SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Nzuri za Blackberry na Bei Zake (Android)

Brand

Sihaba Mikole

June 26, 2022

Blackberry ni kampuni ya simu ambayo kwa sasa inajikongoja

Kwani tangu 2018 hawakutoa simu mpya

Bali palikuwa na tetesi za toleo la mwaka 2022 lililofahamika kama blackberry vienna 5g

Kwenye hii orodha kuna baadhi ya  simu za blackberry na bei zake ambazo zimetoka kati 2017 – 2018

Hizi ni smartphone zenye batani pia

Blackberry Evolve

Simu ya Blackberry ilitoka mwaka 2018 ikiwa inatumia Android 8

Utendaji wake si mkubwa kwani inatumia processor yenye nguvu ndogo ya Snapdragon 450

Kioo cha Evolve ni aina ya IPS LCD chenye resolution ya 1080 x 2160 pixels

Ukubwa wake wa memori ni GB 64 na RAM ni GB 4

blackberry evolve

Ina kamera mbili ambazo zinatumia ulengaji wa PDAF ila ukusanyaji wa mwanga ni mdogo

Ukaaji wake wa chaji ni wa kuridhisha kutokana na kuwa na betri kubwa la wastani

Ukubwa wa betri ni 4000mAh

Simu hii inaweza kukaa na chaji muda mwingi kwa sababu processor inatumia haili umeme mwingi

Bei ya Blackberry Evolve

Wakati simu inatoka bei yake ilikuwa ni shilingi 737,232.00/=

Kiasi hiki cha pesa kinakupa picha kwa nini simu za blackberry hazikufanya vizuri tangu ujio wa Android na iPhone

Bei ni kubwa kuliko ubora wa simu

Blackberry Key2

Simu ya Blackberry key2 iliingia sokoni mwezi juni mwaka 2018

Ni simu ya android yenye batani pamoja na tachi

Utendaji wake ni wastani kutokana na simu kutumia memori za eMMC 5.1 na chip ya Snapdragon 660

Hii simu pia inalindwa na kioo cha Gorilla 3 upande wa screen

Gorilla 3 huwa ni vioo vigumu kuchunika

blackberry key2

Kioo chake ni cha IPS LCD ambacho kina resolution kubwa ya 1080 x 1620 pixels

Kwenye memori kuna key2 ya GB 64 na GB 128

Hivyo kuna nafasi ya kutosha kuhifadhi mafaili ya kutosha

Ina betri lenye ujazo mdogo wa 3500mAh

Hivyo ukaaji wa chaji ni mdogo

Kamera zake ni nzuri kwani zinaweza kurekodi video za 4K kwa fremu za 30fps

Bei ya Blackberry key2

Wakati imetoka 2018 bei yake ilikuwa ni shilingi 1,228,720.00/=

Hii bei ni kubwa ambayo kwa wakati huo ungeweza kupata simu kali za samsung au redmi zinazoizidi key2 ubora kwa sehemu kubwa

Kwa sasa bei inaweza ikawa imepungua ila upatikanaji wake ni mgumu kwa Tanzania

Blackberry Motion

Blackberry motion ni simu ya Android 7.1 iliyotoka mwaka 2017

Blackberry hii sio simu ya batani  kama zile za mwaka 2018

Chip iliyotumika na Blackberry motion ni Snapdragon 625

Snapdragon 625 ina utendaji wa chini kutokana na kila core kutumia Cortex A53

blackberry mtion

Blackberry motion ni simu isiyopitisha maji

Kama ikizama kwenye maji ya kina cha mita moja maji hayatoingia kwenye simu kwa muda wa nusu saa

Kioo chake ni cha ips lcd ambacho kina resolution ya 1080 x 1920 pixels

Ila memori yake ni ndogo ya GB 32

Betri yake ni la wastani lina ukubwa 4000mAh

Hivyo ukaaji wa chaji ni wa kuridhisha kwa chip yake haitumii umeme mwingi

Kamera yake ina ubora mdogo na resolution yake ni ndogo pia

Bei ya Blackberry Motion

Bei ya Blackberry motion ilikuwa ni shilingi 958,401.60/=

Bado ni kwamba hii bei ni kubwa hata kama ilikuwa ni miaka mitano iliyopita

Blackberry Aurora

Aurora ni blackberry nyingine ya mwaka 2017

Ni simu ndogo yenye kimo cha 5.5 hivyo haina batani

Inakuja na android toleo la 7 yaani Android Nougat

Ina kioo cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1280 pixels

lackberry aurora

Betri yake ni ndogo lina ukubwa 3000mAh

Hivyo ukaaji wake ni wa kiwango cha chini

Utendaji wa simu kiujumla ni mdogo

Kwani simu inatumia processor yenye nguvu ndogo ya Snapdragon 425

Bei ya Blackberry Aurora

Wakati simu inatoka bei yake ilikuwa ni shilingi 500,000/= za Tanzania

Ubora wa simu unaonyesha ni simu ya kuuzwa 150,000/=

Hii ni moja ya sababu simu za blackberry zilikosa soko na zinashindwa kuinuka tena

Blackberry KeyOne

Blackberry KeyOne ni smartphone ya android yenye tachi na batani

Ilitoka mwaka 2017

Ni simu yenye inchi 4,5 hivyo ni simu ndogo inayojaa mkononi

Utendaji wake ni mdogo kutokana na simu kutumia chip ya Snapdragon 625

Snapdragon 625 ina nguvu ndogo

blackberry keyone

Kioo cha blackberry keyone ni aina ya IPS LCD na resolution ya 1080 x 1620 pixels

Ukaaji wa chaji pia si mkubwa

Kwa sababu betri ina ukubwa wa 3500mAh

Ina kamera moja yenye ukubwa wa 8MP

Na haitoi picha nzuri bali inaweza kurekodi video za full hd pekee

Bei ya Blackberry KeyOne

Hii simu bei yake wakati inatoka ilikuwa ni shilingi 712,657.60/=

Kiujumla katika list iliyopo hakuna simu inayoweza ikachuana na simu za miaka karibuni

Hasa ukizingatia kiasi cha pesa ambacho kinahitajika kupata blackberry zilizopo

Hii kampuni kwa sasa 2022 imebaki kuwa historia

Haiwezi kuingia hata kwenye 20 ya makampuni bora ya simu bora

Maoni 3 kuhusu “Simu Nzuri za Blackberry na Bei Zake (Android)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

oppo find x6 pro thumbnail

Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Kuna matoleo mengi ya simu za oppo zenye ubora tofauti tofauti Zipo ambazo zina ubora wa kati, wa juu na wa chini Katika hizo, nyingi zinajitahidi kuwa na kamera zinazotoa […]

No Featured Image

Simu Mpya za Samsung na Bei Zake 2023

Kama unatafuta samsung mpya kwa mwaka 2023 basi upo sahihi Kwenye hii kuna simu zipatazo saba na maelezo mafupi kuhusu sifa zake Kwenye hii orodha ya simu mpya za samsung […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram