd kilicho na resolution ndogo ya 720×1600 pixels

Utendaji wa simu ni mzuri kwani inatumia processor ya daraja la kati aina ya Unisoc Tiger T612

simu ya realme c31

Simu inaweza kukaa na chaji masaa yanayozidi 14(data ikiwa on) kwa sababu ya kuwa na betri kubwa la 5000mAh

Ina mfumo wa memori wenye kasi aina ya UFS 2.1 unaongeza nguvu ya utendaji wa simu

Simu ina bodi imara na kioo kigumu kuchunika sababu imewekewa kioo aina ya panda

Ni realme ya macho matatu yenye kamera zenye ubora mdogo sana

Bei ya realme c31

Bei halisi ya realme c31 ya ukubwa wa GB 32 ni shilingi 305,000/=

Na bei ya realme c31 ya ukubwa wa GB 64 ni shilingi 335,325.19/=

Bei ya simu inavumulika ila upatikanaji wake nchini Tanzania ni mdogo

Hivyo ni vizuri ukainunua simu aliexpress kama ikiwezekana

Simu ya Realme Narzo 50i

Simu ya realme narzo 50i ni simu ya bei nafuu ya android ya mwaka 2021

Simu ina utendaji mdogo kutokana na aina ya processor inayotumia

Ina kamera moja tu ambayo resolution yake sio kubwa

simu ya realme narzo 50i

Uwezo wa kukaa na chaji muda mrefu ni mkubwa kwani betri lake ni la 5000mAh

Ina bands chache za mtandao wa 4G

Kioo cha realme narzo 50i ni cha aina ya ips lcd na kina resolution ndogo vilevile

Kiujumla ni simu inayomfaa mtumiaji anayeanza kutumia simu janja

Bei ya realme narzo 50i

Bei halisi ya realme narzo 50i ni shilingi 228,630.81/=

Hii ni kwa narzo 50i ya ukubwa GB 32

Kama utanunua Tanzania bei inaweza kuzidi 250,000/=

Realme C21Y

Simu ya realme c21y ni simu ya mwaka 2021 yenye toleo la android 11

Simu ina utendaji wa wastani kutokana na kutumia processor ya daraja la kati aina ya Unisoc T610

simu ya realme c21y

Kamera zake tatu ni za kuridhisha japokuwa ni kamera moja tu yenye teknolojia ya ulengaji wa PDAF

Simu inakuja na betri kubwa ya ujazo wa 5000mAh

Kioo cha realme c21 ni cha aina ya IPS LCD chenye resolution ndogo ya 720 x 1600 pixels

Ila hii simu imeundwa kwa plastiki upande wa nyuma na kwenye frem

Bei ya Realme C21Y

Bei ya Realme C21Y yenye ukubwa wa GB 32 ni shilingi 327,881.09/=

Bei inaendana na ubora wa simu na sifa zake.

Ukibahatika kuipata Tanzania bei yake inaweza kuwa zaidi ya hiyo

Simu ya Realme C11

Realme C11 ni simu ya mwaka 2020 yenye toleo la android 10

Utendaji wa simu si mkubwa kutokana na kutumia memori aina ya eMMC na chip ya MediaTek Helio G35

Kioo cha realme c11 kinatumia teknolojia ya ips lcd ambacho huwa na rangi chache.

simu ya realme c11

Lakini pia kioo kina resolution ndogo ya 720×1560 pixels

Linapokuja swala chaji, simu ina uwezo wa kukaa na betri muda mwingi (betri la 5000mAh)

Simu ina kamera mbili tu ambazo zina ubora wa chini katika upigaji picha

Bei ya Realme C11

Bei ya realme c11 ambayo ina ukubwa GB 32 ni shilingi 226,134.94/=

Realme C11 ina matoleo mawili yanayotofautiana ukubwa wa ram

Hivyo bei zake zitakuwa hazitofautiani sana

Simu ya Realme 9 5G

Simu mpya ya realme 9 5g ni simu ya macho manne inayotumia toleo la android 11.

Ni simu ambayo imeingia sokoni mwezi machi 2022

Simu inakubali 4G ya mitandao yote Tanzania kwa sababu ina network bands za 4G zipatazo 12

simu ya realme 9 5g

Processor yake aina ya dimensity 810 inaifanya simu kuwa na uwezo mkubwa wa kufungua app yoyote

Realme 9 5G ni simu inayokubali mtandao wa 5G

Kioo cha Realme 9 5g kina resolution kubwa ya 1080×2400 na ni cha ips lcd chenye refresh rate ya 90Hz

Ina betri kubwa la 5000mAh

Hivyo simu inakaa na chaji muda mrefu wakati huo utendaji ni mkubwa

Bei ya Realme 9 5G

Bei halisi ya Realme 9 5G yenye ukubwa wa GB 64 na RAM ya GB 4 ni shilingi 487,745.73/=

Toleo la GB 128 bei yake inazidi laki tano na nusu.

Elewa kuwa hii ni simu ya daraja la kati ndio maana bei yake ipo juu kidogo

Simu ya Realme narzo 50

Simu ya realme narzo 50 ni simu ya 4G mpya ambayo imetoka mwezi machi 2022

Realme narzo 50 ina kioo chepesi wakati wa kuperuzi kwani kimewekewa refresh rate inayofika 120Hz

Kioo cha narzo 50 ni cha aina ya ips lcd kilichoboreshwa kwa kuwekewa resolution ya 1080×2412 pixels

simu ya realme narzo 50

Simu inaweza kusukuma kila aina ya app kwa sababu inatumia processor yenye nguvu aina ya MediaTek Helio G96

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh na hivyo inaweza kukaa na chaji masaa mengi

Na kizuri simu inawahi kujaa kwa haraka, ina fast chaji inayopeleka umeme kwa kasi inayofikia wati 33

Ni simu ya android 11 inazungukwa na kamera tatu upande wa nyuma

Ila ubora wa kamera sio mkubwa na inaweza kurekodi video za aina ya full hd pekee.

Bei ya Realme narzo 50

Bei ya realme narzo 50 toleo la gb 64 na ram ya GB 4 ni shilingi 396,293.41/=

Na realme ya ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 6 bei yake stahiki haizidi 487,745.73/=

Ila kwa bei za realme Tanzania inazidi laki tano

Simu ya Realme C35

Realme C35 ni simu ya macho matatu yenye android 11 ambayo imetoka mwaka 2022 (Ni simu mpya)

Utendaji wa simu unaweza kufungua app nyingi kwa wepesi kwa sababu ya kutumia processor ya uwezo wa kati ya Unisoc Tiger T616

Ina kamera tatu, kamera kuu ni nzuri zaidi kwa sababu ina PDAF.

simu ya realme c35

Ila PDAF haifikii kiubora teknolojia ya ulengaji ya dual pixel pdaf.

Betri yake ni kubwa (5000mAh) ila chaji yake haipeleki umeme mwingi sana (18W)

Kioo cha realme c35 ni cha ips lcd chenye uangavu mdogo wa 480nits

Ila koo kina resolution nzuri ya 1080 x 2408

Bei ya Realme C35

Bei ya realme c35 ya ukubwa wa GB 64 na RAM GB 4 ni shilingi 466,257.60/=

Kwa ukubwa zaidi ya huo bei yake inaweza kuzidi laki tano

Simu ya Realme C25Y

Simu ya realme c25y ni simu ambayo imetoka mnamo mwaka 2021.

Ina utendaji wa wastani kwa sababu ina processor ya Unisoc T610 na memori za eMMC 5.1

Ina kioo cha ips lcd kilicho na resolution ndogo ya 720 x 1600 pixels

simu ya realme c25y

Simu imeundwa kwa plastiki hivyo si simu imara sana

Ina kamera tatu na kamera kubwa ina resolution ya 50MP

Lakini ubora wake si mkubwa kwa sababu hakuna dual pixel pdaf na OIS

Pia kamera zake hazirekodi video kubwa za 4k

Simu ina betri kubwa la 5000mAh na betri inayochaji kwa spidi inayofikia wati 18

Bei ya Realme C25Y

Bei ya halisi ya realme c25y ni shilingi 335,325.19/=

Hii ni bei ya realme c25y ya gb 64 yenye ram 4G

Lakini ushishangae bei kupanda zaidi ya laki tatu na nusu kwa maduka ya simu dar es salaam

Simu ya Realme C25

Simu ya realme c25 ni simu ya android 11 ya mwaka 2021

Ni simu yenye betri kubwa sana la ujazo wa 6000mAh

Hivyo inaweza kukaa na chaji masaa mengi

Hilo pia linachangiwa na utendaji wa wastani unaochangiwa na processor ya daraja la kati ya Helio G70

simu ya realme c25

Ina 4G yenye bands chache ila inakubali mitandao mingi ya simu nchini

Kioo cha realme c25 ni cha IPS LCD ambacho kina resolution ndogo 720 x 1600 pixels

Betri yake inapeleka umeme wa wastani unaofikia wati 18

Ubora wa kamera ni wa kawaida kwani kamera zake zinarekodi video za full hd pekee na kwa spidi ndogo ya 30fps

Bei ya Realme C25

Bei ya realme c25 yenye ukubwa wa GB 64 ni shilingi 353,102.71/=

Bei inaweza kuongezeka kama hautonunua simu mtandaoni

Kwani maduka ya simu mengi ya Tanzania wanaiuza simu kwa bei ya juu kidogo

Simu ya Realme Narzo 50A

Simu ya realme narzo ni simu ya mwaka 2021 yenye android 11.

Betri ya narzo 50a ina ukubwa wa 6000mAh.

Tegemea simu kukaa na chaji muda mrefu.

Utendaji wake ni wa wastani na wa kuridhisha, inatumia chip ya MediaTek Helio G85

simu ya realme-narzo-50a

Kioo cha realme narzo 50a ni cha aina ya IPS LCD chenye resolution ndogo ya 720×1600

Ni realme ya macho matatu ambayo haina mfumo mzuri sana wa kamera.

Kwa sababu kamera kubwa inatumia PDAF ambayo inazidiwa na dual pixel pdaf

Na pia kamera zake zinarekodi video za ubora wa full hd pekee yake kwa spidi ya 30fps

Bei ya realme Narzo 50A

Bei ya narzo 50a ya ukubwa wa GB 64 ni shilingi 365,809.30/=

Hizi ni bei za India.

Hivyo kwa Tanzania bei yake inaweza kuzidi 400,000/=

 

Wazo moja kuhusu “Simu za Realme za bei rahisi 2022 (na ubora wake)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

No Featured Image

Simu Mbalimbali za Vodacom Tanzania na Bei Yake

Hii ni orodha inayohusisha simu ambazo zinauzwa na kampuni ya vodacom na bei zake Kwenye orodha kuna simu zipatazo nane (8) za bei nafuu, kati na bei kubwa Ni simu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram